Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w74 2/1 kur. 57-63
  • Kuushukuru Wokovu wa Mungu Wetu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kuushukuru Wokovu wa Mungu Wetu
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • “DHAMBI” NA “UKOMBOZI”
  • JAMAA MBILI
  • KUONYESHA SHUKRANI YETU
  • SHUKRANI YENYE UHAKIKA
  • Kifo cha Yesu Chamaanisha Nini Kwako?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Fidia—Zawadi Bora Zaidi Kutoka kwa Mungu
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
  • Endelea Kuthamini Fidia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2021
  • Fidia ya Kristo Njia ya Mungu ya Wokovu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
w74 2/1 kur. 57-63

Kuushukuru Wokovu wa Mungu Wetu

1, 2. Ni kosa gani kubwa linalofanywa na wengi wa wanadamu, na kwa matokeo gani?

JE! SISI tunamwia Mungu jambo fulani? Watu wengi wanatenda kana kwamba tunamwia. Wanauona uhai kama jambo la kutumiwa kwa ajili ya faida tu na anasa ya kichoyo. Lakini wao hawapati uradhi wa kweli kutokana na maisha. Hii ni kwa sababu wanaivunja amri ya kwanza na ya pili kama zilivyosemwa na Yesu Kristo: “Ya kwanza ni, ‘Sikia, Ee Israeli, Yehova Mungu wetu ni Yehova mmoja, nawe inakupasa kumpenda Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote na kwa akili zako zote na kwa nguvu zako zote.’ Ya pili ndiyo hii, Inakupasa kumpenda jirani yako kama ujipendavyo mwenyewe.’”​—Marko 12:29-31, NW.

2 Ni wachache sana wa wanadamu wanaopendezwa na kuzitii amri hizi leo. Wao ni kama tajiri katika mmojawapo wa mifano ya Yesu aliyesema: “Ee nafsi yangu, una vitu vyema vingi ulivyojiwekea akiba kwa miaka mingi; pumzika basi, ule, unywe, ufurahi.” Lakini mtu huyo aliipoteza nafsi yake usiku ule ule. (Luka 12:16-21) Ndivyo ilivyo na leo. Wale wanaokosa kuwa tajiri kuelekea Mungu, lakini ambao, mahali pake, wanajifanyia paradiso yao wenyewe ya kufuatia mambo ya kimwili katika hii taratibu ya mambo, karibuni watapoteza vyote wakati wa “dhiki kubwa” ambayo i karibu kuipiga dunia kwa ghafula. Mapendezi yao ni ya kimwili, yanayoonekana​—siyo ya kiroho.​—Mt. 24:21, 22; Yer. 25:31-36; Yak. 5:1-5.

3. Tofautisha maoni ya wakati ujao ya “mtu wa kimwili” na yale ya “mtu wa kiroho.”

3 Namna alivyo mjinga huyu “mtu wa kimwili”! Mambo ya roho ya Mungu ni upumbavu kwake, hivyo kwamba hawezi kuona mbele kupita muda wa maisha wa miaka 70 au 80. Lakini “mtu wa kiroho” anaweza kuona hata umilele. Hata ‘watu wa kiroho’ ambao wana mali za kimwili wanashauriwa “watende mema, wawe matajiri kwa kutenda mema, wawe tayari kutoa mali zao, washirikiane na wengine kwa moyo; huku wakijiwekea akiba iwe msingi mzuri kwa wakati ujao, ili wapate uzima ulio kweli kweli.” ‘Matendo mema’ yanahitajiwa kwetu sote tunaoutafuta “uzima ulio kweli kweli.” Katika kioo cha sheria kamilifu ya Mungu twaweza kuona ni kwa kadiri gani tunavyoyafikia matakwa ya uzima wa milele. “Aliyeitazama sheria kamilifu iliyo ya uhuru, na kukaa humo, asiwe msikiaji msahaulifu, bali mtendaji wa kazi, huyo atakuwa heri katika kutenda kwake.”​—1 Kor. 2:14, 15, NW; 1 Tim. 6:18, 19; Yak. 1:25.

4. Nini kilicho cha lazima, ikiwa tutaichunguza hekima ya Mungu?

4 Akizungumza juu ya wokovu uwajiao Wayahudi kwanza, kisha mataifa, Paulo anatangaza: “Jinsi zilivyo kuu utajiri na hekima na maarifa ya Mungu! hukumu zake hazichunguziki, wala njia zake hazitafutikani!” (Rum. 11:33) Je! hii maana yake ni kwamba hekima ya Mungu ni kuu mno tusiweze kuzifahamu njia zake wakati wo wote? Tofauti yake kabisa! Lakini lazima tulijie Neno la Mungu tukiwa na nia inayofaa ya akili na moyo. Tusiitazamie Biblia iseme kama kitabu cha hadithi cha kilimwengu, ambacho kusudi lake ni kufurahisha tu. Biblia inahitaji funzo, pamoja na kusudi lifaalo. Katika siku za Yesu walikuwako wengine waliomjia wakiwa na makusudi mabaya, wakitafuta faida fulani ya kichoyo au njia ya kumtegea. (Yohana 6:26, 27; Luka 20:20-26) Lakini, Yesu alitoa ufahamu wa mambo ya kiroho makubwa zaidi ya Neno la Mungu kwa wale waliomtafuta kwa unyenyekevu kwa moyo safi peke yao. (Mt. 13:10-15; Luka 13:23, 24) Ni jambo la muhimu kwamba sisi, vile vile, tupate ufahamu wa moyoni wa mafundisho ya Biblia, ambayo ni tofauti sana na filosofia za kilimwengu.

“DHAMBI” NA “UKOMBOZI”

5. (a) Nini maoni ya Maandiko juu ya “dhambi”? (b) Kuwekwa huru na dhambi ni fadhili zisizostahili namna gani?

5 Kwa mfano, lichukue shauri la “dhambi.” Huenda tukaishi katika jamii yenye kuruhusu au ya namna nyingine isiyofahamu maana ya “dhambi.” Lakini “dhambi” imekuwapo sikuzote tangu uasi katika Edeni. Ni kuikosa shabaha ya ukamilifu, au kupungukiwa na haki ya Mungu. (Rum. 3:23, 24) Tulirithi dhambi kwa babu yetu wa kale asiyetii Adamu, na kwa hiyo sote tu wenye dhambi. Katika nyakati za kale, ilihitaji sheria ya Mungu iliyotolewa kupitia kwa Musa kujulisha waziwazi dhambi ni nini, hata ingawa mauti iletwayo na dhambi ilikuwa imekuwa ikitawala kama mfalme juu ya wanadamu kwa maelfu ya miaka. Sheria hiyo vile vile ilionyesha waziwazi kwamba mwanadamu hawezi kupata uhuru wa dhambi mwenyewe. Leo, vile vile, imetupasa tujihadhari sana na dhambi na matokeo yake. (Rum. 5:12-14; 7:7, 21-25) Namna sisi wenyewe tusivyostahili kuwekwa huru na dhambi na matokeo yake! Lo! ni fadhili zisizostahili kama nini, basi, zinazoonyeshwa na Mungu katika kutoa uhuru wa dhambi, juu ya msingi wa dhabihu kamilifu ya Mwanawe!​—Efe. 2:4-8.

6. (a) Nini msingi wa uhuru wa dhambi? (b) Ni akina nani ambao hawataona ni vigumu kuufahamu ukombozi?

6 Hii inaelekeza kwenye fundisho la Biblia la “ukombozi.” Uhuru wa dhambi unakuja juu ya msingi wa dhabihu ya ukombozi ya Yesu. Je! shauri hili la “ukombozi” ni gumu sana kwamba hatuwezi kulifahamu, hata kuweza kulieleza wazi kwa wengine? Lisisemwe hilo kamwe! Kwa kweli, fundisho la Biblia la ukombozi, linapofahamika sawasawa, linashangaza kwa uzuri, ni lenye kutia imani! Kama tungeyakubali mafundisho ya viongozi wa kidini wa Kristendomu, wanaomsimulia Yesu kama “Mungu mwenye mwili” na kwa hiyo kama namna ya nusu-Mungu, nusu-mwanadamu, au kama tungevutwa fikira katika filosofia ya Mashariki kwamba wapaswa mradi wa mtu uwe usahaulifu wa raha nyuma ya kufa, huenda tukaona ukombozi ni mgumu kufahamika. Lakini ikiwa tunafuatia “haki, na imani, na upendo, na amani, pamoja na wale wamwitao Bwana kwa moyo safi,” basi haitakuwa vigumu mno kuufahamu na kuufurahia mpango wa ajabu wa Yehova wa ukombozi.​—2 Tim. 2:22.

7. “Ukombozi” unaweza kuelezwaje?

7 Kama mwanadamu mkamilifu​—⁠si zaidi ya hapo, si chini ya hapo​—na mfano ule ule wa Adamu aliyekuwa mkamilifu wakati mmoja, Yesu angeweza ‘kujitoa mwenyewe kama ukombozi unaolingana kwa ajili ya wote,’ yaani, kwa ajili ya wazao wote wasiokamilika wa Adamu mwenye dhambi. (1 Tim. 2:5, 6, NW) Neno la Kigiriki antiʹly·tron, linalotumiwa mahali hapa pamoja tu katika Maandiko, linafafanuliwa hivi: “ukombozi, bei ya ukombozi, au mahali pake ukombozi unaolingana. ‘Kwa kufaa linamaanisha bei ambayo kwayo wafungwa wanakombolewa kutoka kwa adui; na ile namna ya badilisho ambamo uhai wa mtu unakombowa kwa uhai wa mwingine.’ Kwa hiyo Aristotle anatumia kiarifa antilytróo kwa kukomboa uhai kwa uhai.”a Ndiyo, hata Aristotle mwenye kiburi alilifahamu shauri la “ukombozi.” Lakini kama angaliishi karne nne nyumaye, filosofia zake​—zikikubali miungu ya utatu, mageuzi na kutokufa kwa nafsi​—bila shaka zingalimzuia asione ubora wa ukombozi wa Yesu.b

8. Ni kwa njia gani, na katika taratibu gani, wote ‘watahuishwa’?

8 Nafsi ya mwanadamu mwenye dhambi siyo isiyokufa! Haina haki ya uzima. Fundisho la Biblia li wazi: “Nafsi itendayo dhambi​—hiyo yenyewe itakufa.” (Eze. 18:4, 20, NW; Mt. 10:28) Ndiyo, nafsi ya mwanadamu mwenye dhambi inakufa, lakini Biblia inatoa tumaini la ajabu: “Kwa kuwa kama katika Adamu wote wanakufa, kadhalika na katika Kristo wote watahuishwa. Lakini kila mmoja mahali pake; limbuko ni Kristo; baadaye walio wake Kristo, atakapokuja.” Kama vile Kristo alivyoinuka kutoka kwa wafu, ndivyo sasa, wakati wa kuwapo kwake kusikoonekana, kundi dogo la wafuasi wake waliotiwa mafuta ‘wanavyohuishwa’ pamoja naye. (1 Kor. 15:20-23) Vile vile, katika taratibu ya haki, wengine wa wanadamu wanaotumia imani wanaweza kutazamia kutolewa “katika utumwa wa uharibifu, hata viingie katika uhuru wa utukufu wa watoto wa Mungu.”​—Rum. 8:21.

JAMAA MBILI

9. Ni kwa njia gani wafuasi wa Yesu wanavyotofautiana na jamaa ya Adamu?

9 Fundisho hili la ukombozi linaleta kwenye fikira zetu jamaa mbili​—jamaa ya Adamu na jamaa ya Yesu Kristo. Jamaa zote mbili zinasimuliwa kama zenye watu “wengi.” (Rum. 5:15) Hakuna takwa lo lote la pekee la kuwa mmojawapo wa jamaa yenye dhambi ya Adamu. Wote wanazaliwa ndani yake kwa njia ya utaratibu wa asili wa uzazi. Lakini, juu ya alivyofanya Yesu, imeandikwa: “Kwa maana Mwana wa Adamu naye hakuja kutumikiwa, bali kutumika, na kutoa nafsi yake iwe fidia ya wengi.” (Marko 10:45; Mt. 20:28) “Wengi” kadiri gani? Kama tulivyoona tayari, alijitoa mwenyewe kuwa “ukombozi unaolingana kwa ajili ya wote.” Yeye alionja mauti “kwa ajili ya kila mtu.” (1 Tim. 2:5, 6, NW; Ebr. 2:9) Mnamo miaka 6,000 iliyopita, jamaa ya Adamu imeongezeka kuwa mabilioni. Kristo aliwanunua wote. Lakini ili kufurahia hali yenye kibali kwa Mungu iliwapasa kutumia imani katika Yesu Kristo kama yeye ambaye kupitia kwake Mungu amewatolea uzima wa milele. (Yohana 3:16, 36) Imeandikwa hivi juu ya wafuasi wa Yesu: “Wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake [Yesu]; waliozaliwa, si kwa damu, wala si kwa mapenzi ya mwili, wala si kwa mapenzi ya mtu, bali kwa Mungu.”​—Yohana 1:12, 13.

10. Kwa sababu gani Yesu hakukuza jamaa ya asili?

10 Ndivyo ilivyo na kwa wale ambao, kupitia kwa ubora wenye kulipia dhambi wa dhabihu ya Yesu, wanapata uzima wa milele katika jamaa ya Yesu duniani. Vile vile, wao lazima watumie imani katika damu ya Yesu, ambayo ndio msingi wa ukombozi wao kutoka dhambi na mauti. (Ebr. 9:12, 28; Rum. 5:8-11) Kama mwanadamu mkamilifu, Yesu angaliweza kuoa na kukuza jamaa yake mwenyewe, na lo! jamaa hiyo ingekuwa yenye akili nyingi, yenye kutokeza namna gani! Lakini je! hicho ndicho alichokitaka Yesu? Hilo ndilo lililokuwa kusudi la Yehova katika kumtuma Yesu duniani? Yesu alishughulikia kuyafanya mapenzi ya Baba yake, yaliyotia ndani maulizo yenye maana zaidi kuliko kuanzisha jamaa mpya yake mwenyewe. (Yohana 5:30; 6:37-40) Zaidi ya hayo, Yesu alipendezwa katika kuona jina takatifu la Yehova na kusudi vikishuhudiwa kwa habari ya jamaa ya kwanza ya kibinadamu. Kwa maana Mungu alikuwa amepumzika katika kazi zake za kuumba akiwa na matumaini kwamba kusudi lake kubwa la kuijaza dunia ya paradiso na wazao wenye haki wa Adamu lingetimizwa mwishoni mwa ‘siku yake ya kupumzika’ yenye urefu wa miaka 7,000.​—Mwa. 2:1-3; 1:27, 28.

11. (a) Yesu anakuwaje “Baba wa milele”? (b) Ni akina nani anaowalea Mungu kwanza kama wana wa kiroho?

11 Mwanadamu kama kuumba kwa Mungu alikuwa amekuwa mkamilifu, na kulikuwako njia ambayo kwayo ukamilifu ungeweza kurudishwa. Kwa hiyo sababu gani jamaa mpya ya kibinadamu ianzishwe? Mahali pake, kilichohitajiwa kilikuwa dhabihu ya Yesu mkamilifu, ili kwamba wenye kumpenda Mungu, walio watiifu kati ya wazao wa Adamu waweze kuhamishwa, walelewe kana kwamba ilikuwa, kuingia katika jamaa ya Yesu, yeye akiwa kama “Baba wa milele” wake kwa uwezo wa ukombozi. (Isa. 9:6) Lakini kwanza katika kusudi la Mungu, “malimbuko,” hesabu ndogo kutoka jamaa ya Adamu ingelelewa kama wana wa kiroho, juu ya msingi wa imani yao katika dhabihu ya Yesu, washiriki na Yesu kwa njia ya ufufuo wa kiroho katika ufalme wake wa kimbinguni juu ya jamaa ya kibinadamu.​—Rum. 8:23; Yak. 1:18.

12. (a) Ukombozi unawawezeshea wanadamu nini? (b) Imetupasa tuuitikieje mpango wa ukombozi?

12 Ukombozi unafungua njia kwa baraka zisizo na kifani kwa wanadamu wote​—paradiso iliyorudishwa duniani pote, wokovu wa wapenda haki wengi kuingia katika paradiso hiyo, ufufuo wa mabilioni ya wafu wa kibinadamu na kuondolewa kwa ugonjwa, dhambi na mauti. Unawezesha amani, uradhi na kupatana kwa kuumba kote kwa Yehova. (Zab. 37:10, 11; 72:7, 8; Yohana 5:28, 29; Isa. 33:24) Lo! namna fikira juu ya mambo haya matukufu yatakayokuja zinavyotufanya tufurahi tukiwa na shukrani kwa ajili ya upendo wa ajabu na fadhili zisizostahili za Yehova kama zinavyoonyeshwa kupitia kwa Mwanawe! Kwa kweli hizi ni “fadhili zisizostahili juu ya fadhili zisizostahili”! (Yohana 1:14, 16, 17, NW) Si ajabu kwamba wanafunzi wa Yesu waliandika kwa shukrani sana juu ya ukombozi! (Rum. 3:21-26; 1 Pet. 1:18, 19; 1 Yohana 1:7; Yuda 20, 21) Je! moyo wako mwenyewe haububujiki kwa shukrani kwa ajili ya upendo mkuu wa Mungu kwa kutoa ukombozi na yote yatokanao nao?​—Rum. 8:38, 39; Isa. 65:17, 18.

KUONYESHA SHUKRANI YETU

13, 14. (a) Shukrani ya ukombozi imepaswa itufanye tuongezeke katika nini? (b) Nini ambacho kimepaswa kituzuie tusizoee dhambi wakati wo wote?

13 Kwa waamini wenzake mtume Paulo aliandika: “Na hii ndiyo dua yangu, kwamba pendo lenu lizidi kuwa jingi sana, katika hekima na ufahamu wote; mpate kuyakubali yaliyo mema; ili mpate kuwa na mioyo safi, bila kosa, mpaka siku ya Kristo; hali mmejazwa matunda ya haki, kwa njia ya Yesu Kristo, kwa utukufu na sifa ya Mungu.” (Flp. 1:9-11) Ikiwa shukrani ya ukombozi inatuvuta sisi kuongezeka zaidi na zaidi katika upendo, imepaswa vile vile itufanye tuongezeke katika kuchukia yaliyo mabaya.

14 Mungu anatoa msamaha wa dhambi juu ya msingi wa dhabihu ya Yesu, lakini hii haitupi sisi ruhusa ya kufanya dhambi. Ni kweli, kama inavyosemwa katika 1 Yohana 2:1, kwamba, kwa sababu ya kutokamilika kulikorithiwa, “mtu akitenda dhambi tunaye Mwombozi kwa Baba, Yesu Kristo mwenye haki.” Ah, lakini twapokea msaada huo ikiwa tunatenda dhambi kwa kupenda? Je! twaweza kuutazamia ubora wenye kulipia dhambi wa dhabihu ya Yesu utumike kwetu kama tukijifanya wagumu katika njia za dhambi? Yohana wa Kwanza 3:2, 6, 8 anatuambia: “Wapenzi, sasa tu wana wa Mungu . . . Kila akaaye ndani yake hatendi dhambi; kila atendaye dhambi hakumwona yeye, wala hakumtambua. Atendaye dhambi ni wa Ibilisi; kwa kuwa Ibilisi hutenda dhambi tangu mwanzo. Kwa kusudi hili Mwana wa Mungu alidhihirishwa, ili azivunje kazi za Ibilisi.” Yeye anafanya hili kupitia kwa mpango wake wenye upendo wa ukombozi. Kwa hakika hakuna aushukuruye mpango huo wa ajabu kwa njia ya Kristo ambaye angetaka wakati wo wote kuingia katika mazoea ya dhambi!

15. Kwa sababu gani si hekima kujitia katika dhambi tukiwa na maoni ya kwamba dhabihu ya Yesu italeta msamaha?

15 Huenda mtu akafikiri kwamba kupata anasa iliyo karibu na mpaka bila ya kuingia kabisa katika dhambi, si kubaya sana. Au huenda mwingine akafikiri, ‘Mara moja tu na si zaidi ya hapo, nayo dhabihu ya Yesu itaniletea msamaha.’ Lakini je! huko ni kufikiri kwenye busara? Ni mwanzo wa kusitawisha mwonjo wa kazi za mwili, tofauti ya kusitawisha tunda la roho, na Biblia inaonya waziwazi “ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu.” (Gal. 5:19-24) Ni vyepesi sana kuangukia mazoea mabaya! Upinge ushawishi, kwa moyo safi. (Mt. 5:8) Tunapokutana na jaribu kufanya mabaya, imetupasa tuvutwe kusema: ‘Hapana. Mimi sitashiriki hilo hata kidogo. Nyuma ya yale Mungu na Kristo wametufanyia katika kuutoa ukombozi, nawezaje kufanya jambo kama hilo ambalo lingeonyesha ukosefu huo wa shukrani?’ Katika kufikiri habari za ukombozi, sikuzote na tuseme kutoka moyoni: “Lakini sisi hatumo miongoni mwao wasitao na kupotea, bali tumo miongoni mwa hao walio na imani ya kutuokoa [nafsi] zetu.”​—Ebr. 10:39, na vile vile tazama mstari wa 29.

16. Twawezaje kuepuka ‘kusita’ na kuingia katika dhambi?

16 Mahali pa ‘kusita,’ na kuingia katika dhambi na ukosefu wa imani, ebu na tumkaribie Mungu wetu zaidi kuliko wakati mwingine wo wote. Hii inamaanisha kuwakaribia ndugu zetu zaidi, vile vile. Imetupasa tuwapende ndugu zetu kwa moyo. “Mtu ye yote asiyetenda haki hatokani na Mungu, wala yeye asiyempenda ndugu yake. Maana, hii ndiyo habari mliyoisikia tangu mwanzo, kwamba tupendane sisi kwa sisi.” (1 Yohana 3:10, 11) Twauonyeshaje upendo huu kwa mtu na mwenzake? Kwa kutumia wakati tukiwa mtu na mwenzake​—mbele ya mikutano, nyuma ya mikutano na penye nafasi nyingine. (Zab. 133:1; Rum. 12:9, 10) Ndiyo, kwa kupendezwa katika mtu na mwenzake, kwa kujengana kwa upendo, kwa kufurahia kushiriki mtu na mwenzake baraka nzuri za kiroho zinazotolewa na Yehova kupitia kwa Bwana Yesu Kristo.​—1 The. 5:11-13.

SHUKRANI YENYE UHAKIKA

17. (a) Ni wonyesho gani hakika wa imani yetu uwezao kufanywa? (b) Mara nyingi hii inatia nini ndani yake?

17 Umepaswa ukombozi utuvute kwenye matendo hakika, kazi za imani zinazoonyesha shukrani zetu za moyoni kwa ajili ya yote ambayo Yehova na Kristo wametufanyia. Hivyo twaweza kuhakikisha kuwa kati ya wale wanaotajwa katika Zaburi 11:7: “Kwa kuwa [Yehova] ndiye mwenye haki, apenda matendo ya haki, wanyofu wa moyo watamwona uso wake.” Leo wako mashahidi wa Yehova zaidi ya milioni moja na nusu duniani mwote wanaofanya matendo ya haki kwa ajili ya wengine wenye mioyo minyofu. Huduma yao inatia ndani kutembelea nyumba za wengine, kuwafundisha Biblia bure na kuwaonyesha njia ya uzima wa milele uwezao kupatikana kupitia kwa ujuzi wa kweli peke yake juu ya Mungu, Kristo na mpango wa ukombozi. (Yohana 17:3; 14:6) Huduma hii yote inafanywa kwa kujitolea na bila ya kufikiria kupata thawabu ya kimwili. Vile vile, mara nyingi inatia ndani kushika ukamilifu unapokutana na kupinga kusiko kwema na hata kwa ukatili.​—Mt. 10 28-39.

18. Mtoto wa miaka mitano alionyeshaje ubora wa mpango wa Yehova?

18 Kwa mfano, mchukue mtoto huyu wa kike mwenye umri wa miaka mitano: Mama yake alimfundisha kwa uaminifu, hivi kwamba akakuza upendo mwingi kwa Yehova na Mwanawe. Lakini baba yake asiyeamini akampeleka kwenye chuo cha watoto wadogo cha watu wa Buddha. Hapa imani zake za Kikristo zilijaribiwa vikali. Alikataa kumsujudia Buddha alipokuwa anaingia mlangoni pa shule. Katika darasa, akakataa kuiinamia sanamu ya Buddha. Mwalimu wake alimkemea mara kwa mara. Lakini ilikuwako ibada ya namna ifaayo ambayo angeweza kuifanya, hata katika chuo hicho cha watoto. Mbele ya chakula chake cha mchana, aliinama kichwa chake kidogo kila siku katika sala kwa Yehova kupitia kwa Kristo. Mwalimu alikasirishwa na hili vile vile, naye akajaribu kumkomesha, lakini ilikuwa kazi bure! Mwishowe, mwalimu aliposhindwa kumfanya ashiriki katika sikukuu ya watu wa Buddha, alimwuliza mtoto huyu wa kike, “Ni kwa sababu mama yako alikuambia usifanye hivi?” Mtoto akajibu, “Hapana, ni kwa sababu isingempendeza Yehova Mungu.” Lo! wonyesho mzuri kweli kweli wa imani yenye msingi wa ukombozi!

19. (a) Yehova anawabarikije wale wanaomtafuta yeye kwa moyo safi? (b) Mzee mmoja alionyeshaje shukrani ya baraka hiyo?

19 Mpango wa Yehova wa ukombozi unawezesha uzima wa milele kwa watu wa namna zote. Kwa kutumia malaika zake yeye anawakusanya wale wanaoonyesha tamaa yenye bidii ya kujifunza na kuyafanya mapenzi yake. (Ufu. 14:6, 7) Barua ifuatayo ilipokewa na afisi ya tawi ya Watch Tower Society: “Mimi ni mwenye umri wa miaka 68 na kipofu kabisa. Nimeishi hospitalini miaka mingi, bila ya mtu wa kutegemea. Mwishowe, katika Novemba mwaka wa 1970, nikaacha kutaka kuishi nami nikajitoa nife. Kisha, asubuhi moja, nikasimama karibu na madhabahu takatifu ya Shinto ukumbini, nikasema sala hii: ‘Niruhusiwe mara moja tu, mbele ya kufa, nikutane na Mungu wa kweli, asiye namna ya mungu aliyemo katika madhabahu hii.’ Hata nilipokuwa nikisali bado nilishtuka kusikia sauti mlangoni. Kumbe, mtu mwenyewe alisema, ‘Mimi natangaza habari njema kama shahidi wa Mungu wa kweli, Yehova.’ Nikamwomba yule mtu aingie mara moja, nami nikayasikiliza yote yaliyosemwa kwa shauku. Tangu siku hiyo, sijaweza kukosa mkutano wa Mashahidi wa mahali pangu. Katika Mei wa mwaka wa 1971, mimi mwenyewe nilipata kuwa mhubiri wa nyumba kwa nyumba, na katika tarehe ya Desemba 4 ya mwaka ule ule, nikauonyesha wakf wangu kwa ubatizo wa maji kwenye kusanyiko la mzunguko la mashahidi wa Yehova. Tangu tarehe ya 25 ya mwezi ule ule nikaingia katika huduma ya upainia wa muda. Katika miaka yote 68 iliyopita ya maisha yangu, pamoja na miaka 28 ambayo nilitumia macho yangu, hazijapata siku zangu kujazwa na tumaini kama hilo wala furaha wakati wo wote mwingine.” Kwa kuonyesha furaha yake wazi, dada huyu mpendwa wa Kikristo alitia ndani ya barua yake mchango wa ukarimu kwa ajili ya mpango wa ujenzi wa mpanuko wa kitheokrasi katika nchi yake.

20. Yehova ‘anakuja na kuwaokoa’ watu wake namna gani?

20 Kwa kweli Yehova ameitimiza ahadi yake ya ‘kuja na kuwaokoa’ watu wake. Amewaokoa kutoka Babeli Mkuu wa kidini naye amewaleta kwenye ujamaa wa kirafiki naye, ndiyo, kuingia katika paradiso ya kiroho. Kuwamo kwa mtu katika paradiso hii ya kiroho kunamaanisha baraka zisizohesabika kwa waamini waliokombolewa. “Ndipo macho ya vipofu [kwa kiroho] yatafumbuliwa, na masikio ya viziwi [kwa kiroho] yatazibuliwa. Ndipo mtu aliye kilema [kwa kiroho] ataruka-ruka kama kulungu, na ulimi wake aliye bubu [kwa kiroho] utaimba.” Hata katika siku yetu wenyewe unabii unatimizwa: “Na hapo patakuwa na njia kuu, na njia [kutoka nje ya Babeli Mkuu], nayo itaitwa, Njia ya utakatifu; wasio safi hawatapita juu yake; bali itakuwa kwa ajili ya watu hao; wasafirio, wajapokuwa wajinga, [hawatatanga-tanga] katika njia hiyo.” Kuingia katika njia hii hakuna malipo kwa wote wanaotumia hekima ya kweli kwa kujifunza juu ya matakwa ya Yehova kwa unyenyekevu na kuukubali mpango wake wa uzima kupitia kwa Kristo. “Na hao waliokombolewa na [Yehova kutoka utumwani mwa Babeli Mkuu] watarudi, watafika Sayuni [ufalme wa Mungu wa Kimasihi] wakiimba; na furaha ya milele itakuwa juu ya vichwa vyao; nao watapata kicheko na furaha, huzuni na kuugua zitakimbia.”​—Isa. 35:4-6, 8, 10.

21. Tunalo tumaini gani, nalo limepaswa liwe na matokeo gani juu yetu?

21 Karibuni miujiza hiyo ya kiroho itakuwa namna ile ile! Wakati gani? Chini ya ufalme ujao wa Mungu wa miaka 1,000 kupitia kwa Mwanawe Yesu Kristo. Hata alipokuwa duniani miaka mia kumi na tisa iliyopita, Yesu Kristo alifanya miujiza hakika ya namna hizo. Kama Mfalme atafanya mambo hayo tena, katika paradiso hakika ya kidunia iliyorudishwa. (Luka 23:43) Lo! tumaini lenye furaha hilo! Nao unabii unaotimizwa sasa waonyesha kwamba twasimama pale pale penye mwanzo wa wakati huu wa shangwe. Bila shaka sasa ndio wakati wa nyakati zote wa kujitahidi wenyewe kwa uhodari, ili tuweze kutembea katika urafiki kweli kweli na Mungu wa wokovu​—⁠moja kwa moja kupita “dhiki kubwa” na kuingia katika baraka za milele zilizoko ng’ambo ya pili.​—Luka 13:24.

​—Kutoka The Watchtower, Aug. 1, 1973.

[Maelezo ya Chini]

a A Greek and English Lexicon of the New Testament ya Parkhurst, uk. 47.

b “Katika Karne ya Nne B.C. Aristotle aliandika: ‘Vitu vyote ni vitatu, navyo vitatu ni vyote: na ebu tutumie hesabu hii katika ibada ya miungu; kwa maana, kama wasemavyo Wapaithagoreo, kila kitu na vitu vyote vinafungwa katika mafungu ya vitu vitatu, kwa maana mwisho, katikati, na mwanzo vina hesabu hii katika kila kitu, navyo hivi vinafanyiza hesabu ya Utatu.’”​—⁠Arthur Weigall, katika kitabu chake The Paganism in Our Christianity, uk. 198.

[Picha katika ukurasa wa 58]

Mungu ametoa uhuru wa dhambi juu ya msingi wa dhabihu ya Kristo

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki