Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w74 8/1 kur. 357-358
  • Je! Watu Wanakuona Wewe Kuwa “Mpole na Mnyenyekevu wa Moyo”?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Watu Wanakuona Wewe Kuwa “Mpole na Mnyenyekevu wa Moyo”?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • ROHO IFAAYO INAMFANYA MTU AWE ANAYEWEZA KUFIKIWA NA WENGINE
  • “Jifungeni Hali ya Akili ya Kujishusha Chini”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • Je! Wewe Unaambilika Kweli?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Jivikeni Upole!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • “Umati Mkubwa Ukamkaribia”
    ‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
w74 8/1 kur. 357-358

Je! Watu Wanakuona Wewe Kuwa “Mpole na Mnyenyekevu wa Moyo”?

LO! MANENO ya Mwana wa Mungu yanapendeza namna gani: “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha . . . kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu.” (Mt. 11:28, 29) Je! sisi tunajitahidi tuwe kama yeye?

Wanaume wanaotumikia kama waangalizi (wazee) katika kundi la Kikristo watafahamu kwamba haja ya watu ya burudisho haimaliziki kwa kujienda mara wamalizapo kujielekeza kwenye Mwana wa Mungu na kuwa wanafunzi wake. Wakiwa wanaishi katika hali za ulimwengu zilizopo zenye kulemea, wanafunzi wa Kikristo wanapatwa kila siku na magumu mengi ambayo lazima watu kwa jumla wayavumilie. Zaidi ya hayo, huenda wakawa ‘wakitaabika kwa ajili ya haki’ inapokuwa lazima wavumilie upinzani kutoka kwa wenzi na jamaa wasioamini, kutoka kwa matajiri, wafanya kazi wenzao, wanashule au kutoka kwa vyanzo vingine. Wanaweza kufaidika kutokana na wazee wafadhili na wakarimu kama nini!

Ndiyo, kwa kuwa wazee wanaiwakilisha serikali ya ufalme wa Kristo, imewapasa wajitahidi kutenda kulingana na masimulizi ya “wakuu” yanayotolewa katika Isaya 32:1, 2, wakiwa wenye kuburudisha “kama mahali pa kujificha na upepo, na mahali pa kujisitiri na dhoruba; kama mito ya maji mahali pakavu, kama kivuli cha mwamba mkubwa katika nchi yenye uchovu.”

ROHO IFAAYO INAMFANYA MTU AWE ANAYEWEZA KUFIKIWA NA WENGINE

Bila shaka, ili tuwe hivyo lazima tuwe watu wawezao kufikiwa na wengine bila kizuizi. Pengine twaweza kudhani ndivyo tulivyo. Lakini ingefaa kila mmoja wetu ajiulize maulizo kama haya: ‘Ni watu wa namna gani wanaonifikia mimi? Je! kati yao wamo wanyenyekevu na hata wenye haya? Namna gani ikiwa wale wanaonifikia ni wale wenye kuvutia zaidi​—pengine hata watu wanaoelekea kusifu-sifu kwa uongo au, kwa upande mwingine, wanaoelekea kulaumu-laumu bila kuogopa? Hii isingeonyesha mtu anaweza kufikiwa kwa hiari.’​—Yak. 4:6.

Mengi yanategemea roho tunayoionyesha. Maneno ya Yesu katika Mathayo 20:25-28 yanakataza wanafunzi wake wasiwe na roho ya watu wa kilimwengu ya mamlaka. Hakuna nafasi ya kujiona kuwa wakuu na kujitenga na wengine​—sivyo iwapo udugu wa kweli utakuwapo. Ndivyo ilivyo na kwa ‘unyenyekevu wao wa uongo.’ Bila shaka tumewaona watu Wenye vyeo vya juu vya kilimwengu wanaotaka waonekane kana kwamba wananyenyekea wawe kama watu wasio matajiri. Na hali maoni yao ya ukuu yanajionyesha katika njia fulani ili wakukumbushe cheo chao, wasikuache kamwe usahau ‘wao ni akina nani hasa’ usije ukajiona mwenye hiari sana ya kushughulika nao unapokuwa nao. Je! nyakati nyingine ndivyo tulivyo?

Wajapokuwa wanaonekana kuwa wenye tabia nzuri na wanaopendezwa na watu, ni mara nyingi namna gani ambapo watu wenye vyeo vya kilimwengu wanakuwa wanafiki. Namna ilivyo tofauti na mfano wa Mwana wa Mungu! ‘Upole wake na unyenyekevu wa moyo’ havikuwa maneno matupu. Wale ‘waliomjia yeye’ waliona kwamba ukaribishaji wake ulikuwa wa kweli kwa vile alivyowatendea.

Shauri zuri la mtume Paulo katika Warumi 12:16 (New English Bible) linafaa kweli hapa: “Angalianeni kila mtu na mwenzake kama vile mnavyojiangalia wenyewe. Msiwe wenye kiburi, bali enendeni na watu wanyenyekevu [mwongozwe pamoja na vitu vinyenyekevu, New World Translation]. Msiendelee kufikiria namna mlivyo wenye hekima.” Kama watu wenye vyeo vya madaraka wangezidi kushirikiana na wale wenye vyeo kama hivyo peke yao, au na watu wanaofanikiwa katika mambo ya kimwili, je! hii isingetokeza kizuizi kati yao na wale waliomo kati ya “watu wanyenyekevu”? Na, kwa habari ya waangalizi wa Kikristo, hii ingeweza kuzuia wasiwe na ufahamu mzuri wa maoni na haja za ndugu zao. Ingeweza kuwafanya wasizifahamu hali zenyewe. Kwa kweli, kufanyiza “tofauti za vyeo” za namna yo yote kunadhuru afya ya kiroho ya kundi linaloongozwa na Mwana wa Mungu.​—Yak. 2:1-9, NW.

Lazima tujihadhari tusije tukawa wenye hekima wala ‘wenye busara machoni petu wenyewe,’ tukiona kwamba uamuzi wetu, uwezo na njia za kufanya mambo ni bora kupita za wenzetu, kwa maana hii ingeweza kujionyesha wazi kwa usemi na mwenendo. (Rum. 12:16, NW; Luka 6:45) Unyenyekevu wa moyo wa Yesu uliwavuta watu kwake. Wazee wa Kikristo wanayo sababu kubwa zaidi ya kuwa na unyenyekevu, kwa maana, tofauti na Mwana wa Mungu, wao ni wasiokamilika kama wanadamu; wanafanya makosa.

Jaribu la unyenyekevu wao wa moyo laweza kuwa wakati wanapoonyeshwa kosa au wakati mzee mwenzao au mtu mwingine anapotoa shauri la maendeleo katika mpango fulani wa kundi. Mtu aliye “mnyenyekevu wa moyo” hataelekea kuyaona mashauri hayo kama jambo la kipekee, kama kulaumiwa kwa makusudi yake au njia ya kufanya mambo. Kufanya hivyo kungeweza kuwafanya wanyenyekevu waanze kuogopa kumfikia yeye. (Mhu. 7:9) Imempasa awe mwenye nia ya kupokea shauri na kulitoa vile vile. (Rum. 2:21) Kwa njia hiyo anaonyesha yeye si kama wale wakuu wa Israeli walioanza kujiona kama “miungu” kati ya watu, kama wasiohitaji kushauriwa au kusahihishwa kwa vile walivyo wazuri. (Linganisha Zaburi 82:6, 7; Isaya 40:13, 14.) “Kondoo” watawafikia “wachungaji” wapole kweli kweli wakiwa na matumaini ya kupokea mema tu.​—Zab. 23:1-6.

Bila shaka hakuna ye yote kati yetu anayetaka kuizidisha taabu aliyo nayo ye yote kati ya ndugu zetu bali, twataka kumburudisha. Na hali twaweza kuongezea mzigo wao tukiwa wenye haraka au wasiosubiri tunapofikiwa nao. Tukiwa tunajua kwamba “moyo wa mwenye haki hufikiri jinsi atakavyojibu,” haitupasi kukata maneno haraka haraka, kukaripia au kukemea, bila ya kulisikia shauri lote. (Mit. 15:28; 29:20; Yak. 1:19) Tungeweza kuongezea ugumu zaidi kwa maoni ‘yenye kulemea’ ya ndugu zetu tukionyesha shuku juu ya makusudi yao au tukifanya haraka kutoa maoni ya kwamba wao hawakuwa wakifanya wanayopaswa kuyafanya au kadiri ambavyo wamepaswa kufanya. Haitupasi kuwa na maelekeo ya ‘kutazamia mabaya zaidi’ bali, yatupasa ‘kutumainia matokeo yaliyo bora’ tukiongozwa na upendo.​—1 Kor. 13:7; Gal. 6:1.

Bila shaka wazee wale wanaokuwa kama Mwana wa Mungu katika upole wake na unyenyekevu wa moyo wanaweka mfano bora kwa kundi zima. (1 Pet. 5:3) Kwa hiyo, wale wanaowafikia wazee wa kundi imewapasa vile vile waonyeshe sifa njema izi hizi. Haiwapasi kuwa wenye kudai sana au wasio na adabu wanapowafikia ndugu hawa, wala kutaka watumie wakati wao bure tu, bila ya kufikiria wengine ambao huenda wakataka msaada wao. (Ebr. 13:17) Kuliko kuwa wenye haraka katika maneno yao au wasiosubiri, huenda wakaona yafaa kutafakari ulizo lao au ugumu mapema kuona kama kweli unafaa kuletwa kwa mzee. Huenda wakaona jibu linapatikana kwao tayari, likihitaji jitihada ndogo tu ya kipekee au funzo.

Lo! namna inavyoburudisha kuwamo kati ya watu wanaozionyesha sifa nzuri za Yehova Mungu na Mwanawe! Ndiyo, ni mwonjo wa namna maisha yatakavyokuwa katika taratibu mpya ya Mungu yenye haki inayokaribia.​—Zab. 133:1-3.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki