Wakati Uliotumiwa Vizuri
● Mashahidi wa Yehova wa Kikristo wanafahamu kwamba ibada ya kweli ni yenye thamani. Imewapa furaha ya kweli na kusudi katika maisha. Ndiyo sababu wana hamu ya kutumia wakati vizuri katika kuwaeleza wengine juu ya imani zao zenye msingi wa Biblia.
Chukua mfano wa mmoja wa mashahidi wa Yehova katika nchi ya Minnesota. Usiku mmoja alikuwa akifanya kazi na mwanamume mwingine juu ya jembe la kupakulia mchanga la umeme. Kwa kuwa kulikuwa na mvua kubwa usiku huo, wanaume wawili hao walitumia wakati mwingi katika gari kubwa wakijipasha moto na kujikausha. Walipokuwa wanaendelea kufanya kazi ya jioni mazungumzo yalielekea kwenye dini. Baada ya kujibu ulizo la mfanya kazi mwenzake juu ya mashahidi wa Yehova wanavyofanya juu ya upaji, Shahidi akataja funzo la nyumbani la Biblia na kusema hivi: “Hilo ni jambo ambalo imekupasa ujifaidi nalo. Halilipiwi pesa zo zote na twaweza kulifanyia nyumbani mwako mwenyewe wakati ukufaao.” Mfanya kazi mwenzake akajibu: “Wajua, nimekuwa nikifikiria hilo. Waweza kuja wakati gani?”
Matokeo ya wakati uliotumiwa vizuri katika mazungumzo ya Biblia yenye kujenga yalikuwa nini? Mfanya kazi huyo na mkewe pia walifanya maendeleo hata wao wenyewe wanasaidia wengine kupata maarifa ya Neno la Mungu wakiwa mashahidi wa Yehova walio wakf na waliobatizwa.