Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w75 3/1 kur. 99-104
  • Uaminifu—Njia ya Maisha

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Uaminifu—Njia ya Maisha
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • KANUNI YENYE UAMINIFU
  • JE! UWEZO WA KUZALIWA NAO UNAHUSIKA?
  • UNYENYEKEVU UNAPOHUSIKA
  • KUWA NA JINA JEMA NA YEHOVA
  • Je, Wewe Ni Mwaminifu Katika Mambo Yote?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
  • Kwa Uaminifu Uendelee Kuishi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Uaminifu Unathawabishwa
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Thawabu Njema ya Uaminifu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
w75 3/1 kur. 99-104

Uaminifu​—Njia ya Maisha

“Inayohitajiwa katika mawakili, ndiyo mtu aonekane kuwa mwaminifu.”​—1 Kor. 4:2.

1, 2. (a) “Mwaminifu wa Kale” ni nini, nayo ilipata jina lake kwa njia gani? (b) Lakini ni nini kinachopendwa hata zaidi kuliko ukawaida wa chemchemi ya maji yenye moto?

“MWAMINIFU WA KALE” ndilo jina la mojawapo ya chemchemi nyingi zenye maji ya moto katika Yellowstone National Park katika United States. Ilipata jina lake kutokana na uhakika wa kwamba miaka ya kuanzia na wa 1920 na kuanzia na wa 1930 ilibubujika kwa kawaida kila dakika 65. Na kwa sababu hiyo, ikajulikana sana kama mahali penye kuvutia watalii.

2 Watu wanapenda uaminifu si katika chemchemi yenye maji ya moto tu inayotupa kwa kawaida galani 10,000 za mvuke na maji ya moto futi 100 mpaka 150 urefu wa kwenda juu, bali hasa katika watu walio na njia ya maisha inayowafanya wenye kutegemeka na wenye kutumainiwa. Hata katika ulimwengu wa biashara kinachotazamiwa kwa mtu aliyekabidhiwa madaraka ni uaminifu. Pengine hiyo ndiyo sababu U.S. Marine Corps (jeshi la baharini la United States) walichagua usemi wao uwe Semper fidelis, ‘waaminifu sikuzote.’​—Linganisha 1 Wakorintho 4:2.

3, 4. Ni nani mfano mkuu zaidi wa uaminifu, nazo ni nini ishara zifaazo za kutegemeka kwa kusudi lake?

3 Lakini linapokuwa shauri la kuonyesha kadiri bora ya uaminifu, wewe unamfikiria nani hasa? Hapaswi kuwa mwingine ila Yehova Mungu, “Muumba mwaminifu” wa mbingu na dunia. (1 Pet. 4:19) Ijapokuwa chemchemi yenye maji ya moto yaweza kuwa mfano ufaao wa uaminifu kwa wanadamu, bila shaka ingekuwa mfano usiofaa wa uaminifu usiobadilika wa Yehova. Chemchemi zote zenye maji ya moto zinauwa zenye kubadilika-badilika au kuacha kutenda muda upitapo. Sivyo alivyo Yehova. Kwa hiyo, jua na mwezi unaoendelea kuwapo ni ishara zinazofaa zaidi za kutobadilika kwa kusudi lake, kutumainika na kutegemeka kusiko na mawaa.​—Zab. 89:36, 37; 104:19.

4 Mwanadamu aweza kupanga na kufanya kazi akiwa na hakika, akiitumaini imara ya kazi za Muumba, kama mwanadamu anapanda shamba la mboga au anaunda mashine ya kuhesabia itakayomwongoza kwenye mwezi na kumrudisha. Hiyo ni sababu ya kuwaza kwamba mwanadamu aweza kujifunza mengi bila kikomo kutokana na Mungu mwaminifu ambaye ameonekana mwenye kutegemeka sana, si katika ambayo ameyasema tu, bali pia katika ambayo ameyafanya. Juu ya Mungu huyu mwaminifu, twasoma hivi: “Mpeni ukuu Mungu wetu. Yeye Mwamba, kazi yake ni kamilifu; maana, njia zake zote ni haki. Mungu wa uaminifu, asiye na uovu, yeye ndiye mwenye haki na adili.”​—Kum. 32:3, 4.

5. Ni sifa, gani inayotazamiwa kati ya waabudu wa Mungu, ya Yeye anachunguza nini?

5 Imepaswa itazamiwe kwamba huyu “Mungu wa uaminifu” angetazamia sifa ii hii kati ya wale wanaomwabudu yeye kwa kweli. Yeye kwa kweli ndiye Mungu na Mwokozi “hasa wa walio waaminifu.” (1 Tim. 4:10, NW) Akiwa na uwezo wake kamili wa kuchunguza, Mungu aliye hai Yehova anafahamu kwa usahihi jitihada za wale wanaojaribu kumtumikia. Macho yake ya wazi kuziona njia zote za wana wa wanadamu, na ni kwake ambako lazima hesabu itolewe. (Yer. 32:19; Ebr. 4:13) Kama vile Mithali isemavyo: “Macho ya [Yehova] yako kila mahali; yakimchunguza mbaya na mwema.”​—Mit. 15:3.

6. Ikiwa hivyo, imetupasa tujiulize maulizo gani?

6 Uangalizi wa Yehova wenye upendo na ulinzi wake wa hali njema ya watu wake ni wazi sana. Akiujua uhakika huu, kwamba Muumba mwenye upendo awaona sana wema na wabaya pia, na anayofanya kila mmoja wao, yampasa mtu ajiulize hivi: ‘Ikiwa Yehova ahitaji uaminifu kati ya watu wake, je! yeye aniona mimi kama mwabudu wa namna hiyo? Je! njia yangu ya maisha ni ya uaminifu? Nawezaje kujua kama anikubali mimi?’

KANUNI YENYE UAMINIFU

7. Ni sheria au kanuni gani ambayo Yehova ameifanya ipatikane kwa wanadamu kwa ujumla?

7 Je! haifai kudhani kwamba Mungu wa uaminifu angekuwa na sheria au kanuni ambayo ingewaeleza waabudu wake yaliyo haki na yaliyo makosa, yaliyo mema na yaliyo mabaya, yaliyo kweli na yaliyo uongo? Ndiyo, inafaa. Na zaidi ya hayo, Mungu wa utaratibu na amani ametoa kanuni hiyo ya kimungu, Biblia Takatifu, ipate kuwafundisha na kuwaongoza wanadamu wote. Hakuna kitabu kingine cho chote cha mafundisho ambacho kimeenezwa ulimwenguni pote au kiwezacho kuendewa na wingi wa wanadamu kama hicho.​—1 Kor. 14:33.

8, 9. Kwa sababu gani kushikamana kwa uaminifu na Neno la Mungu si kwepesi sikuzote?

8 Basi, je! njia yako ya maisha yalinganaje na ile inayokubaliwa katika Maandiko? Katika kutokamilika kwako huna haja ya kuvunjika moyo unapoelekeana na kanuni kamilifu zilizoandikwa katika Neno la Mungu. Maneno yenye kutumainisha ya Zaburi 103:14 yasema hivi: “Kwa maana Yeye anatujua umbo letu, na kukumbuka ya kuwa sisi tu mavumbi.” Yehova ajua kutokamilika kwetu kulikorithiwa. Madai yake hayapiti tuwezayo kufanya kamwe.

9 Hata hivyo, kushikamana na mwendo mwaminifu si kwepesi sikuzote; hasa hivi ndivyo ilivyo leo wakati ambapo watu wengi wanapenda kufanya yaliyo haki machoni pao na kufuata njia ya ulimwengu. Walakini, uaminifu mnyofu na wa moyo wote unatiwa moyo ujapokuwa ukubwa wa jaribu.

10, 11. (a) Ni lazima tupatwe na majaribu makubwa na magumu ili tuhakikishe uaminifu wetu? Toa mfano. (b) Twawezaje kutumia kanuni iliyotajwa na Yesu juu ya shauri la uaminifu katika maisha zetu za kila siku, na kwa matokeo gani yenye faida?

10 Kwa upande mwingine, kufanya jambo kubwa si takwa la kuhakikisha uaminifu wetu sikuzote wala la kupata baraka na kibali ya Yehova. Yehova hakuwawekea Adamu na Hawa jaribu kubwa katika bustani ya Edeni. Wepesi wa jaribu hilo lililowapasa wanadamu wawili wa kwanza ni mfano bora wa kanuni iliyotajwa zaidi ya miaka 4,000 baadaye na Mwana wa Mungu mwenyewe, yaani, “Aliye mwaminifu katika lililo dogo sana, huwa mwaminifu katika lililo kubwa pia; na aliye dhalimu katika lililo dogo, huwa dhalimu katika lililo kubwa pia.”​—Luka 16:10.

11 Leo, karibu karne kumi na tisa baada ya maneno hayo kusemwa, yangali yasikika kuwa kweli sana, na kanuni ile ile yatumika katika kila upande wa maisha kati ya waabudu wa kweli wa Yehova Mungu. Mara nyingi unaiona katika mambo madogo anayofanya mtu kila siku yanayoonyesha wema wa moyo ulio mwaminifu na wa kweli kwa Yehova. Pengine wewe hutatakiwa uwe katika hali fulani ukionyesha kinachoweza kuitwa na watazamaji uaminifu wa kutokeza. Lakini kuendelea kwako kufanya yaliyo haki, ukawaida wako na kutegemeka kwako katika mambo madogo, kutatoa ushuhuda mwema wa kuthamini kwako kwingi kanuni za kimungu za yaliyo kweli na ya uaminifu. Walio waaminifu katika mambo madogo ndio “[Yehova] huwahifadhi.”​—Zab. 31:23.

12. Eleza namna wakati na hali zinavyohusiana na shauri hili la uaminifu.

12 Kwa hiyo si lazima mtu awe na cheo cha ukubwa katika kundi la Kikristo ili afurahie baraka ya Yehova anayowamiminia waaminifu. Katika utendaji wako wa kila siku, kama unatia biashara au raha, kama ni kati ya wengine au wewe mwenyewe tu, uaminifu na ukamilifu kwa upande wako utakuwa wenye mfano wa Mungu aliye mwenye haki na mwaminifu. Kama vile inavyohitaji wakati kwa habari ya kuhakikisha uvumilivu, ndivyo inavyohitaji wakati pia kuhakikisha uaminifu wa mtu. Yamaanisha kuzoea kweli kila siku, kufanya utii kwa sheria na kanuni za Maandiko njia yako ya maisha. Halafu, Yehova akubariki, kama ilivyoandikwa: “Mtu mwaminifu atakuwa na baraka tele.”​—Mit. 28:20.

13, 14. (a) Imetupasa tupime kadiri ya uaminifu wetu na nini? (b) Ni nini mengine ya maeneo ambamo twaweza kupima uaminifu wetu kwa Yehova?

13 Ukitazama nyuma kwa kitambo, waweza kudhani hakuna jambo la maana sana limetokea maishani mwako. Ukiamua kulingana na kanuni za ulimwengu za kutimiza mambo na kuwa na matokeo mema, pengine hukutimiza lo lote lililo kuu. Lakini je! unajaribu kuiga njia za nani? Umekuwa ukijaribu kufikia kanuni za nani? Ikiwa umekuwa ukikuza kumbukumbu la maisha umpendeze Yehova, halitasahauliwa haraka na Mungu huyo wa uaminifu.

14 Simama ufikiri. Wengine wanakuonaje? Ni nini sifa yako kati ya marika yako na washiriki wako? Je! wanaona kwamba u mtu anayetimiza ahadi yake sana? Je! una sifa ya mtu alipaye deni zake na afuataye mpango wa wepesi juu ya kila jambo? Pengine ni shauri la kuwa wa kawaida katika utumishi wa Ufalme na penye mikutano kwa ajili ya ibada. Haya yaweza kuonekana kama mambo madogo, lakini yaweza kufanya wengine wakuone wewe kama mtu mwaminifu. Sasa, ikiwa wengine wameona namna ambavyo umekuwa ukiongoza maisha yako, je! Baba yako mbinguni hakuona pia?

JE! UWEZO WA KUZALIWA NAO UNAHUSIKA?

15, 16. (a) Uwezo waweza kuelezwaje, na je! unahusika katika uchaguzi wa wazee kundini? (b) Zaidi ya uwezo mbalimbali wa kuzaliwa nao, ni sifa gani za maana zaidi lazima wazee waliowekwa wawe nazo?

15 Uwezo wasemekana kuwa ndiyo nguvu ya kufanya mambo. Hakuna shaka kwamba uwezo wa kuzaliwa nao waweza kuwa baraka kuu. Lakini je! uwezo wa kuzaliwa nao ndilo jambo la maana analohitaji Mungu kati ya watu wake?

16 Ni kweli, katika kuchagua wazee kundini, uwezo unafikiriwa. Pengine wengine wana karama (majaliwa) kwa njia fulani. Kwa mfano, ili kuwa mzee lazima mtu awe “mwenye kustahili kufundisha.” (1 Tim. 3:2, NW) Lakini hii yatia mengi zaidi ya uwezo wa kuzaliwa nao. Mwalimu astahiliye kundini apaswa kuwa na maarifa ya kweli. Lazima ajue sababu za mambo na kuwa na ufahamu mwingi wa Maandiko Matakatifu. Na zaidi ya kuwa na maarifa, lazima awe mwenye busara, mwenye subira na mwenye kupendezwa na watu wengine ili awe mwalimu mwenye matokeo mema. Mtume Paulo alimwagiza Tito aweke wanaume wazee, akitaja kwamba lazima mwangalizi awe “mwenye kushikamana sana na neno la uaminifu kwa habari ya ustadi wake wa kufundisha, apate kuweza kutia moyo kwa fundisho ambalo ni lenye afya na kukaripia pia wale wanaopinganisha.” (Tito 1:9, NW) Hao wenye kuaminiwa hawategemei uwezo wao waliozaliwa nao bali wanamtegemea Mwalimu wao Mkuu kwa uongozi katika kusaidia wengine kundini.

17. Wale wenye uwezo mbalimbali wa kuzaliwa nao na majaliwa ya pekee wamepaswa wajihadhari na nini?

17 Uwezo kadiri fulani wahitajiwa mara nyingi kufanya namna nyingine za kazi kundini. Lakini uwezo au majaliwa ya mtu mwenyewe yasipewe sifa ya matokeo yapatikanayo. Kwa kweli, wale waliobarikiwa kwa uwezo wa kuzaliwa nao wamepaswa wajiangalie wasitegemee ufahamu wao wenyewe, bali wamtegemee Yehova, wakimwomba aongoze hatua zao. (Mit. 3:5, 6) Kwa kawaida uchunguzi utaonyesha kwamba wanaotumikia kati yetu kama wazee, na wengine wanaojitahidi sana, wanastahili kupitia kwa funzo lenye bidii na matumizi ya mambo wajifunzayo. Kwa kipindi fulani wamejiangalia sana na mafundisho yao, wakisikiliza maagizo ya Mungu. Wametaka kuifanya kazi yake kama atakavyo ifanywe, nalo ni jambo la kusifika kuona namna wanavyomwacha Yehova atumie wakati wao na uwezo wao kwa njia mbalimbali kuendeleza ibada yake.

18. Je! Mungu anawaona wazee na watumishi wa huduma kama wanaume wenye uaminifu mkubwa zaidi kundini? Eleza.

18 Basi, je! Mungu anawaonaje wale wanaotumikia kama waangalizi waliowekwa? Je! anawaona kama bora zaidi kuliko wengine? Kama walio waaminifu zaidi kuliko wengine? Sivyo, ni vema kuona mambo yafaavyo kuonwa. Wale waliochaguliwa wasimamie wako kwa kweli ili watumikie kama watumwa au watumishi, nao wakiwa hivyo lazima watumie uwezo wao na majaliwa kwa ukamili katika kuhakikisha uaminifu wao. Hawafurahii mapendeleo yao kwa sababu ya walivyo. Bali, wako katika vyeo vyao mbalimbali kwa sababu ya uhitaji uliofanyizwa na watangazaji wa Ufalme. Wakifuata shauri la Yesu, wanatumikia waliomo kundini ambao wao (waangalizi) ni watumwa kwao. (Luka 22:26; Gal. 5:13) Waangalizi waaminifu wanajua kwamba kazi yao inahusiana na wahubiri wenzao wa habari njema, ambao wote ni bora machoni pa Mungu wanapoonyesha uaminifu.

19. Ni nini basi kinachohitajiwa katika waangalizi waliowekwa katika kundi la Kikristo?

19 Daraka la kazi za kusimamia za wakili zaonyesha kwa kufaa huduma ya mwangalizi wa Kikristo. Uaminifu wahitajiwa sana kwao, kama unavyotiliwa mkazo na aliyoyaandika mtume Paulo kwa Wakorintho, aliposema: “Inayohitajiwa katika mawakili, ndiyo mtu aonekane kuwa mwaminifu.” (1 Kor. 4:2) Mtume uyu huyu alimwandikia Tito, akisema hivi: “Kwa maana yampasa mwangalizi awe bila shtaka kama wakili wa Mungu . . . mkaribishaji wa wageni, mpenda mema, timamu katika akili, mwenye haki, mwaminifu, mwenye kujiweza.” (Tito 1:7, 8, NW) Kwa hiyo, uwezo wo wote ambao huenda wakili akawa nao, wa kuzaliwa nao au wa kujipatia, unapaswa ufuatane na sifa nzuri ya uaminifu. Hata Daudi, aliyemfananisha Kristo Yesu, alisema: “Macho yangu yatawaelekea waaminifu katika nchi, hao wakae nami. Yeye aendaye katika njia kamilifu, ndiye atakayenitumikia.”​—Zab. 101:6.

20. Kwa sababu gani uaminifu, wala si uwezo, ndilo jambo Yehova analohitaji kati ya wale anaowakubali?

20 Uwezo ni jambo awezalo mtu kupata kwa Yehova kama zawadi. Kwa mfano, katika Kutoka twasoma namna Yehova alivyowapa wengine waliofanya kazi ya kujenga hema zuri huko jangwani hekima, ufahamu na maarifa. (Tazama Kutoka 35:30–36:1.) Lakini linapokuwa shauri la uaminifu, hili si jambo Mungu analompa mtu. Wala si jambo linalorithiwa au linalopokewa kwa kujitokeza lenyewe wakati wa ubatizo. Lazima litafutwe kwa bidii, likuzwe. Inachukua wakati, jitihada, uvumilivu kukuza kumbukumbu linaloshuhudia njia ya mtu ya maisha. Ni juu ya mwabudu mwenyewe kulionyesha anapofanya kazi yake, akiendesha uwakili wake kwa uaminifu.​—1 Pet. 4:10.

UNYENYEKEVU UNAPOHUSIKA

21. Linapokuwa shauri la kujivuna, Maandiko yanashauri nini?

21 Linapokuwa shauri la kujifikiria ifaavyo, Yehova anatoa shauri jema hili: “Hekima hukaa na wanyenyekevu.” (Mit. 11:2) Mtu anayetembea kwa unyenyekevu na Mungu ajua kwamba hana la kujisifia, ujapokuwa uwezo wake au mambo aliyotimiza. Ikiwa ataka kujivuna, na ajivunie Mungu mzuri sana anayemtumikia. Hivyo ndivyo Biblia inavyosihi isemapo kwamba mtu asijisifu kwa sababu ya uwezo au mali zake. Bali, na ajisifu kwa sababu amjua Yehova kuwa Mungu wa fadhili za upendo, haki na rehema.​—Yer. 9:23, 24.

22, 23. (a) Imetupasa tuoneje mali zo zote za kimwili tuwezazo kuwa nazo? (b) Tukiisha kufanya yote tuwezayo, yatupasa bado tujioneje? (c) Ni nini kitakachomsaidia mtu asichoke wala kuvunjika moyo?

22 Wengine wanaweza kuwa na mali zaidi za ulimwengu huu kuliko wengine. Wengine wanaweza kuelekea kuwa na cheo bora maishani. Lakini agizo ni la wazi sana kwamba haimpasi Mkristo kujitumainia kupita kiasi, akitegemea vitu alivyo navyo, bali, yampasa ajifanyizie wokovu wake mwenyewe kwa woga na kutetemeka. (Luka 12:15; FIp. 2:12) Njia hii ya maisha inayopendekezwa yamaanisha kuendelea kuwamo sana katika ibada safi, kuwa tajiri katika matendo mema.​—1 Tim. 6:17-19.

23 Mali zo zote au majaliwa ya mtu yamepaswa yaonwe kama mali iliyowekwa kama hazina ya kutumiwa kwa heshima na utukufu wa Mungu. Kwa njia hii itamlinda mtu asije akajitutumua kwa kiburi kwa sababu ya mambo aliyoyatimiza katika kumtumikia Yehova. Nia njema apaswayo kila mtu kuisitawisha baada ya kufanya mambo aliyogawiwa ni: “Sisi tu watumwa wasio na faida; tumefanya tu yaliyotupasa kufanya.” (Luka 17:10) Kutumikia kama Mungu aamuruvyo, kufanya hivyo kwa furaha na nia na kutegemewa, kama ni kwa njia kubwa au sivyo, ni jambo la kukubalika kwake. Walakini, hakuna apaswaye kujisikia kuvunjika moyo au kuona hafai kitu, hata ingawa huenda kazi inayofanywa ikawa ile ile isiyobadilika sikuzote. Kumbuka, jambo analoendelea kutazamia Yehova kati ya watumishi wake ni kwamba waonekane waaminifu sikuzote katika lo lote awapalo walifanye.

24. Shauri lililomo katika Warumi 12:16 lina faida gani kwa walio waaminifu kwa Yehova?

24 Maarifa ya kweli juu ya njia za Mungu yasaidia kumnyenyekeza mtu na kumzuia asinie makuu. (Rum. 12:16) Yanamlinda mtu asijivunie mambo ambayo amefanya na kumsaidia akaze fikira za moja kwa moja kwenye Chanzo cha wema na ukuu. Ikiwa mtu ana cheo kikubwa, na iwe hivyo kwa sababu ya utumishi mwaminifu kwa Mungu wa kweli na kwa sababu ya kujitoa bila choyo atumikie wengine. Jina lifaalo na Yehova ndilo limepaswa liwe jambo la kutamaniwa, kuwa na sifa njema kwa sababu ya uaminifu​—hiyo ndiyo njia ya maisha aikubaliyo Mungu.​—Mhu. 7:1.

KUWA NA JINA JEMA NA YEHOVA

25. Kufuata Pentekoste 33 C.E., tuna uhakikisho gani kwamba mitume kumi na wawili wote walikuwa waaminifu mpaka kufa kwao?

25 Ingawa Biblia haitaji wengi wa mitume kumi na wawili kufuata Pentekoste ya 33 C.E., na ingawa hakuna kumbukumbu la Biblia juu ya walivyokufa, mbali na Yakobo na maneno ya unabii kumhusu Petro, ushuhuda waonyesha kwamba wote waliendeleza uaminifu wao mpaka kufa. Twaweza kuwa na hakika walitumia vyote walivyokuwa navyo katika utumishi mtakatifu kwa Mungu aliye hai. Na twaweza kuwa na hakika kwamba Yehova hakusahau wo wote kati yao hata hivyo. Kama ushuhuda wa sikuzote wa uaminifu wao majina yao yameandikwa juu ya misingi ya Yerusalemu Mpya.​—Ufu. 21:14.

26. Wakongwe wanawezaje kutia moyo ndugu na dada zao wachanga zaidi?

26 Leo tuna wakongwe wengi wanaoshirikiana na makundi ya Kikristo ambao kwa miaka mingi wameendelea kuwa waaminifu kwa Yehova kwa imara wakikabili vipingamizi vingi. Sasa wanazidi kuzeeka na kuwa dhaifu na wengi wao hawawezi kukubali madaraka mazito kundini. Lakini lo! ni baraka namna gani kuwa nao! Upendo wao na bidii ni kichocheo kwa wahubiri wenzetu wasonge mbele katika kazi ya Bwana. Ingawa wengine ni dhaifu sana kimwili, yatia moyo kuona wakitumia nguvu kiasi fulani kwa ajili ya mikutano ya Kikristo na utumishi wa shambani.

27, 28. (a) Dada katika makundi wanafanya utumishi gani wenye thamani? (b) Eleza namna mwili wa kibinadamu ulivyo mfano mwema wa kundi la Kikristo.

27 Zaidi ya hayo, wako wanawake wengi katika makundi nao hawa hawastahili kuwa wazee wala watumishi wa huduma. Wao pia wanahitajiwa sana na ni msaada mkubwa katika kuhubiri “habari njema” za Ufalme katika ulimwengu wote kabla ya mwisho kuja. Mtu akumbushwa Zaburi 68:11, 12: “[Yehova] analitoa neno lake; wanawake watangazao habari [njema] ni jeshi kubwa. . . . Na mwanamke akaaye nyumbani agawa nyara.”

28 Ziko kazi nyingi za kufanywa na viungo mbalimbali katika mwili wa kibinadamu. Kwa hiyo pia katika kundi la Kikristo ziko kazi mbalimbali ambazo watu mbalimbali waweza kufanya. Hakuna apaswaye kujisikia hatakiwi wala kumwambia mwingine, “Sina haja na wewe.” Mpango mzima wa kundi unasaidia kutokeza Wakristo waliokomaa kwa utukufu wa Mungu,​—1 Kor. 12:4-7, 21, 22.

29. Wakati wote kundini wanapofanya kazi pamoja kwa amani na umoja, ni nini kinachotimizwa? Toa mfano.

29 Matokeo makubwa yanapatikana wakati wazee na vijana wanapofanya kazi pamoja kwa bidii kutimiza agizo lao kulihubiri Neno. Huenda ukaamsha kupendezwa kwa mtu kwa kumtia moyo asome kitabu cha kusaidia kujifunza Biblia. Wakati unapita na mtu mwingine aweza kunywesha mbegu ya kupendezwa. Mwingine aweza kusitawisha mara kwa mara, naye Mungu aendelea kufanya ikue. (1 Kor. 3:6) Baadaye, pengine miaka mingi baadaye, waweza kujulishwa kwa mtu yule yule kusanyikoni​—sasa akiwa ndugu au dada yako wa kiroho! Kwa hiyo, ikiwa yachukua muda kuona matokeo ya kuhubiri kwetu, hii isituvunje moyo tusiseme na kila mtu tunayekutana naye, tukifanya hivyo kwa moyo wenye kujawa na upendo kwa Yehova. (Rum. 10:10) Waweza kuvuta rafiki na majirani pia kwenye ujumbe juu ya Mungu wetu Yehova na kuwaacha wautazame mwenendo wako safi wa Kikristo.​—2 Pet. 3:11, 12.

30. Uamuzi wetu umepaswa uwe nini tunaposimama katika ukingo wa Har–​Magedoni?

30 Ni jambo zuri sana kuona wengi wakigeukia haki na utumishi wa Mungu wetu, wakiweka maisha zao wakf wafanye mapenzi ya kimungu katika hizi “siku za mwisho.” Karibuni twawaona wao nao wakisaidia wengine wasitawishe upendo kwa Yehova. Kuna furaha nyingi kuwa na sehemu yo yote, hata sehemu ndogo sana, katika kazi hii ya kukusanya inayoendelea katika sehemu zote za dunia. Tunaposimama katika ukingo wa Har–​Magedoni na kuziona baraka zisizolinganika zitakazofuata karibuni, sasa sio wakati wa kutazama nyuma kwa majuto. Ni wakati wa kusitawisha sifa njema ya uaminifu, kwa maana hiyo ndiyo Mungu anatazamia katika wale walioazimu kumwabudu kwa moyo wote.

31. Ni nini cha kutamaniwa zaidi kuliko mali za kimwili, nacho chaweza kupatikanaje?

31 Mali zote awezazo kukusanya mtu haziwezi kulingana na jina na sifa anayofanya na Muumba wake Mpaji wa Uzima. “Heri kuchagua jina jema kuliko mali nyingi.” (Mit. 22:1, New English Bible) Tukiwa na kanuni ya Biblia kutusaidia tupambanue kati ya yaliyo haki na mabaya, na tuwe wenye bidii katika kufuata njia ya maisha anayoikubali Mungu, yaani, ya uaminifu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki