Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w77 3/1 kur. 115-116
  • “Kuwa Tayari kwa Kila Kazi Njema”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Kuwa Tayari kwa Kila Kazi Njema”
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
  • Habari Zinazolingana
  • Nguvu Zenye Kuchochea za Ukarimu wa Kristo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • Ukarimu Unaleta Thawabu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
  • Watu Wanaotoa kwa Ukarimu Ni Watu Wenye Furaha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2018
  • Upaji wa Kikristo—Ni wa Maana Kadiri Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
w77 3/1 kur. 115-116

“Kuwa Tayari kwa Kila Kazi Njema”

MAANDIKO yaliyoongozwa na Mungu yanaonya Wakristo kwa upole ‘wawe tayari kwa kila kazi njema.’ (Tito 3:1) Watumishi wa Mungu waliojitoa wanatakiwa wafanye nini ndiyo wawe hivyo? Wanatakiwa watimizie wengine mahitaji yao bila kusitasita. Ikiwa twaweza kusaidia mtu, isingetupasa kamwe kuahirisha kumsaidia wala kuacha mtu mwingine amsaidie. Bali, yatupasa tuwe na nia hata ya kujinyima vitu sisi wenyewe, ikiwa lazima, ili tusaidie wanaostahili.

Yako mambo mengi yanayoweza kuitwa “kazi njema,” yenye kufaidi jirani zetu na kumpendeza Mungu wetu. Kwa mfano, iko kazi ya kutia waamini wenzetu moyo kwa kusema nao na kuwawekea mfano. Kuna nafasi nzuri ajabu ya kufanya hivyo katika mikutano ya Kikristo. Mtume Paulo alisihi hivi: “Yatupasa kuona jinsi kila mmoja wetu awezavyo kuamsha wengine wawe na upendo na wema wenye juhudi, bila kukaa mbali na mikutano yetu [ya Kikristo], kama wengine wafanyavyo, bali tuwe tukitiana moyo, zaidi sana kwa sababu mwaiona ile Siku ikikaribia.” (Ebr. 10:24, 25, New English Bible) Naam, kuwa katika mikutano ya kundi la Kikristo kwa kawaida, ili kuchangamsha, kutia moyo na kujenga ndugu zetu, ni “kazi njema.” Hata ikiwa sisi wenyewe hatuna afya nzuri sana kimwili, tunaweza kutia wengine ‘ moyo waonapo tukiwa wenye nguvu kwa msaada wa roho ya Yehova, ingawa tu dhaifu.

Katika makusanyiko hayo huenda wakawako wengine walio na huzuni, walioshuka moyo na kufadhaika. Ukihudhuria unakuwa katika hali ya kuweza kuwasaidia. Unaweza kuwasisimua waanze kufikiria mambo bora ukionyesha unataka kuona wakiwa na hali njema, na ukizungumza nao kwa uchangamfu. Usisahau kwamba unaweza kuwatia moyo kwa kujibu maulizo yanayoulizwa jukwaani.

Ni roho ya Yehova hasa itakayokuwezesha uchochee waamini wenzako “wawe na upendo na wema wenye juhudi.” Roho hiyo iliyokuwa juu ya Yesu Kristo ilimwezesha “kuwafariji wote waliao . . . wapewe taji ya maua badala ya majivu, mafuta ya furaha badala ya maombolezo, vazi la sifa badala ya roho nzito.” (Isa. 61:2, 3; Luka 4:17-21) Kwa kumwiga Yesu Kristo, je! wewe unafariji hivyo hata wale ambao hawajawa bado waamini wenzako, kwa msaada wa roho ya Mungu?

Tukishiriki katika kazi ya lazima ya kuzitangaza “habari njema” za ufalme wa Mungu tunaweza kufariji wengi kweli kweli. Kwa hiyo, yatupasa tuhakikishe tumeweka kando wakati wa kufanya utumishi huo wa lazima wa kwenda nyumbani kwa watu katika ujirani wetu, kujaribu kuwafanya wapendezwe na ujumbe ambao Mungu anatolea watu wa kizazi hiki.

Sisi wenyewe tunajitia nguvu sana tunapozidi kuvumilia katika kazi hii. Kwa kuwa Maandiko yanaeleza kwamba ni kazi ya kutafuta “kondoo” waliopotea, hatuwezi kutazamia kupata mtu mnyofu mwenye mfano wa kondoo katika kila barabara au katika kila mji au kijiji. (Linganisha Mathayo 10:6, 14.) Kwa hiyo tusivunjike moyo tukikuta watu wasioitikia. Bali, yatupasa tustahimili wasipoitikia, wakitupinga kwa kutojali na kukufuru. Ustahimilivu huo hutokeza uvumilivu.​—Rum. 5:3-5.

Yatupasa pia tutumie vizuri nafasi tunazopata kila siku za kuonana na watu, ili tuwafahamishe ahadi zenye kufariji zilizomo ndani ya Biblia. Huenda tukakutana na watu tunapongojea gari, au tunaposafiri, au huenda tukapata nafasi ya kusema kifupi na watu tusiowajua. Je! tunapowaonyesha yanayosemwa na Biblia juu ya hali zilizopo za ulimwengu na utimizo wa unabii, haionyeshi ‘tuko tayari’ kwa “kazi njema”? Kwa kuwa sisi huwa na nafasi kama hizo mara nyingi, twaweza kuwa na mazoea ya kuchukua kitabu cha kusaidia kujifunza Biblia, kijitabu au gazeti, tunachoweza kutolea wale wanaoonyesha wanapendezwa na ujumbe wa Ufalme.

Torati waliyopewa Waisraeli kupitia kwa Musa iliwaamuru wafikirie wale walioingia katika umaskini. (Kum. 15:7, 8, 11) Leo Wakristo wanaomwabudu Yehova wamepaswa wajitahidi wawe na nia zaidi ya kuona mahitaji ya ndugu zao maskini na kuyatimiza kadiri iwezekanavyo. Wale walio na juhudi ya kufanya kazi ya Ufalme, waliojitoa sana wamtumikie Yehova Mungu, ingawa wana magumu, ndio wanaostahili kusaidiwa na kuonyeshwa ukarimu nao. Twapaswa kuiga ukarimu wa Kornelio. Hata kabla ya kubatizwa watu walimjua kuwa mtu “mchaji wa Mungu” ambaye “alikuwa akiwapa watu” vitu kwa ukarimu na “kumwomba Mungu daima.” Katika njozi, malaika alimwambia hivi: “Sala zako na sadaka zako zimefika juu na kuwa ukumbusho mbele za Mungu [au, “na kwa sababu yazo Mungu amekukumbuka,” New American Bible].”​—Matendo 10:2-4.

Siku zetu, kama vile ilivyokuwa wakati wa mitume, wako wajumbe wenye kusafiri wa kundi la Kikristo lililoko ulimwenguni kote, wanaokwenda huku na huko wakifanya akina ndugu wazidi kulithamini pendeleo kuu la kumtumikia Yehova, na kuwapa mawaidha na mambo yaliyoonwa yenye manufaa, yanayohusu utumishi huo. Ndugu hao wanaosafiri wanastahili kusaidiwa nasi kwa ukarimu na kwa moyo wote, kama vile mtume Paulo alivyopendekeza katika barua aliyomwandikia Tito (3:13, 14): “Zena, yule mwanasheria, na Apolo, uwasafirishe [“uwape vifaa,” New Berkely Version] kwa bidii, wasipungukiwe na cho chote. Watu wetu nao wajifunze kudumu katika matendo mema, kwa matumizi yaliyo lazima, ili wasiwe hawana matunda.”

Bila shaka, huenda tusijue sikuzote mahitaji ya kimwili na ya kiroho ya waabudu wenzetu, hasa wale wanaoishi nchi za mbali. Lakini hata iwapo hivyo, tunaweza kufanya “kazi njema” kwa ajili yao. Ikiwa sisi wenyewe hatuwezi kuwapelekea kitu walio na uhitaji, twaweza kufanya hivyo kupitia kwa shirika la kisheria linalotumiwa na mashahidi wa Kikristo wa Yehova, yaani, Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania. Michango linayopelekewa shirika hilo hutumiwa kuendeleza faida za kiroho duniani mwote. Vilevile, kwa sababu ya ukarimu na uelekevu wa nia za mkutano mkubwa wa ndugu, pesa zinapatikana zitumiwe na Sosaiti kupelekea msaada wale waliopatwa na msiba fulani wa asili au wanaoteswa sana.

Tunahakikisha tunamtumainia Mungu tunapokuwa “tayari kwa kila kazi njema.” Kwa hiyo tunaweza kuwa na hakika kwamba yeye atatubariki sasa na wakati ujao. Ndivyo alivyoonyesha mtume Paulo alipokuwa akipendekeza tuwe na roho ya ukarimu. Alimwonya Timotheo kwa upole atie waamini fulani moyo “watende mema, wawe matajiri kwa kutenda mema, wawe tayari kutoa mali zao, washirikiane na wengine kwa moyo; huku wakijiwekea akiba iwe msingi mzuri kwa wakati ujao, ili wapate uzima ulio kweli kweli.” (1 Tim. 6:18, 19) Lo! ni vizuri namna gani kuweza kushiriki katika “kazi njema” na kumwiga Mungu kwa njia hiyo, ambaye huwapa watu wote vitu vya kimwili na vya kiroho kwa ukarimu!​—Mt. 5:45; Yak. 1:5.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki