Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w75 9/1 kur. 406-408
  • Imani Katika Mungu Yathawabishwa kwa Kuhifadhiwa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Imani Katika Mungu Yathawabishwa kwa Kuhifadhiwa
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • KUHATIRISHWA NA SHAMBULIO LA MATAIFA YOTE
  • WOKOVU KWA KUMTEGEMEA YEHOVA KABISA
  • KUTEMBEA MBELE ZA YEHOVA KATIKA NCHI YA WALIO HAI
  • Simameni, Mkauone Wokovu wa Yehova!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
  • Uhai Wako Ni Wenye Thamani Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Ni Ulinzi Gani kwa Watu wa Mungu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
w75 9/1 kur. 406-408

Imani Katika Mungu Yathawabishwa kwa Kuhifadhiwa

Makala hii ni ya kutumia kwa mafunzo ya kitabu ya kundi

1, 2. Ni nini yaliyo mbele ya dunia, na kwa wanadamu juu yake?

LEO tuko karibu na wakati wenye maana kwa dunia. Ijapokuwa wanaanga waliitazama dunia kutoka angani ikionekana kama kito bora katika sayari nyingi historia yake tangu mara mwanadamu alipokwisha kutokea duniani yapata miaka 6,000 iliyopita imekuwa yenye uchafu, ubaya na uharibifu wa polepole. Lakini ushuhuda wote waelekeza kwenye mwisho wa taratibu ya mambo ambayo sasa inaongoza mambo ya dunia. Unabii wa Biblia unaonyesha kwamba kuna mwisho kweli kweli, na kwamba si mwisho utakaoletwa na wanadamu, bali na Mungu.

2 Ndipo dunia itakapokombolewa, iondolewe uchafu ambao imepata, nayo itaingia katika kipindi chenye utukufu cha miaka elfu moja ya kurudishwa kwenye hali bora na kupambwa. Walakini, mbeleni ziko nyakati zenye maana sana, lakini zenye taabu. Lakini jamii ya kibinadamu haitafutiliwa mbali. Wengi watashindwa kuwa na imani katika ahadi ya Mungu ya kutoa wokovu, hata hivyo ye yote anayetamani sana kufanya hivyo aweza kuitumia nafasi sasa.

3. Ni nini linalotakiwa ili kuokoka katika nyakati hizi zenye hatari?

3 Kuokoka nyakati hizi zenye hatari kunataka imani katika Mungu​—imani hasa ya kukubali yale anayosema kisha kuyafuata. Mtume Petro aliandika hivi: “Na mwenye haki akiokoka kwa shida, yule asiyemcha Mungu na mwenye dhambi ataonekana wapi?” Ndipo alipowashauri Wakristo “wamwekee amana [nafsi] zao, katika kutenda mema, kama kwa Muumba mwaminifu”​—1 Pet. 4:18, 19.

4. Ni nini litakalotukia karibuni sana?

4 Ni nini hasa yaliyo mbele? Biblia yaonyesha kwamba karibuni serikali za kisiasa zitaigeukia dini ya uongo, kutia na matengenezo ya kidini ya Jumuiya ya Wakristo na viongozi wao, na zitaiharibu. Namna mambo haya yatakavyotokea ilizungumzwa katika toleo lililotangulia la gazeti hili juu ya sura kumi na saba na kumi na nane za kitabu cha Biblia cha Ufunuo. Katika sura hizo tunaonyeshwa namna dini ya uongo itakavyoanguka. Wale wanaomtumikia Mungu kweli kweli hawatapatwa na uharibifu huu, bali watakuwa tofauti kama wajumbe wa Mungu, kama wasio sehemu ya taratibu hii ya ulimwengu.​—Yohana 17:14; linganisha Ezekieli 33:33.

KUHATIRISHWA NA SHAMBULIO LA MATAIFA YOTE

5. Ni wakati gani mkazo mkuu utakapowajia watu wa Mungu?

5 Bila shaka kutakuwako shida wakati wa msukosuko utakaofuatana na uharibifu wa dini ya uongo. Lakini mkazo mkubwa sana juu ya wale wanaomtumikia Mungu utakuja baada ya kuharibiwa kwa dini ya uongo wakati watawala wa kisiasa watakapowageukia wale wenye amani, wanaojifurahisha ufanisi wa kiroho. Hawa hawatakuwa na nguvu ya kijeshi, bali watategemea ulinzi usioonekana wa Mungu tu. Shambulio hili litakuwa chini ya uongozi wa “mtawala wa ulimwengu huu,” “mungu wa taratibu hii ya mambo,” Shetani Ibilisi.​—Yohana 12:31; 2 Kor. 4:4, NW.

6, 7. Biblia inaonyeshaje kwamba shambulio litawajia watu wa Mungu, na matokeo yatakuwa nini?

6 Biblia inatupashaje habari kwamba shambulio hili litawajia wale wanaomtumikia Mungu kwa roho na kweli? Njozi ile ile katika Ufunuo inayosimulia juu ya uharibifu wa dini ya uongo inasema pia kwamba wafalme wa dunia “watafanya vita na Mwana-Kondoo, na Mwana-Kondoo atawashinda, kwa maana Yeye ni Bwana wa Mabwana na Mfalme wa Wafalme.” (Ufu. 17:12-14) Kwa kuwa Mwana-Kondoo Yesu Kristo yuko mbinguni, wafalme wa kidunia na majeshi yao wanaweza kupigana naye kwa kushambulia wafuasi wake duniani tu, wanaokubali na kunyenyekea mamlaka yake ya kifalme. Ufunuo sura ya 19 unasimulia vita hiyo.

7 Kuongezea njozi ya unabii ya Ufunuo, nabii Ezekieli aliongozwa na Mungu aandike juu ya shambulio hilo katika maneno ya mfano. Shetani Ibilisi anaonyeshwa kwa jina la “Gogu” kama akiongoza majeshi yake juu ya watu wa Yehova. Gogu atadhani kwamba hawana “kuta” au ulinzi. Gogu huyu anasemekana kama akisema hivi: “Nitapanda juu, niiendee nchi yenye vijiji visivyo na maboma; nitawaendea watu wanaostarehe, wanaokaa salama, wote wakikaa pasipo kuta, ambao hawana makomeo wala malango.” (Eze. 38:2, 11) Wafalme, chini ya uongozi wa Gogu, hawatauona ulinzi usioonekana kama “ukuta wa moto.” (Linganisha Zekaria 2:5; 2 Wafalme 6:11-17.) Ndipo Yehova, kupitia kwa “Mfalme wa Wafalme,” “Mwana-Kondoo,” atawaharibu.​—Eze. 38:21-23; 39:1-4; Ufu. 19:19-21.

8, 9. (a) Ni jambo gani ambalo Mungu aliandikisha linalowapa watu wake nguvu wakiwa katika hatari kubwa? (b) Mtunga Zaburi alisimuliaje hatari iliyompata?

8 Ye yote awezaje kuwa na imani ya kusimama imara chini ya shambulio hilo kutoka kwa majeshi yote ya dunia, akitumainia mtu fulani asiyeweza kumwona? Ili kuwasaidia wale wanaomtumaini, Yehova alimwongoza mtunga Zaburi aandike juu ya yale yaliyompata mwenyewe kama jambo lenye kutia moyo na nguvu. Kuhifadhi kwa Mungu wale wanaomtumaini kunatajwa waziwazi kwetu. Mwandikaji angeweza kuwa alikuwa akisema kwa namna ya kuwakilisha taifa zima lake, kwa sababu si yeye mwenyewe, bali pia watu wake, watu wateule wa Yehova Mungu, ambao waliogofishwa na kifo, kwa uharibifu wakati huo. Alisema hivi:

9 “Nampenda [Yehova] kwa kuwa anaisikiliza sauti yangu na dua zangu. Kwa maana amenitegea sikio lake, kwa hiyo nitamwita siku zangu zote. Kamba za mauti zilinizunguka, shida za kuzimu zilinipata. Naliona taabu na huzuni; nikaliita jina la [Yehova]. Ee [Yehova], nakuomba sana, uniokoe nafsi yangu. [Yehova] ni mwenye neema na haki, naam, Mungu wetu ni mwenye rehema. [Yehova] huwalinda wasio na hila; nalidhilika, akaniokoa.”​—Zab. 116:1-6.

WOKOVU KWA KUMTEGEMEA YEHOVA KABISA

10. Hali hiyo ilionekanaje kwa mtunga Zaburi, na aliokolewaje?

10 Mtunga Zaburi hakutaka kufa. Hata hivyo mauti ilionekana kuwa jambo la hakika kwake. Ilikwisha kuwa kana kwamba mauti ilimfunga sana kwa kamba zake zisizokatika, kuzuia njia zote za kuokokea. Ilikuwa kana kwamba alikwisha kuwa katika Sheol (kaburi la kawaida la wanadamu), akiona taabu ya kubanwa na kuta nyembamba za kaburi. Lakini alimlilia Yehova akaokolewa. Mtunga Zaburi aliongozwa aonyeshe upendo wake mwingi kwa Muumba na Mwokozi wake kwa sababu ya neema, haki na rehema hii ya Mungu.

11. Yatakayowapata watu wa Yehova katika Har–​Magedoni yatakuwaje sawasawa na hayo?

11 Vile vile, watu wa Mungu watakapookoka uharibifu wa taratibu hii ya mambo katika Har–​Magedoni, watakumbuka na kushukuru wokovu ambao Mungu Mwenye Nguvu Zote amewatendea. (Ufu. 16:14, 16; Luka 21:36) Ilikuwa hali yenye kukaribia mauti ambayo waliokolewa kwayo. Hawakuzijua njia za werevu na mbaya za ulimwengu huu na hawakuomba msaada wa kibinadamu. Hakuna mtu ambaye angeweza kuwaokoa ila Yehova​—hawakuweza kuita juu ya jina jingine. Katika hali yao yenye kuhatirishwa, isiyo na msaada wote wa kidunia, tegemeo lao lote lilipaswa liwe juu yake Yeye. Nalo halikuwa la bure. Lo! namna wale ambao Yehova ataokoa watakavyokuwa wenye shukrani! Lo! watamwonyesha Mungu wao upendo wao milele kama nini kwa maneno na matendo ya moyo wote!

KUTEMBEA MBELE ZA YEHOVA KATIKA NCHI YA WALIO HAI

12, 13. Alipokwisha kuokolewa, mtunga Zaburi alisemaje?

12 Wakihifadhiwa na hali hiyo yenye kuogofya, waokokaji wanaweza kusema, kama alivyosema mtunga Zaburi:

13 “Ee nafsi yangu, urudi rahani mwako, kwa kuwa [Yehova] amekutendea ukarimu. Maana umeniponya nafsi yangu na mauti, macho yangu na machozi, na miguu yangu na kuanguka. Nitaenenda mbele za [Yehova] katika nchi za walio hai. Naliamini, kwa maana nitasema, Mimi naliteswa sana. Mimi nalisema kwa haraka yangu, wanadamu wote ni waongo.”​—Zab. 116:7-11.

14. Watu wa Mungu wataonaje, na watafanya nini baada ya kuokolewa kwao katika Har–​Magedoni?

14 Baada ya kuokolewa na shambulio la adui, ambalo bila shaka litawaletea wenye kuhatirishwa taabu, waokokaji wa Har–​Magedoni wanaweza kutusha nafsi zao, kujiweka wenyewe katika raha. Huenda wakashikwa na woga wa ghafula kwa kitambo wakati wa kushambuliwa, wakijua kwamba hakuna mwanadamu ambaye angeweza kuwasaidia hata ikiwa angeahidi au kujaribu kufanya hivyo. Imani katika Mungu ndiyo itakayowaletea wokovu wao. Kisha, wakiwa wamehifadhiwa na kuanguka kwenye kuleta mauti, wataazimu kuendelea ‘kuenenda mbele za Yehova katika nchi za walio hai.’

15. Kwa kufikiria maneno ya mtume Paulo katika 2 Wakorintho 4:8, 9, ni kutia moyo gani ambako watu wa Yehova wanaweza kupata wakati huo wenye mkazo?

15 Leo wote walio na imani katika Mungu wanaweza kupata nguvu kutokana na maneno ya mtunga Zaburi kupatana na shauri lenye kufariji la mtume Paulo katika 2 Wakorintho 4:8, 9: “Pande zote twadhikika, bali hatusongwi; twaona shaka, bali hatukati tamaa; twaudhiwa, bali hatuachwi; twatupwa chini, bali hatuangamizwi.”

16. Mungu ‘atawatendeaje watu wake ukarimu’ watakaposhambuliwa na adui?

16 Mtume Paulo aliendelea kusema, akikumbuka Zaburi 116 hivi: “Naliamini, na kwa sababu hiyo nalinena.” (2 Kor. 4:13) Vile vile watu wa Mungu wanaweza kusema kwa imani kamili, isiyo na shaka katika ulinzi wa Mungu. Sababu gani? Kwa sababu Mungu ‘atawatendea ukarimu.’ (Zab. 116:7) Tendo lake ni lenye kufaa kabisa na lenye kupatana na ahadi zilizoandikwa katika Neno lake. Yeye “huwapa thawabu wale wamtafutao.” (Ebr. 11:6) Hili pia lapatana na fadhili zake za upendo na kusudi lake la kushuhudia jina lake kwa kushindwa kwa adui zake na kusudi lao baya sana.

17. Je! wengine zaidi ya waokokaji wa Har–​Magedoni watapata faida kwa sababu ya fadhili za upendo za Mungu?

17 Watakapokwisha kuokoka shambulio la adui na kuingia katika dunia safi, waokokaji wataona wokovu mwingine ukifanywa mbele ya macho yao. Huo ni wokovu wa mabilioni ya watu kutoka kaburini kwa ufufuo. Wakisaidiwa na waokokaji hawa watajifunza juu ya Mungu wa wokovu. Idadi zisizo na hesabu za hawa wataonyesha imani na wataweza pia ‘kuenenda mbele za Yehova katika nchi za walio hai,’ wakifikia mwishowe uzima wa milele katika ukamilifu duniani kama “watoto wa Mungu.” (Rum. 8:21; Ufu. 20:11-15) Imani katika Mungu inathawabishwa kwa kuhifadhiwa, na kuhifadhiwa huko kunaongoza kwenye uzima wa milele.

​—Kutoka Kitabu God’s Kingdom of a Thousand Years Has Approached.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki