Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w75 5/15 kur. 219-221
  • Thawabu Njema ya Uaminifu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Thawabu Njema ya Uaminifu
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • WAKATI “MTUMWA” ALIPOPASWA KUPOKEA THAWABU
  • KUWEKWA JUU YA MALI ZOTE ZA BWANA
  • “Ni Nani kwa Kweli Mtumwa Mwaminifu na Mwenye Busara?”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • “Mtumwa” Ambaye Ni Mwaminifu na Mwenye Busara
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2004
  • Wakristo Wanalishwaje Kiroho?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Utendaji Uliopanuliwa Wakati wa Kuwapo kwa Kristo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
w75 5/15 kur. 219-221

Thawabu Njema ya Uaminifu

Makala hii ni ya kutumia kwa mafunzo ya kitabu ya kundi

1. Mithali yaonyeshaje kwamba mtu mwaminifu hatafuti faida zake mwenyewe kwanza?

UAMINIFU ni sifa inayothaminiwa na kila mtu. “Mtu mwaminifu atakuwa na baraka tele,” yasema mithali ya Biblia. Mtu mwaminifu hatafuti faida zake mwenyewe kwanza. Kwa hiyo, mithali yaendelea kutilia hili mkazo kwa fungu la maneno lenye kutofautisha: “lakini afanyaye haraka kuwa tajiri hakosi ataadhibiwa.”​—Mit. 28:20.

2. Yehova ni Mungu wa namna gani, na yatupasa tutambue nini ikiwa twatazamia kupata kibali yake?

2 Yehova Mungu “ndiye Mungu [wa kweli]; Mungu mwaminifu, ashikaye agano lake na rehema zake.” (Kum. 7:9) Jambo jema juu yake ni kwamba yeye ndiye Mungu athaminiye uaminifu wa wengine, na mtu hawezi kumtumikia bila kuitambua sifa njema hii. Kwa kweli, “mtu amwendeaye Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko, na kwamba huwapa thawabu wale wamtafutao.”​—Ebr. 11:6.

3. Ni lazima mtu afanye matendo makuu awe mwaminifu?

3 Si lazima matendo ya uaminifu ambayo huenda mtu akafanya yawe makubwa au mazuri ajabu. Kanuni ambayo kwayo mtu anathawabishwa ni uaminifu katika mambo yote, hata yawe madogo namna gani. Yesu Kristo alisema: “Aliye mwaminifu katika lililo dogo sana, huwa mwaminifu katika lililo kubwa pia; na aliye dhalimu katika lililo dogo, huwa dhalimu katika lililo kubwa pia.”​—Luka 16:10.

4. “Mtumwa mwaminifu mwenye akili” ni nani, nao wanapokea thawabu ya uaminifu kupitia kwa nani?

4 Hivyo ndivyo ilivyo kwa watu wote wanaomtumikia Mungu kwa kweli. Wote ni “watumwa” wake, wanaofanya kulingana na amri yake, na wote wanategemea Mungu kwa thawabu yao halisi na ya kudumu, si wanadamu. Kama kundi, jamii au kikundi, ndugu za Yesu Kristo waliotiwa mafuta na kuzaliwa kwa roho wanaitwa ‘mtumwa wake mwaminifu mwenye akili’ wanapokuwa duniani. Thawabu yao ya uaminifu inatolewa kwao kupitia kwa Yesu Kristo, Kichwa cha kundi la Kikristo. Alitoa mfano wa unabii wa jambo hili. Akizungumza juu ya kurudi kwake katika mamlaka ya Ufalme, aliwaambia wanafunzi wake hivi: “Ni nani basi yule mtumwa mwaminifu mwenye akili, ambaye bwana wake alimweka juu ya nyumba yake, awape watu chakula kwa wakati wake? Heri mtumwa yule, ambaye bwana wake ajapo atamkuta akifanya hivyo. Amin, nawaambieni, atamweka juu ya vitu vyake vyote.”​—Mt. 24:45-47.

5. Maneno “mtumwa” na “nyumba” yamaanisha nani, na kwa njia gani?

5 Katika toleo lililotangulia la Mnara wa Mlinzi tumezungumza mfano huu ambamo neno “mtumwa” lamaanisha Wakristo hawa waliotiwa mafuta walioko duniani kama jamii na neno “nyumba” lamaanisha wao kama watu mmoja mmoja. Wote wanasaidia kuona kwamba kila mmoja wa hesabu yao analishwa kiroho.

WAKATI “MTUMWA” ALIPOPASWA KUPOKEA THAWABU

6. “Mtumwa mwaminifu mwenye akili” alipaswa apokee thawabu yake wakati gani?

6 Thawabu ilipaswa ije baada ya ukaguzi kuona namna “mtumwa” alivyokuwa amekuwa akiendesha kazi yake ya kulisha “nyumba.” Bwana alikuwa amekwenda akapokee mamlaka kubwa zaidi, kama alivyofanya bwana katika mfano wa mina. Mtu huyu alikwenda nchi ya mbali akapokee mamlaka ya kifalme. Kristo ndiye “bwana” huyo katika mfano, naye aonyeshwa kama akifanya hesabu na watumwa wake aliporudi. (Luka 19:12-27, NW) Vivyo hivyo lazima “mtumwa mwaminifu mwenye akili” apokee thawabu yake wakati wa kurudi kwa Kristo katika kuwapo kusikoonekana akiwa na mamlaka ya Ufalme na kabla Kristo hajachukua hatua ya kuiondoa taratibu hii ya mambo isitawale dunia. Mtume Petro alitaja kanuni ya kwamba ‘lazima hukumu ianze katika nyumba ya Mungu’ na baada ya hapo iendelee kwa ulimwengu kwa ujumla.​—1 Pet. 4:17.

7. Kwa sababu gani kulisha “nyumba” hakukuwa kazi nyepesi kwa “mtumwa,” hasa wakati wa miaka michache iliyofuata 1914 C.E.?

7 Kulisha “nyumba” ya Kristo kiroho hakukuwa jambo jepesi kwa “mtumwa mwaminifu mwenye akili,” hasa miaka michache baada ya Yesu kuja bila kuonekana awakague na kuwathawabisha. Kulikuwa na upinzani mwingi na mateso makali kutoka kwa matengenezo ya kidini yaliyodai kuwa na haki ya peke yake kutoa chakula cha kiroho kwa “kundi,” walilosema lilikuwa lao. Walakini, matengenezo haya ya Jumuiya ya Wakristo (Kristendomu) yalikuwa yamejifanyia kumbukumbu yenye vita, kumbukumbu iliyo wazi ya hatia ya damu ilionyesha kwa uzito uongo wa dai lao kuwa wanafunzi na watumwa wa Yesu Kristo. Zaidi ya hayo, walitumia mchafuko wa vita kama nafasi ya kukusanya makundi ya watu yafanye ghasia za kuwashambulia washiriki wa mabaki madogo ya mashahidi wa Yehova wa Kikristo, kuwakamata, kuwafunga na kuwaua. Jambo hili, pamoja na hali za wakati wa vita na vizuizi, ilifanya iwe vigumu kwa kikundi kidogo cha “mtumwa” kutoa kwa kawaida habari za Biblia kwa “nyumba” ya watu mmoja mmoja. Lakini walifanya hivyo kwa uaminifu yajapokuwa magumu hayo.

8. Ni unabii gani wa Zekaria uliotimia juu ya wanafunzi wa Kristo wakati wa kufa kwake?

8 Haya yote yalilingana na yaliyowapata wanafunzi wakati wa kifo cha Yesu mwaka wa 33 C.E. Yesu alikuwa amekwisha sema kwa unabii wa Zekaria juu ya hali hii, ambao wasema hivi: “Mpige mchungaji, nao kondoo watatawanyika; nami nitaugeuza mkono wangu juu ya wadogo.” Baada ya kusalitiwa kwa Yesu, maandishi ya Biblia yatuambia hivi: “Ndipo wanafunzi wote wakamwacha, wakakimbia.” “Kondoo” walitawanyishwa kweli.​—Zek. 13:7; Mt. 26:31, 56.

9. Ni nini kilichotukia nyakati za kisasa, kwa njia ya ulinganifu?

9 Kwa njia inayolingana na hiyo, kazi ya jamii ya “mtumwa” aliyetiwa mafuta ilikaribia kuvunjwa kabisa mwaka wa 1918 C.E., washiriki wenye kuongoza wa jamii hiyo wakiwa wamekwisha hukumiwa kuwa katika gereza ya serikali kwa miaka mingi. Yaliyopaswa kufuata hayakujulikana. Uaminifu kwa agizo lao ulijaribiwa.

10. Ni kwa njia gani Mungu ‘aliugeuza mkono wake juu yao’?

10 Lakini Mungu ‘aliugeuza mkono wake juu yao.’ Hiyo ilimaanisha kugeuka kwa kuwapa kibali. Wale waliokuwa katika gereza ya serikali waliachiliwa na kuondolewa mashtaka yote. “Kondoo” waliotawanyika walikusanywa tena wawe jamii iliyotengenezwa ya “nyumba” nao wakaendelea na kazi ya kulisha kwa kujitahidi, wakipanua jitihada zao kwa nguvu hata zaidi katika kuhubiri habari njema za Ufalme.

KUWEKWA JUU YA MALI ZOTE ZA BWANA

11, 12. Kristo alimwekaje “mtumwa” juu ya “vitu” vyake vyote, nako huku kulikuwaje kupewa cheo kikubwa zaidi?

11 Kristo alimwekaje “mtumwa” juu ya “vitu” vyake vyote, na huku kulikuwaje kupewa cheo kikubwa zaidi?

12 Basi, muda mfupi baada ya ufufuo wake, Yesu alikuwa amekwenda “nchi ya mbali,” ndani ya mbingu yenyewe na ndani ya kuwapo kwa Baba yake, Yehova Mungu. Baada ya muda fulani wa kuketi mkono Wake wa kuume akingojea wakati wa Mungu uliowekwa, Yesu alipokea mamlaka ya kifalme juu ya ulimwengu mwaka 1914. (Ebr. 10:12, 13) Halafu, mwaka wa 1919, wakati wa Bwana wa kumpa “mtumwa” wake mwaminifu thawabu ulifika baada ya kipindi cha ukaguzi. Alipoikuta jamii hii ya mtumishi ikiwa nyaminifu kweli kweli katika kulisha nyumba ya imani, Yesu alimpa “mtumwa” cheo kipya. “Mtumwa” alikuwa amekuwa akiilisha “nyumba,” lakini sasa alikuwa na cheo kilichofanywa kikubwa zaidi juu ya “vitu vyake [Kristo] vyote.” Hivi vilikuwa vingi zaidi kuliko hapo kwanza. Bwana alikuwa amepokea mamlaka ya kifalme, na sasa “mtumwa” angeshiriki katika faida zilizoongezwa za Bwana. “Mtumwa” mwaminifu sasa angekuwa akiwakilisha na kutangaza Ufalme wenye kutawala dunia yote sasa, si ufalme ulioko mbali sana. Sasa “mtumwa” aliwakilisha mfalme wa Kimasihi aliyetawazwa, ambaye utawala wake kamili juu ya dunia kwa miaka elfu ungeanza karibuni!

13. Vingine vya “vitu” ambavyo “mtumwa” alipata daraka la kuviangalia vilikuwa nini?

13 Zaidi ya hayo, jamii ya “mtumwa” sasa ingependelewa sana kupewa mgawo wa kutimiza daraka linalohusiana na kazi ipaswayo kufanywa duniani kabla ya mwisho wa taratibu hii ya mambo. Hii ilipanua madaraka na baraka zao. Wangeweza kujitoa kama vyombo vya kutimizia unabii mbalimbali wa Ufalme unaoelekea kutimia kabisa tangu kutawazwa kwa Mfalme mwaka wa 1914. Huu ulitia na utimizo wa mifano mingi myema katika kitabu cha Ufunuo. Lo! ni daraka namna gani, na lo! fahari kama nini!

14. Ni faida gani nyingine ya Ufalme iliyo ya maana ambayo jamii ya “mtumwa” imefurahia kuiangalia?

14 Tena, ingawa jamii ya “mtumwa” ilikuwa imekuwa nyaminifu katika kulisha maelfu machache yaliyobaki ya mwili wa Kristo wa ndugu 144,000 wa kiroho, sasa wangelisha “mkutano mkubwa” pia wa waabudu wanaozidi “nyumba” kwa hesabu mara nyingi sana. Waabudu hawa wameingia “kama wingu” kujiunga na “mtumwa” na kushiriki sehemu kubwa kuona kwamba habari njema zahubiriwa kwenye miisho ya dunia. Wao wamekuwa mali yenye thamani kubwa sana ya Kristo na wanapendwa sana na jamii ya “mtumwa” kwa sababu ya usaidizi wao wenye uaminifu na bidii. (Ufu. 7:9-17; Isa. 60:8) Kitabu cha Ufunuo chawasimulia hawa kama wakiiokoka ‘dhiki kubwa’ itakayoiharibu taratibu hii ya mambo na kuwa msingi wa jamii mpya yenye haki ya kibinadamu duniani. Bila shaka “mkutano mkubwa” huu, wanaolishwa kiroho na jamii ya “mtumwa,” ni sehemu ya “vitu” vya Bwana.

15. Ni thawabu gani ambayo ingali yawangoja washiriki wa jamii ya “mtumwa” wabakio waaminifu mpaka mwisho?

15 Wakiwa jamii yenye Wakristo wengi walioonyeshwa wazi na neno “mtumwa,” ndugu za kiroho wa Kristo sasa wanafurahia hali njema iliyotukuzwa mbele ya Kristo na Baba yake. Kama jamii wao ndio “mtumwa mwaminifu mwenye akili.” Lakini kama watu mmoja mmoja, kama “nyumba,” lazima kila mmoja abaki ameungana na ndugu zake kwa uaminifu na karibu karibu kama sehemu ya jamii ya “mtumwa.” Akionekana mwaminifu mpaka mwisho, kila mmoja atapokea thawabu ya kutokufa kwa kimbinguni. Akimaliza mwendo wake katika mauti, kila mmoja atafufuliwa kwenda mbinguni akawe mmoja wa wafalme na makuhani wa Mungu na wa Kristo wake na atashiriki katika utawala wake juu ya dunia. (1 Kor. 15:50-54; Ufu. 20:4, 6) Wakati huo ataweza kulisha na kuchunga kiroho pamoja na ndugu zake wengine 144,000 ambao wametumikia nyakati zilizopita, tangu wakati wa mitume mpaka sasa. Zaidi ya hayo, jamii hii ya makuhani 144,000 itafurahi sana kutumia ustahili wa dhabihu ya Kristo yenye kupatanisha kwa “mkutano mkubwa” na kwa mamilioni ya maelfu watakaofufuliwa, wakiwaponya na kuwapa ukamilifu wa uzima wale watakaokuwa waaminifu kwa kumtii Mungu.

16. Twatiwaje moyo na matendo ya Kristo kwa “mtumwa mwaminifu mwenye akili”?

16 Kwa hiyo, je! si jambo linalostahili kuwa mwaminifu? Mungu ajua kwamba aliye mwaminifu katika machache atakuwa mwaminifu juu ya mengi. Amehakikisha kwamba aweza kuthawabisha jamii yake ya “mtumwa” kwa daraka lililo kubwa zaidi duniani wakati huu, na kwa baraka za ajabu hata zaidi wakati ujao. Yatutia moyo sote tutumikie kwa uaminifu, tukijua kwamba uaminifu wetu hautasahauliwa, na kwamba Mungu athawabisha waaminifu kupita lo lote ambalo wamepata kujionea.​—Ebr. 6:10.

​—Kutoka Kitabu God’s Kingdom of a Thousand Years Has Approached.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki