Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w74 5/1 kur. 214-215
  • Mahali Ambapo Hapana Migawanyiko ya Kitaifa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mahali Ambapo Hapana Migawanyiko ya Kitaifa
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Habari Zinazolingana
  • Sababu kwa Nini Watu wa Namna Zote Wanakuwa Mashahidi wa Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Jamii Zote Ziishipo Pamoja kwa Amani
    Amkeni!—1993
  • “Umtazame Mtu Mnyofu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • Je! Ilifaa Nijitahidi Kushinda Watu Wote?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
w74 5/1 kur. 214-215

Mahali Ambapo Hapana Migawanyiko ya Kitaifa

LEO maoni ya kikabila na kitaifa yanakuwa yenye nguvu sana mara nyingi. Mara nyingi maoni haya yameshiriki kuleta udhalimu, uadui na hata matendo ya jeuri. Watu wengi wanyofu wangependa kuona mwisho wa mambo hayo. Wana hamu ya kupata watu walio na upendo wa kweli kwa wanadamu wenzao. Lakini je! kuna watu leo wanaoonyesha wazi upendo wa kweli kwa wanadamu wenzao bila ya kujali kabila, taifa au hali katika maisha? Wewe, kama wengine, waweza kupata jibu la ulizo hili kwa kwenda kwenye Jumba la Ufalme la Mashahidi wa Yehova.

✔ Mwanamke mmoja wa nchi ya Virginia alizizuia jitihada za ndugu yake juu ya kweli za Biblia alizokuwa akijifunza kutoka kwa mashahidi wa Yehova. Nyumaye, mwanamke huyu na mumewe wakahamia kwenye mtaa mpya, nao wakatembelewa na Mashahidi huko. Anasimulia: “Kwa kawaida niliyachukua magazeti yao, lakini sikuzote niliyatupa. Kwa hiyo nilishangaa sana kujua kwamba mume wangu alikuwa amechukua vitabu fulani naye kwa kweli alikuwa akivisoma. Niliona kwamba anarukwa na akili nami nikamchokoza sana juu ya jambo hili. Mwishowe tukaketi chini tuyazungumze tuliyokuwa tumeyasoma. Alipozungumza juu ya mambo hakika yanayomtaja Muumba mwenye akili nyingi, mimi nisingeweza kubisha hili. Niliahidi kuhudhuria mkutano pamoja naye, na penye mkutano huo maoni yangu yaligeuka. Watu waliokuwamo katika kundi hili zima walikuwa wenye urafiki wa kweli kwangu nao walipendezwa nami na jamaa yangu.”

Hii ilikuwa tofauti sana na yaliyokuwa yamempata wakati uliopita. Kama alivyoeleza: “Tulikuwa tumekuwa na mwanamke msuriama (asiye mweupe wala mweusi) katika kanisa letu nilipokuwa mchanga. Lakini sikuzote aliketi peke yake.”

Wakati mmojawapo wa Mashahidi alipojitolea kujifunza naye na mumewe, walikubali. “Ijapokuwa wakati huo sikuamini kwamba tulikuwa tumeipata kweli,” anasema, “ilipendeza sana kuwa tu pamoja na watu hao wenye upendo.”

✔ Kijana mmoja wa Kiyahudi kutoka nchi ya Massachusetts anasimulia:

“Maono yangu yalianza nilipokuwa nikihudhuria chuo kikuu. Mwanafunzi mwenzangu, msichana (aliyekuwa akijifunza Biblia na mashahidi wa Yehova) alianza kuniuliza maulizo nisiyoyafikiria hapo kwanza, kama, ‘Ikiwa Mungu aliiumba sayari hii, sababu gani hafanyi jambo fulani aipe hali yake nafuu?’

“Kwa kuwa nilikuwa Myahudi wa Kiorthodokis na kwa kuwa nilikuwa nimekwisha kuona unafiki katika dini nyingi sana, sikupendezwa na kujitia katika tengenezo lo lote la kidini, lakini nisingeweza kuyatupilia mbali maulizo yake. Aliniambia kwamba maulizo haya na mengine zaidi ningeweza kujibiwa na mashahidi wa Yehova na, kama nikienda kwenye mmojawapo wa mikutano yao, ningeona jambo fulani la ajabu sana. Kwa hiyo nikahudhuria mmojawapo, nami nikagundua kile kile alichomaanisha.

“Kwa kuwa nilihudhuria shule katika mtaa wa Wayahudi, nilikuwa nimeona chuki nyingi ya kitaifa. Lakini hapa, mle mle katikati ya mtaa wa Wayahudi, kulikuwamo kikundi cha watu waliojua kulikuwako taifa moja tu, taifa la kibinadamu. Wao walikuwa wenye kufikiria watu wengine, wenye fadhili na wenye upendo kwa mtu na mwenzake na kwangu, ijapokuwa sura yangu [nywele ndefu na nywele za mashavuni, masharubu, na suruali fupi yenye kubana ya bluu na makubazi (viatu) yangu]. Karibuni rafiki yangu mmoja na mimi tukaanza kujifunza na mashahidi wa Yehova.”

Halafu rafiki huyu anaongeza maelezo yake mwenyewe: “Siku moja nilikuwa nikizungumza na rafiki yangu mkubwa [yule kijana wa Kiyahudi] juu ya sikukuu niliyokuwa nimehudhuria. Nikamweleza namna ambavyo nilipendezwa kwamba zaidi ya watu 300,000 walikusanyikia huko na hali kulikuwako upendo mwingi sana kati ya watu hao. Nilipomaliza kumweleza juu yake, yeye akasema, ‘Ikiwa wataka kujua upendo kwa kweli ni nini, njoo kwenye mkutano wa mashahidi wa Yehova.’ Kwa hiyo nikaenda, nikiwa na mashaka juu ya namna ambavyo wataona juu ya sura yangu chafu-chafu.

“Sikufahamu kilichokuwa kikiendelea jukwaani, lakini mimi niliwachunguza watu wale. Walikuwa wachangamfu na wanyofu, nao walionyesha upendo wa kweli kwa mtu na mwenzake bila ya kujali rangi wala tofauti ya umri. Nilistaajabishwa na jambo hili. Nisingeweza hata kueleza kwa maneno nilivyojisikia.”‏

Leo vijana hawa wawili ni mashahidi wa Yehova waliobatizwa. Juu yao mzee katika kundi leo anasema: “Wote wawili wana sura ya Kikristo na ya kiungwana. Kweli, mageuzi katika wanaume hawa yauonyesha uwezo wenye kugeuza wa kweli, nalo kundi lote laufurahia ushirika wao sana.”

Ikiwa wewe unapendezwa na kushirikiana na watu ambao hawagawanywi na vizuizi vya kitaifa lakini wanaojitahidi kusitawisha upendo kama ilivyoamriwa katika Biblia, twakutia moyo ujifunze Maandiko Matakatifu na mashahidi wa Yehova. Tunasadiki kwamba utakayojifunza yatakuwa chanzo hakika cha kiburudisho cha kiroho kwako.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki