Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • it uku. 1133
  • Utakatifu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Utakatifu
  • Ufahamu wa Kina wa Maandiko
  • Habari Zinazolingana
  • Inamaanisha Nini Kuwa Mtakatifu?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Watakatifu wa Kweli Wanaweza Kukusaidiaje?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
  • Lazima Mwe Watakatifu Kwa Sababu Yehova Ni Mtakatifu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • “Lazima Muwe Watakatifu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2021
Pata Habari Zaidi
Ufahamu wa Kina wa Maandiko
it uku. 1133

WATAKATIFU

Watu ambao ni safi, hasa katika maana ya kiroho au kiadili; linamaanisha pia watu waliotengwa kwa ajili ya utumishi wa Mungu, mbinguni au duniani.

Yehova, aliye msafi na mwadilifu kuliko wote, ndiye pekee Mtakatifu Zaidi. (Ho 11:12) Mara nyingi anaitwa “Mtakatifu wa Israeli.” (2Fa 19:22; Zb 71:22; 89:18) Mtume Yohana aliwaambia hivi Wakristo wenzake katika kutaniko la Kikristo: “Mmetiwa mafuta kutoka kwa yule mtakatifu.” (1Yo 2:20) Yesu Kristo anaitwa “aliye mtakatifu na mwadilifu” kwenye Matendo 3:14. Malaika wa Yehova mbinguni ni watakatifu, wamejitoa kabisa katika utumishi wa Mungu, wao ni safi na waadilifu.​—Lu 9:26; Mdo 10:22.

Katika Nyakati za Kale. Wanadamu waliotengwa kwa ajili ya utumishi wa Mungu wameitwa pia “watakatifu.” (Zb 34:9) Waisraeli walifanya agano pamoja na Mungu, wakawa mali yake ya pekee na wakiwa taifa walikuwa watakatifu kwake. Hiyo ndiyo sababu mtu mmoja-mmoja aliyejihusisha na ukosefu wa usafi au dhambi alifanya taifa zima liwe chafu na likose kibali cha Yehova, ikiwa hatua ya kumwondoa haikuchukuliwa mara moja. Mfano mmoja ni Akani mwenye pupa na asiyetii; dhambi yake ilileta matatizo juu ya Waisraeli wote mpaka alipogunduliwa na kuuawa kwa kupigwa mawe.​—Yos 7.

Haruni, aliyewekwa rasmi kuwa kuhani mkuu wa taifa hilo kwa kutiwa mafuta kwa mafuta matakatifu, alikuwa mtakatifu kwa njia ya pekee na iliyokweza. (Zb 106:16) Hiyo ndiyo sababu matakwa ya kuwa na cheo chake yalikuwa magumu sana. (Law 21:1-15; ona pia mambo ambayo yangefanya makuhani wakose kustahili cheo hicho katika mstari wa 16-23; ona KUHANI MKUU.) Ikiwa kuhani mkuu angetenda dhambi (kwa mfano, kutoa hukumu isiyofaa kuhusu jambo fulani) angewafanya watu wote wawe na hatia ambayo ingefunikwa kwa dhabihu ya ng’ombe dume mchanga, dhabihu iliyofanana na ile iliyotolewa kwa kosa la kusanyiko lote.​—Law 4:3, 13, 14.

Wakristo Watakatifu. Watu walio katika uhusiano pamoja na Mungu kwa msingi wa agano jipya wametakaswa, wamesafishwa, na kutengwa kupitia “damu ya agano” ya Yesu Kristo kwa ajili ya utumishi wa Mungu tu. (Ebr 10:29; 13:20) Kwa sababu hiyo wanaitwa “watakatifu.” Hawawi “watakatifu” kwa amri ya mwanadamu au tengenezo fulani, badala yake ni kwa amri ya Mungu, ambaye hufanya agano pamoja nao kupitia damu ya Yesu Kristo. Neno “watakatifu” linawahusu wote walio katika muungano na Kristo na urithi pamoja naye, halihusu watu wachache tu wanaoonwa kuwa na utakatifu wa pekee. Katika Biblia wanatajwa kuwa watakatifu tangu mwanzo wa maisha yao yaliyotakaswa wakiwa duniani, hawasubiriwi hadi wafe ndipo waitwe “watakatifu.” Petro anasema ni lazima wawe watakatifu kwa sababu Mungu ni mtakatifu. (1Pe 1:15, 16; Law 11:44) Ndugu wote wa Kristo makutanikoni wanaitwa “watakatifu.”​—Mdo 9:13; 26:10; Ro 1:7; 12:13; 2Ko 1:1; 13:13.

Likiwa kama “mke” wa Kristo, kutaniko linasemwa kwamba limevaa kitani bora, changavu, safi, kinachowakilisha “matendo ya uadilifu ya watakatifu.” (Ufu 19:7, 8) “Mnyama wa mwituni” wa kisiasa wa Shetani Ibilisi anaonekana akipigana vita dhidi ya watakatifu wakiwa duniani. (Ufu 13:3, 7) Kwa sababu hiyo uvumilivu wa watakatifu hao unajaribiwa vikali, lakini wanashinda kwa kushika amri za Mungu na kuwa na imani katika Yesu.​—Ufu 13:10; 14:12.

Tumaini lao. Katika maono yanayofanana na hayo, Danieli anaona mnyama wa mwituni akipigana na watakatifu wa Mungu; hilo lilifuatwa na maono ya mahakama ambapo “Mzee wa Siku” alitoa hukumu kwa faida ya watakatifu nao wakapewa Ufalme wa milele, “ufalme na utawala na utukufu wa falme chini ya mbingu.”​—Da 7:21, 22, 27.

“Watakatifu” hao hawatumii mamlaka yao ya kifalme wakiwa duniani, lazima wasubiri hadi watakapojiunga na Kristo mbinguni. (Efe 1:18-21) Lazima kwanza wawe ‘washindi.’ (Ufu 3:21; linganisha Ufu 2:26, 27; 3:5, 12.) Watatenda wakiwa makuhani na kutawala wakiwa wafalme pamoja na Kristo wakati wa Utawala wake wa Miaka Elfu Moja. (Ufu 20:4, 6) Mtume Paulo anasema kwamba watakatifu watauhukumu ulimwengu, na vilevile malaika, ikionyesha kwamba watashiriki kuwahukumu waovu.​—1Ko 6:2,  3; Ufu 2:26, 27.

Kushambuliwa kwa “Kambi ya Watakatifu.” Kwenye Ufunuo 20:7-9 imetabiriwa kwamba Shetani Ibilisi atayaongoza mataifa katika vita dhidi ya “kambi ya watakatifu na lile jiji linalopendwa” baada ya miaka elfu moja ya utawala wa Kristo. Unabii huo unarejelea uasi utakaokuwa hapa duniani dhidi ya enzi kuu ya ufalme wa Mungu juu ya dunia, ambao utakuwa kama shambulizi juu ya “watakatifu.” Katika muktadha huo hao ni wanadamu waliorudishwa kwenye uhusiano mzuri pamoja na Mungu na wanaodumisha utimilifu wao kwa Mungu na Mfalme wa Ufalme wake wa Kimasihi.​—Ona UTAKATIFU.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki