Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w74 7/15 kur. 335-336
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Habari Zinazolingana
  • “Wokovu Una Bwana”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
  • Sikukuu na Maadhimisho
    Shule na Mashahidi wa Yehova
  • Kanuni za Adili Zinazostahili Staha
    Mashahidi wa Yehova na Elimu
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
w74 7/15 kur. 335-336

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

● Ni kwa sababu gani wengine kati ya mashahidi wa Yehova wa Kikristo wanasimama wakati wa kusalimu bendera lakini wasisimame wakati wimbo wa taifa unapoimbwa?​—U.S.A.

Mashahidi wa Yehova wa Kikristo wanajaribu kufuata Neno la Mungu na maamuzi ya dhamiri zao zilizozoezwa na Biblia. Kama Wakristo katika karne ya kwanza, wanajiona wenyewe kama ‘wasafiri’ katika ulimwengu wa wanadamu wasioamini na wanatoa uaminifu wao kwa ufalme wa Mungu kupitia kwa Kristo. (1 Pet. 2:11) Ni kwa sababu hii wanajiepusha na matendo yote, kutia na yale ya kitaifa, ambayo yangeonyesha kutokuwa waaminifu kwa Mungu na kwa Mfalme wake Yesu Kristo aliyewekwa.

Na ikumbukwe kwamba bendera ya taifa ni zaidi ya kipande cha nguo. Kwa rasmi inatazamwa kama mfano mtakatifu wa taifa na inatendewa kwa heshima. Kwa mfano, wakati inapochakaa desturi ya kitaifa mara nyingi inaamuru kwamba bendera hiyo isitupwe ivi hivi bila sherehe, bali yapaswa ‘iharibiwe katika njia yenye heshima, zaidi kwa kuteketezwa.’ Vile vile kuna sheria zinazoongoza namna ya kupandisha bendera, kushusha, kukunja, kupeperusha na kuonyeshwa kwa bendera. Kusalimu au kutoa kiapo cha utii kwa bendera kunaonwa kama tendo lenye heshima, tendo la uaminifu mtakatifu, na kwa kuwa bendera ni mfano wa Serikali, tendo kama hilo linakuwa namna ya ibada ya sanamu.​—⁠ Linganisha Kutoka 20:4-6; 1 Yohana 5:21.

Ijapokuwa hawawazuii wengine wasiisalimu bendera ya taifa lo lote, mashahidi wa Yehova wa Kikristo wanaona kwamba wanaweza kutoa ibada hiyo kwa Yehova Mungu peke yake. Wanayo heshima inayofaa kwa bendera ya nchi zao, lakini kusifu mno bendera ya taifa lo lote na kushiriki katika matendo ya kuabudu mfano wa Serikali ingekuwa kwao tendo la kutoaminika kwa Mungu na kukosa uaminifu kwa ufalme wa Mwana wa Mungu.

Kwa kawaida, desturi ambayo wote wanaohudhuria sherehe ya kusalimu bendera wanatakiwa ni kusimama na kila mtu kuisalimu bendera kama kiapo cha utii kwa mfano huu wa Serikali. Katika hali hiyo tendo la kusimama peke yake halielekei kutazamwa kama tendo la ibada. Kwa hiyo, Wakristo wengi wa kweli wameona haikatazwi kusimama kwa heshima, lakini bila kusalimu bendera na kutoa kiapo. Bila shaka, hapa dhamiri inatiwa ndani. Ijapokuwa Mashahidi wengine wanafuata mwendo huu, huenda wengine wakaongozwa na dhamiri zao kuketi bila kusimama au kujiepusha wenyewe wasiwepo mahali ambapo sherehe inafanyiwa.

Kwa habari ya wimbo wa taifa, mara nyingine wanaohudhuria wanatazamiwa kusimama na kuimba. Basi, hali hii ingelingana na ile ambayo imetajwa sasa hivi kwa habari ya bendera ya taifa. Walakini, kwa kawaida wahudhuriaji wanatazamiwa kusimama tu wakati wimbo wa taifa unapoimbwa. Katika hali hii, kusimama kwa mtu kungeonyesha kukubaliwa kwa maneno na maono ya ndani yanayoonyeshwa na wimbo. Kwa habari ya nyimbo hizo za taifa The Encyclopedia Americana kinasema hivi: “Kupenda nchi ya uzaliwa na kujivunia nchi ndiyo mambo makuu ya karibu nyimbo zote za taifa, na katika nyingi, maoni ya kidini yanachanganywa na maoni ya kupenda nchi. Mara nyingi nyimbo za taifa zinahusiana na nyimbo za watu wa nchi au zinatokana na vita na mapinduzi.” Kwa kuwa Yehova Mungu ndiye Muumba wa dunia, na mataifa yote yana baba yao mmoja, Adamu, hakuna msingi wa Maandiko wa kuwa na kiburi cha kitaifa na kuwa na maoni ya kwamba taifa la mtu fulani ndilo bora kuliko mataifa mengine. (Matendo 17:26) Basi pengine ingeulizwa hivi, Je! Mkristo angeonyesha katika njia yo yote kwamba anakubaliana na maoni ya kujivunia taifa? Je! ingefaa kwake kushiriki nyimbo zinazokubali vita na mapinduzi?

Uhakika huu usipitiwe: Maoni hayo ya mashahidi wa Yehova si yenye kutoheshimu serikali hata kidogo. Mashahidi wa Yehova hawashiriki kabisa siasa za nchi yo yote. Hawashiriki hata kidogo katika ghasia zo zote, mapinduzi au maasi katika kujaribu kuiangusha serikali. Si watu wasio na uaminifu hata kidogo, hawashiriki hata kidogo katika kufitini serikali au matendo ya namna yo yote ya kuipinga serikali. Kwa kweli, Biblia inasema kwamba serikali za kilimwengu ni “agizo la Mungu” na ‘zimeamriwa na Mungu.’ Zaidi ya hayo, mashahidi wa Yehova wako chini ya amri kuzipa ‘mamlaka zilizo kuu’ kodi, ushuru na heshima.​—Rum. 13:1-7.

Kwa hiyo, mashahidi wa Yehova wanasimama kwa kufaa au wanainama au hata kuanguka kifudifudi mbele ya mtawala kwa kuheshimu cheo chake, ikiwa ndivyo ilivyo desturi ya nchi. (Mwa. 23:7; 42:6; 44:14) Lakini hawatamsifu mtawala huyo wa kibinadamu kama mungu. Wala hawatasujudu au kusalimu au kubusu au kuchoma uvumba kwa tendo la kuabudu mbele ya picha au sanamu ya mtawala au sanamu ya Serikali, kama ile iliyosimamishwa na Nebukadreza katika uwanda wa Dura, au kama bendera za kisasa za mataifa. (Matendo 12:21-23; 14:12-15; Dan. 3:1-29) Basi ikiwa serikali hazitungi sheria zilizo tofauti na sheria za Mungu kama zilivyoandikwa katika Biblia, Wakristo leo, kama Wakristo wa karne ya kwanza watakuwa watii kwa kumpa “Kaisari yaliyo ya Kaisari,” na wakati uo huo wampe Mungu “yaliyo ya Mungu,” yaani, ibada na utumishi wao.​—Matendo 4:19; 5:29; Marko 12:17.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki