Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w74 6/1 kur. 243-247
  • N’nini Kinachozuia Amani ya Ulimwengu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • N’nini Kinachozuia Amani ya Ulimwengu?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • “MNYAMA”
  • “KAHABA”
  • KUKIONDOA KIZUIZI CHA PILI
  • HAR-MAGEDONI SI YA MUDA MREFU
  • WAOKOKAJI
  • Kupambana na Hayawani Wawili Wakali Sana
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
  • Kitabu cha Ufunuo Kinamaanisha Nini kwa Maadui wa Mungu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2022
  • Maswali kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
  • Amani, Usalama, na Ile ‘Sanamu ya Mnyama’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
w74 6/1 kur. 243-247

N’nini Kinachozuia Amani ya Ulimwengu?

Makala hii ni ya kutumia kwa mafunzo ya kitabu ya kundi

1-8. N’nini kimojawapo cha vizuizi vikubwa vya amani ya ulimwengu, nao watu wenye ujuzi wanaonyeshaje wanaanza kufahamu hivyo?

HATA wajaribu namna gani, watu wa ulimwengu wameshindwa kupata amani ya kweli. Kwa sababu gani?

2 Visipoondolewa vizuizi viwili, amani ya kweli haiwezi kuja kamwe.

3 Cha kwanza cha vizuizi hivi, kulingana na Biblia, ni taratibu za ulimwengu za dini za uongo. Watu wenye ujuzi vile vile wanaanza kuziona dini za ulimwengu kama kizuizi.

4 Chini ya kichwa cha habari “Sasa Kanisa Lafadhaisha Ulimwengu,” John Chamberlain, mfafanuzi wa magazeti wa King Features Syndicate, anakazia fikira kwenye kujitilia kwa makanisa katika siasa, hata kupita kiasi kwayo kwa kutegemeza mashauri ya fitina juu ya serikali. Yeye anaandika:

5 “Maadui walio wakubwa zaidi wa roho inayokua ya mazungumzo ya ulimwengu wote juu ya ukamatano wenye mashaka kati ya mataifa ni watumishi fulani wachache wanaojidai kuzungumza kwa jina la Ukristo. The World Council of Churches (Baraza ya Ulimwengu ya Makanisa) ndiye mkosaji aliye mbaya zaidi. Lakini Kanisa la Katoliki limejitokezea wataka mapinduzi, ambao lazima liwakatae.”​—The Daily Oklahoman, Agosti 8, 1973.

6 Naye rais wa United States, katika hotuba yake ya Agosti 15, 1973 katika televisheni kwa taifa, aliwatia viongozi wa dini hatiani wanaojidukiza katika siasa na uhalifu aliposema kwamba, kuanzia mwaka wa 1960 na kuendelea,

7 “watu mmoja mmoja na vikundi walizidi kutetea haki ya kutwaa sheria mikononi mwao wenyewe, wakisisitiza kwamba makusudi yao yalimaanisha adili ya juu zaidi. Kisha, nia yao ilisifiwa katika magazeti na hata kutoka nyingine za jukwaa zetu kama ushuhuda wa elimu mpya. Wale ambao kati yetu walisisitiza juu ya amri za kale, walioonya juu ya kuudharau umuhimu wa kutenda kulingana na sheria na kanuni, walishtakiwa kuwa wapinga maendeleo.

8 “Nia ile ile ilileta uhalifu mwingi na hofu, ghasia na uteketezaji wa nyumba za watu na mashamba kwa makusudi na kulipua makombora, yote haya yakifanywa ili amani na haki viwepo.”

9, 10. (a) Kwa sababu gani dini za ulimwengu zimechukiwa na Mungu, naye atatumia chombo gani kuziharibu? (b) N’nini, sasa hivi, ulio ujamaa wa viongozi wa kidini na watawala katika mataifa yanayojidai kumtumikia Mungu?

9 Kwa kweli, Biblia yasema kwamba watumishi wa kweli wa Mungu wamepaswa kujitenga kabisa na siasa, kutokuwamo kabisa, nao yawapasa kuutangaza ufalme wa Mungu kama tumaini la ulimwengu. Lakini, kuliko hivyo, dini ya ulimwengu, hasa makanisa ya Kristendomu, imejidukiza katika siasa, imeunga mkono ugomvi wa kitaifa na kumwakilisha Mungu isivyofaa. Kwa hiyo yachukiwa naye. Yeye amesema kwamba ataiharibu. Kwa njia gani?

10 Chombo cha Mungu kitakuwa watu wa siasa ambao matengenezo ya kidini ‘yamefanya ukahaba’ nao. Lakini hata sasa, katika mataifa mengi yanayoitwa “ya Kikristo,” viongozi wa kidini wananyweana kikombe kimoja kwa kupokezana pamoja na wanasiasa nao mara nyingi wanaonekana sana katika makusanyiko yao ya kisiasa. Ijapokuwa watawala wengine ni wasiomcha Mungu, isitazamiwe kwamba watu wa siasa wenyewe, wangeweza kutenda kwa umoja kuharibu dini ya uongo. N’nini, basi, kitakachowafanya watende hilo? Angalia tendo ambalo Mungu anasema ataitenda dini ya ulimwengu yenye mfano wa kahaba.

“MNYAMA”

11. Hakikisha kwamba wanyama wa mwitu wanatumiwa katika Biblia kufananisha serikali.

11 Katika Neno lake Biblia Mungu analisimulia tengenezo kuu la ulimwengu la kisiasa kama “mnyama.” Twajua hayo kutokana na yale ambayo Mungu aliyafunua karne nyingi zilizopita kupitia kwa nabii wake Danieli. Danieli alipewa njozi ambamo aliona wanyama​—simba, dubu, chui na mnyama wa kuogofya mwenye meno ya chuma. Malaika wa Mungu alieleza, “wanyama hao wakubwa walio wanne ni wafalme wanne watakaotokea duniani.” Hawa walipata kuwa Babeli (iliyokuwa yenye mamlaka wakati huo), Wamedi na Waajemi wakiwa wameungana, Ugiriki na Rumi.​—Dan. 7:4-7, 17; linganisha Danieli 8:3-8, 20, 21.

12. “Mnyama” wa Ufunuo 13:1, 2 anafananisha nini?

12 Vivyo hivyo, katika kitabu cha Ufunuo mtume Yohana atoa habari juu ya njozi ambayo katika hiyo aliona “mnyama” mwenye vichwa saba na pembe kumi. Mnyama huyu, akiwa mwenye sehemu nyingi, analifananisha tengenezo la ulimwengu la kisiasa lililoonyesha mamlaka yake kupitia kwa mamlaka saba za ulimwengu. (Ufu. 13:1, 2) Ibilisi aonyeshwa kuwa mtawala wake halisi na mungu.​—2 Kor. 4:4; Mt. 4:8, 9.

“KAHABA”

13. (a) N’nini “sanamu” ya “mnyama,” na ni nani anayeonyeshwa kama anayempanda? (b) “Kahaba” anamwelekeza “mnyama” akapambane na nani?

13 “Sanamu” ya “mnyama” wa mfano, tengenezo la mataifa yote la amani na usalama, sasa lijulikanalo kama Umoja wa Mataifa, limeundwa, ushirika wake ukiwa wenye mamlaka za kisiasa zilizo kuu za dunia na kumfanyiza “mnyama” wa kisiasa. “Pembe kumi” zake zinafananisha watawala wote wa kitaifa waliomo humo. “Sanamu” hii, vile vile inayoitwa “mnyama mwekundu sana,” inapandwa na “kahaba” “Babeli Mkuu,” milki ya ulimwengu ya dini ya uongo. Anaonyeshwa akimwelekeza “mnyama” huyu kwenye vita kamili juu ya “Mwana-Kondoo,” Yesu Kristo, na faida zake za Ufalme duniani. Dini ya uongo imekuwa na maongozi yenye nguvu katika kuwaelekeza watawala wa kisiasa wapambane na mashahidi wa Yehova, nao wameteswa vikali sana. Maongozi yenye nguvu ya “Babeli Mkuu” yanamfanya yeye kuwa “milki” ya kidini juu ya tengenezo la kisiasa la dunia, kama vile Biblia isemavyo: “Na yule mwanamke uliyemwona, ni mji ule mkubwa, wenye ufalme juu ya wafalme wa nchi.”​—Ufu. 17:1-3, 5, 13, 14, 18.

14-16. Mwisho wa “Babeli Mkuu” unakujaje, na n’nini hasa kinachoziharakisha “pembe” kutenda?

14 Je! mwisho wa taratibu nzima ya dini ya uongo unakujaje? Biblia yajibu: “Zile pembe kumi ulizoziona [watawala wote wa kitaifa], na huyo mnyama [mwekundu], hao watamchukia yule kahaba, nao watamfanya kuwa, mkiwa na uchi, watamla nyama yake, watamteketeza kabisa kwa moto.”​—Ufu. 17:16.

15 N’nini kinachowaharakisha kutenda, kwa maana wao hawajafanya hivyo wajapokuwa wanayaona makanisa yakijidukiza katika mambo ya kisiasa? Ni Yehova Mungu mwenyewe. “Maana Mungu ametia mioyoni mwao kufanya shauri lake, na kufanya shauri moja, na kumpa yule mnyama ufalme wao hata maneno ya Mungu yatimizwe.”​—Ufu. 17:17.

16 Kwa hiyo mwisho wa dini ya uongo utakuja mara kwa kushangaza, wakati anapodhani, “Nimeketi malkia, wala si mjane, wala sitaona huzuni kamwe.” Lakini Mungu asema: “Kwa sababu hiyo mapigo yake yatakuja katika siku moja, mauti, na huzuni, na njaa, naye atateketezwa kabisa kwa moto. Kwa maana Bwana Mungu aliyemhukumu ni mwenye nguvu.”​—Ufu. 18:7, 8.

KUKIONDOA KIZUIZI CHA PILI

17, 18. N’nini kizuizi cha pili cha amani ya ulimwengu, na kwa sababu gani?

17 N’nini, basi, kile kizuizi cha pili cha amani ya ulimwengu? Ndicho “mnyama” mwenyewe, tengenezo la duniani pote la kisiasa linaloutawala ulimwengu huu.

18 Kumbukumbu la “mnyama” ni baya kweli. Ni kumbukumbu la miaka mingi ya vita zaidi sana kuliko ya amani. Na hata mnamo wakati wa amani mamilioni ya watu sikuzote wameonewa au kutumikishwa. Sasa utukuzo wa taifa wafanyiza kizuizi kielekeacho kuwa kisichopenyeka cha amani ya ulimwengu. Kwa hiyo Neno la Mungu latuambia kwamba, dini ya uongo itakapokwisha ‘kuteketezwa kwa moto,’ pale pale visiginoni pake utakuja uharibifu wa “mnyama” na wote wale wamwungao mkono.

19. Je! uharibifu wa mamlaka za ulimwengu unaletwa, na vita ya atomiki?

19 Je! uharibifu huu unaletwa na vita ya makombora ya atomiki? Silaha hizi za kutosha sasa zimelundikwa ziliharibu taifa zima la kibinadamu. Lakini sivyo, Biblia yaonyesha kwamba “mnyama” mzima anapigana na Mungu na ufalme wake ukiwa mikononi mwa Kristo Yesu. Kutoka mbinguni, Kristo anawashinda. Hili ndilo pigano linalotukia katika mahali pa mazidio ya ulimwengu panapoitwa Har–​Magedoni, kama ilivyoandikwa: “Wakawakusanya [wafalme wa dunia] hata mahali paitwapo kwa Kiebrania, Har–​Magedoni.”​—Ufu. 16:14-16.

20, 21. (a) Kwa sababu gani ni kazi bure kwa wanadamu kujaribu ‘kumfuga’ au kumtiisha “mnyama”? (b) Kwa ufupi lisimulie pigano la Har–​Magedoni.

20 Kwa hiyo, waongozi wasidhani kwamba kwa mateto na maandamano yao ya kutetea mambo yao wanaweza kumfanya “mnyama” awe ‘mnyama wa amani’ wa kufugwa, akiyahakikishia mataifa yote ya dunia haki za kibinadamu. Wala wataka maasi wasidhani kwamba kwa njia ya uhalifu, hila za mapigano au maogofyo wanaweza kumwondosha “mnyama” asiiongoze dunia. Kitabu cha Ufunuo, kikisimulia Har–​Magedoni, chafunua njia ya pekee ambavyo “mnyama” aweza kutiishwa:

21 “Kisha nikamwona huyo mnyama, na wafalme wa nchi, na majeshi yao, wamekutana kufanya vita na yeye aketiye juu ya farasi yule, tena na majeshi yake. Yule mnyama akakamatwa, na yule nabii wa uongo pamoja naye, yeye aliyezifanya hizo ishara mbele yake, ambazo kwa hizo aliwadanganya watu wale walioipokea ile chapa ya huyo mnyama, nao walioisudujia sanamu yake; hao wawili wakatupwa wangali hai katika lile ziwa la moto liwakalo kwa kiberiti; na wale waliosalia waliuawa kwa upanga wake yeye aliyeketi juu ya yule farasi, upanga utokao katika kinywa chake. Na ndege wote wakashiba kwa nyama zao.”​—Ufu. 19:19-21.

22, 23. “Nabii wa uongo” n’nini?

22 Aliyeketi juu ya farasi anasimuliwa mapema (mistari 11-16) kama “Mfalme wa wafalme na Bwana wa mabwana.” N’nani mwingine ila “Mwana-Kondoo,” Bwana Yesu Kristo, ambaye angeweza kuwa yeye aliyeketi juu ya farasi, akipigana pigano hili la “upatilizo wa Mungu Bwana mwenye enzi yote”? (Ufu. 19:15, The New English Bible) Linalofaa kuangaliwa ni kwamba, pamoja na “mnyama” aonekana “nabii wa uongo.” Kwa wazi hii ingekuwa sehemu ya majeshi ya “mnyama” ikitenda kama mnenaji mkuu. Na twaona kwamba huyu “nabii wa uongo” ndiye yule yule aliyesema sana kwa sauti kuu kuifanya “sanamu ya mnyama” isimamishwe ili watu waiabudu, waitazamie kwa amani ya ulimwengu na usalama.

23 Ndiyo, huyo ni kimojawapo cha vichwa vya mnyama naye mwenyewe ni “mnyama” anapoonwa kama mamlaka moja ya ulimwengu, kama zilivyokuwa Babeli, mamlaka ya Wamedi na Waajemi wakiwa wameungana, Ugiriki na Rumi. Afananishwa na mnyama ‘mwenye pembe mbili.’ (Ufu. 13:11-15) Anakuwa ndiyo mamlaka ya saba ya ulimwengu, yenye “pembe mbili,” mamlaka mbili za kisiasa zilizo mbali mbali lakini kwa kawaida zikishirikiana, Uingereza na United States.

HAR-MAGEDONI SI YA MUDA MREFU

24, 25. (a) Hali ya watumishi wa Mungu wa kidunia itakuwa nini penye Har–​Magedoni? (b) Je! Har–​Magedoni itachukua muda mrefu?

24 Kwa hiyo, hakuna sehemu ya hii taratibu ya kisiasa ya ulimwengu itakayokosa kushiriki. Hata hivyo, majeshi ya kimbinguni yakiongozwa na Yesu Kristo hayatachukua muda mrefu kuyafutilia mbali majeshi yote ya dunia na zana zao penye Har–​Magedoni. Bila shaka, silaha za kidunia haziwezi kuyagusa majeshi ya kimbinguni. Lakini silaha zaweza kuwatisha wale waliomo duniani wanaosimama upande wa enzi ya Mungu. Na hali watumishi hawa wa kidunia wa Mungu hawatajitia katika pigano lo lote. Wao wanayategemea majeshi ya kimbinguni ya Kristo, ambayo “mnyama” hawezi kuyakwepa, hata awe mwenye nguvu na hila ya namna gani. ‘Atakamatwa’ anapofanya makosa yake ya mwisho juu ya waabudu waaminifu wa Yehova Mungu.

25 Ikiwa malaika mmoja wa Mungu aliweza kuangamiza wakuu na viongozi 185,000 wa jeshi la Ashuru katika usiku mmoja, ingeyachukua maelfu yote ya malaika muda gani kuyaangamiza majeshi ya ulimwengu huu kwa amri ya Kristo, hata wawe ni makumi ya mamilioni?​—2 Fal. 19:35; 2 Nya. (Sik.) 32:21; Dan. 7:9, 10, 13, 14.

26. N’nini kinachotukia kwa “mnyama” na majeshi yake?

26 Penye Har–​Magedoni Mfalme wa wafalme anatoa amri ya kuharibiwa kwa adui za Mungu mikononi mwa malaika wa kimbinguni wanaoongozwa naye. ‘Yangali hai’​—vyama vyenye nguvu, vinavyotenda kazi​—matengenezo ya kisiasa yanaharibiwa kwa kutupwa ndani ya “ziwa la moto.” Lo! ni mchafuko na mvurugo wa namna gani unaoletwa na uharibifu huu wa tengenezo lao kati ya askari! Lakini inakuwa kuchelewa mno kukimbia na kazi bure kabisa kupigana. Yesu Kristo, kwa kuutumia “upanga utokao katika kinywa chake,” anaamuru wauawe kana kwamba upanga mrefu wa mkuu mwenye mamlaka ulikuwa ukitumiwa.

WAOKOKAJI

27. Je! Har–​Magedoni itaiacha dunia bila ya wakaaji?

27 Angalia kwamba habari haisemi kwamba Mungu ataiteketeza dunia ya halisi kwa moto iliyotawaliwa na taratibu ya ulimwengu ya kisiasa kwa karne nyingi na iliyochafuliwa nayo na kuharibiwa sana. ‘Wala unabii hausemi kwamba dunia itakuwa mahali pasipo na uhai, pasipokaliwa. Watakuwako waokokaji. Twajuaje?

28. Yesu Kristo alionyeshaje wangekuwako waokokaji wa “dhiki ile iliyo kuu”?

28 Yesu Kristo mwenyewe alionyesha kutakuwako wokovu kwa kutoa maagizo juu ya wokovu kisha akasema: “Basi, kesheni ninyi kila wakati, mkiomba, ili mpate kuokoka katika hayo yote yatakayotokea, na kusimama mbele za Mwana wa Adamu.”​—Luka 21:36.

29. Je! kutakuwako watiwa mafuta wo wote wa Mungu watakaookoka duniani?

29 Kwa hiyo, si wote watakaomwabudu “mnyama” au “sanamu” yake. Mkazo unaotumiwa kumfanya kila mtu afanye hivyo unaleta jaribu la uvumilivu kwa ndugu za Kristo waliomo duniani. (Ufu. 13:7-10) Lakini wao wanazishinda jitihada za “mnyama” na kuwa ‘washindi’ wa ulimwengu bila vita yenye silaha.​—Yohana 16:33; Ufu. 2:7, 17, 26.

30, 31. Onyesha kwamba kutakuwako waokokaji wengine wa kidunia.

30 Mbali na ndugu hawa wa kiroho wa Kristo, walio na matumaini ya kimbinguni, kwa wazi Biblia yaonyesha kwamba kuna wengine wasiomwabudu “mnyama.” Hawa ndio “mkutano mkubwa” wa Ufunuo 7:9-17, wanaosemwa waziwazi kuwa “wanatoka katika dhiki ile iliyo kuu” na ambao Mungu atatandaza juu yao “hema” ya ulinzi, naye Mwana-Kondoo “atawaongoza kwenye chemchemi za maji yenye uhai.” Hawa si wa “kiumbe kipya” wanaofanyiza “Israeli wa Mungu.” (Gal. 6:15, 16) Mtume Yohana aliwaona wakitokea alipokwisha kukushuhudia kutiwa muhuri kwa wale 144,000 wa Israeli wa kiroho.

31 Vile vile, hawa wanaonyeshwa kuwa “kondoo” wanaotendea ndugu za kiroho wa Kristo mema mnamo kuwapo kwake katika mamlaka ya Ufalme. Wanakaribishwa: “Urithini ufalme mliowekewa tayari tangu kuumbwa ulimwengu.”​—Mt. 25:34.

32. Matokeo ya Har–​Magedoni yatakuwa nini?

32 Kwa hiyo hakutakuwako utupu, dunia isiyokaliwa. Mungu ataisafisha dunia isiwe na wachafuaji tu, waiharibuo. (Ufu. 11:18) Atawaharibu adui zake. Wote watakaookoka wataiona aibu ya wale wanaopigana na Mungu, nao wote walio hai watamsifu yeye kwa haki yake, uadilifu na rehema.​—Zab. 145:9-21.

​—Kutoka Kitabu God’s Kingdom of a Thousand Years Has Approached.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki