Kazi ya Kutaipu Iliyobadili Maisha
● Katika India, mmoja wa Mashahidi wa Yehova wa Kikristo aliyepewa mgawo wa kuhutubu katika “Ushindi wa Kimungu” Kusanyiko la Wilaya alipanga mfanya kazi mwenzake amtaipie (ampigie chapa) maandishi yake. Mfanya kazi huyo alivutwa sana na maandishi hayo hata akataka kujua kama yeye pia aweza kuhudhuria kusanyiko hilo. Bila shaka angeweza, naye alilihudhuria. Siku ya kwanza ilimvuta sana hata akaomba ruhusa ya kutokuwa afisini. Alipopewa ruhusa, alihudhuria kusanyiko lote. Baada ya hapo akaanza kujifunza Biblia kwa makini, akaanza kuhudhuria mikutano yote ya Mashahidi wa Yehova na karibuni akaanza kueleza wengine mambo aliyokuwa akijifunza. Ingawa ametoka katika jamaa yenye kushikamana sana na dini ya Kibanyani na ingawa amepingwa, amesimama imara akitaka kuwa mwanafunzi mwaminifu wa Yesu Kristo.