Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w75 7/1 kur. 291-296
  • Je! Wewe Unaonyesha Kuthamini

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Wewe Unaonyesha Kuthamini
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • UHUSIANO WA JAMAA
  • KUTHAMINI AMBAKO YEHOVA ANAONYESHA
  • KUONA UBORA MWINGI WA UHUSIANO MWEMA NA MUNGU
  • Faida Zenye Kudumu Kutokana na Kuifuata Biblia Kama Jamaa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Ubora wa Kutia Adabu katika Upendo
    Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha
  • Zoeza Mtoto Wako Tangu Utoto Mchanga Sana
    Siri ya Furaha ya Familia
  • ‘Sikiliza Nidhamu Uwe na Hekima’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2018
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
w75 7/1 kur. 291-296

Je! Wewe Unaonyesha Kuthamini

“Jipatie hekima, jipatie ufahamu. . . . Uthamini sana, nao utakutukuza.”​—Mit. 4:5, 8, NW.

1, 2. (a) Vingine vya vitu tunavyopaswa kuthamini maishani ni nini? (b) “Kuthamini” hasa maana yake nini, nako kwaonyeshwaje?

VIKO vitu vingi maishani tunavyopaswa kweli tuthamini. Imetupasa tuwathamini baba na mama zetu. Wao ndio waliotuingiza ulimwenguni wakatumia wakati mwingi sana wakitulea. Imetupasa tuuthamini uangalizi waliotupa sisi. Ikiwa tuna rafiki za kweli, tuna sababu nzuri kuwathamini wao pia. Na namna gani juu ya mambo tunayojifunza, kazi tunayofanya na zawadi tunazopokea​—je! tunaonyesha kuthamini vitu vyote hivi? Mara nyingi, zawadi inapopokewa mtu anayeipokea anasema, “Asante, naithamini sana.” Lakini ulizo linaweza kuulizwa: Je! mtu huyo anaithamini kweli? Je! kweli yeye anatamani kwamba ingalikuwa afadhali kama angalipewa kitu kingine, au hata asipewe cho chote? Yeye ataitumiaje? “Kuthamini” kuna maana gani hasa?

2 Neno “kuthamini” lina maana ya “kuheshimu sana, kuona ubora mwingi, kukubali kwa uchangamfu.” Wewe mwenyewe unaheshimu sana watu gani? Ni mambo gani unayoonea ubora mwingi na kuyakubali kwa uchangamfu? Unaonyeshaje hivyo? Ikiwa kweli kuthamini kupo, kutakuwa wazi katika mambo unayosema na kufanya.

UHUSIANO WA JAMAA

3. Ingawa kwa kawaida kuna ukamatano wenye nguvu kwa wazazi wa mtu, mtoto anawezaje kuonyesha kwamba kweli hawathamini wao?

3 Mtoto mdogo sana kwa kweli hana maono ya kuthamini. Walakini, ana ukamatano wa asili na baba yake na mama yake ambao ni wenye nguvu. Kunapokuwa na hatari, anajua kwa kukimbilia apate ulinzi. Kwa mfano, mtoto anaweza kuwa anaruka-ruka katika ua, na mtoto huyo anaweza kushikwa na woga. Anakimbia na kumshika mama yake kwa nguvu na kuficha kichwa chake katika rinda la mama yake, naye anajiona kulindwa. Ikiwa mama amemtendea mtoto huyo kwa njia ya upendo siku zilizopita, mtoto anajiona salama hapo. Kwa kweli anadhani kwamba huu ndio ulinzi wote anaohitaji asipatwe na mshambuliaji ye yote. Lakini mtoto anajihangaikia kwa njia ya asili. Anapokaripiwa kwa sababu ya mwenendo fulani mbaya inaweza kuonekana wazi kwamba kwa kweli mtoto anaweza kukosa kuthamini mama yake na uongozi wake.​—Mit. 12:1.

4. (a) Baadaye, ni nini kinachoweza kusaidi kufanya mtu athamini wazazi wake? (b) Kuthamini huko kunapositawi, kunaweza kuonyeshwaje?

4 Walakini, mtu anapokuwa mtu mzima anakuwa na maoni tofauti sana juu ya mambo na yale aliyokuwa nayo alipokuwa mtoto. Mtume Paulo alisema hivi: “Nilipokuwa mtoto mchanga, nalisema kama mtoto mchanga, nalifahamu kama mtoto mchanga, nalifikiri kama mtoto mchanga; tokea hapo nilipokuwa mtu mzima, nimeyabatilisha mambo ya kitoto.” (1 Kor. 13:11) Ili awe na kuthamini lazima mtu awe na maarifa, na lazima maarifa hayo yaufikie moyo. Mtu anapokua awe mtu mzima anajipatia maarifa, na mambo yanayompata mwenyewe yanaweza kufanya maarifa yauvute moyo wake. Sasa anafikia hatua ambapo anaweza kuthamini au kuona ubora wa waliyomfanyia baba na mama yake alipokuwa kitoto kichanga. Pengine sasa analea watoto wake mwenyewe, anakutana na magumu ya kutia adabu, anakosa usingizi awaangalie watoto wanapokuwa wagonjwa, na anafanya kazi saa nyingi ahakikishe kwamba wanalishwa na kuvalishwa na kupata makao. Sasa yeye mwenyewe anajifunza saburi na kuhangaika kwenye upendo kunakotakiwa kulea watoto wa mtu katika “adabu na rekebisho la moyoni la Yehova.” (Efe. 6:4, NW) Mambo haya yanayompata yanaweza kumfanya yeye na mkewe wafikirie siku zilizopita walipokuwa watoto wadogo, na pengine kwa mara ya kwanza katika maisha zao wanathamini kabisa mambo ambayo wazazi wao waliwafanyia. Sasa wanaweza kuona ubora mwingi na kukubali kwa uchangamfu sana mambo ambayo wazazi wao wenyewe walifanya. Kuthamini huko kunapositawi, ni vizuri kukuonyesha, na hii inaweza kufanywa tena na tena, kwa njia mbalimbali.​—1 Tim. 5:4.

5. Kwa habari ya nia ambayo hata watoto wadogo wamepaswa wasitawishe juu ya wazazi wao, Biblia inasema nini?

5 Ingawa itatazamiwa kwamba kuthamini yale ambayo wazazi wa mtu wamefanya kunaweza kukosa kusitawi kabisa mpaka mtu afikie utu mzima, Maandiko yanasema hivi hata kwa watoto wadogo: “Waheshimu baba yako na mama yako; kama [Yehova], Mungu wako, alivyokuamuru, siku zako zipate kuzidi, nawe upate kufanikiwa.” (Kum. 5:16) Ukimheshimu baba yako na mama yako, utakuwa ukionyesha heshima nyingi au kuwathamini.

6. (a) Wewe umeona nini kinachotoa ushuhuda wa ukosefu mzito wa watoto kuthamini wazazi wao? (b) Ni mambo gani yanayoweza kushiriki kuleta hali hiyo nyumbani, lakini ni nini kinachoweza kusaidia kuiepuka?

6 Kwa kutofaa, watoto wanaonyesha ukosefu wenye kushangaza unaoendelea kuwapo wa kuwathamini wazazi wao. (2 Tim. 3:1, 2; Kum. 27:16) Ugumu mkubwa unaweza kuwa kwamba wazazi wenyewe hawathamini watoto wao. Pengine wao hawakuwataka hasa na kwa hiyo hawawaoni kwa njia inayosemwa katika Zaburi 127:3: “Tazama, wana ndio urithi wa [Yehova], uzao wa tumbo ni thawabu.” Kwa kukosa maoni hayo yafaayo, pengine wazazi hawatumii wakati wakiwa pamoja na watoto wao, hawashiriki nao inavyotakiwa na hawajibu maulizo yao mengi. Nyakati nyingine, watoto ndio wamekosa kuitikia uangalizi wenye upendo wa wazazi wao wakiongozwa na mashirika mabaya. Lakini wazazi na watoto pia wakitumia mashauri yafaayo ya Neno la Mungu kwa bidii yatasaidia kuzuia hali hiyo isiyopendeza isisitawi. Walakini, imepaswa ifahamike kwamba kusema tu kwamba mtu ana kuthamini hakuhakikishi hivyo. Je! nia ya mtu na matendo ya kila siku yanatoa ushuhuda wa jambo hilo?

7. (a) Nia ya baba kutia adabu au ukosefu wake inaonyesha nini juu ya maoni yake kwa watoto wake? (b) Adabu hiyo imepaswa itiweje?

7 Katika kujibu ulizo hilo, nia inayoonekana wazi nyumbani juu ya kutia na kupokea adabu imepaswa ifikiriwe. Baba anayependa watoto wake atahakikisha kwamba wanapokea adabu inayohitajiwa. (Mit. 13:24) Kitabu cha Mithali, katika sura ya nne, mstari wa 1, kinatuomba tuthamini adhabu, kikisema hivi: “Wanangu, yasikilizeni mausia ya baba yenu, tegeni masikio mpate kujua ufahamu.” Sikuzote adabu haina maana ya kuadhibu kwa kuonyesha makosa au kuzoeza kwa kutaabisha. Maana ya kwanza hasa ya “adabu,” kulingana na kamusi ni “kutendewa kunakofaa mwanafunzi, elimu, kusitawisha uwezo mbalimbali kwa kufundisha, kuzoeza, kulea, kuwe ni kwa njia ya kimwili, akili au adili.” Kwa hiyo tunaposoma juu ya kutia kwa baba adabu tusifikirie mwanamume anayetoa amri kwa ukali kwa watoto wake kisha anawapa adhabu ya kimwili wasipofanya wanayoambiwa. Tunazungumza juu ya baba anayeangalia watoto wake kweli kweli, anayetumia wakati akiwa pamoja nao na kupendezwa sana na ukuzi wao wa kimwili, wa akili na adili. Yeye anataka kusaidia watoto wake wapate kumjua Mungu wa kweli na njia Zake kama baba anavyomjua. Yeye anataka wawe na hakika katika uangalizi wa Mungu na katika utimizo wa kila jambo ambalo Yeye ameahidi. (Mwa. 18:19; Kum. 11:18, 19) Baba wa namna hiyo atasaidia watoto wake kwa saburi wasitawishe sifa za kimungu kama vile upendo, furaha, amani, ustahimilivu, fadhili, wema, imani, upole na kujiweza. (Gal. 5:22, 23) Kwa hiyo, ingawa ni kweli kwamba ziko nyakati ambapo adhabu inaweza kuhitajiwa, wakati Biblia inaposema, “Wanangu, yasikilizeni mausia [“adabu,” NW] ya baba yenu, tegeni masikio mpate kujua ufahamu,” imetupasa tufikirie hasa baba anayetoa mafundisho ya akili na adili kwa watoto wake kwa saburi.

8. Imewapasa watoto waitikieje kutiwa adabu na wazazi, na kwa sababu gani?

8 Vijana wa kiume na wa kike wanaoheshimu wazazi wao, na kwa njia hii wanamheshimu Mungu, hawatadharau kwa uasi adabu hiyo. Watasikiliza Maandiko yanapowaambia hivi: “Mpumbavu hudharau kurudiwa [‘kutiwa adabu,’ NW] na babaye; bali yeye aangaliaye maonyo hupata busara.” (Mit. 15:5) Wao watafikiria kwa uzito yaliyoandikwa katika Mithali 4:13: “Mkamate sana elimu [“adabu,” NW], usimwache aende zake; mshike maana yeye ni uzima wako.” Je! wewe unaitikiaje?

9. Maana yake nini ‘kujipatia hekima,’ na kijana anawezaje kuonyesha kwamba atathamini ubora wake?

9 Mithali zilizoongozwa na Mungu zinaendelea kuomba hivi: “Jipatie hekima, jipatie ufahamu. Usisahau, wala usigeuke kando uziache semi za kinywa changu. Usiuache, nao utakuhifadhi. Upende, nao utakulinda. Hekima ndilo jambo bora. Jipatie hekima; na pamoja na yote utakayojipatia, jipatie ufahamu. Uthamini sana, nao utakutukuza. Utakuadhimisha kwa sababu unaukumbatia.” (Mit. 4:5-8, NW) Kijana anaposikiliza mafundisho ya baba yake, akikubali adabu yake, atajipatia hekima. Atajifunza namna ya kutumia mambo ambayo baba yake amemwambia katika maisha yake mwenyewe. Yeye hataacha mafundisho hayo ‘yaingilie sikioni moja na kutokea katika jingine.’ Wakati kijana anapoelewa kweli maana ya onyo la upole la Maandiko, akifahamu kwamba “hekima ndilo jambo bora,” atakuwa mwenye nia ya kusikiliza wazazi wake na atakuwa mwenye bidii ya kufaidika kutokana na maono yao katika maisha. ‘Atathamini sana’ hekima wanayotoa, na hasa inapopatana na Neno la Mungu mwenyewe, Biblia.

10. Hekima ya kimungu pia inahusuje uhusiano wa mume na mke kwa njia yenye mafaa?

10 Hekima ya kimungu inapoongoza kuwaza kwa wazazi, si kwamba tu watapata matokeo mazuri katika kushughulika na watoto wao, bali pia uhusiano watakaokuwa nao mmoja na mwenzake kama mume na mke utakuwa wenye kujenga na kutia nguvu. Mke hatakuwa na wasiwasi unaotokana na kumfanyia mambo mume asiyethamini, naye mume atakuwa na hakika juu ya kuungwa mkono kwa uaminifu na mke wake. Kikiwasaidia wasitawishe roho ya kuthaminiana, Kitabu cha hekima ya kimungu kinasema hivi: “Apataye mke [mwema] apata kitu chema; naye ajipatia kibali kwa [Yehova].” (Mit. 18:22) Pia, “mke asikose kumstahi mumewe.”​—Efe. 5:33.

11. Badala ya kudai mumewe amthamini, mwendo bora kwa mke ni nini?

11 Ingawa ni kweli kwamba waume na wake wanapaswa kuthaminiana, wonyesho wa kuthamini unamaanisha mengi zaidi wakati wasipodaiwa wafanye hivyo bali wanapoongozwa na kutaka kuvuta moyo wa mwenzao. Hii inaweza kufanywaje? Ingawa ni jambo la kawaida kwa mwanamke kutaka awe mwenye kuvutia kwa njia ya kimwili, mambo mengine ni ya maana hata zaidi. Mithali 31:30, NW inasema hivi: “Mapendezi yanaweza kuwa ya uongo, nao urembo unaweza kuwa wa bure; lakini mwanamke anayemwogopa Yehova ndiye anayejipatia sifa.” Baadaye, hata mwanamume ambaye pengine haamini mara kwa mara anavutwa na “mwenendo safi pamoja na heshima nyingi sana” kwa upande wa mke wa Kikristo. (1 Pet. 3:1, 2, NW) Mwanamke anayejihakikisha kuwa “mwenye uwezo,” mwenye bidii katika kazi yake, ndiye anayepata kibali yenye uchangamfu ya mumewe. Kumbuka kwamba “-thamini” maana yake ni “kuona ubora mwingi.” “Ubora wake ni mwingi zaidi kuliko ule wa marijani,” inasema mithali. “Katika moyo wake mwenyeji wake ameweka tumaini, na hakuna faida inayokosekana. Yeye amemthawabisha mumewe kwa mema, si mabaya, siku zote za maisha yake [mke].” (Mit. 31:10-12, NW) Ikiwa mtu ana “mke mwema,” basi itatazamiwa kwamba ‘atamsifu’ kama inavyosemwa katika Mithali 31:28, NW.

12. Ni mambo gani yanayoweza kufanya mke na watoto wathamini kichwa cha jamaa?

12 Vivyo hivyo, mume wa Kikristo anatamaniwa kwa upendo na mkewe anapoonyesha sifa njema. Ikiwa yeye ni mkali na asiyehurumia washiriki wengine wa jamaa, wanaweza kuheshimu cheo chake lakini waone ni vigumu kuonyesha kuthamini au kuona ubora wake mwingi sana kama mtu. Kwa upande mwingine, anapotumia ukichwa wake akiona sana wajibu wake kwa aliye kichwa chake, Bwana Yesu Kristo, na kwa kufuata mfano wake huyo, basi washiriki wa nyumba yake wataitikia kwa vyepesi kwa njia yenye kuthamini. (1 Kor. 11:3; Mt. 11:28-30) Haitoshi kwake kuwa mwenye ukarimu kwa anavyotumia wakati wake na watu wasio wa nyumba yake; jamaa yake mwenyewe inastahili kufikiriwa pia. Mwanamume anayetumia wakati fulani kila siku katika mazungumzo yenye kujenga pamoja na jamaa yake bila shaka atathaminiwa zaidi sana kuliko yeye anayeleta pesa tu nyumbani kisha kuanza kusoma gazeti au kutazama televisheni. Na ingawa mke wake anaweza kumpenda kwa sababu ya kusaidia wengine mtaani, nia yake ya kuweka kando wakati kwa kawaida ili kujifunza Biblia pamoja na mke ndiyo itakayotia nguvu upendo wake kwake.

KUTHAMINI AMBAKO YEHOVA ANAONYESHA

13. (a) Hata ingawa washiriki wa jamaa wanaweza kukosa kuthamini jitihada za mtu za kufanya mema, ni nani anayeona? (b) Daudi alionyeshaje matumaini katika hili?

13 Nyakati nyingine, hata tunapotia jitihada kuonyesha fadhili za upendo kwa wengine, hatuitikiwi kwa kuthaminiwa. Lakini inatupasa tufahamu kwamba yuko mtu mwingine anayeona na anayethamini tunayofanya, naye huyo ndiye Yehova. Daudi, mwana wa Yese, alifahamu hivyo. Maisha yalifanywa yawe magumu kwake na Mfalme Sauli wa Israeli ambaye alijaribu kubomoa nyumba ya Daudi ingawa alikuwa mkwewe, na mwishowe akamwoza mke wa Daudi Mikali kwa mwanamume mwingine, akajaribu kumwua Daudi mwenyewe mara nyingi. Ni watu wangapi wamepatwa na mambo makali kama hayo? Na hali Daudi alimtendea mfalme huyo kwa fadhili za upendo mara nyingi. Na, ingawa Daudi hakutazamia kuthaminiwa na mfalme, alisema hivi: “[Yehova] atamlipa kila mtu haki yake, na uaminifu wake.” (1 Sam. 26:23) Ndiyo, Yehova anahakikisha kwamba fadhili za watumishi wake hazipiti bila kuthawabishwa.​—Mit. 25:21, 22.

14. Ni katika njia gani Yehova ameonyesha. kupendezwa Kwake kwenye upendo na wanadamu wote?

14 Yehova anapendezwa sana na wanadamu, naye anaonyesha hivi kwa mipango yake yenye ukarimu ili waifurahie. Hata kwa watu wasiokuwa waabudu wa Mungu wa kweli, mitume Paulo na Barnaba wangeweza kusema hivi kwa haki: “Hakujiacha pasipo ushuhuda, kwa kuwa alitenda mema, akiwapeni mvua kutoka mbinguni, na nyakati za mavuno, akiwashibisha mioyo yenu chakula na furaha.” (Matendo 14:17) Naye Mfalme Sulemani aliandika hivi akiwa chini ya uongozi wa Mungu: “Nimeiona [kazi] ambayo Mungu amewapa wanadamu, ili [waifanye]. Kila kitu amekifanya kizuri kwa wakati wake; . . . Mimi najua ya kwamba hakuna jema kwao kupita kufurahia, na kufanya mema maadamu wanaishi. Tena ni karama ya Mungu kila mtu apate kula na kunywa, na kujiburudisha kwa mema katika kazi yake yote.” (Mhu. 3:10-13) Ni wazi kwamba Mungu anaupenda ulimwengu wa wanadamu, naye anawataka waifurahie dunia hii, wathaminiane na kumpenda yeye na kumthamini kama Muumba.

15. Kati ya viumbe vyote vya dunia, je! wanadamu peke yao ndio wanaohangaikiwa na Mungu kwa upendo?

15 Lakini Mungu haonyeshi kuhangaika kwenye upendo kwa wanadamu peke yao. Kwa maana Yesu Kristo alisema hivi alipokuwa akiwaeleza mitume wake juu ya upendo wa Mungu kwao: “Je! mashomoro wawili hawauzwi kwa senti moja? Wala hata mmoja haanguki chini asipojua Baba yenu; lakini ninyi, hata nywele za vichwa vyenu zimehesabiwa zote. Msiogope basi; bora ninyi kuliko mashomoro wengi.” (Mt. 10:29, 30) Fikiria hilo​—Mungu anapendezwa hata na ndege ambao pengine wanadamu wanawaona kama wenye “thamani ndogo” (NW). Na kwa sababu gani asifanye hivyo? Wao pia ni kazi ya mikono ya Mungu. Yehova aliwaumba akawahifadhi wakaokoka gharika ya siku za Nuhu.

16. Lakini Mungu ameonyeshaje upendo wa pekee kwa viumbe vyake vya kibinadamu?

16 Walakini, Mungu anapenda wanadamu kwa njia ya pekee. Si wakati alipokuwa akiumba wanyama bali ni wakati alipokuwa akijitayarisha kufanya wanadamu Mungu alipomwambia Mwanawe hivi: “Na tufanye mtu kwa mfano wetu.” (Mwa. 1:26) Hata ingawa wazazi wetu wa kwanza wa kibinadamu waligeukia dhambi, Mungu hakupoza upendo wake kwa jamaa ya kibinadamu. Kwa upendo alifanya mipango ili wote ambao wangeitikia kwa imani na kwa kumthamini Muumba wao waweze kuishi milele. Kama vile Yesu alivyoeleza: “Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.”​—Yohana 3:16.

17. Kwa sababu gani tumaini la uzima wa milele katika utumishi wa Yehova linapendeza sana?

17 Lo! tumaini la uzima wa milele katika utumishi wa Yehova ni lenye kupendeza kama nini! Yeye si Bwana asiyethamini. Hata sasa, ingawa utumishi wetu unaharibiwa na kutokamilika kwetu, yeye anatupa uhakikisho mwingine. Ili atutie moyo alimwongoza mtume Paulo aandikie Wakristo waaminifu hivi: “Mungu si dhalimu hata aisahau kazi yenu, na pendo lile mlilolidhihirisha kwa jina lake, kwa kuwa mmewahudumia watakatifu, na hata hivi sasa mngali mkiwahudumia.” (Ebr. 6:10) Kwa kuwa Ibrahimu alikuwa ameonyesha imani ya kweli katika Yehova mara nyingi, yeye aliambiwa na Mungu hivi: “Thawabu yako kubwa sana.” (Mwa. 15:1) Na kwa habari ya “maamuzi ya hukumu” ya Yehova, mtunga zaburi aliandika hivi: “Katika kuyashika kuna thawabu kubwa.” (Zab. 19:11, NW) Ndiyo, Yehova anathawabisha wale wanaofanya mapenzi yake kwa kuwathamini, matendo yao yawe madogo au makubwa. Kuijua nia hii yenye kuthamini sana kwa upande wa Mungu kunatuhusuje? Je! sisi, pia, tunaitikia kwa kuthamini?

KUONA UBORA MWINGI WA UHUSIANO MWEMA NA MUNGU

18. Linapokuwa shauri la kufurahia uhusiano na Yehova, ni hali gani inayotuelekea sote?

18 Kuwa na uhusiano wenye kibali na Yehova si jambo ambalo sisi wanadamu tunaweza kuchukua vivi hivi tu. Hatuzaliwi nao. Bali, hali yetu ni kama ile ya Mfalme Daudi, aliyeandika hivi: “Tazama, mimi naliumbwa katika hali ya uovu; mama yangu alinichukua mimba hatiani.” (Zab. 51:5) Hakuna wo wote kati yetu walio tofauti. Maandiko yanasema hivi kwa kweli: “Wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu.” (Rum. 3:23; tazama pia 1 Yohana 1:8, 10.) Lakini Yehova ametoa njia ambayo kwayo tunaweza kupata kibali yake.

19, 20. Ni njia gani ya pekee ambayo kwayo tunaweza kuingia katika uhusiano na Yehova, na kwa sababu gani ni pendeleo kubwa sana kumtumikia yeye?

19 Tunapotua tufikirie wanadamu ni nini wakilinganishwa na Mungu, mpango huo umepaswa uvute mioyo yetu. Mtu ye yote ambaye amesafiri kwa ndege-ulaya anajua kwamba wanadamu wanaelekea kutoweka na nyumba zao na magari yanaonekana kama vibaramwezi, hata wanapokuwa futi maelfu machache tu juu. Basi, Yehova anapotazama chini duniani akiwa mahali pake pa mbali zaidi sana, bila shaka wanadamu wanaonekana kwake wadogo sana sana! (Isa. 40:15) Je! ni ajabu kwamba mtunga zaburi aliandika hivi: “Nikiziangalia mbingu zako, kazi ya vidole vyako, mwezi na nyota ulizoziratibisha; mtu ni kitu gani hata umkumbuke, na binadamu hata umwangalie?”​—Zab. 8:3, 4.

20 Lakini, Yeye huyu Aliye Juu sana, Muumba, Mtawala Mwenye Enzi wa ulimwengu wote, anatutolea sisi nafasi ya kuwa na uhusiano na Yeye. Naye alimtuma Mwanawe mzaliwa wa pekee duniani atoe uhai wake kama dhabihu yenye kulipia dhambi, ili afanye jambo hili liwezekane. Mwana huyo, Yesu Kristo, alieleza hivi mwenyewe: “Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.” Yeye aliwaambia pia mitume wake hivi: “Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi.” (Yohana 3:16; 14:6) Baada ya kifo chake mwenyewe na ufufuo, Yesu aliamuru wanafunzi wake hivi: “Ninyi mtakuwa mashahidi wangu mimi katika Yerusalemu na katika Uyahudi wote na katika Samaria na kwenye sehemu ya mbali zaidi sana ya dunia.” (Matendo 1:8) Wakithamini namna lilivyo pendeleo kubwa kutumikia kwa njia hii, wao walifanya alivyowaagiza.

21. Mwaka jana, watu duniani mwote walionyeshaje kwamba wanaona ubora mwingi sana wa uhusiano mwema na Mungu?

21 Kwa sababu hiyo, watu katika sehemu zote za dunia wamefahamiana na Yehova, Mungu wa pekee wa kweli, na Mwanawe Yesu Kristo. Mwaka jana watu walikuwa wakisaidiwa kwa njia hiyo na mashahidi wa Yehova wa Kikristo katika nchi 207. Wengine walithamini waliyosikia. Hawa waliona uhitaji wa kutubu juu ya mwendo wao wa zamani, kugeuka na kutumia maisha zao katika kufanya mapenzi ya Mungu. Walipopata kuuthamini mpango mzuri sana uliofanywa na Mungu kukomboa wanadamu kutoka utumwa wa dhambi na mauti, walijikana na kubatizwa kwa kuonyesha wakf wao kwa Yehova wafanye mapenzi yake. (Mt. 16:24; 28:19, 20) Si wachache tu waliochukua hatua hii ya maana. Mwaka jana watu walibatizwa katika nchi 181. Kwa ujumla, watu 297,872 walijitoa wabatizwe na mashahidi wa Yehova wakati wa kipindi cha mwaka mmoja tu. Wote ni watu ambao wamejifunza Biblia, wanajua inayofundisha nao hawaachi kufanya tangazo la waziwazi la imani yao. (Rum. 10:9, 10) Walishiriki kwa bidii ili wastahili ubatizo kwa sababu wao wanaona ubora mwingi sana wa uhusiano mwema na Mungu. Je! wewe, pia, unathamini hivyo? Baraka za ajabu zimo akibani sasa na wakati ujao, kwa wale wanaofanya hivyo.

[Picha katika ukurasa wa 293]

Wazazi wanaopenda watoto wao kweli kweli watahakikisha kwamba wanapata adabu inayohitajiwa​—si adhabu tu, bali pia mafundisho ya kipekee yanayoendeleza ukuzi wa akili na adili

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki