Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w74 5/15 kur. 219-223
  • Wakati Bora Kuwa Hai

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wakati Bora Kuwa Hai
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • FAIDA YA WANADAMU YAFIKIRIWA
  • WONYESHO WA UKWELI NA UWEZO WA MUNGU
  • JE! KITABU KILICHOANDIKWA NA WANADAMU CHAWEZA KUWA CHENYE KUTEGEMEKA?
  • WAKATI BORA WENYE NAFASI
  • Kufumbua Fumbo la Ule Mti Mkubwa
    Sikiliza Unabii wa Danieli!
  • Mfalme Atawala!
    “Ufalme Wako Uje”
  • Ndoto Inafunua Kwamba Wakati Umesonga Sana
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Mfuatano wa Matukio Katika Biblia Unaonyesha Nini Kuhusu Mwaka wa 1914?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
w74 5/15 kur. 219-223

Wakati Bora Kuwa Hai

Makala hii ni ya kutumia kwa mafunzo ya kitabu ya kundi

‘OH! AFADHALI SIKU NZURI ZA KALE!’

1-5. Kuna kosa gani kusema, ‘Oh, afadhali siku nzuri za kale’?

2 Wewe umesema hivyo mara ngapi?

3 Lakini je! kweli wewe ungalitaka kuishi katika wakati wa babu yako? Ebu ifikirie Vita ya Ulimwengu ya Kwanza na labda hata Vita ya Ulimwengu ya Pili, ambayo ungalipaswa uivumilie.

4 Au, kama ungaliishi kale sana sana. Je! ingalikupasa uzivumilie taabu chache zaidi zilizokuwako huko? Je! ungalikuwa na tumaini bora?

5 Biblia inapinga kutamani sana siku za kale. Inaonya hivi: “Usiseme, Kwani siku za kale kupita siku hizi? Maana si kwa hekima uulizavyo neno hilo.”​—Mhu. 7:10.

6-8. (a) Kwa sababu gani sasa ndio wakati bora wa kuishi? (b) Twawezaje kuwa na hakika kwamba maoni yetu ni sawa?

6 Ijapokuwa kuongezeka kwa taabu duniani, kwa kweli SASA ndio wakati bora kuwa hai.

7 Kwa sababu gani? Kwa sababu sisi tu karibu zaidi na utimizo wa kusudi la Mungu juu ya dunia. Sisi tu karibu na utawala wenye amani wa miaka elfu wa ufalme wa Mungu, utakaowaletea wanadamu baraka zidumuzo.

8 Hili si tumaini la uongo. Si namna ya kuwazia-wazia tu. Liko juu ya uhakika. Liko juu ya ahadi ya Muumba​—si juu ya ahadi tu, bali juu ya maneno yenye hakika ya unabii ya Mmoja ambaye amekwisha kuhakikishwa vile vile kwamba anaweza kutabiri jambo hilo.

FAIDA YA WANADAMU YAFIKIRIWA

9, 10. Ni ufunuo gani wa ajabu aliopewa mtume Yohana?

9 Mungu Mwenye Nguvu Zote alichagua ampe mtume Yohana aliyekuwa amekuwa mtumishi mwaminifu wa Bwana Yesu Kristo miaka 65, njozi ya wazi ya ufalme huo. Yohana alikaribishwa atazame kwa wakati wa mbele, ili aione serikali hiyo ikisimamia kweli mambo yote ya dunia. Yohana aliyaandika mambo aliyoyaona katika kitabu cha Biblia kiitwacho Ufunuo.

10 Kwa sababu Yohana aliendelea kuzitangaza habari njema za ufalme wa Kristo utakaokuja alikuwa amehukumiwa na Milki ya Kirumi kama mvunja sheria​—akawa amehamishwa kupelekwa katika kisiwa cha Patmo kilicho katika Bahari Kuu. Bila shaka njozi hii ya ajabu ilikuwa faraja kubwa kwake. Ilikuwa thawabu yake kwa miaka mingi ya kazi ya uaminifu, kuwa ndiye wa kwanza kuyatazama mambo mengi juu ya ufalme huo na kujua kwamba utatawala kwa miaka elfu, ukiifanya dunia kuwa paradiso. Habari hiyo vile vile yaweza kuwa yenye kufariji sana kwetu sisi.​—Ufu. sura 20, 21.a

11. Nani watakaofaidika kweli kweli na utawala wa Ufalme wa miaka elfu?

11 Ufalme huu utatawala kwa faida ya wanadamu. Kweli, utamletea Mungu heshima na utasimamisha enzi yake milele juu ya kila kitu duniani. Utaipatanisha sayari hii yenye uasi na sayari nyingine za ulimwengu wake wote. Lakini watu hasa watakaofaidika watakuwa ni jamii ya wanadamu. Mfalme wake ni “uzao” ambao kupitia kwa huo “mataifa yote ya dunia watajibarikia.”​—Mwa. 22:18.

WONYESHO WA UKWELI NA UWEZO WA MUNGU

12, 13. Wakati Mungu alipotoa unabii juu ya kutumia utawala wake juu ya wanadamu, hali ya ulimwengu wa kale ilikuwaje?

12 Lakini namna gani uhakika wa tumaini katika utawala huu wenye kufaidi​—kutegemeka kwa ahadi? Ebu angalia alivyofanya Mungu, akiuonyesha uwezo wake wa kutumia utawala juu ya wanadamu, na kutangulia kusema atakalolifanya miaka ya wakati ujao.

13 Zapata karne 25 zilizopita mfalme fulani, Nebukadreza wa Babeli, alikuwa ndiye mtawala peke yake wa ulimwengu. Babeli ilikuwa imeishinda Serikali ya Ulimwengu ya Pili, Ashuru, na sasa Babeli ikawa Serikali kuu ya Ulimwengu ya Tatu ya historia ya Biblia.

14, 15. (a) Ni kosa gani alilofanya Mfalme Nebukadreza wa Babeli? (b) Mungu aliitikiaje, na Danieli alitokezwaje?

14 Lakini mfalme wake, Nebukadreza, alifanya kosa zito. Katika kiburi na kujivuna kwake hakujali uhakika wa kwamba Mungu wa mbinguni alikuwa amemruhusu tu kuwa alipokuwa. Mungu alikuwa amemruhusu achukue taifa la Kiyahudi, watu wake mwenyewe, katika uhamisho kwa sababu ya kutokutii kwao, kama adhabu. Haikuwa nguvu ya Nebukadreza iliyomwezesha autwae Yerusalemu. Ili aonyeshe mfano wa hili kwa Nebukadreza na kwa vizazi vifuatavyo, Mungu alimpelekea Nebukadreza ujumbe katika ndoto iliyomsumbua mfalme sana.

15 Akiisha kuzungumza na waaguzi wa kidini na wanajimu wake asipate maelezo ya kufaa juu ya ndoto, Nebukadreza alimwita mtumwa wa Kiyahudi, nabii Danieli.​—Dan. sura ya 4.

16, 17. Sauti kutoka mbinguni ilithibitishaje kwa Nebukadreza tafsiri ya Danieli ya ndoto yake, na chini ya hali gani?

16 Danieli alieleza maana ya ile ndoto. Ilimwambia Nebukadreza adhabu kutoka kwa Mungu ya kutwezwa kwa miaka saba. Hata hivyo, mwaka uliofuata, Nebukadreza alianza kutakabari, akijivunia mji wake mkuu wa Babeli. Na alipokuwa hajamaliza majivuno yake alisikia sauti ikitoka katika makao yasiyoonekana​—kutoka mbinguni, ikisema:

17 “Ee mfalme Nebukadreza, maneno haya unaambiwa wewe; Ufalme huu umeondoka kwako. Nawe utafukuzwa mbali na wanadamu, na makao yako yatakuwa pamoja na wanyama wa kondeni; utalishwa majani kama ng’ombe, na nyakati saba zitapita juu yako, hata utakapojua ya kuwa Aliye juu ndiye anayemiliki katika ufalme wa wanadamu, naye humpa amtakaye, awaye yote.”​—Dan. 4:29-32.

18. Je! maandishi ya Kibabeli yanasimulia juu ya wazimu wa Nebukadreza? Kwa sababu gani?

18 Ni jambo gani lililofuata mara hiyo? Lile lile ambalo Mungu alisema lingetukia. Limo katika habari ya Danieli. Maandishi ya Kibabeli ambayo yamechimbuliwa hayatoi habari juu ya uhakika wa kwamba Nebukadreza alishikwa na wazimu kwa miaka halisi saba, kama Biblia inavyoonyesha kuwa ndivyo ilivyotukia. Lakini je’ sisi tungewatazamia wasaidizi na watumishi wa mfalme mwenye mamlaka peke yake kuandika habari za kutwezwa kwake? Ikiwa Hitler angeanza tena kutawala kama alivyofanya Nebukadreza mwishoni mwa wazimu wake wa miaka saba, hatuwezi kuwazia kwamba wanahistoria wake wangeandika habari za kushindwa kwake. Vile vile mataifa mengine yamefuata maongozi ya kuficha matendo mabaya ya watawala na serikali zao, kama tuwezavyo kuona katika habari za Misri, Ashuru ya kale na nchi nyingi za kisasa. Lakini Biblia inatupa habari ya kihistoria ya kweli na yenye kuaminika kabisa.

19, 20. (a) Ni mambo gani ambayo Nebukadreza hakupata kujua, yaliyofunuliwa na unabii huu wa ndoto? (b) Sisi twaishi sasa katika wakati gani, kulingana na unabii huu pamoja na uthibitisho mwingine wa Biblia?

19 Wakati akili ya Nebukadreza iliporudishwa na Mungu, yeye alifahamu kidogo kwamba “nyakati saba” zilipaswa ziwe na utimizo mkubwa zaidi wa siku moja ya miaka ya unabii saba yenye siku 360 kila moja ikiwa mwaka mmoja, jumla ya miaka 2,520 (7 x 360). Yeye hakufahamu sana kwamba huo ulikuwa unabii ukifunua kwamba, tangu kupinduliwa kwa ufalme wa Mungu wenye kuwakilisha wakati Yerusalemu ulipoharibiwa katika mwaka wa 607 B.C.E., kwa miaka 2,520 asingekuwako mfalme wa ukoo wa Daudi akitawala mambo ya wanadamu. Wakati wa muda huu ‘Yerusalemu ungekanyagwa na mataifa mpaka majira ya Mataifa yatimie’​—yaani, Mungu angeruhusu utawala wa Mataifa juu ya dunia, bila mfalme katika kiti cha enzi akimwakilisha Mungu. Mwishoni mwa kipindi cha miaka 2,520 ungefika wakati wa Mungu wa kumweka Masihi wake katika kiti cha enzi katika mbingu. Kulingana na orodha ya tarehe ya Biblia na hali za ulimwengu zinazotimiza unabii, haya “majira ya Mataifa” yalimalizika katika mwaka wa 1914 C.E.​—Luka 21:24; Eze. 21:27.

20 Hii ingemaanisha kwamba sasa tumo katika kipindi kifupi kabla ‘haujaja’ ufalme wa Kimasihi juu ya taratibu mbovu iliyopo ya mambo na kuanzisha utawala wenye amani wa miaka elfu.​—Mt. 6:10.

JE! KITABU KILICHOANDIKWA NA WANADAMU CHAWEZA KUWA CHENYE KUTEGEMEKA?

21, 22. (a) Kwa sababu gani Biblia, ijapokuwa iliandikwa na wanadamu, isingekuwa neno la wanadamu? (b) Je! Nebukadreza alijifunza na yaliyompata?

21 Huenda wengine wakasita kuitegemea Biblia, kwa vile iliandikwa na wanadamu. Lakini mara nyingi watungaji wanawaambia wengine wanaotenda kama makarani wao tu mawazo yao. Vile vile, maandishi ya kihistoria si mawazo ya waandikaji. Ijapokuwa ni kweli kwamba Biblia iliandikwa na wanadamu, si neno la wanadamu. Katika kurasa zake Biblia inajidai kuwa kazi iliyoongozwa na roho ya Mungu, nayo imeandikwa kwa jina la “Yeye aliye juu, . . . Yeye aishiye milele.” Alipokwisha kutwezwa, Nebukadreza mwenyewe alifahamu na akakiri kwamba maneno ya Danieli ya tafsiri ya ndoto hayakuwa maneno matupu ya Danieli. Yeye alikubali hivi:

22 “Hata mwisho wa siku hizo, mimi, Nebukadreza, nikainua macho yangu kuelekea mbingu, fahamu zangu zikanirudia; nikamhimidi Yeye aliye juu, nikamsifu na kumheshimu Yeye aishiye milele; kwa maana mamlaka yake ni mamlaka ya milele, na ufalme wake hudumu toka kizazi hata kizazi; na watu wote wanaokaa duniani wamehesabiwa kuwa si kitu; naye hufanya kama atakavyo, katika jeshi la mbinguni, na katika hao wanaokaa duniani; wala hapana awezaye kuuzuia mkono wake, wala kumwuliza, ‘Unafanya nini wewe?’” ​—Dan. 4:34, 35.

23. Kwa sababu gani ni kwa faida yetu kwa vile Biblia iliandikwa na wanadamu?

23 Kwa kweli, uhakika wa kwamba wanadamu walitumiwa kama makarani katika kuandika yale ambayo Mungu alitaka katika Biblia hauifanyi iwe isiyo ya kweli au isiwe yenye maana kwa wanadamu. Yaliyowapata Ayubu, Daudi, Danieli na wanadamu wengine, maoni yao, majaribu, kushika kwao ukamilifu chini ya majaribu, yanatoa uhakika na kujiona kuwa karibu kusikoweza kutolewa na jambo jingine. Tena, inatutia moyo sisi kama wanadamu wa kawaida, kwa maana twaweza kujiona wenyewe kama tukipatwa na mengi ya mambo yale yale, na kujua kwamba ukamilifu waweza kuendelezwa na wanadamu ikiwa wanaendelea kumtumaini Mungu. Inaipa Biblia hali nzuri iliyo changamfu, yenye kufariji na ukweli wenye nguvu zaidi kuliko ambavyo kitabu kilichoangushwa kutoka mbinguni kingeweza kutoa.

24. Ni mambo gani ambayo Mungu amefanya yanayoonyesha uwezo wake wa kutabiri utawala wa Kristo wa miaka 1,000?

24 Ebu yafikirie mambo haya ya hakika: Mungu aliweza kutabiri kwa usahihi kwamba Nebukadreza angekuwa na wazimu kwa miaka saba kisha arudishwe kwenye kiti chake cha enzi. Yesu Kristo mwenyewe aliutaja unabii huu juu ya “majira ya Mataifa” kama ni hakika, na akaonyesha kwamba wakati fulani kufuata siku zake duniani, haya yangemalizika. Ndipo ujiulize mwenyewe hivi: Je! isingewezekana kwa Mungu, vile vile, kuitabiri miaka elfu ya utawala wa Masihi wake?

25, 26. (a) Mawaziri wengi wa serikali, wanasayansi na wengine wanatazamia nini kwa wanadamu? (b) Ni katika nini twaweza kutofautiana na maoni ya watu hawa wa ulimwengu wanaotazamia mwisho wa wanadamu? Kwa sababu gani?

25 Bila shaka wanadamu hawawezi kuitokeza miaka elfu yenye amani. Kwa kweli, hawawezi hata kuutokeza utawala wa ulimwengu wa miaka elfu. Hitler alijaribu ati autokeze, ila akaendelea kwa miaka kumi na miwili tu. Na hasa sasa, watu wengi wanaochunguza sana serikali na hali za ulimwengu​—mawaziri wa serikali, wanasayansi na wengine​—wanasema kwamba wanadamu hawataweza hata kuishi mpaka mwaka 2000 C.E. Wao wanaweka maoni yao, si juu ya Biblia, bali juu ya mambo ya hakika ya leo na juu ya mfulizo wa sasa usiogeuzika wa mambo yanayotutia na sisi sote. Biblia inasimulia juu ya nyakati hizi zenye taabu tunazopata kama ishara ya kukaribia kwa mwisho wa taratibu hii.​—2 Tim. 3:1-5.

26 Twaweza kuisadiki sana Biblia juu ya kukaribia kwa mwisho wa taratibu hii. Lakini hatuna msingi wa kusadiki utabiri wenye msiba wa uharibifu wa wanadamu, au madai ya zamani yanayotolewa mara nyingi na wanasiasa juu ya amani ya ulimwengu kupitia kwa utawala wenye kuendelea wa serikali za wanadamu. Sisi hatuna msingi ambao juu yake twaweza kuzisadiki ahadi hizi. Lakini sisi tunao msingi wa kumsadiki Muumba, na imetupasa tuyakubali matabiri yake. Haya si matabiri ya msiba kwa jamii ya kibinadamu, bali ni matabiri ya utawala wa miaka elfu utakaowakamilisha wanadamu. Mungu anatuambia kwamba yeye ataifanya dunia hii kuwa mahali pazuri ajabu na watu wake wapatane. Zaidi, yeye anaahidi uzima wenye kuendelea milele duniani, pamoja na furaha.

WAKATI BORA WENYE NAFASI

27. Eleza juu ya sababu gani huu ndio wakati bora kuishi.

27 Ikiwa twamsadiki Mungu, kweli huu ndio wakati bora wa kuishi ndani yake. Kwa maana, kati ya vizazi vyote vya watu, sisi ndio tulio na nafasi ya kuuona uharibifu wa uovu, kutakaswa kwa dunia, na kuokoka kuingia katika taratibu mpya yenye haki. Je! wewe wasadiki kwamba Mungu analo kusudi hili bora kwa dunia? Ikiwa ndivyo, chukua hatua za mara hii ili uwe na hakika ya kupata kibali chake wakati mfalme wake wa Kimasihi atakapoifikiliza hukumu juu ya taratibu hii mbovu ya mambo.

28. Ni mwendo gani ulio wa akili kuchukuliwa na mtu aliye na mashaka?

28 Ikiwa wewe ni mtu anayeelekea kuwa mwenye mashaka, sababu gani usiyafikirie kwa uangalifu mambo anayoyasema Mungu na kuyalinganisha na mambo yanayotolewa na wanadamu? Je! kuna tumaini jingine lo lote la kulinganisha na ahadi ya Mungu? Na anayoyaahidi Mungu hayapatani na tamaa za asili za wanadamu? Je! si yenye akili hata zaidi kuliko wanayoyaahidi wanadamu? Itumie vizuri nafasi ya pekee ya leo ili uyafikirie anayoyasema na kujifunza makusudi yake. Mashahidi wa Yehova watafurahia kukusaidia wewe, nyumbani mwako, bila malipo. Au unaweza kuhudhuria mikutano katika Majumba ya Ufalme yao ili uyasikie mambo haya yakizungumzwa huko.

​—Kutoka Kitabu God’s Kingdom 0f a Thousand Years Has Approached.

[Maelezo ya Chini]

a Katika mfululizo mkubwa wa makala katika matoleo yatakayofuata, Mnara wa Mlinzi unakusudia kuzungumza utawala wa miaka elfu wa Yesu Kristo​—yatakayotukia mbele ya kuanza miaka elfu, ishara za kukaribia kwa Ufalme, utakavyokuwa na maana kwa wanadamu, nani watakaokuwa wasimamizi wake mbinguni na duniani, raia zake, ufufuo wa wafu na kuhukumiwa kwao, na mambo mengine ya utawala wa Ufalme wa miaka elfu. Msingi wa makala hizi utakuwa kitabu cha kujifunza God’s Kingdom of a Thousand Years Has Approached, kilichochapwa na Sosaiti Brooklyn, New York (1973).

[Sanduku katika ukurasa wa 221]

Ufalme wa Ulimwengu Ulikabidhiwa kwa Kristo

Biblia ilitabiri kwamba Mungu angempa Kristo “ufalme wa ulimwengu” (Ufu. 11:15)

Huu ungekuwa wakati gani? Zikiisha kumalizika “nyakati saba” za mfano (Dan. 4:10-17)

Mti mkubwa sana unafananisha uwezo wa kifalme ‘uliokatwa’ wakati Yerusalemu ulipoanguka, 607 B.C.E. “Nyakati saba” zikiisha kumalizika, “pingu” zingeondolewa; mti ungekua

“Nyakati saba” zingeendelea kwa muda gani? Kwa zaidi ya miaka saba

Alipokuwa duniani, Yesu alionyesha “nyakati” za mfano zilikuwa bado kumalizika. (Luka 21:24) Ufunuo 12:6, 14 unaonyesha siku 1,260 kuwa sawa na “nyakati” tatu na nusu

Kila mmoja wa “nyakati” wapaswa uwe siku 360 (3 1⁄2 × 360 = 1,260)

Kila siku moja ya “nyakati” za unabii ni mwaka (Hes. 14:34; Eze. 4:6)

Hivyo “nyakati saba” (7 × 360) ni miaka 2,520

“Nyakati saba” za mfano (miaka 2,520) zilianza wakati gani?

Katika Septemba au Oktoba 607 B.C.E. nchi ya ufalme wa mfano wa Mungu katika Yuda ilipoachwa ukiwa

“Nyakati saba” za mfano zilimalizika wakati gani?

Miaka 2,520 ingetuleta kwenye mwaka wa 1914 C.E. (606 1⁄4 + 1913 3⁄4 = 2,520)

1914 C.E.​—ndio mwaka “ufalme wa ulimwengu” ulipokabidhiwa kwa Kristo

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki