Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w75 10/1 kur. 455-456
  • Maswali Kutoka Kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka Kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Habari Zinazolingana
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • Kujua Yaliyo Katika Habari
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Je, Wajua?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Ngono Bila Ndoa—Sababu Inaumiza
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
w75 10/1 kur. 455-456

Maswali Kutoka Kwa Wasomaji

● Mkristo akivunja uchumba wake (awe ni kijana wa kiume au wa kike) bila kupatana na mwenzake, hii ingekuwa na matokeo gani juu ya kama atatumiwa katika kundi kama mfano mwema?

Kufanya uchumba na kuuvunja vile vile ni hatua nzito, zisizo za kuchukuliwa vivi hivi tu. Walakini, hatua zote mbili zinahusu wenye kuzifanya peke yao. Hakuna haja kwa wazee wa kundi kuuliza juu ya mambo hayo isipokuwa mmoja wa wanaohusika akiwaletea lalamiko au ikionekana kwamba watu wengi kundini wameudhika, na mwenye kuuvunja uchumba vile vile akiwa haonyeshi heshima. Nyakati nyingine pengine wanaoudhika wamepaswa wafahamishwe vizuri kanuni zinazohusika.

Tunaweza kuangalia kwamba wanawake waliochumbiwa walionwa kama wamefungwa na uchumba huo chini ya mpango wa Kiisraeli, na kama wangekuwa na hatia ya uzinzi, torati ya Musa ilisema watendewe ambavyo mwanamke aliyeolewa angetendewa. (Kum. 22:23, 24) Mwanamume Mwisraeli alikuwa na uhuru mwingi zaidi naye angeweza kuvunja uchumba, kama vile Yusufu wa Nazareti alivyopanga kufanya. Mathayo 1:19 anasimulia kwamba, alipokwisha kujua kwamba Mariamu alikuwa na mimba, “yeye akiwa mwanamume mwenye, kufuata kanuni, na wakati uo huo akitaka kumwokoa na fedheha, Yusufu akataka maafikiano ya ndoa yaondolewe mbali kwa kimya.” (New English Bible; linganisha Kumbukumbu la Torati 24:1.) Walakini, Wakristo hawako chini ya agano la Torati, na mahali pengi leo mwanamke aliyechumbiwa haonwi kama amefungwa kwa kadiri ilivyokuwa wakati huo.

Katika Mathayo 5:37 Yesu alisema hivi: “Bali maneno yenu yawe Ndiyo, ndiyo; Siyo, siyo; kwa kuwa yazidiyo hayo yatoka kwa yule mwovu.” Maneno yanayozunguka haya yanaonyesha hapa alikuwa akitoa shauri juu ya mazoea ambayo Wengi walikuwa nayo ya kuapa-apa mara nyingi Wakiisha kusema maneno fulani, kuapa-apa mbingu au Yerusalemu au kitu kingine. Lakini kwa kutoa onyo hili juu ya kuapa hivyo kupita kadiri, Yesu hakusema kwamba ni vibaya kufanya bidii kusahihisha kosa mtu akijua amefanya kosa zito. Mithali 6:1-5 inazungumza juu ya mtu anayekuwa mdhamini wa mwingine ‘akategwa kwa maneno’ ya kinywa chake, ‘akakamatwa’ nayo, inashauri kwamba mtu huyo achukue hatua ya kujikomboa, ikisema hivi: “Nenda ukanyenyekee, na kumsihi jirani yako.” Mtu ambaye amechumbia au aliyechumbiwa huenda vile vile akaja kujua kwamba amechukua hatua isiyo ya hekima. Ni kweli kwamba kabla ya kuchumbiana mwanamume au mwanamke kwa kawaida anajifanya mzuri kama awezavyo, anajitokeza kweli kweli aonekane. Walakini, baada ya kuchumbiana huenda mtu akaanza kuonekana alivyo hasa. Mmoja kati ya watu wale wawili sasa huenda akaona magumu mazito ambayo hayakuonekana hapo kwanza.

Katika visa vya pekee ambamo wazee hawaoni ni lazima waulize-ulize juu ya kuvunjwa kwa uchumba, imewapasa watake kuhakikisha sababu za kufanya hivyo zilifaa. Sababu ‘inayofaa’ inaweza kuwa nini? Katika “Swali Kutoka kwa Wasomaji” lililochapwa katika Mnara wa Mlinzi wa Februari 1, 1970, mifano miwili ilitolewa. Angalia hapa mifano mingine michache. Wakati wa uchumba huenda mwanamke akaonyesha nia ya ‘kupiga ubwana,’ bila kuonyesha heshima ya kweli ya ukichwa, hivyo akitoa ushuhuda wa kutosha wa kwamba yeye ni namna ya mtu anayeelezwa katika Mithali 19:13; 21:9; 27:15, 16. Au, wakati huo, huenda mwanamume akafanya kosa zito, pengine akalewa, akajitia katika ufisadi fulani au tendo fulani la udanganyifu mkubwa. Au mmoja kati ya watu wale wawili anaweza kuona udhaifu wa wazi wa kiroho, pengine nia yenye nguvu ya kutaka sana mali za kimwili katika mwenzake, naye anaweza kuona kwa dhamiri yake kwamba kusonga mbele na kuoa au kuolewa kunaweza kumtwisha mzigo mzito ulemee nguvu zake za kiroho, pengine mzito kuliko yeye anavyoona anaweza kuchukua bila kuumia. Walakini, hii haimaanishi kwamba katika kila habari yule mwingine ataonekana kama mwenye kasoro au asiyefaa kitu. Mtu anaweza kuona kwamba mwenzake ni mtu mzuri sana lakini anaweza kuona kwamba ziko tofauti kubwa sana katika utu au maoni ambazo zingewaletea magumu sana wote wawili katika uhusiano wa ndoa. Basi, hizi ni nyingine za sababu zinazoweza kufanya mtu aamue kuvunja uchumba baada ya kufikiri kwa uangalifu na kusali, lakini si hizi peke yake. Bila shaka, mapatano ya watu wawili ya kuvunja uchumba yangekuwa afadhali zaidi kuliko hatua ya mtu mmoja peke yake. Lakini pengine yule mtu mwingine haoni ugumu uliopo, au hata pengine anapendelea kuupuza.

Haya yote yanakazia ubora wa kutofanya haraka haraka kuingia katika uchumba wa kuoa au kuolewa bali kujaribu kwanza kumjua yule mtu mwingine vya kutosha. Upendo kwa jirani umepaswa uzuie mtu ye yote asiwe na maoni ya kudharau uchumba, akijua kuvunja uchumba wenyewe kunavyoweza kuumiza maoni ya moyoni ya yule mwingine.

Katika visa ambavyo mtu amefiwa na mwenzi au akampoteza kwa kufanya kwake uzinzi (na kwa talaka inayolingana na Maandiko), huenda akajisikia moyoni akitaka urafiki amalize upweke. Huenda kukawa na maelekeo ya kuingia katika uchumba upesi zaidi kuliko vile ambavyo angeingia akiwa katika hali nyingine. Akiisha kupata usawa wa maoni ya moyoni, huenda mtu huyo akatambua kwamba uchumba huo ulikuwa usio wa hekima. Kwa habari ya mzee, huenda hii ikaharibu au isiharibu kufaa kwake. Lazima hali ziangaliwe.

Basi, kwa habari ya mtu aliye katika cheo cha kuwekea wengine mfano mwema, kama vile cha mzee au mtumishi wa huduma, mshiriki wa jamaa ya Betheli, au mtu mwingine aliye katika utumishi wa wakati wote, baraza ya wazee imepaswa itazame hali yote ya mtu na si kutazama tendo lile moja tu la kuvunja uchumba bila kupatana na mwenzake. Ikiwa mwendo wa mtu wa zamani unaonyesha yeye ana maelekeo au desturi ya kuchukua mambo hayo vivi hivi tu, basi wazee wanaweza kuona inafaa kupendekeza aondolewe katika cheo cha kuwekea wengine mfano mwema. Wanaweza kuona kwamba sababu ya kuvunja uchumba ni kwamba mtu huyo ameacha fikira zake na mapendezi yake yaanze kuelekea mtu mwingine, nao huo ni mwendo wa kigeugeu. Ikiwa watu wengi kundini wanaonyesha kutomheshimu huyo, jambo hili pia litafikiriwa inavyofaa. Lazima nia na hali za nchi zifikiriwe, kwa maana nchi au majimbo fulani ya ulimwengu yanachukua kwa uzito zaidi mipango hiyo kuliko vile mengine yanaichukua.

Walakini, ikiwa mambo haya yasiyofaa hayaonekani naye mtu huyo amejionyesha kuwa mzito, mwaminifu na mwenye kufikiria wengine, si lazima uamuzi wa kumaliza uchumba bila kupatana na mwenzake uhitaji aondolewe katika cheo cha mfano mwema wala si lazima awekewe kizuizi cha mapendeleo ya kundi. Litakaloamua sikuzote ni sababu zinazofaa au kama hakuna sababu zinazofaa za kuvunja uchumba.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki