Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w77 4/15 kur. 191-192
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
  • Habari Zinazolingana
  • ‘Kunyakuliwa Ili Kumlaki Bwana’—Jinsi Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • “Waliokufa Katika Kristo Watafufuliwa Kwanza”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • Faraja Kotoka kwa Yule Mungu wa Amani
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • “Nina Tumaini kwa Mungu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2017
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
w77 4/15 kur. 191-192

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

● 1 Wathesalonike 4:17 ina maana gani inaposema, ‘Sisi tulio hai, tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja katika mawingu, ili tumlaki Bwana hewani’?​—U.S.A.

Wanaotajwa hapa ni warithi wenzi wa Yesu Kristo wanaoishi wakati wa kuwapo kwake katika mamlaka ya Ufalme.

Mstari huo unafahamika zaidi kwa kuulinganisha na habari ambayo mtume Paulo alikuwa akizungumza alipoandikia Wathesalonike. Twasoma hivi: “Ndugu, hatutaki msijue habari zao waliolala mauti, msije mkahuzunika kama na wengine wasio na matumaini. Maana, ikiwa twaamini ya kwamba Yesu alikufa akafufuka, vivyo hivyo na hao waliolala katika Yesu, Mungu atawaleta pamoja naye. Kwa kuwa twawaambieni haya kwa neno la Bwana, kwamba sisi tulio hai, tutakaosalia hata wakati wa kuja kwake Bwana, hakika hatutawatangulia wao waliokwisha kulala mauti. Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu; nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza. Kisha sisi tulio hai, tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu, ili tumlaki Bwana hewani; na hivyo tutakuwa pamoja na Bwana milele. Basi, farijianeni kwa maneno hayo.”​—1 The. 4:13-18.

Inaweza kuonekana kwamba jambo linalozungumzwa ni kufufuliwa kwa warithi wenzi wa Kristo. Warithi wote wenzake waliokufa kabla ya kuwapo kwake katika mamlaka ya Ufalme walibaki wamelala katika kifo. Lakini, baada ya kuwapo kwake kuanza, wafu hao wote wangefufuliwa wawe na uzima wa kiroho usiokufa, wakaungane na Bwana wao. Hilo lilikuwa wazo lenye kufariji Wakristo wa Thesalonike kweli kweli kwa sababu ya dhiki walizokuwa nazo!​—1 The. 1:6.

Lakini hatuna sababu inayolingana na Maandiko ya kuazimia kwamba Yesu alipaswa kupanda mbinguni kwa njia halisi na kwamba wanadamu duniani watawaona wanaolala katika kifo wakifufuliwa na kutukuzwa. Kwa sababu gani hatuna? Kwa sababu Yesu Kristo, akiwa mtu wa kiroho mbinguni, “amekaa katika nuru isiyoweza kukaribiwa.” “Hakuna mwanadamu aliyemwona, wala awezaye kumwona” katika hali hiyo. (1 Tim. 6:16) Kwa hiyo hali yake inaweza kulinganishwa na ya Baba yake wa mbinguni. (Ebr. 1:2, 3) Kwa hiyo Yesu Kristo ‘ashuka’ katika maana ile ile ambayo Biblia yamtaja Yehova Mungu akishuka. Kwa mfano, Maandiko Matakatifu yanasema juu ya Yehova hivi: “Aliziinamisha mbingu akashuka; kukawa na giza kuu chini ya miguu yake.” (2 Sam. 22:10) “Angalieni, [Yehova] anakuja akitoka mahali pake, naye atashuka, na kupakanyaga mahali pa dunia palipoinuka.” (Mik. 1:3) Ni wazi kwamba Mungu hakuacha mahali anapokaa katika mbingu zisizoonekana, bali kwamba alielekeza fikira zake juu ya wanadamu duniani, akawaonyesha uwezo wake. Vivyo hivyo, katika kuwapo kwa Yesu Kristo, yeye angeelekeza fikira zake duniani na kutumia uwezo wake kufufua warithi wenzake wanaolala katika kifo, kama mtume Paulo alivyoonyesha.

Je’ wangeonekana na wanadamu wakifufuliwa? Haiwezi kuwa hivyo. Kwa sababu gani? Kwa sababu ‘wameunganika na Yesu Kristo kwa mfano wa kufufuka kwake.’ (Rum. 6:5) Wanapata ufufuo kama wake. Kwa habari ya ufufuo wa Yesu, Maandiko yatuambia kwamba “alihuishwa katika roho.” (1 Pet. 3:18, NW) Ili Yesu aweze kuonekana na wanafunzi wake, ilimpasa kuvaa mwili wa kibinadamu. Hiyo ilisaidia kuwahakikishia kwamba kweli alikuwa amefufuliwa. (Matendo 1:3) Hata hivyo, wanadamu hawakuona akifufuliwa. Walinzi waliokuwa katika kaburi la Yesu ‘walitetemeka, wakawa kama wafu,’ kwa sababu ya malaika aliyelibingirisha jiwe kutoka kaburini, si kwa sababu ya kumwona Yesu aliyefufuliwa.​—Mt. 28:3, 4.

Vivyo hivyo, ufufuo wa warithi wenzi wa Yesu Kristo hauonekani. Lakini, Maandiko hayaonyeshi watabaki katika ujirani wa dunia halafu mara wafufuliwapo tu wajifunue kwa waamini wenzao kwamba wako hai.

Kwa kutegemea msingi huo, tunaweza kufahamu kwamba walio hai wanapotajwa kuwa ‘watanyakuliwa’ hiyo haiwezi kumaanisha kwamba miili yao ya nyama na damu itaanza kuelea juu ikutane na Bwana Yesu Kristo katika kile kinachoitwa na watu wengine “upeo wa raha.” Yeye hatakuwa katika hewa halisi juu ya wingu halisi, kwa maana “amekaa katika nuru isiyoweza kukaribiwa” katika mbingu zilizo juu zaidi, makao ya kiroho yasiyoonekana. Hata hivyo, ‘kunyakuliwa’ bila shaka kunahusiana na jambo ambalo latukia kuhusu ufufuo.

Je! lahusiana na ‘kunyakuliwa’ kwao kutoka ulimwengu wa wanadamu uliohukumiwa kuangamia? Je! lamaanisha kutukuzwa kwao, ‘kuketishwa pamoja na Kristo Yesu’ kwa sababu wamepewa urithi wa mbinguni pamoja naye? (Efe. 1:3; 2:6) Sivyo, hivyo sivyo Paulo alivyokuwa akisema katika barua aliyoandikia Wathesalonike.

Mtajo wa ‘kunyakuliwa’ ulikuwa jambo ambalo Wakristo Thesalonike wangeweza kutumia wao kwa wao kufarijiana, warithi wenzi wa Yesu wakifa. Kwa wazi, uhakika wa kwamba warithi wenzake wametenganishwa sasa na ulimwengu uliohukumiwa kuangamia sio hasa unaofariji wakati kifo kinapotokea katika kundi la watu wa Mungu. Halafu, tena, kutenganishwa kwa njia hii na kuunganishwa na Yesu katika maana ya kiroho kusingeweza kumaanisha ‘kuwa pamoja na Bwana milele.’ Warithi wenzi wa Kristo waishapo kumaliza mwendo wao wa kidunia, hali hiyo inakwisha, kwa maana wafufuliwapo wakati huo wao wenyewe watakuwa pamoja na Bwana wao milele. Bila shaka, ulimwengu uliohukumiwa utaangamia pia. Tena, huenda mtu sasa akiwa duniani akawa ametenganishwa na ulimwengu kwa muda lakini baadaye apoteze thawabu ya kuwa pamoja na Bwana Yesu Kristo kwa sababu ya kutoaminika.​—Ufu. 2:10.

Kwa hiyo, maneno ambayo Paulo aliandikia Wathesalonike yaonyesha kwamba kuna tofauti kati ya ufufuo wa wale waliokufa kabla ya kuwapo kwa Kristo katika mamlaka ya Ufalme na wale wanaomaliza mwendo wao wa kidunia na kufa wakati wa kuwapo kwake. Tofauti hiyo yaweza kufahamika kutokana na Ufunuo 14:13, ambapo twasoma: “Heri wafu wafao katika Bwana tangu sasa [yaani, tangu kuja kwake katika utukufu wa Ufalme]. Naam, [yasema roho], wapate kupumzika baada ya taabu zao; kwa kuwa matendo yao yafuatana nao.” Ingawa warithi wenzi wa Kristo waliokufa kabla ya kuwapo kwake walipaswa kulala katika kifo, wale wanaomaliza mwendo wao wa kidunia wakati wa kuwapo kwake hawalazimiki kufanya hivyo. Wanafufuliwa mara moja na kupewa uzima mbinguni. Wanapumzika baada ya taabu zao za duniani na kuingia moja kwa moja katika utumishi wa mbinguni. Wakiwa watu wa kiroho wasioonekana, ‘wananyakuliwa,’ kama kwamba wamo katika mawingu (ambayo ni ishara ya kutoonekana), wawe pamoja na Bwana wao asiyeonekana milele. Hiyo yapatana na maneno ambayo mtume Paulo aliandikia Wakorintho pia: “Hatutalala sote [yaani, hatutabaki katika hali ya kufa tukingojea ufufuo wakati ujao], lakini sote tutabadilika, kwa dakika moja, kufumba na kufumbua.”​—1 Kor. 15:51, 52.

Hivyo, maneno ambayo Paulo aliandika katika 1 Wathesalonike 4:13-18 yalikuwa yenye ujumbe huu wa lazima wenye kutia moyo: Wakristo waliotiwa mafuta wanaokufa kabla ya kuwapo kwa Bwana wanalala katika kifo. Kuwapo wanakongoja kukianza, wanafufuliwa na kupewa uzima wa mbinguni wawe viumbe vya kiroho visivyoweza kufa. Lakini, Wakristo waliotiwa mafuta walio hai wakati huo hawalali katika mauti. Wafapo wanabadilika papo hapo, wanapelekwa mbinguni wakawe na Kristo milele.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki