Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w74 12/1 kur. 546-549
  • “Nuru ya Ulimwengu” kwa Miaka 1,900

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Nuru ya Ulimwengu” kwa Miaka 1,900
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • NI AKINA NANI WALIO ‘NURU’ YA KWELI?
  • “TAA” NA “MAFUTA”
  • “BWANA ARUSI ALIPOKAWIA”
  • Sababu Kwa Nini Yesu Alitoa Mfano Wa “Wanawali Kumi”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Nuru ya Elimu Wakati wa “Umalizio wa Mfumo wa Mambo”
    Usalama Ulimwenguni Pote Chini ya “Mwana-Mfalme wa Amani”
  • Wale Wanawali Wenye Hekima na Wapumbavu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Hakuna “Upungufu wa Nguvu” wa Kiroho kwa Wenye Busara
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
w74 12/1 kur. 546-549

“Nuru ya Ulimwengu” kwa Miaka 1,900

Makala hii ni ya kutumia kwa mafunzo ya kitabu ya kundi

1-4. Je! sayansi imeunurisha ulimwengu kweli kweli?

NI Kikundi gani cha watu kilichounuririsha ulimwengu?

2 Wengine wanasema, ni wanasayansi. Vitabu vinaandikwa vikitoa historia ya uvumbuzi wa taratibu wa sayansi juu ya mafumbo ya “asili.” Nayo mavumbuzi yao yameleta nuru kwa njia fulani. Twajua mengi zaidi juu ya umbo la vitu, ulimwengu wote, mwili wa mwanadamu, chembe ya atom. Tuna njia bora za kufanyia mambo, kuwasiliana na usafirishaji wa haraka zaidi.

3 Lakini pia tunalo kombora la atomiki, silaha za vita zenye vijidudu vyenye kueneza maradhi. Msingi wa jamii yetu ni uchumi ambao ungekwisha njia za kufanyiza umeme na za usafirishaji zikikosekana. Mazingira yetu ya asili ni machafu na yaliyoharibiwa, kwa maana wanadamu hawana nuru ya kweli kuweza kuyatumia mavumbuzi kwa njia inayowafaidi wanadamu wote.

4 Ulizo laweza kuulizwa, Je! idadi ya watu wa ulimwengu ina furaha zaidi kwa sababu ya “maendeleo” ya sayansi chini ya usimamizi wa kibinadamu?

5. Je! dini za ulimwengu, hasa Kristendomu, inayojidai kuongoza, zimeunurisha ulimwengu?

5 Namna gani juu ya dini? Dini za Kristendomu zimeongoza katika kuwa ‘nuru,’ viongozi wake wakiwa wakuu kati ya ‘nuru’ ya ulimwengu huu. Lakini je! zinawapa watu au serikali uongozi wo wote wa kweli katika wakati huu wenye magumu ya namna zote? Je! zimewaleta watu karibu na Mungu zaidi na sifa za kimungu za upendo na amani?

NI AKINA NANI WALIO ‘NURU’ YA KWELI?

6. Yesu alimaanisha nini alipowaambia wasikiaji wake hivi: “Ninyi ni nuru ya ulimwengu”?

6 Kwa hiyo, Yesu Kristo alimaanisha nini alipowaambia wenye kumsikiliza hivi: “Ninyi ni nuru ya ulimwengu”? (Mt. 5:14) Mitume wake na wanafunzi wake bila shaka walikuwa “nuru” wakati wa karne ya kwanza. Lakini ni nani ambao wangewafuata wao kama “nuru”? Ni wale ambao wangekifuata kielelezo cha Yesu na mitume wake. Wangewapa watu nuru ya ufahamu juu ya Mungu na makusudi yake. Wangewaleta watu karibu na Mungu zaidi. Agizo lao halikuwa kuugeuza ulimwengu mzima. Lakini habari njema za ufalme wa Mungu walizozitangaza zingeleta amani kwa wale wenye kuzisikia na kuzitii, nazo zingewawezesha waishi maisha zenye furaha sasa, furaha kamili ikiwajia wao, na wanadamu chini ya utawala huo wa Ufalme. Watu hawa wenye nuru wangekuwa na kusudi la kuishi na wangetia kusudi katika maisha za wale wanaousikia ujumbe wao.

7, 8. Mfano wa ngano na magugu unatusaidiaje tuelewe ni akina nani hasa waliotumikia kama “nuru”?

7 Katika mfano wa ngano na magugu Yesu alionyesha kwamba wakati wote wa vizazi wangekuwako wengine ambao wangekuwa wakiishi kama Wakristo wa kweli. Hawa wasingekuwa wakuu wa ulimwengu. (1 Kor. 1:26-28) Wao wangekuwa wakimtumikia Mungu wa kweli, wakati ule ule kungekuwako jeshi la Wakristo wa uongo wakijionyesha kuwa “nuru.”​—Mt. 13:36-42.

8 Yesu alisema jamii hizi mbili zingeendelea kuwapo, bila ya kupambanuliwa vizuri moja kwa nyingine, mpaka wakati wa “mavuno,” ambao ni “mwisho wa dunia.” Halafu zingetenganishwa kabisa. “Ndipo,” alisema, “wenye haki watakapong’aa kama jua katika ufalme wa Baba yao.”​—Mt. 13:43.

9. Mungu amekuwa akifanya kazi gani tangu kupaa kwa Kristo mbinguni?

9 Kwa hiyo, wakati wa kipindi hicho kirefu cha zaidi ya miaka 1,900 tangu kupaa kwa Kristo mbinguni, Mungu amekuwa mteuzi sana. Yeye hakuwa akijaribu kuuokoa ulimwengu. Kuokolewa kwa wanadamu wote watakaoziitikia amri za Mungu kwa utii kutatimizwa wakati wa utawala wa Kristo wa miaka elfu juu ya dunia. Wakati wa kipindi cha miaka 1,900 iliyopita Mungu amekuwa akiwachagua wale watakaokuwa wafalme na makuhani pamoja na Kristo na watakaotawala wakati wa hiyo miaka elfu kuwaletea wanadamu baraka. Baraza hii yenye kuongoza ya kifalme itakuwa kikundi cha kimbinguni nacho hesabu yacho ni watu 144,000 tu. (Ufu. 7:1-8; 14:1-4; 20:4, 6) Bila shaka kuchagua hawa kati ya wanadamu kwa kipindi cha zaidi ya miaka 1,900 kumehitaji uchaguzi mzuri. Hawa waliochaguliwa wakati wa hiyo miaka 1,900 wametumikia kama nuru kwa wale waliosikia na kufahamu na ambao mioyo yao ilikuwa yenye tamaa yenye nguvu ya kumtumikia Yehova Mungu. Wenye kufahamu nao wamekuwa washiriki wa kikundi hicho kilichochaguliwa.

10, 11. (a) Ni nini kinachofananishwa na mfano wa wanawali, na kwa sababu gani walikuwa kumi? (b) Mfano ulianza kutimia wakati gani?

10 Mfano wa “wanawali kumi” waonyesha mwendo wa wale ambao wamekuwa “nuru ya ulimwengu” kweli kweli. Wamekuwa ndio wale ambao wamekubali wajibu wa kufanya kama Yesu alivyosema: “Nuru yenu na iangaze mbele ya Watu, wapate kuyaona matendo yenu mema, wamtukuze Baba yenu aliye mbinguni.” (Mt. 5:16) Kwa hiyo inakuwa wazi wale “wanawali kumi” wa mfano katika Mathayo 25:1-12 ni akina nani.

11 Kwa kuwa “wanawali” ni kumi, hesabu inayosimamia ukamilifu katika mambo ya kidunia, kama jamii, wanawafananisha Wakristo wote watakaoupata au wanaodai wataupata ufalme wa kimbinguni kama warithi wenzi wa Yesu Kristo. Mfano huo ulianza kutimia siku ya Pentekoste ya mwaka wa 33 C.E. Namna gani hivyo? Huo ndio wakati ambao wa kwanza walizaliwa kwa roho, wakawekwa katika cheo cha kuwa “warithi wa Mungu, warithio pamoja na Kristo.”​—Rum. 8:17.

12. Kwa sababu gani warithi wenzi wa Yesu wanafananishwa na “wanawali” katika mfano huu na hali wao ni “wana”?

12 Wao ni wana wa kiroho, lakini katika mfano wanaonyeshwa kama wanawali. Hii ni kwa sababu wanaelekea kuwa “bibi-arusi” wa Bwana-arusi mkuu, Yesu Kristo, kama kikundi au jamii. (Yohana 3:28-30; Ufu. 19:7-9; 21:9-11; Efe. 5:23-27; linganisha Mathayo 22:1-14.) Mfano unaendelea kutimia muda wote wa miaka 1,900 kufikia wakati wa “mavuno” hata wakati wa kukoma kwayo.

13. Ni jambo gani la maana juu ya uhakika wa kwamba wanawali watano wa mfano walikuwa “wenye busara” na watano “wapumbavu”?

13 Walikuwako wanawali watano “wenye busara” na watano “wapumbavu.” Kuwako kwa hesabu inayolingana kila upande kwaonyesha kwamba wote walipata nafasi inayolingana na pia kwaonyesha kwamba kusingekuwako kwa lazima wengi zaidi wa namna moja kuliko wa namna nyingine. Walakini, uhakika wa kwamba walikuwa “wapumbavu” waonyesha kwamba si wote wale wanaoanza wakiwa “wanawali” wangeonekana mwishowe kustahili kukubaliwa kwenye “karamu ya arusi ya Mwana-Kondoo.”​—Luka 12:35-38.

“TAA” NA “MAFUTA”

14. Katika utimizo, ni nini kilichofananishwa na “taa”?

14 Wale wanawali walikuwa na taa (kama ilivyokuwa desturi katika arusi hizo za kale). Wote walijua kwamba wangezihitaji taa hizi zikiwaka mpaka mwisho wa maandamano ya arusi, ili kujulisha wao ni akina nani na kuruhusiwa waingie katika karamu ya arusi. Kwa hiyo wangehitaji mafuta ya kutosha kudumu mpaka bwana-arusi atokee, na saa nyingi zingeweza kupita kabla hajatokea. Hii yamaanisha kwamba wanafunzi wa Kristo wenyewe wangekuwa kama taa zilizowashwa. Wangalipaswa wajulishwe ni akina nani kwa kuwa na utu wa kweli wa Kikristo na kuuendeleza na kwa kuangaza hivyo kama nuru katika huu ulimwengu uliotiwa giza. (2 Kor. 4:4; Isa. 60:2) Mtume Paulo alilionyesha hili alipowaandikia wachukua taa wenzake: “Yatendeni mambo yote pasipo manung’uniko wala mashindano, mpate kuwa wana wa Mungu wasio na lawama, wala udanganyifu, wasio na ila kati ya kizazi chenye ukaidi, kilichopotoka; ambao kati ya hao mnaonekana kuwa kama mianga katika ulimwengu, mkishika neno la uzima.”​—Flp. 2:14-16.

15. Ni nini kilichofananishwa na “mafuta”?

15 Ni nini kilichofananishwa na “mafuta”? Basi, ni nini chanzo cha nuru waliyo nayo Wakristo? Yanatia mengi zaidi ya “neno la uzima” ambalo lazima ‘walishike sana.’ “Neno lako ni taa ya miguu yangu, na mwanga wa njia yangu,” kasema mtunga zaburi. (Zab. 119:105, 130) “Mafuta” ya mfano yanatia ndani na roho ya Mungu, ambayo ni ya lazima ili kulielewa Neno la Mungu. Zaidi ya hayo, roho takatifu ya Mungu inatokeza matunda ya roho kama vile upendo, furaha, amani, uvumilivu, fadhili, wema, imani, upole, kujiweza. “Mafuta” hayo ya kiroho yana uwezo wenye kunurisha, ukitokeza sifa za Kikristo zinazofanana katika wengine.

16. (a) Ni nini kilichofananishwa na vyombo vilivyojaa mafuta vya wanawali wenye busara? (b) Wao wanaipataje akiba hii iliyo nyingi?

16 Wanawali wenye busara walikuwa na mafuta katika vyombo vyao na pia katika taa zao. Walitaka kuhakikisha kwamba, bwana-arusi akikawia muda mrefu zaidi kuliko ilivyotazamiwa, wasingeikosa nafasi nao wangefuatana na maandamano ya arusi na kuingia katika karamu ya arusi. Katika utimizo hii yamaanisha kwamba jamii ya “ufalme wa mbinguni” ina Neno la Mungu, pamoja na ufahamu, na roho takatifu ya Mungu. Washiriki mmoja mmoja wa jamii ya wanawali wanapokea akiba pamoja na wengine wote. Wanahitaji akiba ya kutosha kuweza kuvumilia kwa uaminifu katika ulimwengu huu wanapotoka wakamlaki Bwana-arusi. Wanajazwa na Neno la Mungu lenye kunurisha na roho yake. “Mafuta” haya wanayoyahitaji sana wanayapata kwa wingi kwa kuendelea kujifunza na kushirikiana na “wanawali” wenzao na kwa kujazwa na roho ya Mungu. Pia, wanajitahidi sana katika kusitawisha utu wa Kikristo nao wanajitia kwa bidii katika utangazaji wa habari njema za Ufalme kwa wengine. Hawa “wenye busara” ndio wale “wanaoendelea kumfuata Mwana-Kondoo [Yesu Kristo] bila ya kujali anakokwenda.”​—Ufu. 14:4, NW.

17. Je! tuna mifano ya “Wakristo” ambao wameonyesha kuwa na akiba tele ya “mafuta” ya mfano leo?

17 Kuwa huku na “mafuta” ya kiroho tele na uwezo wayo wa kumtetea Mkristo kama mtu mwenye mfano wa Kristo kwashuhudiwa wakati wetu na Wakristo wenye tumaini la kimbinguni waliopata taabu miaka mingi katika kambi za mateso na magerezani, wengine wakiwa wametiwa kifungoni miaka mingi kwa kutengwa kabisa na watu wengine. Wengine wamejaribiwa kwa njia nyingine. Wamevumilia, wakiwa waaminifu katika hali zo zote walimojikuta. Ni nini kilichowaendeleza kuwa hai na timamu kwa kiroho? Ni uhakika wa kwamba wao walikuwa wameitumia nafasi yao kujijaza na Neno la Mungu na roho yake walipokuwa na wakati na katika hali ya kujifunza Neno la Mungu na kushirikiana na watu wake. Pia, waliendelea kumwomba Mungu ‘wajazwe roho,’ naye Mungu akazisikia sala zao.​—Efe. 5:18.

“BWANA ARUSI ALIPOKAWIA”

18. (a) Je! Bwana-arusi alitokea katika karne ya kwanza? (b) Ni nini kilichopaswa kutokea kabla ya kufika kwake?

18 Iliwapasa “wanawali” wamngojee Bwana-arusi muda mrefu namna gani? Huenda ikawa wengine walitazamia atokee mapema zaidi​—kwa kweli, wengine ‘walichoka, wakazimia mioyoni mwao’ wakati mataraja yao ya kipekee yaliposhindwa. (Ebr. 12:3) Kutokea kwa Bwana-arusi hakukuwa mwishoni mwa taratibu ya mambo ya Kiyahudi Yerusalemu ulipoharibiwa na Warumi mwaka wa 70 C.E. Naye mtume mzee Yohana alisema hivi alipokuwa akiimalizia habari yake ya Ufunuo, akiandika karibu mwaka wa 96 C.E.: “Na uje, Bwana Yesu.” (Ufu. 22:20) Lakini mitume Yohana na Paulo walikuwa wamekwisha tabiri kwamba mpinga Kristo, “mtu wa kuasi,” angefanikiwa kwa kitambo kabla ya kuwapo kwa Yesu katika mamlaka ya Ufalme.​—1 Yohana 2:18; 2 The. 2:1-3, 7, 8.

19. “Wanawali” ‘walisinziaje wakalala usingizi’?

19 Hali ilipata kuwa kama ilivyotabiriwa katika mfano wa wanawali kumi: “Hata bwana arusi alipokawia, wote wakasinzia wakalala usingizi.” (Mt. 25:5) Wakati Konstantino Mkuu mwenye unafiki ‘alipoongolewa’ kwenye Ukristo, aliufanya Ukristo wa kujidai kuwa Dini ya Serikali ya Milki ya Kirumi. Kwa njia hiyo ilifanywa ionekane kwamba Kristo alikuwa akitawala kupitia kwa Kanisa na kwamba kurudi kwa Kristo hakukuwa kwa lazima. Maaskofu wa kujidai wa Kikristo walikuwa wamelala usingizi kwa habari ya madaraka ya Kikristo.

20. “Wanawali” waliolala usingizi walilinganaje na sehemu ya mfano wa ngano na magugu?

20 Hali hii ya kidini ilielekea kulingana na alivyotabiri Yesu katika mfano wa ngano na magugu: “Ufalme wa mbinguni umefanana na mtu aliyepanda mbegu njema katika konde lake; lakini watu walipolala, akaja adui yake akapanda magugu katikati ya ngano, akaenda zake.”​—Mt. 13:24, 25.

21. “Mavuno” yalipokuwa yakimalizwa, ni kazi gani nyingine Bwana Yesu Kristo amekuwa akifanya?

21 Ndipo Yesu alipoendelea kuyaeleza mavuno ambayo yangetokea wakati wa kurudi kwake. Leo, pamoja na mavuno ya “wana wa ufalme” walio wa kweli, Kristo anafanya kazi nyingine, ile ya kukusanya mkutano mkubwa wa “kondoo wengine” ambao hawatakuwa wafalme wa kimbinguni, kwa kuwa hawakaribishwi kwenye karamu ya arusi ya kimbinguni. Hawa watabaki duniani kama msingi wa “dunia mpya” (NW) ya jamii yenye haki ya kibinadamu wakati wa kipindi kijacho cha miaka elfu chenye baraka kwa wanadamu. Watu wengi leo wanaweza kunurishwa na “nuru ya ulimwengu” na kukusanywa pamoja na huu “mkutano mkubwa.”​—Yohana 10:16; Ufu. 7:9-17.

​—Kutoka Kitabu God’s Kingdom of a Thousand Years Has Approached.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki