Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • rr uku. 10
  • Ibada Ni Nini?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ibada Ni Nini?
  • Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
  • Habari Zinazolingana
  • Wakristo Hupata Furaha Kutumikia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
  • Kutoa Utumishi Mtakatifu Usiku na Mchana
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
  • Kuona Ubora wa Hazina ya Utumishi Mtakatifu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
  • Ibada ya Kweli Itaongeza Furaha Yako
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2022
Pata Habari Zaidi
Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
rr uku. 10
Familia ikifanya ibada ya familia.

SANDUKU LA KUFUNDISHIA LA 1A

Ibada Ni Nini?

Ibada inaweza kufafanuliwa kuwa “tendo la kumwonyesha mungu fulani heshima na upendo.” Katika Biblia, maneno ya awali yanayotafsiriwa kuwa “ibada” yanaweza kuwa na wazo la mtu anayeonyesha heshima kubwa, au kujitiisha kwa viumbe. (Mt. 28:9) Maneno hayo yanaweza pia kumaanisha tendo la ibada kuelekea Mungu au miungu. (Yoh. 4:23, 24) Muktadha unasaidia kuelewa maana ya maneno hayo.

Yehova peke yake, Muumba na Mwenye Enzi Kuu ya Ulimwengu Wote, ndiye tu tunayepaswa kumwabudu. (Ufu. 4:10, 11) Tunamwabudu Yehova kwa kuheshimu enzi yake kuu na kwa kuliheshimu jina lake. (Zab. 86:9; Mt. 6:9, 10) Mambo hayo mawili—enzi kuu ya Yehova na jina lake—yanatajwa sana katika kitabu cha Ezekieli. Maneno “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova” yanatumiwa mara 217 katika Ezekieli peke yake, na maneno “kujua kwamba mimi ni Yehova,” mara 55.—Eze. 2:4; 6:7.

Hata hivyo, ibada yetu haihusishi hisia tu; badala yake, ibada ya kweli inahusisha matendo. (Yak. 2:26) Tunapojiweka wakfu kwa Yehova, tunatoa kiapo kwamba katika kila jambo maishani mwetu, tutamtii akiwa Bwana Mwenye Enzi Kuu na kuliheshimu sana jina lake. Kumbuka kwamba alipokuwa akijibu jaribu la tatu, Yesu alihusianisha ibada na “utumishi mtakatifu.” (Mt. 4:10) Tukiwa waabudu wa Yehova, tunatamani kumtumikia.a (Kum. 10:12) Tunamtolea Mungu wetu utumishi mtakatifu tunapofanya matendo yanayohusiana moja kwa moja na ibada yetu na yanayohitaji kujidhabihu. Ni matendo gani hayo?

Mkusanyo wa picha: Utumishi mtakatifu. 1. Dada akitoa maelezo kwenye mkutano. 2. Ndugu na dada wakifanya usafi katika eneo la kusanyiko.

Utumishi mtakatifu unahusisha mambo mengi, na mambo hayo yote ni yenye thamani kwa Yehova. Tunatoa utumishi mtakatifu tunapowahubiria wengine, tunaposhiriki mikutano katika Jumba letu la Ufalme, na tunapotunza na kujenga majengo yetu ya ibada. Isitoshe, tunatoa utumishi mtakatifu tunaposhiriki katika ibada ya familia, tunapounga mkono kazi ya kutoa msaada kwa waabudu wenzetu walio na uhitaji, tunapojitolea kwenye makusanyiko, au kwa kutumikia Betheli. (Ebr. 13:16; Yak. 1:27) Ibada safi inapokuwa jambo muhimu zaidi katika akili na mioyo yetu, tunatoa “utumishi mtakatifu mchana na usiku.” Tunafurahia kumwabudu Mungu wetu, Yehova!—Ufu. 7:15.

Angalia sura ya 1, fungu la 9

a Neno la Kiebrania linalotoa wazo la ibada pia linamaanisha “kutumikia.” Basi ibada inahusisha utumishi.—Kut. 3:12, maelezo ya chini.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki