Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w75 3/1 kur. 104-110
  • Kwa Uaminifu Uendelee Kuishi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kwa Uaminifu Uendelee Kuishi
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • ULINZI MWAMINIFU WA MUNGU JUU YA WATU WAKE
  • KUTUMIA NGUVU ZA MTU KWA UAMINIFU
  • UENDELEE KUISHI UKITHAMINI UTAWALA WA MUNGU
  • UENDELEE KUWA MWAMINIFU NA KUENDELEA KUISHI
  • Uaminifu—Njia ya Maisha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Je, Wewe Ni Mwaminifu Katika Mambo Yote?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
  • Endelea Kuwa Thabiti Kama Kwamba Unamwona Yeye Asiyeonekana
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • Kuthamini Mambo ya Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
w75 3/1 kur. 104-110

Kwa Uaminifu Uendelee Kuishi

“Lakini mwenye haki ataishi kwa imani yake.”​—Hab. 2:4.

1. Ni nini kinachotazamiwa kwa wale waliomo katika tengenezo la Mungu, na Yeye anawapa nini?

MUNGU mwaminifu ambaye jina lake ni Yehova ana mahali katika tengenezo lake kwa wapenda haki wote. Bila shaka, wale wakubalio ukaribishaji wake wenye fadhili wanaona kwamba unaambatana na kazi nyingi ya kufanywa. Lazima migawo mbalimbali iangaliwe. Lakini katika kuukubali mgawo huo hakuna apaswaye kudharau uwezo wa Mungu kumsaidia mtu atimize daraka na kazi inayohusika. Na, kama ilivyo lazima, Mungu aweza kutoa mafundisho, adabu na mazoezi yanayohitajiwa.​—Flp. 4:13; 1 Kor. 12:18.

2. Uaminifu unahusiana sana na nini, ikifanya nini kiwe cha lazima kwa upande wa wale wanaomtumikia Yehova?

2 Hii yaonyesha nini? Uaminifu kwa upande wa Yehova na kusisitiza kwake kwamba wale wote awakubalio wawe waaminifu pia. Uaminifu unahusiana sana na haki ya Mungu, ambayo ni mojawapo ya sehemu zenye kuvuta za ufalme wa Mungu. (Mt. 6:33) Kwa hiyo ni lazima kwa wale wanaoutafuta ufalme huo na wanaouweka kwanza maishani mwao waishi kulingana na kanuni zenye haki za Yehova. Lazima waondoe nyutu zao za kale zisizo haki na kuvaa nyutu mpya ‘zilizoumbwa kulingana na mapenzi ya Mungu katika haki ya kweli na uaminifu.’ Kisha, kwa mwenendo wao, wataionyesha haki ya Mungu wao mtakatifu Yehova.​—Efe. 4:23, 24, NW; Kol. 3:5-14.

3. Wale walio waaminifu na wenye kutegemeka wanawezaje kutofautishwa na wale wasio waaminifu?

3 Mabadiliko ya lazima yanatokea kwa kipindi fulani katika maisha za wale watakaoendelea kuishi chini ya mpango wa Mungu. Wanaendelea kukua katika maarifa ya kweli mpaka wanapoacha ‘kutupwa huku na huku, na kuchukuliwa na kila upepo wa elimu, kwa hila ya watu.’ Au, kama vile usemavyo mstari wa wimbo wa zamani, wao si ‘wasio na imani kama pepo au bahari’ tena. Bali, wanaimarika, wasitikisike, wakizidi sana kutenda kazi ya Bwana sikuzote,’ wakiwa waaminifu na wenye kutegemeka katika mgawo wo wote unaotolewa.​—Efe. 4:14; 1 Kor. 15:58.

4. Uaminifu wa mtu waonyeshwaje?

4 Waabudu hao imara wa Yehova wanauthamini ubora wa kuishi ndani ya mipaka iliyo salama iliyowekwa na Mungu wao. Si shauri la kujua njia ya kuishi ifaayo, bali kufanya hasa mapenzi ya Mungu yaliyo mema na yenye kukubalika na makamilifu, kuishi kwa uaminifu kulingana na sheria zake, kanuni yake ya haki.​—Yak. 4:17.

ULINZI MWAMINIFU WA MUNGU JUU YA WATU WAKE

5. Tunao uhakikisho gani kutoka kwa Maandiko kwamba Yehova anawaangalia watu wake?

5 Mungu mwaminifu Yehova aweza kutegemewa awatunze na kuwaangalia wale waliojitoa kwake. Yeye aangalia “wanadamu” wote, ‘wabaya na wema’ pia, lakini, hasa, “macho ya [Yehova] huwaelekea wenye haki, na masikio yake hukielekea kilio chao.” (Zab. 11:4; Mit. 15:3; Zab. 34:15) Akihakikisha hili, Mfalme Daudi pia aliandika hivi: “Nalikuwa kijana nami sasa ni mzee, lakini sijamwona mwenye haki ameachwa, wala mzao wake akiomba chakula.”​—Zab. 37:25.

6, 7. (a) Ni wapi tulipo na ushuhuda kwamba Yehova aliuona uaminifu wa wanaume na wanawake zamani? (b) Ni nini nyingine za sifa zenye kutokeza walizo nazo waaminifu hawa wa zamani?

6 Kama ushuhuda wa kwamba Yehova aliwaangalia waliokuwa waaminifu kwake nyakati zilizopita yeye anatupa mengine ya majina yao. Kwa mfano, mna orodha ya majina kadha katika sura ya kumi na moja ya Waebrania. Masimulizi haya yaliyofupizwa yanaeleza kwa uchangamfu mengine ya mambo ambayo katika hayo wenye haki hawa walipitia ili kuhakikisha uaminifu wao. Walimjua Yehova kuwa msaidizi wao. Waliyosema na kufanya wengine yalishindwa kuwafadhaisha au kuwaondoa wasimtumikie Yehova kwa uaminifu. Walivumilia namna zote za majaribu na mateso, nao “ulimwengu haukustahili kuwa nao.” Lakini walikuwa wenye thamani sana machoni pa Mungu na katika kumbukumbu lake nao watathawabishwa kabisa kwa ufufuo walioutumainia.​—Ebr. 11:38.

7 Walijitahidi wasitawishe kumbukumbu jema na hali yenye haki mbele za Mungu. Mojawapo ya sifa zenye kutokeza zilizoonyeshwa na mashahidi hao wa kale ilikuwa nguvu zao nyingi sana sana, bidii yao ya yaliyokuwa haki. Mtu anavutwa pia na imani, uaminifu na upendo ambao watu hawa wa kale walionyesha katika utumishi wao kwa Mungu. Walishikamana kwa imara na waliyoijua kuwa ndiyo njia ya Mungu ya uzima. Kumbukumbu la wanaume na wanawake hawa wa zamani wenye imani limehifadhiwa mpaka sasa kututia moyo.​—Rum. 15:4; 1 Kor. 10:11.

8. Ni mifano gani mingine iwezayo kutajwa ya wale walioishi kwa imani zamani?

8 Mifano mingine ya wale walioendelea kuishi zamani kwa njia iliyompendeza Yehova ni Zakaria na Elisabeti mkewe. Mwenzi wa mtume Paulo Luka anatoa habari hizi juu yao: “Wote wawili walikuwa wenye haki mbele za Mungu, wakiendelea katika amri zote za [Yehova] na maagizo yake bila lawama.” Na kwa hiyo baadaye sala zao zilijibiwa, naye Zakaria na mkewe wakawa wazazi wa Yohana Mbatizaji, mtangulizi wa Masihi.​—Luka 1:5-13.

9. (a) Wengine wa wajane waaminifu wanaotajwa katika Biblia walikuwa akina nani? (b) Ni somo gani la uaminifu tuwezalo kujifunza kutokana na masimulizi yaliyomo katika Marko 12:41-44?

9 Wajane fulani wenye imani nyingi wanatajwa kwa majina katika Biblia, kama vile Naomi, Ruthu, Abigaili na Hana nabii wa kike. Zaidi ya hayo, baada ya kuwatazama waabudu wakiweka fedha katika masanduku ya hazina ya hekalu, Yesu alikaza fikira za wanafunzi wake kwenye mjane mmoja asiyeonyeshwa jina lake, akisema: “Amin, nawaambia, Huyu mjane maskini ametia zaidi kuliko wote wanaotia katika sanduku la hazina; maana hao wote walitia baadhi ya mali iliyowazidi; bali huyu katika umaskini wake ametia vyote alivyokuwa navyo, ndiyo riziki yake yote pia.” (Marko 12:41-44) Hatumjui jina lake, lakini anatajwa kwa upendeleo nao mchango wake mdogo waweza kutufundisha somo la uaminifu katika kutegemeza ibada ya kweli. Ukubwa wa mchango hautoi maoni ya kweli kwa lazima juu ya ukarimu wa mpaji. Mjane huyu alitaka kuonyesha upendo wake kwa Yehova na kufanya hivyo kwa njia yake ya unyenyekevu.

10. (a) Je! kumbukumbu la Biblia linatoa majina na orodha ya matendo ya watumishi waaminifu wote wa zamani wa Mungu? (b) Kwa hiyo twaweza kujifunza nini kutokana na hili?

10 Kwa vyo vyote si kila mtu ambaye amepata kuwa mwaminifu kwa Yehova amehifadhiwa jina lake au matendo yake katika kumbukumbu la Biblia. Je! hii yamaanisha kwamba Yehova alikosa kuuona mwendo wao wa maisha au kwamba matendo yao ya uaminifu ameyasahau? Sivyo, hata kidogo. Yehova amekuwa akiyatambua sana yote waliyosema na kufanya. Hakuna mmoja wa waaminifu hao walioonyesha ukamilifu katika ibada yao ya Mungu Aliye Juu Zaidi amesahauliwa na Mungu wa umilele. Wao pia ni sehemu ya “wingu kubwa la mashahidi” litakalothawabishwa uzima katika taratibu mpya kwa sababu ya uaminifu wao. (Ebr. 12:1) Wao pia ni mifano myema kwetu tuwaige. Kwa njia gani? Kwa sababu tunayofanya hayapaswi yawe “utumwa wa macho tu kama wajipendekezao kwa wanadamu” wala kwa ajili ya kusifiwa au kukumbukwa na wanadamu.​—Efe. 6:6; Kol. 3:22; linganisha Mathayo 6:1-4.

11, 12. Kuna ushuhuda gani kwamba Yehova aliwajua sana wote wale waliokuwa waaminifu kwake siku za Eliya?

11 Wengine wa mashahidi hawa wasiotajwa jina waliishi katika karne ya kumi B.C.E. Ulikuwa wakati ambapo macho ya Yehova yaliwaona waliokuwa wanafuata ibada yake katika taifa la Israeli. Wakati huo Ahabu mwovu na mkewe Yezebeli walidhamini ibada ya Baali nchini, naye nabii Eliya akaona ni lazima awatoroke akaokoe uhai wake. Akiwa amejificha pangoni, alimweleza Yehova kwamba aliona alikuwa ndiye mwabudu wa pekee wa Yehova katika Israeli yote, mtu wa pekee aliyekuwa mwaminifu kwa utumishi wa Yehova. Walakini, Yehova alisahihisha mawazo yake juu ya jambo hili, kwa njia hiyo akionyesha kwamba Yeye alijua yaliyokuwa yakiendelea taifani. Walikuwako wengine wengi zaidi ya nabii huyo mwaminifu wasiokubali ibada ya uongo.​—1 Fal. 19:1-10, 18.

12 Akiwapambanua wema na wabaya, Yehova alimwambia Eliya kwamba walikuwako “wengi, ndiyo, elfu saba zaidi ya nabii, wasiokuwa wamempigia Baali magoti wala kumbusu mungu huyo wa kuchukiza sana. Kupiga magoti mbele ya sanamu na kuzibusu kama tendo la kuheshimu mno kulikatazwa sana na Yehova. (1 Fal. 19:14; Kut. 20:4, 5) Hapa tena, ingawa hatupewi orodha ndefu ya majina yao, ni wazi kwamba Mungu aliwajua wote, maelfu haya waliokuwa wenye haki kwa kushikamana na ibada ya kweli na kuepuka kuchafuliwa na ibada ya uongo ya Baali, hata ingawa hii iliwatia katika hatari ya kuuawa na Yezebeli mwovu.

13. Kijana mwanamke Mwisraeli asiyetajwa jina alihakikishaje uaminifu wake kwa Yehova?

13 Si miaka mingi baada ya matukio haya aliishi “kijana mwanamke” aliyetekwa na vikosi vya watekaji vya Washamu. Hatuambiwi jina lake, lakini Yehova alijua naye bila shaka atamthawabisha kwa sababu ya matendo yake ya uaminifu kwake. Ajapokuwa mtumwa katika nchi ngeni, yeye hakusita kumtolea ushuhuda mke wa Naamani, mkuu wa jeshi la Shamu, juu ya uwezo mkuu aliokuwa ameuonyesha Mungu wake Yehova kupitia kwa nabii wake mwaminifu.​—2 Fal. 5:1-4.

14. Mpwa wa mtume Paulo alijaribiwaje kwa habari ya uaminifu wake?

14 Wala mwana wa dada ya mtume Paulo hatajwi jina, lakini kijana huyu mwanamume alimpasha Paulo habari, kisha jemadari wa jeshi, namna mpango wa hila ulivyokuwa umepangwa na zaidi ya watu 40 wamwue mjomba wake Paulo. Maoteo yalitatanishwa na tendo hili la haraka kwa upande wa kijana mwanamume aliye mwaminifu. Bila shaka Yehova awapenda vijana kama hawa wanaotanguliza faida za watu wa Mungu mbele ya faida zao wenyewe. Lo! ni mfano mwema namna gani kwa vijana leo kuangalia kwa uaminifu faida za Ufalme walizokabidhiwa!​—Matendo 23:12-22.

15. Masimulizi haya ya Biblia ni yenye faida gani ya pekee kwetu leo?

15 Ni chanzo cha kutia moyo kusoma katika Biblia masimulizi ya mifano ya kale ya maisha ya uaminifu. Kwa maana kwa kuchunguza maandishi hayo twaona namna Yehova alivyowapenda na kuwalinda watumishi wake. Hili nalo linaamsha katika Mashahidi wa kisasa tamaa ya kumtumikia Mungu yule yule anayeishi milele kwa uaminifu.

KUTUMIA NGUVU ZA MTU KWA UAMINIFU

16, 17. (a) Twaona nini duniani leo kinacholingana na “wingu kubwa la mashahidi” nyakati za kale? (b) Wanaonyeshaje kwamba ‘wanaendelea kuishi’ kwa uaminifu?

16 Kutoka mataifa yote leo “mkutano mkubwa” wa watu unajiunga na “mabaki” ya ndugu za Bwana kuzihubiri “habari njema” za Ufalme kama ilivyoelezwa kwa unabii na Yesu Kristo. (Ufu. 7:9; Mt. 24:14) Wamejifunza kwamba kuna furaha nyingi katika kuyashiriki mambo mema wanayoyajua sasa na wengine. (Matendo 20:35) “Mkutano” huu, ambao sasa ni mamia mengi ya maelfu, hawajidai kuwa na uwezo wo wote wa mwujiza​—ni tamaa ya unyofu tu ya kumtumikia Yehova kwa moyo wao wote, akili na nafsi. Kwa hiyo wamekata maneno kuendeleza faida za Ufalme wakiwa na nguvu chache walizo nazo.

17 Wakiwa wanaishi karibu na mshindo wa Har–​Magedoni na baraka zisizolinganika za uzima zitakazofuata, mashahidi hawa wa kisasa wa Yehova wanajua kwamba sio wakati wa kufuata mwendo wa maisha wa vivi hivi. Bali, kwao ndio wakati wa maana kuliko nyakati zote, kipindi cha kutumia wakati wao wote, nguvu zao chache na uwezo wao mbalimbali wa asili katika utumishi wa Mungu. Wao wanajua kwamba kupewa karama za miujiza za roho kuliishia na mitume katika karne ya kwanza. Kwa hiyo, ni kwa kujifunza kwa bidii na kuyatumia wanayojifunza, na kwa kuitumia kwa faida mipango yote yenye kuelimisha iliyotolewa na Yehova, kwamba wapya hawa wanaweza kufanya maendeleo ya haraka wakawe tayari kabisa kwa kazi iliyopo. Wanafanya hili pia kwa bidii.​—2 Tim. 3:16, 17.

18, 19. (a) Leo utawaona wapi wale walio na roho ya Mfalme Hezekia wa kale? (b) Taja mifano.

18 Yampasa mtu atembelee tu mojawapo la makundi zaidi ya 32,000 ya mashahidi wa Yehova aone mifano ya kweli ya wale ambao leo wanayo roho ya Mfalme wa kale Hezekia, kama inavyoelezwa katika 2 Mambo ya Nyakati (Siku) 31:21: “Aliifanya [kazi] kwa moyo wake wote, akafanikiwa.” Kwa mfano, kundi moja lilifurahi kuuona uvumilivu wa ndugu painia akiwa katika mwaka wake wa 90. Tena alikuwa akitumikia kama mwangalizi wa shambani, na alikuwa akihudhuria mikutanoni sikuzote. Baada ya kutumia miaka 58 akiwaeleza wengine habari njema za Ufalme, lo! alikuwa mwenye furaha namna gani kuyaona matokeo ya kazi yake​—nyingine za ‘barua zake mwenyewe zenye sifa’ zikitumikia pamoja naye katika kundi lile lile!​—2 Kor. 3:1-3.

19 Ukienda kwenye Jumba la Ufalme kwa kawaida, baadaye nawe pia utafahamiana kwa kipekee na wengine kati ya wale wanaoendelea katika njia ya uzima bila kuiacha, watu wanaotumia miaka yao ya ukongwe maishani katika kumsifu Muumba wao mkuu na kusaidia wengine walijue jina na kusudi lake. Wao ni watu wanaoendelea kutoa nguvu zao chache kila siku wanapoishi maisha yao kwa uaminifu, hata mpaka kufa. (Ufu. 2:10) Shahidi mmoja wa kike, akieleza alivyoona juu ya kuwa mzee na mgonjwa, alisikitika kwamba alikuwa anakuwa msahaulifu kidogo na aliona shida nyingi kufanya mambo katika mwendo mmoja na mashahidi wachanga zaidi wa Yehova. Lakini watu kama hao wanaweza kufarijika kwa kujua kwamba wanaendelea kuwa mfano wa imani na uvumilivu wa kuigwa na walio wachanga zaidi. Kama mtume Paulo, wanaweza kusema, “Iweni waigaji wangu mimi, kama mimi nilivyo mwigaji wa Kristo.”​—1 Kor. 11:1, NW.

20. Ni nini mengine ya magumu ambayo lazima Mashahidi washindane nayo katika kuhakikisha uaminifu wao kwa Yehova?

20 Yawapasa Mashahidi wengi washinde vizuizi vingine zaidi ya udhaifu wa ukongwe wanapofuata mwendo wa uaminifu kwa Yehova. Wengine wamepoteza macho yao ya kimwili. Wengine wana magumu ya kusikia; wengine bado ni viwete. Hali twaona kwamba wao pia wanatumia nguvu zao kwa uaminifu katika utumishi wa Yehova ‘wanapompa Mungu dhabihu ya sifa, yaani, tunda la midomo iliungamayo jina lake.’​—Ebr. 13:15.

21. Ni njia gani ya kale ya kusafiria ambayo ingali ikitumiwa sana na mashahidi waaminifu wa Yehova?

21 Wasio wa kusahauliwa ni Mashahidi wengi ambao kwa miaka mingi wamekuwa wakienda mlango kwa mlango katika kazi ya ushuhuda, nao wamekuwa wakifanya hivyo bila faida ya kusafiria. Wahubiri wengine wazee walio waaminifu wanaweza kukadiri wametembea umbali gani katika utumishi huo wa shambani, nao wanasema kwamba, nyakati nyingine, umbali wote unakuwa kama kuizunguka dunia mara moja au zaidi. Katika habari yao andiko linaelekea kufaa sana lisemalo hivi: “Ni mizuri kama nini miguu yao wahubirio habari ya mema!”​—Rum. 10:15.

UENDELEE KUISHI UKITHAMINI UTAWALA WA MUNGU

22. Baada ya kuangalia masimulizi haya, mtu aachwa akiwa na maoni gani?

22 Katika kurudia kuangalia masimulizi ya maisha ya watumishi waaminifu wa Yehova, mtu anavutwa na uhakika wa kwamba wanaume na wanawake hawa, wa zamani na wa sasa pia, waliithamini sana enzi kuu ya Mungu hata wakahatirisha maisha zao wakiitetea. Hii yatuonyesha kwamba namna ya watu ambao Yehova ataka waendelee kuishi ni wale wanaomtumikia kwa sababu ya kumpenda yeye na sifa zake zenye haki. Wanampenda yeye kwanza na zaidi ya wote. (Mt. 22:37, 38) Watu ambao wamevumilia sana wanaweza kushuhudia kwa unyofu kwamba wanaupendelea kweli utawala wa Mungu kuliko mwingine wo wote. Shahidi mmoja alieleza hivi: “Nashukuru nilikuwa na miaka niliyokuwa nayo kumtumikia Yehova. Mimi sisikitiki hata dakika moja juu yake, ingawa zilikuwako nyakati nyingi zenye kujaribu.”

23. Wakiithamini enzi kuu ya Yehova, ni nini nia ya mashahidi wa Yehova juu ya watawala wa kisiasa wa ulimwengu huu?

23 Wateteao yaliyo haki na kweli na mema wanamtegemea Mpaji wa sheria aliye mkuu kupita wote, wakikaza fikira sana kwenye sheria zake na kanuni kama ziwezazo kutumika katika maisha yao ya kila siku. Hakuna mahali pengine po pote ambapo wangependa wawe isipokuwa ndani ya mpango wa Yehova kwa waabudu wake. (Zab. 84:10) Sikuzote wanapata burudisho kwa kwenda nyumba kwa nyumba, wakitafuta wale wanaoomba ufalme wa Mungu uje, na mapenzi yake yenye haki yatendwe duniani, na watakao kuishi milele chini ya serikali hiyo kamilifu. (Mt. 6:9, 10; 6Yohana 17:3) Wao wasingeridhishwa kamwe na ahadi za mwanasiasa wa kidunia, wala wasingechagua kamwe kuwa na mfalme wa kibinadamu juu yao. (Linganisha 1 Samweli 8:1-9.) Wakati wa wakf, watu hawa waliamua kutegemeza enzi kuu ya Yehova, na tangu wakati huo wamejitahidi kufanya maamuzi yao yote yategemee uchaguzi huo wa kwanza.

24. (a) Mara nyingi walimwengu wanawaonaje Mashahidi? (b) Lakini ni kwa njia gani peke yake Mashahidi wawezavyo kuendeleza dhamiri safi kabisa mbele za Mungu?

24 Mashahidi hao wa Yehova waliobatizwa lazima watembee kwa uangalifu sana kati ya waovu wa kizazi hiki, wakijua kwamba wana daraka kwa mtu aliye juu zaidi katika ulimwengu wote, Mpaji wa sheria na Hakimu mkuu. (Yak. 4:12) Ingawa watu wengine wanaweza kushangazwa na kushikamana kwao na kanuni za Biblia, sababu gani waiache njia ya haki au hata wajaribu kuzivunja au pengine kuzipinda sheria za Mungu kwa ajili ya kujifaidi wenyewe? (1 Pet. 4:3-5) Kwa hakika yeye aliyeumba vyote anayo haki ya kuwa wa kwanza katika maisha za watu wake. Yeye pia anastahili kupata ibada yao na utii wao wote. Kuheshimu kwao Bwana Mwenye Enzi Kuu katika mawazo na njia zao zote, kutawasaidia sana watende mbele zake wakiwa na dhamiri safi kabisa.​—Mit. 3:5; Matendo 23:1.

25, 26. (a) Tuko wapi katika kipindi cha wakati, hii aitokeza uhitaji gani? (b) Kwa kuitikia, twaona nini likitukia kupatana na 1 Yohana 5:3?

25 Kuthamini utawala wa Mungu kumepaswa kuvute watu wenye mioyo ifaayo leo wauitikie mwito Wake wa utumishi. Kuna uhitaji wa wafanya kazi zaidi wenye nia katika tengenezo la Mungu linalopanuka sikuzote na kuhubiri na kufundisha. Tukiwa tumesimama karibu sana na tukio lililo kubwa zaidi kupita yote katika historia, wote wapendao haki wamepaswa watende sasa kihodari, wakijua kwamba mwendo wo wote watakaofuata utahusu matumaini yao ya uzima wa milele.​—2 Pet. 3:11-14.

26 Makumi ya maelfu ya watu wa hali zote na ujuzi wa maisha wanapata maarifa ya kweli kila mwaka na kupatanisha maisha zao na sheria na kanuni za Mungu. Bila shaka yamaanisha mabadiliko mengi​—kuondosha tabia za zamani, kufanya mpya. Yamaanisha kukubali maagizo, mazoezi na elimu. Yamaanisha kujifunza kumpenda na kumtii Yehova. Lakini hiyo ni vigumu sana? Mtume Yohana alisema: “Kwa maana huku ndiko kumpenda Mungu, kwamba tuzishike amri zake; wala amri zake si nzito.”​—1 Yohana 5:3.

UENDELEE KUWA MWAMINIFU NA KUENDELEA KUISHI

27. Je! imani peke yake ndiye inayohitajiwa ili kuwa na kibali ya Yehova?

27 “Mwenye haki wangu ataishi kwa imani,” ndio usemi wa waziwazi upatikanao katika Waebrania 10:38. Kisha Maandiko yaonyesha lazima mtu aongezee imani hiyo mambo mengine kama wema, maarifa, kujiweza, saburi, utauwa, upendano wa ndugu na upendo. (2 Pet. 1:5-7) Ni jambo la maana pia kutumia uwezo wa asili alio nao mtu katika utumishi mtakatifu wa Mungu ikiwa anataka kweli afurahie maisha.

28. Kwa sababu ya kuwekwa (kwa wazee) katika makundi, imempasa kila mtu ajiulize nini?

28 Wengine wa wanaume waaminifu ambao wamejitumia kwa njia hiyo wanawekwa wawe waalimu kundini, na kama ‘wachungaji wa kundi la Mungu’ wanachukua daraka zito. Waalimu hawa wenye kustahili wanahitajiwa wasaidie wengine kuufikia umoja katika imani pamoja na maarifa ya kweli. (1 Pet. 5:2; 2 Tim. 2:2; Efe. 4:11-13) Yafaa kulingana na Maandiko wanaume waliokomaa kundini wafikie pendeleo hili la ziada kama waangalizi; ni “kazi njema.” Ni vema wewe ujichunguze uone kama unasonga mbele. Jiulize, ‘Je! naweza kuendeleza uwezo wangu mbalimbali au nguvu zangu zisizokomaa bado ili niweze kuwa mwenye mafaa zaidi kundini na hivyo niishi kwa kulingana zaidi na utukufu wa Mungu?’​—1 Tim. 3:1-13.

29. Twawezaje kuonyesha twathamini kadiri ya uzima tulio nao mmoja mmoja, na kwa matokeo gani?

29 Itaridhisha kujua kwamba tumeonekana waaminifu. Kwa hiyo na tuthamini sana na kutumia kwa hekima kadiri ya uzima tulio nao, tukizaa tunda lenye haki kila siku kwa heshima na sifa ya Mungu. Tuwe wapya au wazee katika njia ya uzima, na tuufanye uamuzi wetu uwe kutoacha cho chote kitutenganishe na Yehova Mungu. Nao upendo wa Mungu usiovunjika utatutegemeza katika mwendo wetu wa uaminifu hata chini ya jaribu kali. (Rum. 8:38, 39) Kufanya kwetu mambo yote kwa utukufu wa Mungu kutatuzuia tusiruke mipaka au kuiacha njia ya haki iliyoonyeshwa wazi iongozayo kwenye uzima wa milele.

30. Twawezaje pia kushiriki katika kuufurahisha moyo wa Yehova?

30 Sikuzote tamaa yetu kubwa na iwe kuendeleza ukamilifu kwa Mungu wetu mwaminifu na kuhakikisha kwamba hakuna ye yote, hata adui ya Mungu Ibilisi, awezaye kutuondoa katika mwendo huu. Kwa njia hii twaweza kuufurahisha moyo wa Yehova.​—Mit. 27:11.

—Kutoka The Watchtower, Sept. 1, 1974.

[Picha katika ukurasa wa 106]

Kijana mwanamke Mwisraeli aliyetekwa alionyesha uaminifu kwa Yehova kwa kumpasha habari mke wa Naamani juu ya Elisha, nabii wa Mungu wa kweli

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki