Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w74 9/15 kur. 411-414
  • Ni Ulinzi Gani kwa Watu wa Mungu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ni Ulinzi Gani kwa Watu wa Mungu?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • MATENDO YA MUNGU YANA KUSUDI
  • YANAYOTIWA KATIKA “DHIKI KUBWA”
  • WACHUKIAO WATU WA MUNGU WAOKOKA KWA KITAMBO
  • WOKOVU KWA ULINZI WA KIMUNGU
  • Endelea Kuwa Mwaminifu Wakati wa “Dhiki Kuu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2019
  • Ukombozi Kuingia Katika Ulimwengu Mpya Mwadilifu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Waokolewa Wakiwa Hai Kupitia Dhiki Kubwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • ‘Kaeni Mkikesha na Mbaki Mkiwa na Fahamu Zenu’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
w74 9/15 kur. 411-414

Ni Ulinzi Gani kwa Watu wa Mungu?

YEHOVA Mungu aweza kuwalinda watu wake. Hakuna shaka juu yake, kwa sababu amefanya hivyo mara nyingi nyakati zilizopita. Lakini huenda ikatumikia kusudi lake nyakati nyingine kuwaacha wafe katika uaminifu kwake. Wakijua hivyo, wahamishwa watatu wa Kiebrania walimwambia Mfalme Nebukadreza wa Babeli hivi, wakikabiliwa na tisho la kufa katika tanuru ya moto: “Kama ni hivyo, Mungu wetu tunayemtumikia aweza kutuokoa na tanuru ile iwakayo moto; naye atatuokoa na mkono wako, Ee mfalme. Bali kama si hivyo, ujue, Ee mfalme, ya kuwa sisi hatukubali kuitumikia miungu yako, wala kuisujudia hiyo sanamu ya dhahabu uliyoisimamisha.”​—Dan. 3:17, 18.

Kwa sababu gani Yehova Mungu analinda wengine wa watumishi wake huku akiacha wengine wataabike na hata kufa? Je! itakuwa tofauti wakati “dhiki kubwa” itakapoanza juu ya hii taratibu ya mambo isiyomcha Mungu? Je! kila mtu mwenye hali yenye kukubalika mbele za Yehova ataokolewa, kwa mwujiza ikiwa lazima?

MATENDO YA MUNGU YANA KUSUDI

Yehova Mungu afanyapo jambo fulani, lina kusudi. Kwa hiyo haikuwa bila sababu nzuri kwamba Yehova akaacha watumishi wake wapatwe na mateso makali na wengine hata kupatwa na kifo kibaya sana. Sababu hiyo yahusu ulizo la maana katika ulimwengu wote. Kwa kweli, Shetani Ibilisi alidai kwamba hakuna ye yote kati ya viumbe vya Mungu vyenye akili aliyemtumikia kwa sababu ya upendo bali kwamba wote walivutwa na vitu ambavyo wao wenyewe walituzwa. Alizidi kushikilia kwamba vitu hivyo vikiondolewa, wangeacha kuwa watumishi waaminifu wa Mungu. Akimtaja Ayubu, Shetani alimwambia Mungu hivi: “Ngozi kwa ngozi, naam, yote aliyo nayo mtu atayatoa kwa ajili ya uhai wake. Lakini sasa nyosha mkono wako, uuguse mfupa wake na nyama yake, naye atakukufuru mbele za uso wako.”​—Ayubu 2:4, 5.

Wakati ulihitajiwa kulimaliza ulizo alilokuwa amelitokeza Shetani. Naye Yehova Mungu alimpa Shetani wakati ajaribu kulihakikisha dai lake na pia akamruhusu alete mkazo juu ya viumbe vyote vyenye akili. Kwa hiyo, katika muda wa historia, hakuna namna yo yote ya jaribu au mateso ambayo wengine wa watumishi wa Mungu hawakupatwa nayo. Mara nyingi Yehova ameruhusu kujaribiwa kufikie hatua ya kifo. Wakiufahamu uhalali wa upande wa Mungu wa ulizo, wengi wamekuwa wenye nia ya kuufia. Wameliona kama pendeleo kushiriki katika kushuhudiwa kwa jina la Mungu na kwa njia hiyo kulihakikisha dai la Ibilisi kuwa uongo. Mtume Paulo, aliyemtumikia Mungu kwa uaminifu kama mwanafunzi wa Yesu Kristo, alisema hivi: “Mimi, licha ya kufungwa, ni tayari hata kuuawa katika Yerusalemu kwa ajili ya jina lake Bwana Yesu.”​—Matendo 21:13.

Walakini, adui hakuruhusiwa wakati wo wote awafutilie mbali watu wote wa Mungu. Majaribio ya kuwaangamiza watu wa Mungu wa kale, Israeli, yalishindwa. Wakati Farao wa Misri alipojaribu kuliangamiza taifa la Israeli kwa kuagiza vitoto vyote vya kiume viuawe, alishindwa. (Kut. 1:15-21) Vivyo hivyo, wakati Hamani alipofanikiwa katika kupitishwa kwa amri ya kuangamiza Wayahudi wote wakati wa Milki ya Wamedi na Waajemi, kujitia kwa kimungu kuliileta hila yake kwenye hakuna.​—Esta 6:1–9:22.

Zaidi ya kuwaokoa watu wake kwa jumla, nyakati nyingine Yehova Mungu amewalinda watumishi wake mmoja mmoja. Mfano mmoja wa hili ni ukombozi wa ajabu sana wa wahamishwa watatu wa Kiebrania waliotajwa mapema kutoka katika tanuru ya moto. (Dan. 3:24-27) Kwa habari yao jaribu la ukamilifu wao lilikuwa la kutosha kuhakikisha uaminifu wao kwa kukabiliwa na kifo. Na uaminifu wao ulimpa Yehova Mungu nafasi nzuri kuuonyesha uwezo wake wa kuokoa. Kwa kweli, uwezo huo wa kuokoa ulikuwa umetiliwa shaka, kwa maana Mfalme Nebukadreza alikuwa amewaambia wale wanaume watatu hivi: “Naye ni nani Mungu yule atakayewaokoa ninyi na mikono yangu?” (Dan. 3:15) Kwa hiyo kwa kuwaokoa, Yehova alijifanyia sifa kuu, akimlazimisha Nebukadreza akubali: “Hakuna Mungu mwingine awezaye kuokoa namna hii.”​—Dan. 3:29.

Hivyo matendo ya Yehova wakati uliopita yafunua kwamba aweza kuwalinda watu wake kwa ujumla na kama watu mmoja mmoja. Lakini je! tutazamie kukombolewa kwa kila mmoja wa watumishi wake kuhusiana na “dhiki kubwa” itakayoijia taratibu mbovu iliyopo?

YANAYOTIWA KATIKA “DHIKI KUBWA”

Ili kujibu ulizo hili, lazima tujue yanayotiwa katika “dhiki kubwa.” Alipokuwa akiwaandikia Wakristo katika Thesalonike, mtume Paulo aliitaja hukumu ya Mungu ya kufisha juu ya wasiomcha yeye kama dhiki. Twasoma:

“Hii yakumbusha kwamba ni haki kwa upande wa Mungu kuwalipa dhiki wale wanaowaletea dhiki, lakini, kwenu ninyi mpatao dhiki, faraja pamoja nasi wakati wa kufunuliwa kwa Bwana Yesu kutoka mbinguni pamoja na malaika zake wenye nguvu katika moto uwakao, atakapoleta kisasi juu ya wale wasiomjua Mungu na wale wasiozitii habari njema juu ya Bwana wetu Yesu.”​—2 The. 1:6-8, NW.

Si watu mmoja mmoja peke yao na vikundi bali pia matengenezo ya duniani pote yamewaletea dhiki watu waaminifu wa Mungu. Kitabu cha Ufunuo chamtaja “mnyama” (anayefananisha taratibu ya kisiasa inayoonekana ya utawala wa ulimwengu ya Shetani) na ‘Babeli Mkuu’ (milki ya ulimwengu ya dini ya uongo) kama wakiwamo kati ya watesi wakali. Juu ya matendo maovu ya ‘Babeli Mkuu,’ tunaambiwa: “Nikamwona yule mwanamke amelewa kwa damu ya watakatifu, na kwa damu ya mashahidi wa Yesu.” (Ufu. 17:6) Na juu ya dhiki iletwayo na “mnyama,” twasoma: “Akafunua kinywa chake amtukane Mungu, na kulitukana jina lake, na maskani yake, nao wakaao mbinguni. Tena akapewa kufanya vita na watakatifu na kuwashinda, akapewa uwezo juu ya kila kabila na jamaa na lugha na taifa.”​—Ufu. 13:6, 7.

La kwanza kati ya matengenezo haya kushuka katika uharibifu ni ‘Babeli Mkuu.’ Kwa hiyo inaonekana kwa busara kwamba “dhiki kubwa” inaanza mara tu anapoingia katika shambulio linaloongoza kwenye kuangamizwa kwake kabisa.

WACHUKIAO WATU WA MUNGU WAOKOKA KWA KITAMBO

Vyombo vya kutimiza hili ni taratibu za kisiasa na watawala wazo. (Ufu. 17:16, 17) Hawa hawawapendi watu wa Mungu kama vile wasivyozipenda taratibu za kidini watakazoziharibu. Tayari kabla ya uharibifu wa ‘Babeli Mkuu’ hizi taratibu za kisiasa zinakuza kumbukumbu la matendo ya jeuri juu ya watumishi wa Yehova. Kuchukua kwao hatua juu ya ‘Babeli Mkuu’ hakubadili nia yao ya kupinga dini. Hii ni wazi kutokana na uhakika wa kwamba Biblia inawaonyesha kama wamejipanga kupigana na Mfalme Yesu Kristo.​—Ufu. 19:11-16, 19.

Halafu, tena, wengine watakaookoka uharibifu wa ‘Babeli Mkuu’ wanajutia hasara ya mambo ya kimwili inayowapata anapoharibiwa, kwa maana wanaonyeshwa wakimwomboleza. (Ufu. 18:9-23) Watu hawa walipata faida kutokana na ‘Babeli Mkuu’ nao wakakubali kumwaga kwake damu yenye haki. Walicho nacho ni chuki tu kwa watu wa Mungu na, wasipotaka dini yo yote iokoke, je! hawatajaribu kuionyesha hasira ya uuaji juu ya watumishi waaminifu wa Mungu? Kama Gogu wa nchi ya Magogu wataona uchungu juu ya ufanisi wa kiroho wa waabudu wa Yehova.​—Eze. 38:1-18.

Twaweza kuwa na uhakika wa kwamba wafanya biashara watakaookoka wenye kushughulika na ‘Babeli Mkuu’ na pia watu waliouleta uharibifu wake moja kwa moja hawatataka kujiweka chini ya utawala wa Kristo. Kama wanadamu hawawezi kupigana moja kwa moja na Yesu Kristo na majeshi yake ya kimalaika. Lakini wanaweza kumpinga Kristo kwa kuwashambulia wanafunzi wake duniani. Hii ni kupatana na kanuni zilizonenwa na Yesu: “Kadiri mlivyomtendea mmojawapo wa hao ndugu zangu walio wadogo, mlinitendea mimi.” “Kadiri msivyomtendea mmojawapo wa hao walio wadogo, hamkunitendea mimi.”​—Mt. 25:40, 45.

Kwa sababu ya kumbukumbu la Shetani la wakati uliopita na la taratibu zisizomcha Mungu zinazoongozwa naye, je! tudhani kwamba adui za Mfalme Yesu Kristo watajizuia wasiwajilie raia zake waaminifu duniani? Bila shaka sivyo! Twaweza kutazamia shambulio kamili, ambalo lingeweza kufanya wengine wa watumishi wa Mungu wafe. Kwa kweli, kitabu cha Biblia cha Ezekieli kinatabiri shambulio hilo chini ya uongozi wa “Gogu” wa mfano, Shetani Ibilisi:

“Nawe [Gogu] utakuja kutoka mahali pako, kutoka pande za mwisho za kaskazini, wewe, na watu wa kabila nyingi pamoja nawe, wote wamepanda farasi, kusanyiko kubwa, na jeshi kuu; nawe utapanda juu uwajilie watu wangu.”​—Eze. 38:15, 16.

Walakini, wengine kati ya watu wa Mungu wakifa wakati wa shambulio hili hawataangamia milele. Watakufa, si kwa kujiona wamepoteza upendeleo wa Mungu, bali wakiwa na matumaini kamili kwamba Mungu atawafufua katika taratibu mpya yake kwa sababu ya uaminifu wao kwake. Hata hivyo, shambulio hilo juu ya watu wa Mungu halitafikia upeo. Litakomeshwa kwa nguvu. Neno la Yehova, kupitia kwa Ezekieli, laendelea kusema hivi:

“Nami nitaita upanga, uje juu yake katika milima yangu yote, asema Bwana [Yehova]; nao upanga wa kila mtu utakuwa juu ya ndugu yake. Nami nitamhukumu kwa tauni, na kwa damu; nami nitanyesha mvua ifurikayo, na mvua ya mawe makubwa sana, na moto na kiberiti juu yake, na vikosi vyake, na watu wa kabila nyingi walio pamoja naye.”​—Eze. 38:21, 22.

Kwa kuwa nguvu za asili zitatumiwa juu ya washambuliaji, njia fulani za kutumikia watu zilizo za lazima zitavunjwa. Hii italeta matatizo ya kimwili juu ya kila mtu, kutia na watumishi wa Mungu. Kwa sababu ya magonjwa au udhaifu mwingine wa kimwili, mkazo wa hali hiyo huenda ukawa mwingi mno kwa wengine wasiweze kuvumilia na kwa hiyo wengine wa watu wa Mungu huenda wakafa. Wakati uo huo twajua kwamba Yehova Mungu aweza kuwatia watu wake nguvu na kuwakinga ujapokuwa udhaifu wao. Lakini, kwa habari ya kadiri ambavyo huenda yeye akaona yafaa kufanya hivyo, inatupasa tungoje tuone. Hata hivyo, Yehova mwenyewe siye anayewaua waabudu wake waaminifu.

Ijapokuwa wakati barabara hatuujui, hali zenye kutaabisha hazitaendelezwa. Hii yaonyeshwa na yaliyoupata Yerusalemu wa kale mwaka wa 70 C.E. Dhiki iliyowapata wakaaji wa mji huo uliozingirwa ‘ilifupizwa,’ ikifikia kikomo chake baada ya muda unaopungua miezi sita.​—Mt. 24:21, 22.

WOKOVU KWA ULINZI WA KIMUNGU

Wakati “dhiki kubwa” itakapoiharibu taratibu hii isiyomcha Mungu bila shaka watakuwako waokokaji. Kwa kweli, Biblia inataja “mkutano mkubwa” ambao “wanatoka” au kuokoka hii “dhiki kubwa.” (Ufu. 7:9, 14) Yehova Mungu hatawaruhusu wachukiao watu wake waonyeshe hasira yao kufikia hatua ya kuwaangamiza kabisa. Kwa kumtumia Mwanawe na majeshi ya kimalaika, atakuja kuwakinga watu wake, akiwaokoa wasiangamizwe kabisa. Kwa kuwa wao ni “waaminifu” wake, kifo chao kama jamii ya watu kingekuwa chenye “thamani” mno, chenye hasara mno, machoni pake. (Zab. 116:15, NW) Pia watakingwa wasiuawe katika hukumu ya kimungu. Yesu Kristo wala majeshi yake ya kimalaika hawatakosea. Hakuna ye yote wa watumishi wa Mungu atakayefutiliwa mbali pamoja na waovu.

Kufikilizwa kwa hukumu ya Mungu kwa wakati uliopita kwahakikisha hili. Nuhu na jamaa yake waliokoka gharika iliyowaharibu wasiomcha Mungu. Lutu na binti zake, kwa kujifaidi na nafasi ya kuokoka kupatana na amri ya kimungu, hawakutoweka pamoja na wakaaji wa Sodoma na Gomora.

Zaidi ya hayo, mtunga zaburi, yaelekea Musa, alimkubali Yehova kama kimbilio na ngome yake. Akiwa na matumaini katika uwezo wa Mungu wa kulinda watu wake kama kundi, aliandika hivi:

“Nitasema, [Yehova] ndiye kimbilio langu na ngome yangu, Mungu wangu nitakayemtumaini. Maana Yeye atakuokoa na mtego wa mwindaji, na katika tauni iharibuyo. Kwa manyoya yake atakufunika, chini ya mbawa zake utapata kimbilio; uaminifu wake ni ngao na kigao. Hutaogopa hofu ya usiku, wala mshale urukao mchana, wala tauni ipitayo gizani, wala uele uharibuo adhuhuri, ijapo watu elfu waanguka ubavuni pako. Naam, kumi elfu mkono wako wa kuume! hata hivyo hautakukaribia wewe. Ila kwa macho yako utatazama, na kuyaona malipo ya wasio haki.”​—Zab. 91:2-8.

Kwa kweli, basi, hatuna haja ya kuogopa kuja kwa “dhiki kubwa.” Twaweza kuwa na matumaini yote katika ulinzi wa kimungu. Hata wengine wakifia mikononi mwa adui, kifo chao kitasaidia kulishuhudia jina takatifu la Mungu. Je! upendo wako ni bora kwamba, ukikabiliwa na kifo, ungelihesabu kama pendeleo kumhakikishia yeye uaminifu wako bila ya kujali hasara yenyewe? Msimamo huo imara ungemtukuza Yehova nao ungelikanusha dai la Shetani kwamba utumishi wako kwa Mungu msingi wake ni vitu unavyotuzwa.

Jambo moja twalijua wazi: Yehova Mungu hataacha kamwe watumishi wake waaminifu wafutiliwe mbali kutoka duniani. Na hakuna hata mmoja wao atakayetoweka mikononi mwa Yesu Kristo au mwa majeshi yake yenye kufisha. “[Yehova] ajua kuwaokoa watauwa na majaribu, na kuwaweka wasio haki katika hali ya adhabu hata siku ya hukumu.” (2 Pet. 2:9) Pia anajua namna ya kuthawabisha wale wanaoonyesha uaminifu wao kwake zaidi sana kuliko wanavyotarajia. Na tupatikane kati ya wale watakaokuwa upande wake wakati “dhiki kubwa” itakapoufyatukia ulimwengu huu mwovu ulio chini ya uongozi wa Shetani Ibilisi.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki