Utangulizi wa Sehemu ya 13
Yesu alikuja duniani ili kutoa uhai wake kwa ajili ya wanadamu wasio wakamilifu. Ingawa alikufa, yeye aliushinda ulimwengu. Yehova alikuwa mshikamanifu kwa Mwana wake, hivyo alimfufua. Alipokuwa hai hapa duniani, Yesu aliwatumikia watu kwa unyenyekevu na kuwasamehe walipokosea. Baada ya kufufuliwa, Yesu aliwatokea wanafunzi wake. Aliwafundisha jinsi ya kufanya kazi muhimu aliyokuwa amewapa. Ikiwa wewe ni mzazi, msaidie mtoto wako kuelewa kwamba sisi pia tunapaswa kushiriki katika kazi hiyo.