“Wajibu wa Kila Mkristo”
Kitabu A Handbook of Christian Theology kinasema hivi kuhusu Wakristo wa kwanza: “Katika ule ushirika mdogo wa Yesu na rafikize hakukuwako mgawanyo wa viongozi wa kidini na watu wa kawaida . . . wanafunzi hao, ambao kwa wakati huu wanaweza kuonwa kuwa watu wa kawaida, ndio waliokuwa wahubiri hasa . . . Bila shaka, kulikuwako viongozi na waalimu na wanenaji wa pekee. Walakini walichofanya ni kuonyesha au kuweka uongozi kwa wajibu wa kila Mkristo.