Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lmd somo la 10
  • Azimia Kuwasaidia Watu Wawe Wanafunzi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Azimia Kuwasaidia Watu Wawe Wanafunzi
  • Wapende Watu—Fanya Wanafunzi
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Yesu Alifanya Nini?
  • Tunajifunza Nini Kutoka kwa Yesu?
  • Mwige Yesu
  • Jifunze Kutoka kwa Nikodemo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
  • Amfundisha Nikodemo Usiku
    Yesu—Njia, Kweli, na Uzima
  • Wasaidie Wanafunzi wa Biblia Wachukue Msimamo Upande wa Kweli
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2025
  • Kumfundisha Nikodemo
    Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi
Pata Habari Zaidi
Wapende Watu—Fanya Wanafunzi
lmd somo la 10

KUFANYA WANAFUNZI

Yesu na Nikodemo wakizungumza usiku kwenye ua.

Yohana 3:​1, 2

SOMO LA 10

Azimia Kuwasaidia Watu Wawe Wanafunzi

Kanuni: “Tulijitahidi kuwapa habari njema ya Mungu na hata uhai wetu wenyewe, kwa sababu tuliwapenda sana.”—1 The. 2:8.

Yesu Alifanya Nini?

Jesus and Nicodemus conversing at night in a courtyard.

VIDEO: Yesu Anamfundisha Nikodemo

1. Tazama VIDEO, au soma Yohana 3:​1, 2. Kisha fikiria maswali yafuatayo:

  1. Kwa nini Nikodemo alimtembelea Yesu usiku? —Ona Yohana 12:​42, 43.

  2. Kwa kukutana na Nikodemo usiku, Yesu alionyeshaje kwamba aliazimia kufanya wanafunzi?

Tunajifunza Nini Kutoka kwa Yesu?

2. Kwa sababu tunawapenda watu, tumeazimia kuwasaidia wawe wanafunzi.

Mwige Yesu

3. Jifunze na mwanafunzi wa Biblia kwa wakati na mahali panapomfaa. Anaweza kupendekeza siku fulani katika juma au wakati hususa wa kujifunza. Je, anafurahia kujifunza akiwa kazini, nyumbani au katika eneo fulani la umma? Badili ratiba yako kadiri iwezekanavyo ili ipatane na mahitaji ya mwanafunzi.

4. Mjifunze kwa ukawaida. Ikiwa utasafiri, usisitishe ratiba yenu ya kujifunza. Badala yake, fikiria mambo yafuatayo:

  1. Je, unaweza kuongoza funzo siku nyingine katika juma hilo?

  2. Je, unaweza kuongoza funzo kupitia simu au video?

  3. Je, unaweza kumwomba mhubiri mwingine aongoze funzo?

5. Sali ili uwe na mtazamo mzuri. Mwombe Yehova akusaidie uendelee kuazimia kumsaidia mwanafunzi wako, hata ikiwa si rahisi kwake kujifunza kwa ukawaida au anachukua muda mrefu kutumia ushauri wa Maandiko. (Flp. 2:13) Huenda mwanafunzi wako ana sifa nyingi nzuri; sali kwa Yehova akusaidie uzingatie sifa hizo.

SOMA PIA

Met. 3:27; Mdo. 20:35; 2 Kor. 12:15

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki