Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w76 2/1 kur. 60-65
  • Ni Nani Anayestahili Kuwa Mzee?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ni Nani Anayestahili Kuwa Mzee?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • KABIDHI YA PEKEE KWA WACHUNGAJI
  • KUFIKIRI KWA UTIMAMU KUNATAKIWA
  • KUANGALIA “KONDOO WENGINE”
  • Wachungaji, Waigeni Wale Wachungaji Wakuu Zaidi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Wazee, Chukueni kwa Uzito Madaraka Yenu ya Uchungaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Wachungaji wa Kundi Chini ya Bwana Mmoja
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • “Wachungaji Wenye Kupatana na Moyo Wangu”
    Mungu Asema Nasi Kupitia Yeremia
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
w76 2/1 kur. 60-65

Ni Nani Anayestahili Kuwa Mzee?

“Lichungeni kundi la Mungu lililo kwenu, na kulisimamia, si kwa kulazimishwa, bali kwa hiari kama Mungu atakavyo; si kwa kutaka fedha ya aibu, bali kwa moyo.”​—1 Pet. 5:2.

1. Mungu analiona kundi lake kuwa la maana kadiri gani?

JE! MUNGU analiona kundi lake kuwa la maana, lenye kustahili kuangaliwa sana na waliowekwa naye kuwa wachungaji wadogo? Ni kwa kadiri gani Mungu anavyowaona “kondoo” zake kuwa wa maana? Mwana wake alisema hivi: “Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.” (Yohana 3:16) Kupendezwa kwake kulitosha kumruhusu Mwana wake atoke mbinguni kwa kipindi cha miaka 34 na robo aje duniani akiwa mwanadamu na kufungulia “kondoo” zake waliopotea njia warudi kundini.

2. Tunaweza kuwatumaini Yehova na Yesu kama wachungaji? Eleza.

2 Sisi ni sehemu ya “ulimwengu” huo ambao Mungu alipenda sana na unaopaswa kupatanishwa na Mungu. Ombi alilofanya kwa Waisraeli waliorudi kutoka utumwa wa nchi ya ugenini linatuhusu sisi leo kwa kadiri ile ile: “Nirudieni mimi . . . nami nitawarudia ninyi.” (Zek. 1:3) Mtume Petro aliandika hivi kwa kundi la kwanza la Kikristo: “Mlikuwa mnapotea kama kondoo; lakini sasa mmemrudia Mchungaji na Mwangalizi wa [nafsi] zenu.” (1 Pet. 2:25) Mungu analinda wale wanaomrudia: “Atalilisha kundi lake kama mchungaji, atawakusanya wanakondoo mikononi mwake; na kuwachukua kifuani mwake, nao wanyonyeshao atawaongoza polepole.” (Isa. 40:11) Amemweka pia msaidizi ambaye ndiye Mchungaji Mwema, Yesu Kristo, aliyetoa “uhai wake kwa ajili ya kondoo.”​—Yohana 10:7-15.

3. Paulo alijihakikishaje kuwa mchungaji mwenye daraka?

3 Yehova amepanga kuwe na wachungaji wadogo pia wanaopendezwa kuangalia “kondoo.” Mtume Paulo ni mmoja wao, naye alisema hivi: “Tulikuwa wapole katikati yenu, kama vile mlezi awatunzavyo watoto wake mwenyewe. Vivyo hivyo nasi tukiwatumaini kwa upendo mwingi, tuliona furaha kuwapa, si Injili ya Mungu tu, bali na [nafsi] zetu pia, kwa sababu mmekuwa wapendwa wetu.” Kadiri ambavyo alikuwa na nia ya kutoa nafsi yake inaonyeshwa na aliyoandikia kundi la Korintho: “Nami kwa furaha nyingi nitatapanya, tena nitatapanywa kwa ajili ya [nafsi] zenu.”​—1 The. 2:7, 8; 2 Kor. 12:15; 11:28.

4. Kwa sababu ya maoni yetu juu ya wachungaji hao, lengo na wajibu wa Wakristo leo umepaswa kuwa nini?

4 Tunaweza kupatanisha maisha zetu na kielelezo cha wachungaji hao, yaani, Mchungaji Mkuu, Mchungaji Mwema, na mtume Paulo. Mtume Yohana anasema kwamba “imetupasa na sisi kuutoa uhai wetu kwa ajili ya hao ndugu.” (1 Yohana 3:16) Aliyafahamu sana maneno ya Yesu: “Kwa kuwa nimewapa kielelezo; ili kama mimi nilivyowatendea, nanyi mtende vivyo. Amin, amin, nawaambia ninyi, Mtumwa si mkuu kuliko bwana wake; wala mtume si mkuu kuliko yeye aliyempeleka.”​—⁠Yohana 13:15, 16; linganisha Yohana 15:12, 13.

5. Kwa sababu gani wengine hawajapata bado njia ya kumrudia Yehova?

5 Kwa kuwa Biblia inasema Yehova ni “Mungu wetu, na sisi tu watu wa malisho yake, na kondoo za mkono wake,” ni nini kinachozuia watu wasimtumikie Yehova? Ni kwamba tu hawajui njia ya kumrudia; hawajawa na mtu wa kuwaongoza, yaani, viongozi wao wa kibinadamu wanaodhaniwa kuwa wachungaji wamewapoteza. Yesu alisema katika siku zake kwamba ni wachungaji wa uongo ambao wangewajia “wamevaa mavazi ya kondoo, walakini kwa ndani ni mbwa-mwitu wakali.” Kwa upande mwingine, watu walikuwa wamekonda “na kutawanyika kama kondoo wasio na mchungaji.” Walihitaji kuchungwa inavyofaa, na Yesu aliikubali kazi hiyo.​—Zab. 95:6, 7; Mt. 7:15; 9:36.

KABIDHI YA PEKEE KWA WACHUNGAJI

6, 7. (a)  Ni nani waliomo katika kundi ambalo lazima lichungwe? (b) Wachungaji wanatakiwa watoe hesabu ya nini?

6 Yesu alipanga kuwe na wachungaji wadogo wa kuangalia “kondoo” zake, aliporudia makao yake ya kimbinguni. Leo, wale wanaowekwa na Mchungaji Mwema wana wajibu wa pekee kulisha “kondoo” za Yesu. Petro, ambaye aliagizwa na Yesu kwa njia ya pekee afanye hivyo (tazama Yohana 21:15-17), anaeleza waangalizi wa Kikristo wa leo agizo ilo hilo, akisema hivi: “Nawasihi wazee [waangalizi wa kiroho kundini] walio kwenu [kundi], . . . lichungeni kundi la Mungu lililo kwenu [“lililo katika uangalizi wenu,” NW], . . . kwa hiari . . . kwa moyo.”​—1 Pet. 5:1, 2.

7 Ingawa Wakristo wote walio wakf wanatakiwa ‘wafanye watu wa mataifa yote kuwa wanafunzi, wakiwabatiza na kuwafundisha kuyashika mambo yote niliyoaamuru,’ kabidhi ya pekee ya wachungaji ni kuangalia “kundi la Mungu,” wale ambao wamekwisha kuwa washiriki wa kundi. Lazima wamtolee Yehova hesabu juu ya washiriki hao.​—Mt. 28:19, 20; Ebr.13:17; 4:13.

8. Ni akina nani wanaochaguliwa, na ni akina nani wasiochaguliwa, kuwa wachungaji wa kundi la Mungu?

8 ‘Jamii kubwa ya makuhani waliitii ile Imani’ kwa kumkubali Yesu kuwa Masihi. Lakini hakuna waandishi wala Mafarisayo waliowekwa kuwa wachungaji katika kundi la Kikristo kwa sababu walikuwa “wameketi katika kiti cha Musa.” “Wenye hekima ya mwilini” walioona utukufu kwa kusalimiwa hadharani na kutajwa kuwa “Rabi” hawakuitwa. Hakuna “kiongozi” wa namna hiyo anayepatikana katika kundi la Kikristo la mashahidi wa Yehova. Mashahidi wa Yehova wanamtambua kiongozi mmoja tu, Kristo. Wanaepuka cheo cho chote cha kuheshimiwa kupita kiasi. Yesu alisema hivi: “Nyote ni ndugu.”​—Matendo 6:7; Mt. sura ya 23; 1 Kor. 1:26-29.

9. Kumepaswa kuwe na wazee wangapi katika kundi, nao wanachaguliwa kati ya akina nani?

9 Ili kuangalia faida za kundi la mashahidi wa Yehova inavyofaa, “Mungu ameweka wengine katika [kundi],” kutia na waalimu, waangalizi, wachungaji. Katika kundi la kwanza wote waliostahili kulingana na Maandiko walitumikia. Hakuna hesabu ya watu ya wazi iliyoonyeshwa; walikuwa wengi katika Efeso, kama inavyoonekana Paulo anapopeleka ujumbe kwa “wazee” wakutane naye Mileto wapokee maagizo ya kazi zao. Vivyo hivyo, hakuna hesabu ya wazi inayoonyeshwa katika kundi la Kikristo la kisasa. Hawana haja ya kuhitimu katika chuo fulani cha kidini kilichopangwa na mwanadamu, kama katika makanisa ya Jumuiya ya Wakristo (Kristendomu). Lakini imewapasa wafanye kwa bidii kazi ya kuhubiri, wakiwa wanafunzi wa kawaida na wenye bidii wa Neno la Mungu, na kufanya yanayosemwa katika amri mbili zilizo kuu, yaani, kumpenda Mungu na jirani.​—1 Kor. 12:28; Mt. 22:36-39.

10, 11. Inawezekanaje mtu akawa “bila lawama,”‏ na kwa sababu gani kanuni hiyo ya juu inawekwa?

10 Katika 1 Timotheo sura ya tatu, Paulo anaweka sifa za Maandiko kwa mtu anayejaribu kufikia cheo cha mwangalizi. Lazima awe bila lawama. Hiyo inawezekana kwa kiumbe cha kibinadamu kisichokamilika? Hiyo isingetaka mtu awe mkamilifu? Je! Paulo anapita kiasi, anataja yasiyowezekana? Hatuwezi kukata shauri kwa njia hiyo, kwa maana bila shaka Paulo aliyajua maneno ya Yesu yaliyomo katika Mathayo 5:48, NW: “Kwa hiyo lazima mwe watakatifu, kama vile Baba yenu wa kimbinguni alivyo mtakatifu.” Paulo alijua pia kwamba Mfalme Daudi hakuweza kuwa bila lawama kabisa, lakini Paulo alilitambua ombi la Daudi kwa Yehova kuwa sehemu ya Maandiko yaliyoongozwa na Mungu: “Ee [Yehova], unihukumu mimi, maana nimekwenda kwa ukamilifu wangu.”​—Zab. 26:1; linganisha 2 Wafalme 20:3.

11 Ni wazi kwamba haiwezekani mwanadamu akawa kama Mungu kabisa kabisa, bila upungufu. Kama sivyo, cheo cha mwangalizi katika kundi la Kikristo kingeachwa wazi bila wa kukichukua. Kwa hiyo, kwa kuwa matakwa ya Maandiko yamewekwa juu, hiyo inaonyesha kwamba kila mtu anayetamani kupata cheo hicho atajitahidi sana kuyatimiza. Kwa mfano, katika shauri la kuwa bila lawama, mzee asingeweza kuangalia wale walio katika kabidhi yake ikiwa anakosa sana sifa hiyo. Lazima mwangalizi aweze kuendelea ‘kuwaonya vijana waume kuwa na kiasi; katika mambo yote akijionyesha yeye mwenyewe kuwa kielelezo cha matendo mema, na katika mafundisho yake akionyesha usahihi.’​—Tito 2:6-8.

12. Imempasa mtu awe ameoa ndiyo astahili kuwa mwangalizi? Eleza.

12 Imempasa mwangalizi awe “mume wa mke mmoja.” Hiyo haimaanishi kwamba mwanamume mjane au mseja hastahili. Sasa, kama ilivyokuwa siku za Paulo, inamaanisha kwamba mtu mwenye wake zaidi ya mmoja au anayeishi na mwanamke bila kuandikisha ndoa hawezi kutumikia kama mwangalizi katika kundi la Kikristo. Kwa kweli, hatuwezi kushirikiana naye kwa kumpendelea. Pamoja na lile takwa jingine katika mstari wa 4 (1 Timotheo 3, NW) ingeonyesha kwamba ingempasa mtu asiwe tineja (au kijana), bali mwenye umri wa kutosha kuwa na jamaa ndio awe mwangalizi.

13. Kwa sababu gani lazima wazee waepuke mazoea ya siku hizi?

13 Mara nyingi vijana wa leo na hata wazee wanaambukiwa na mazoea ya ajabu ya taratibu ya mambo iliyopo. Kuchangamana na wale wanaoelekea mazoea hayo shuleni au biasharani kunaelekea kushawishi Wakristo wajipatanishe nao. Bila shaka Wakristo katika karne ya kwanza walipaswa kushindana na jambo ilo hilo, kwa maana shauri zaidi la Paulo (1 Tim. 3:2, NW) kuwa “mwenye kiasi katika mazoea” lilipaswa lifikiriwe katika kuweka wazee. Kujipatanisha na mazoea ya ulimwengu wa kale kungezuia mtu asiwe na kibali ya Mungu na kuonekana asiyefaa kupata mgawo unaohitaji kuonya wanaume vijana. Mtume Petro anasema kwamba pengine kulikuwa na wakati tulipofuata desturi hizo kwa ujinga lakini sasa lazima tuishi kufanya mapenzi ya Mungu. Pengine hiyo itashangaza tuliokuwa tukishirikiana nao zamani na kuwafanya watusemee mambo yasiyofaa, lakini Yesu alisema hiyo haipaswi kutusumbua.​—Yohana 15:19; 1 Tim. 4:11, 12; 1 Pet. 4:3, 4; Rum. 12:2.

KUFIKIRI KWA UTIMAMU KUNATAKIWA

14. Imempasa mwanamume mzee aoneje cheo chake?

14 Mwanamume mzee katika kundi hana cheo bora zaidi. Mtu akiwa mzee “asinie makuu kupita ilivyompasa kunia; bali awe na nia ya kiasi.” The New English Bible inatafsiri maneno hayo ikisema si “kujivuna” bali ‘kujikadiria kwa kiasi.’ Hiyo ingezuia mtu asitazamie kutendewa kama “mapasta” wa Jumuiya ya Wakristo (Kristendomu), wanaopenda na kutazamia watu wawasifu-sifu sana.​—Rum. 12:3.

15. Kuwa “mwenye utaratibu” kunatia nini ndani?

15 Lazima waangalizi wawe ‘wenye utaratibu, wakaribishaji wa wageni.’ (1 Tim. 3:2, NW) Wachungaji wa uongo hawakuwa na utaratibu hata kidogo. Yehova aliwalaumu, akisema: “Ole wao wachungaji [katika Israeli], wanaoharibu kondoo za malisho yangu na kuwatawanya!” (Yer. 23:1, 2) Kujidai kwao kuwa wachungaji hakukuwaokoa na hukumu ya Yehova. Yesu pia aliwalaumu wachungaji wa uongo wa siku zake. Kwa hiyo lazima wachungaji wa Kikristo wawe wenye utaratibu, wakijitahidi kuleta amani kundini. Nyakati nyingine huenda wakapaswa ‘kuwaonya wale wasiokaa kwa utaratibu,’ wale ambao “hawana shughuli zao wenyewe, lakini wanajishughulisha na mambo ya wengine.” (1 The. 5:14; 2 The. 3:11) Ili maonyo yao yakubalike lazima wao wenyewe waweke kielelezo kwa kushikamana sana na sheria na kanuni za Biblia, si kueneza kamwe mawazo yasiyopatana na kweli.​—1 Kor. 4:6; 14:33; Tito 2:6-8.

16. Kuwa mkaribishaji wa wageni kunahusu kukaribisha wapya katika Jumba la Ufalme tu?

16 Mfalme Sulemani alipoomba ufanisi wakati wa kuwekwa wakf kwa hekalu katika Yerusalemu, aliwataja ‘wageni,’ kwamba watakuja waabudu huko. Bila shaka aliwafanyia mipango ya ukaribishaji. Leo Yehova anatubariki kwa kutupa ongezeko kubwa la ‘wageni,’ yaani, wale ambao hawakuwa waabudu wa Yehova zamani. Lazima mipango ya kutosha ifanywe kuwakaribisha. Hiyo inawekea waangalizi mzigo, si kuwasalimu tu katika Jumba la Ufalme, bali pia kuwasaidia wafanye maendeleo katika njia ya Kikristo. Huo ni ukaribishaji wa kweli, ambalo ni takwa la kuwa mwangalizi.​—1 Fal. 8:41-43; Mik. 4:1, 2; Mt. 9:37; Ebr. 13:1, 2; 3 Yohana 5.

17, 18. (a) Kufundisha kumepaswa kufanyiwe jukwaani tu? (b) Lengo la mwangalizi kama mwalimu ni nini?

17 Yesu alisema, “Imeandikwa katika manabii, Na wote watakuwa wamefundishwa na Mungu.” (Yohana 6:45; Isa. 54:13) Hilo linazidi kuwa jambo la maana tunapokaribia mwisho wa taratibu ya kale ya mambo na kuingizwa kwa ile mpya ikiwa chini ya usimamizi wa Kuhani na Mfalme aliyetiwa mafuta, Yesu Kristo. Yehova Mungu ndiye Mwalimu Mkuu kupita wote, lakini Yesu alisema kwamba kwa kufaa wanafunzi wake walimwita yeye pia Mwalimu. Tena, baada ya kutukuzwa Yesu Kristo “alitoa wengine kuwa mitume; na wengine kuwa manabii; na wengine kuwa wainjilisti; na wengine kuwa wachungaji na waalimu; [kwa sababu gani?] kwa kusudi la kuwakamilisha watakatifu, hata kazi ya huduma itendeke.”​—Efe. 4:11, 12.

18 Kwa hiyo, lazima wazee wawe waalimu wa Neno la Mungu. Hawapaswi ‘kutekenya masikio’ ya kundi, bali kufikia akili na mioyo ya kundi lao lenye mfano wa kondoo. Hiyo haiwanui wawe kama wataalamu au makasisi wenye madaraja waliosomea uanadini, wenye kutoa-toa hotuba tu na basi. Mzee wa Kikristo hafundishi jukwaani tu, bali anafundisha kwa kufaa zaidi watu binafsi. Ni mafundisho ya Biblia.

19. Ni ‘matendo gani ya mwili’ yangemzuia mtu asiwekwe kuwa mwangalizi?

19 Mzee hawezi kuwa “mpiga kelele ya ulevi.” Kutumia vileo kupita kiasi kunafisha ganzi akili za mtu hata kuharibu uamuzi wake juu ya mambo, anarukwa na akili. Mzee hapaswi kuwa “mpigaji,” ama kwa kutumia mwili wake au ulimi. Hapaswi kuwa mtaka vita wala mpenda fedha wala asiyesikiliza shauri. Mambo hayo yangemfanya asistahili kuongoza kundi la Wakristo. Ingawa hayawezi kumzuia asitumikie katika kanisa la Babeli Mkuu, ‘matendo hayo ya mwili’ yangemzuia asitumikie katika kundi la mashahidi wa Yehova.​—1 Tim. 3:3; 6:10.

20. (a) Kwa sababu gani kusimamia nyumba ya mtu mwenyewe kumepaswa kuhesabiwe anapofikiriwa kuwekwa kuwa mzee? (b) Lakini ni nini kinachoweza kukumbukwa?

20 Paulo anauliza ulizo, baada ya kusema lazima mzee awe mwanamume mwenye kusimamia nyumba yake mwenyewe katika adabu nzuri, mwenye kutiisha watoto, yaani, “Ikiwa kweli mwanamume ye yote hajui jinsi ya kusimamia nyumba yake mwenyewe, yeye ataliangaliaje kundi la Mungu?” (1 Tim. 3:5, NW) Paulo alitambua kwamba katika nyumba ya Mungu maisha zaidi zimo hatarini kuliko zile zilizomo hatarini katika nyumba ya mwanamume. Kwa hiyo imempasa astahili sana katika uwezo wake wa kushughulika na mambo katika nyumba yake mwenyewe ili kufaidi wote. Lakini je! hiyo inamaanisha kwamba lazima nyumba yake iwe kielelezo kikamilifu katika kila jambo? Huenda isiwezekane. Huenda akawa anafanya yote anayoweza, na bado huenda mtu fulani katika nyumba yake akakosa kuitikia vile yeye anavyotaka. Huenda mke wake akawa mwasi sana, hata huenda akawa ni mpinga Yehova na Neno lake. (Mt. 10:36) Lakini maulizo ya maana ni haya: Ni kwa kadiri gani mwanamume mwenye nyumba anashiriki kumfanya mkewe awe mwasi, na je! mafarakano yaliyomo nyumbani yanaletwa na hatia yo yote ya mwanamume mwenyewe? Lazima maoni ya kundi juu ya hali hiyo yafikiriwe pia.

21. Kwa sababu gani ni hekima kutoweka “mwanamume aliyegeuka hivi karibuni” awe mwangalizi?

21 Inawapasa waangalizi kufanya maamuzi mazito. Huenda maamuzi hayo yakahusu maisha au kuzuiwa kwa kazi iliyo ya maana kupita zote ya kuzihubiri habari njema. Huenda kukawa na marufuku. Kwa hiyo uamuzi mwema ulio timamu utahitajiwa. Hivyo haimpasi mwangalizi kuwa “mwanamume aliyegeuka hivi karibuni.” (1 Tim. 3:6, NW) Huenda akawa na shauku (enthusiasme) na juhudi waliyo nayo wale ambao wamekaa sana katika imani lakini huenda akakosa ‘akili zilizozoezwa kupambanua mema na mabaya.’ (Ebr. 5:13, 14) Wapya wamepaswa wazoezwe kwanza mpaka wastahili. Kwa sasa, waangalie ‘wale wanaowaongoza, waliowaambia neno la Mungu; tena, kwa kuuchunguza sana mwisho wa mwenendo wao, iigeni imani yao.’​—Ebr. 13:7.

KUANGALIA “KONDOO WENGINE”

22. Mitindo imepaswa ionweje, na imetupasa tufuate mfano wa nani katika jambo hili?

22 Kwa kuwa wao “si wa ulimwengu,” mashahidi wa Yehova hawaigi mitindo ambayo ingewaweka katika fungu moja na watu wanaoonekana kuwa waasi katika jamii ya watu. Kwa hiyo ndugu vijana kundini walikumbuke onyo la Petro kwamba lazima wachungaji wa kundi la Mungu waweke mfano unaofaa. Paulo alikuwa mfano mwema. Alisema hivi: “Mnifuate [“mniige,” NW] mimi kama mimi ninavyomfuata Kristo.” Watu wanaona kwamba mashahidi wa Yehova ni tofauti; mwenendo wa Kikristo, hasa wa waangalizi, umepaswa ulete “ushuhuda mzuri kutoka kwa watu walio nje” ya kundi.​—1 Kor. 11:1; 1 Tim. 3:7, NW; Yohana 17:16; 1 Pet. 5:2, 3.

23. Ni mambo gani mengine yamepaswa yatazamiwe katika waangalizi?

23 Katika sura ya kwanza ya kitabu cha Tito, Paulo alitoa shauri juu ya mambo ya kutazamia katika wazee. Lazima mtu awe “asiye na shtaka,” mwenye sifa zisizotiliwa mashaka. Mtu ye yote asiweze kumlaumu kuwa mwenye tabia mbaya za kipekee. Asiwe “mwenye kutaka yake” au mwenye kulazimisha wengine wafanye yeye atakavyo; asiwe “mwenye kuhamaki,” mwepesi wa hasira; asiwe “mwenye pupa ya mapato ya udanganyifu,” bali mwaminifu sana anapofanya mambo ndani na nje ya kundi.​—Tito 1:6, 7, NW; tazama pia 1 Petro 5:2, 3.

24. Mwangalizi anaonyeshaje ana uaminifu wa kutetea yanayofaa?

24 Ni jambo la maana zaidi mwangalizi awe “mwaminifu” akimwiga Yesu Kristo, kwa kutetea yanayofaa. Uaminifu wake wa kutetea kanuni za haki huenda ukamtaka akaripie “wale wanaopinganisha.” (Tito 1:9, NW) Huenda hiyo isiwe kazi ya kupendeza, lakini kusita kutoa karipio linapotakiwa huenda kukaonyesha yeye anamwunga mkono anayetenda dhambi, kwa njia hiyo akiwa mwenzi wake. (Mit. 29:24) Karipio linalotolewa linamfadhili mtu ambaye huenda akachukua hatua ya uongo bila kujua. (Gal. 6:1) Huenda matendo fulani yasiyofaa yakasahauliwa kwa vyepesi, huenda yakaachiliwa; lakini sivyo ilivyo kwa matendo yanayoweza kuudhi roho takatifu kwa kuleta migawanyiko na madhehebu kundini. Kwa hiyo, nyakati nyingine, uaminifu wa kutetea yanayofaa unahitaji kukaripia.​—Luka 17:3, 4; Efe. 4:30.

25, 26. (a) Kwa sababu gani ni lazima wachungaji hasa wajiangalie wenyewe na kundi la Mungu? (b) Wapya wanaweza kutazamia kuchungwa vema katika kundi la Mungu leo?

25 Paulo alipowaaga wazee wa Efeso, aliwaomba wajiangalie wenyewe na “lile kundi lote nalo . . . mpate kulilisha [kundi] lake Mungu . . . [kwa sababu sasa] mbwa-mwitu wakali wataingia kwenu, wasilihurumie kundi.” (Matendo 20:28, 29) “Mbwa-mwitu” hao wangerarua kundi, wakitatua mavazi yao ya utambulisho wa Kikristo. Onyo hilo linafaa zaidi wakati huu wa maana. Hakuna mwangalizi anayetaka kuwa na lawama la kupotea kwa ye yote wa “kondoo” za Yehova, kwa sababu ya kukosa kutimiza wajibu wake.

26 Yearbook (Annuaire) kinaonyesha ni kwa kadiri gani wengi wa “kondoo wengine” wa Yesu wamejishirikisha na mashahidi wa Yehova wa Kikristo. Bado kuna wengine ambao ‘imempasa Yesu kuwaleta’ kwa sababu ‘sauti yake wataisikia.’ Katika hizi “siku za mwisho” za taratibu ya kale ya mambo wenye kumiminika kuingia ndani ya kundi lile moja la mchungaji yule mmoja wanapokea mafundisho juu ya njia za Yehova. Wanaweza kuwa na uhakikisho wa kupokea uangalizi wenye upendo na huruma kwa wale ambao Yehova ameona wanafaa kukabidhi kazi ya uchungaji.​—Yohana 10:16; Luka 12:32; Mik. 4:1-4; Isa. 32:1, 2.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki