Maswali Kutoka kwa Wasomaji
● Kwa sababu gani kulingana na habari za Mathayo, Yesu alitumia maneno mawili mbalimbali—“uasherati” na “uzinzi”—katika kuzungumza sababu zinazofaa za talaka? Je! “uzinzi” siyo sababu ya pekee ya talaka inayolingana na Maandiko, kama vile neno hilo litumiwavyo kwa kawaida?—U.S. A.
Katika Mathayo 5:32 maneno ya Yesu ndiyo haya: “Lakini mimi nawaambia, Kila mtu amwachaye mkewe isipokuwa kwa habari ya uasherati [Kigiriki, por·neiʹa], amfanya kuwa mzinzi [Kigiriki, moi·kheiʹa]; na mtu akimwoa yule aliyeachwa, azini.” Vivyo hivyo, katika Mathayo 19:9 twasoma: “Nawaambia ninyi, Kila mtu atakayemwacha mkewe, isipokuwa ni kwa sababu ya uasherati [por·neiʹa], akaoa mwingine, azini [moi·kheiʹa].”
Kwa hiyo, habari hii inatumia maneno mawili mbalimbali. Ebu kwanza na tuone yanachomaanisha kisha tuangalie maana ya matumizi yake.
Moi·kheiʹa, mojawapo la maneno yanayotumiwa katika habari ya Mathayo, limetafsiriwa kwa kufaa “uzinzi.” Neno la Kirumi litumiwalo ni adulterare, linalomaanisha, “kugeuza namna” na, kwa maana zaidi, “kuharibu au kuchafua, kama vile kwa kuongeza kitu fulani cha kigeni au kibaya zaidi.” Hivyo twazungumza juu ya ‘kuchafua’ chakula, kwa kuongeza vitu vya kigeni. Ndoa inachafuliwa wakati mwenzi mmojawapo anapouchafua uhusiano wa ndoa kwa kufanya ngono na mtu asiye katika ukamatano huo. Neno hili la kuchafua au kuharibu, na la kukosa uaminifu kwa uhusiano mtakatifu, vile vile limo katika neno la Kigiriki moi·kheiʹa. Kwa hiyo, katika Kigiriki na Kiswahili vile vile, kinachotajwa ni matokeo ya ngono isiyoruhusiwa juu ya uhusiano wa ndoa, mwenzi mzinzi akiwa mwenye hatia ya kumwingiza mtu mwingine katika ukamatano huo, akiuharibu umoja unaopaswa uwe wa mume na mke peke yao.
Namna gani juu ya lile neno jingine linalotumiwa? “Uasherati” unakazia fikira, si kwenye matokeo ambayo ufisadi waweza kuwa nayo juu ya uhusiano wa ndoa, bali kwenye namna au sifa ya tendo la ngono lenyewe. Ndivyo ilivyo, si kwa habari ya neno la Kiswahili “uasherati” tu, bali na kwa neno la Kigiriki por·neiʹa vile vile, linalotumiwa katika habari ya Mathayo. Bila shaka tunapendezwa zaidi na neno la Kigiriki linalotumiwa na mwandikaji wa Injili. Kwa maana, hata neno “uasherati” liwe linaelewekaje na wazungumzao Kiswahili, kilicho cha maana na kinachokata shauri ni namna ambavyo mwandikaji na watu wakati huo walivyolielewa neno linalotumiwa katika Biblia.
“Uasherati” unapotajwa leo, kwa kawaida watu wanafikiria ngono kati ya mwanamume na mwanamke, ngono inayoendeshwa nje ya ndoa lakini ikiwa kwa njia ya ‘kawaida’ au ya asili. Kwa hiyo, wengi wameelewa kwamba, Yesu aliposema kwamba “uasherati [por·neiʹa]” ndiyo sababu ya pekee ya talaka, alimaanisha ngono inayofanywa kwa njia ya kawaida au ya asili kati ya mke na mwanamume asiye mumewe peke yake, au, zaidi ya hapo, kati ya mume na mwanamke asiye mkewe. Lakini je! ndivyo? Je! por·neiʹa, neno linalotumiwa katika habari ya Mathayo, linamaanisha ngono hizo za asili peke yake? Au lilitia ndani na namna zote za ufisadi, kutia na zile zilizo kati ya mwanamume na mwanamume na mwanamke na mwanamke na vile vile namna za ngono zilizogeuzwa vibaya kati ya mwanamume na mwanamke? Por·neiʹa lilimaanisha nini kabisa kwa watu katika karne ya kwanza Yesu alipokuwa duniani? Na je! uchunguzi wa unyofu na uangalifu wa maana hii unahitaji uamuzi mpya juu ya ufahamu wetu wa sababu inayolingana na Maandiko ya talaka?
Uchunguzi wa kutosha wa jambo hili unaonyesha kwamba por·neiʹa linamaanisha namna zote za ufisadi. Ni neno lenye maana nyingi, Kamusi za lugha ya Kigiriki zinaonyesha hili waziwazi.
Zinaonyesha kwamba por·neiʹa linatoka kwa neno la asili linalomaanisha “kuuza,” na linasimulia ngono zilizo za uzinifu na zisizozuiwa (kama vile kuzuiwa na kushikilia kwa vifungo vya ndoa). Hivyo, Thayer’s Greek-English Lexicon of the New Testament, ikizungumza juu ya matumizi ya neno hilo katika nyakati za Biblia inasema kwamba por·neiʹa lilieleza “ngono zisizoruhusiwa kwa jumla.” The Vocabulary of the Greek New Testament cha Moulton na Milligan kinasema ni “ngono isiyo halali kwa jumla.” Kitabu cha sita cha Theological Dictionary of the New Testament kinasema kwamba por·neiʹa laweza kumaanisha “‘ngono’ kwa jumla bila ya kutaja maana ya wazi zaidi.”
Ni kwa sababu ya kuwa kwake neno lenye maana nyingi (nyingi zaidi kuliko ambavyo neno “uasherati” linavyoeleweka na watu wengi wazungumzao Kiswahili) kwamba watafsiri wengi wa Biblia wanatumia maneno kama “ufisadi mbaya sana,” “ufisadi,” “dhambi zinazowapasa mwanamume na mwanamke,” au yanayofanana nayo, wanapotafsiri por·neiʹa.
Je! hii maana yake ni kwamba ngono zisimo za asili na zilizogeuzwa vibaya kama zile zinazoingiliwa na wanaume wawalalao wenzao na wanawake vile vile zimo katika maana ya neno hili lililotumiwa na mtume alipoyaandika maneno ya Yesu? Ndiyo, ndivyo ilivyo. Hii yaweza kuonekana kwa njia ambayo ndugu ya mama-mzazi mmoja na Yesu Yuda alivyotumia por·neiʹa alipokuwa akitaja matendo yasiyo ya asili ya watu wa Sodoma na Gomora. (Yuda 7) Kwa habari ya matumizi ya por·neiʹa ya Wayahudi wenye kuzungumza Kigiriki karibu na mwanzo wa Wakati wa Kawaida, kitabu cha sita cha Theological Dictionary of the New Testament kinasema: “πορνεία [por·neiʹa] vile vile laweza kuwa ‘ukali usio wa kawaida,’ . . . kulawiti.”
Basi, nini maana ya matumizi ya Biblia ya maneno haya nayo inafunua nini juu ya sababu za halali za Biblia za talaka? Inaonyesha kwamba mtu ye yote aliyeoa au kuolewa anayetoka katika kufungo cha ndoa na kujitia katika ufisadi, na mwanamume au na mwanamke au na mwanamke mwenzake au mwanamume mwenzake, uwe ni wa asili au usio wa asili na uliogeuzwa vibaya, yuna hatia ya kufanya por·neiʹa au “uasherati” katika maana ya Biblia. Ngono hizo hazimaanishi makosa madogo ambayo huenda mtu afanye, kama vile busu au kugusa kwa upendano au kumbatio, bali zinamaanisha matumizi ya ufisadi ya viungo vya uzazi katika namna fulani ya ngono, iwe ni ya asili au isiyo ya asili.
Twapata kanuni katika agano la Torati zikiyategemeza maoni haya yaliyoendelezwa. Ni wazi kwamba chini ya Torati hiyo ndoa zilivunjwa wakati mwenzi alipofanya dhambi nzito zinazokamatana na mambo ya ngono, kutia na zisizo za asili, kwa maana mwenzi huyo aliuawa kulingana na maagizo ya Mungu mwenyewe.—Linganisha Kutoka 22:19; Mambo ya Walawi 18:22, 23, 29; 20:10-16; Kumbukumbu la Torati 22:22; na vile vile maneno ya mtume wa Kikristo katika Warumi 1:24-27, 32.
Tukiyachukua maneno ya Yesu yalivyo, basi, mwenzi anapokuwa mwenye hatia ya ufisadi mzito kama huo mwenzi aliye mwaminifu aweza kumtaliki huyo kulingana na Maandiko, ikiwa yeye anataka kufanya hivyo. Yeye anayepewa talaka kwa sababu hizo za Maandiko hata yeye yu huru kuoa tena au kuolewa, bila ya kuwa na shtaka la uzinzi.
Hiyo inaonyesha waziwazi sahihisho katika maoni yaliyosemwa nyakati zilizopita katika safu za gazeti hili, lakini kushikamana kwa uaminifu na yasemavyo Maandiko kwa kweli kunahitaji hili lifanywe. Kunayo mengi zaidi yawezayo kuangaliwa juu ya jambo hili na kwa hiyo yatazungumzwa zaidi katika toleo fulani lijalo la gazeti hili.