Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w74 10/1 kur. 454-455
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Habari Zinazolingana
  • Ule Ufalme na lile Tumaini la Ufufuo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Siku ya Hukumu ya Mungu—Matokeo Yayo Yenye Shangwe!
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
  • Ufufuo
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
  • Wakati Watu Waliokufa Watakapoishi Tena!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
w74 10/1 kur. 454-455

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

● Ufunuo 20:5 unasema hivi: “Hao wafu waliosalia hawakuwa hai, hata itimie ile miaka elfu.” Je! andiko hili linaonyesha kwamba ufufuo utatukia baada ya utawala wa miaka elfu wa Kristo?​—Ecuador.

Sivyo, andiko hili halipaswi kueleweka hivyo.

Hata kuna mashaka kadiri fulani juu ya kama maneno haya yalikuwamo hasa katika yale ambayo mtume Yohana aliandika kwanza. Bila shaka hayapatikani katika Sinaitic Manuscript ya karne ya nne. Iwapo yalikuwamo katika hati ya kwanza, maneno haya yanapaswa hata hivyo kufikiriwa kwa msaada wa maneno yanayozunguka na Maandiko mengine.

Ufunuo 20:4-6 unasema hivi: “Kisha nikaona viti vya enzi, wakaketi juu yake, nao wakapewa hukumu; nami nikaona roho zao waliokatwa vichwa kwa ajili ya ushuhuda wa Yesu, na kwa ajili ya neno la Mungu, na hao wasiomsujudia yule mnyama, wala sanamu yake, wala hawakuipokea ile chapa katika vipaji vya nyuso zao, wala katika mikono yao; nao wakawa hai, wakatawala pamoja na Kristo miaka elfu. Hao wafu waliosalia hawakuwa hai, hata itimie ile miaka elfu. Huo ndio ufufuo wa kwanza. Heri, na mtakatifu, ni yeye aliye na sehemu katika ufufuo wa kwanza.”

Kwa wazi, wale wanaopata “ufufuo wa kwanza” wanakuwa hai kabla ya kumalizika kwa utawala wa miaka elfu, kwa maana wanashirikiana na Bwana wao katika utawala mnamo kipindi hicho. Lakini wale wasiopata “ufufuo wa kwanza,” ufufuo kwenye uzima wa kimbinguni, wanasemekana ‘kutokuwa hai, hata itimie ile miaka elfu.’ Ulizo ndilo hili: Je! huko ‘kuwa hai’ kuna maana ya kufufuliwa kwao?

Sivyo; likiangaliwa kutokana na maneno yanayozunguka, na kwa msaada wa maandiko mengine, ni wazi kwamba sivyo ilivyo. Ukisimulia ufufuo, Ufunuo 20:11-13 unasema hivi: “Nikaona kiti cha enzi, kikubwa, cheupe, na yeye aketiye juu yake; ambaye nchi na mbingu zikakimbia uso wake, na mahali pao hapakuonekana. Nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya hicho kiti cha enzi; na vitabu vikafunguliwa; na kitabu kingine kikafunguliwa, ambacho ni cha uzima; na hao wafu wakahukumiwa katika mambo hayo yaliyoandikwa katika vile vitabu, sawasawa na matendo yao. Bahari ikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake; na Mauti na Kuzimu zikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake. Wakahukumiwa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake.” Halafu, katika Ufunuo 21:1, twasoma hivi: “Nikaona mbingu mpya na nchi mpya; kwa maana mbingu za kwanza na nchi ya kwanza zimekwisha kupita.”

Hivyo maneno yanayozunguka yanaonyesha kwamba ufufuo mkubwa wa wafu unatukia baada ya “mbingu za kwanza na nchi ya kwanza” kupita. Hili linatukia wakati gani? Kulingana na 2 Petro 3:10, mbingu za kwanza na nchi zitapita katika “siku ya Yehova.” (WW) Siku hiyo, kulingana na mstari wa 3 mpaka wa 6, itawanasa wenye dhihaka bila ya kuwa tayari, na kwa hiyo inakuja kabla ya utawala wa miaka elfu wa Kristo.

Katika siku za Nuhu nchi halisi wala mbingu halisi hazikutoweka. Lakini jamii mbovu ya kibinadamu, ikiongozwa na majeshi maovu ya kiroho, ilitoweka katika maji ya gharika. Vivyo hivyo, uharibifu wa “mbingu za sasa na nchi” haumaanishi mwisho kwa dunia halisi wala mbingu zionekanazo. (2 Pet. 3:7) Walakini, jamii ya kibinadamu isiyomcha Mungu itatoweka. Naye Shetani Ibilisi na mashetani zake, ambao wamekuwa kama “mbingu” zenye kutawala wanadamu wasiotii, watakomeshwa au kutiwa shimoni.​—Ufu. 20:1-3, NW.

Kwa kuwa Ufunuo 20:11-13 unaufungamanisha ufufuo mkubwa wa wafu na ‘kukimbia kwa nchi na mbingu,’ lazima ufufuo huo utukie mnamo miaka elfu ambayo Shetani atakuwa shimoni. Kwa hiyo, ‘kuwa hai’ kwa wafu mwishoni mwa utawala wa miaka elfu, kama kunavyotajwa katika Ufunuo 20:5, hakuwezi kukatumiwa kwa ufufuo huo wa wafu katika Kuzimu (Hades, NW). Basi, limepaswa lielewekeje (iwapo ni sehemu hasa ya andiko la Biblia lililoongozwa na roho ya Mungu)?

Biblia inaonyesha kwamba hata walio hai wanaweza kuonwa kama ‘wafu’ kulingana na maoni ya Mungu. Yesu Kristo alisema hivi: “Waache wafu wazike wafu wao.” (Mt. 8:22) Vile vile alizungumza juu ya wale wenye kumkubali kwa kuamini kama ‘wakipita kutoka mautini kuingia uzimani.’ (Yohana 5:24) Vivyo hivyo, mtume Paulo, akiwataja wale wanaotazamiwa kuwa na utawala wa kimbinguni, aliandika hivi: “Na ninyi mlipokuwa mmekufa kwa sababu ya makosa yenu na kutokutahiriwa kwa mwili wenu, aliwafanya hai pamoja naye [Kristo].”​—Kol. 2:13.

Kwa hiyo yaweza kuonekana kwamba mtu hawi hai kulingana na maoni ya Mungu mpaka wakati anapokuwa huru na laana inayotokana na hali ya dhambi. Kwa habari ya wale watakaotawala na Yesu Kristo, kwa msingi wa dhabihu ya Mwanawe Yehova Mungu “huwatangaza kuwa wenye haki” na hivyo anawaona kama wakamilifu, bila ya dhambi, wanapokuwa wangali na mwili wa nyama duniani. (Rum. 8:33, NW) Walakini, wengine wa wanadamu, kutia na watakaofufuliwa duniani mnamo utawala wa miaka elfu wa Kristo, hawatawekwa huru mara ile ile na maelekeo ya dhambi na matokeo yake yenye kufisha. Kwa kweli, kama faida za ukombozi wa Kristo zisingetumiwa kwao wajifaidi nazo, hao waliofufuliwa duniani wangekufa tena. Kwamba ukombozi wa maelekeo yenye dhambi mwishowe utatukia mnamo utawala wa miaka elfu wa Kristo yahakikishwa katika 1 Wakorintho 15:24-28, NW. Hapo twasoma kwamba “adui wa mwisho, mauti,” atakapokwisha kubatilishwa ndipo Yesu ‘atakapoukabidhi ufalme kwa Mungu wake na Baba.’ Huku ‘kukabidhiwa kwa ufalme’ kusingeweza kutukia mpaka utawala wa miaka elfu wa Kristo umalizike. Baada ya hapo Shetani atafunguliwa kutoka shimoni naye ataruhusiwa atiishe wanadamu kwenye jaribu la mwisho.​—Ufu. 20:3, 7-10.

Wale watakaopita jaribu hili watatangazwa kuwa wenye haki na kupewa zawadi ya uzima wa milele. Kwa njia hiyo ‘watakuwa hai’ kwa maana ya kuhesabiwa haki au kutangazwa wenye haki kustahili uzima wa milele. Dhambi wala matokeo yake yenye kufisha haitatenda kazi ndani yao tena. Watakuwa hai kama washiriki wa jamaa ya Mungu, ‘wakiwa huru na kutolewa katika utumwa wa uharibifu, hata viingie katika uhuru wa utukufu wa Mungu.’​—Rum. 8:21.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki