Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w75 10/15 kur. 479-480
  • Maswali Kutoka Kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka Kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Habari Zinazolingana
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Mtaabiko wa Akilini—Wakati Unaposumbua Mkristo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Mambo Unayopaswa Kujua Kuhusu Magonjwa ya Akili
    Amkeni!—2014
  • Matibabu Unayochagua
    Amkeni!—2000
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
w75 10/15 kur. 479-480

Maswali Kutoka Kwa Wasomaji

● Je! Mashahidi wa Yehova wanaona inafaa kumwendea daktari wa akili?

Kama Mkristo atamwendea daktari wa akili, au daktari mwingine ye yote, huo ni uamuzi wake mwenyewe. Walakini, Wakristo wa kweli wanauamini sana uwezo wa Biblia wa kutoa uongozi wenye mafaa. Wanajua kwamba Muumba ana ujuzi mwingi zaidi kuliko mwanadamu​—kutia na ujuzi wa namna akili ya kibinadamu ilivyo. Hivyo, mashahidi wa Yehova wanaona njia yo yote ya matibabu kulingana na “hekima itokayo juu.”​—Yak. 3:17.

Leo watu wanatibiwa sana kwa dawa za kulevya, na hapa tena, ni jambo la hekima kufikiria matokeo kwa uangalifu. Ingawa Wakristo hawakatazwi kutumia dawa za kulevya, na hata nyakati nyingine huenda dawa fulani za kulevya zikaleta kitulizo cha kadiri fulani, imempasa mtumishi wa Mungu ajihadhari sana na kitu cho chote kinachoweza kumfanya mtumwa, kumfanya mzoevu wa kukitumia. (Rum. 6:17; 12:1) Watu wengine wanaochagua kufanyiwa matibabu yasiyohusu dawa za kulevya wanaonyesha matokeo mazuri ya matibabu ya kutumia vitamins nyingi, nayo haya ni matibabu yanayozidi kupendwa leo.

Kwa habari ya kutafuta matibabu, inafaa kuangalia kanuni ya Biblia inayopatikana katika 1 Wakorintho 12:26. Hapa Maandiko yanafundisha kwamba wakati sehemu moja ya mwili inapoumia, sehemu nyingine zinaumia. Kupatana na kanuni hii, wale walio na magumu ya akili au ya neva huenda wakaona inafaa kufanyiwa uchunguzi mwingi wa kimwili, kadiri ambavyo kuna ugumu wa afya wasioujua. Hata wengine waliodhani walikuwa karibu kuwa wenda-wazimu, au waliodhani walikuwa wakisumbuliwa na mashetani, wamegundua kwamba sukari haikuwa nyingi katika damu yao au walikuwa na ugonjwa mwingine.

Bila shaka, yako magonjwa na maradhi mengi yasiyoponyeka. Tena, Yehova anasaidia. Neno lake linaweza kutusaidia tusitawishe uvumilivu wetu. (1 Tim. 6:11, 12) Tena, kwa njia hii tunasaidiwa kuvumilia mabadiliko ya kimwili yenye kuleta maumivu, kama yale yanayotokea nyakati nyingine wakati mwanamke amepita umri wa kuzaa na kuacha kuona mwezi au wakati mtu anapoendelea kuwa mzee.

Lakini namna gani ikiwa ugumu wenyewe si wa kimwili? Namna gani ikiwa mtu anajiona kutendewa kikatili au kuvunjika moyo​—kuwa na magumu ya kupatana na wengine? Yakobo 5:13-16 anasema mtu mwenye magumu ya kiroho au ya mawazo ya moyoni aite wanaume wazee wa kundi la Kikristo, kusudi lake likiwa kwamba wao ‘wampake mafuta,’ yaani, wampe mashauri ya Biblia yenye kufariji, na vile vile “wamwombee.” Matokeo yake yatakuwa nini? Andiko linaendelea kusema hivi: “Na kule kuomba kwa imani kutamwokoa mgonjwa yule, na [Yehova] atamwinua [aache kuvunjika].” Bila shaka, lazima mgonjwa wa kiroho awe mwaminifu na aeleze mambo wazi ikiwa atafaidika. Lazima atafute na kufuata mashauri ya Biblia; lazima atende kupatana na sala zilizotolewa kwa ajili yake.​—Yak. 1:25.

Hii inawapa wazee wa Kikristo daraka kubwa. Lazima watoe sala yenye shauku, wakitafuta uongozi wa Yehova. Kwa kutumia saburi, upendo na fikira juu ya mtu mwenyewe, mara nyingi wanaweza kuona chanzo hasa cha magumu yenyewe. Wazee wamepaswa wasaidie mwenye kusumbuka aone namna Mungu anavyotukaribisha tumtwike mizigo yetu. (Zab. 55:22; 1 Pet. 5:7) Nyakati nyingine ni lazima kusaidia mtu aone namna ya ‘kuweka mbali hasira’ au kukaza fikira kwenye mambo yaliyo safi. (Kol. 3:5-14; Flp. 4:6-8) Na mara kwa mara, huenda mtu mwenye kutubu kweli kweli akajiona ‘mwenye hatia’ au ‘asiyeweza kusamehewa.’ Kwa kuwa ana huzuni nyingi, anahitaji kuhakikishiwa kama vile ilivyoandikwa katika 1 Yohana 1:9.

Kwa hiyo, ingawa mashahidi wa Yehova hawawezi kukataza kabisa uwezekano wa kutibiwa na madaktari waliosomea magumu ya moyo na akili, Shahidi akiendea watu kama hao imempasa achunguze kwa uangalifu sana matibabu yo yote yanayopendekezwa. Asisahau kwamba kushika sheria za Yehova kunamletea afya ya akili leo na uzima wa milele wakati ujao. Ikiwa ana mashaka juu ya kufaa kwa matibabu fulani, basi anaweza kuzungumza jambo hilo na wazee katika kundi la Kikristo​—ingawa yeye mwenyewe (au mzazi au mume pamoja na mke) ndiye atakayefanya uamuzi. Na la maana kupita yote, Wakristo wa kweli watataka kutumia kabisa nguvu anazotoa Yehova kama vile wanavyozitumia katika mambo mengine ya maisha, wakifahamu kwamba Neno na roho ya Mungu zina mafaa mengi sana. “Maana Neno la Mungu li hai, tena lina nguvu . . . tena li jepesi kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo.”​—Ebr. 4:12.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki