SEHEMU YA KWANZA
“Mbingu Zilifunguliwa”
WAZO KUU: Maono ya makao ya Yehova
Hakuna mwanadamu anayeweza kumwona Mungu mweza yote, Yehova, naye aendelee kuishi. (Kut. 33:20) Hata hivyo, Yehova alimpa Ezekieli maono ambayo yanafunua sehemu ya kimbingu ya tengenezo Lake—maono ambayo yanatushangaza na pia yanatufanya tuthamini pendeleo la kumwabudu Mungu wa pekee wa kweli.