Wapangaji Watamanikao
✔ Novemba 24, 1971, mwanamke mmoja alipiga simu kwa afisi ya tawi ya Watch Tower Society katika Wiesbaden, Ujeremani, akisema kwamba alikuwa amenunua nyumba yenye vyumba vingi katika Berlin na alitaka kuipangisha kwa mashahidi wa Yehova. Alipoulizwa sababu gani alitaka mashahidi wa Yehova wawe wapangaji, alijibu kwamba rafiki yake katika Ujeremani wa kusini alikuwa akipangisha kwao na alikuwa amependekeza naye afanye vivyo hivyo. Vile vile alieleza namna ilivyokuwa vigumu kwake kupata wapangaji wenye kutegemewa. Kwa vile alivyokuwa amekwisha kuvutwa na mwenendo wa mashahidi wa Yehova, alisema hivi: “Mimi najua kwamba watu hawa ni wenye kumwogopa Mungu, wako tayari kusaidia, na ni wenye bidii, nami ningefurahi sana ikiwa mngenisaidia nitimize mpango wangu.”