WIMBO NA. 47
Sali kwa Yehova Kila Siku
Makala Iliyochapishwa
1. Sali kwa Yehova, Husikia.
Ni pendeleo kumwakilisha.
Moyo wako umfungulie,
Sikuzote umtegemee.
Tusali kila siku.
2. Sali kwa Yehova, mshukuru.
Atusamehe, tusamehevyo.
Mbele zake Mungu tuungame.
Ndiye Muumba, anatujua.
Tusali kila siku.
3. Sali kwa Mungu ulemewapo.
Ndiye Baba yetu, yu karibu.
Mwombe ulinzi, na msaada;
Mtumaini, usiogope.
Tusali kila siku.
(Ona pia Zab. 65:5; Mt. 6:9-13; 26:41; Luka 18:1.)