Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w77 6/1 kur. 263-264
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
  • Habari Zinazolingana
  • Elimu—Gharama Yake? Faida Yake
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Elimu Yenye Kusudi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Mashahidi wa Yehova Wana Maoni Gani Kuhusu Elimu?
    Maswali Yanayoulizwa Mara Nyingi Kuhusu Mashahidi wa Yehova
  • Elimu—Itumie Kumsifu Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
w77 6/1 kur. 263-264

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

● Inapendekezwa watoto wa jamaa za Kikristo wasome miaka mingapi?

Jamaa nyingi za Kikristo zimeona inafaa watoto wao wajipatie elimu iliyo kanuni ya watu wote katika nchi yao. Wazazi ndio wenye daraka la kuamua watoto wao watapata masomo kiasi gani.​—Mit. 1:8; 6:20-22; Efe. 6:4.

Wazazi Wakristo, pamoja na watoto wao, wanatakiwa “kunyenyekea kwa wenye uwezo na mamlaka.” (Tito 3:1) Hiyo yatia ndani kutii sheria za serikali juu ya masomo ya kilimwengu. Katika nchi nyingi serikali hutaka wanafunzi waendelee kusoma mpaka watimizapo umri fulani, na umri huo waweza kuwa kati ya miaka kumi na mitatu mpaka kumi na minane. Katika nchi nyingine watoto hutakiwa wasome miaka michache tu, halafu inakuwa juu ya jamaa kupanga mambo ya mtoto ya wakati ujao. Mara nyingi hiyo yaonyesha mtoto anaachwa ajitafutie riziki. Lakini sheria ikisema ni lazima watoto waende shuleni miaka kadha, yawapasa watoto Wakristo wafanye hivyo, kwa maana hilo halipingani na amri yo yote ya Biblia.​—Mt. 22:21.

Maandiko yamekabidhi wazazi daraka la kuzoeza watoto wao, nao watoto wanatakiwa watii wazazi wao “katika mambo yote” yasiyopingana na matakwa ya Mungu yaliyotajwa waziwazi. (Kol. 3:20; Mit. 4:1; angalia pia Matendo 4:18, 19.) Hivyo, maadamu watoto ni wadogo, ikiwa sheria yasema wawe chini ya usimamizi wa wazazi, au ikiwa wanaishi katika jamaa na kupewa riziki nayo, lazima wafuate maamuzi ya wazazi wao juu ya kiasi cha masomo wanayopaswa kuwa nayo. Inakuwa ivyo hivyo ikiwa mzazi mmoja au wote wawili si waamini. Hiyo haimaanishi kwamba watoto hawawezi kuzungumza na wazazi wao na kuwaeleza wanavyotaka, lakini ni lazima waheshimu maamuzi ya baba yao, au ikiwa hawana baba, waheshimu maamuzi ya mama yao.

Kanuni nyingine ya Maandiko ni kwamba Wakristo wapaswa kuwa tayari kujipatia riziki wenyewe, nao wanaume waliooa wapaswa kutafuta ya jamaa zao pia. (Efe. 4:28; 1 Tim. 5:8) Kwa hiyo, katika mitaa mingine, ambako bei za vitu zimepanda sana, huenda mtu akatakiwa kuwa na elimu zaidi aweze kujipatia riziki. Kwa ujumla, wazazi na vijana Wakristo katika maeneo hayo wameona inafaa kujipatia elimu ambayo ndiyo kanuni ya watu wengi; katika Amerika inapendekezwa kuwa na masomo ya juu.

Jambo jingine lipaswalo kufikiriwa ni mkazo ambao Yehova hutia juu ya Neno lake lililoandikwa, na vilevile mgawo ambao amewapa watumishi wake kuwa wahubiri na waalimu wa “kila andiko.” (2 Tim. 3:16, 17; Mt. 28:19, 20) Hiyo yaonyesha sana kwamba Yehova ataka mashahidi wake wote, vijana na wazee, wawe wenye elimu. Yawapasa waweze kusoma vizuri Biblia katika lugha yao ya kienyeji na kueleza wengine ujumbe wake kwa ufasaha na usahihi, kwa mdomo na kwa kuandika. Wanaweza kutumia vizuri masomo yao ili wafikie miradi hiyo ya kiroho.​—1 Kor. 2:13; Mhu. 12:10.

Tena, kwa kawaida masomo ya msingi yanayotolewa na serikali yanatia ndani hesabu, historia na habari za afya. Shule nyingi hutoa pia mazoezi ya ziada, kama vile kutumia vyombo vya kazi na mashine, useremala, kuweka vitu vinavyohusu umeme, kutengeneza motokaa, kuchapa, kutengeneza vitu vya utamaduni, kujifunza mambo ya kisayansi, kupiga chapa, muziki na kujifunza lugha. Nao wasichana hupewa masomo ya mambo ya kinyumbani na jinsi ya kulea watoto. Kwa sababu ya masomo hayo mengi yanayopatikana katika nchi nyingi, wavulana na wasichana wanaweza kuongozwa na wazazi wao wachague mambo watakayojifunza na kuwafaidi baadaye. Wazazi wachache wameona inafaa kupangia watoto wao waingie katika masomo mafupi ya kujizoeza ufundi katika shule zenye ujuzi wa mambo hayo, kama vile mambo ya umeme na mashine za hesabu (kompiuta). Kusudi limekuwa kuwasaidia wajiruzuku wanapofanya utumishi wa Yehova.

Leo, wako vijana wengi waliobatizwa wanaomtumikia Yehova. Funzo la kipekee, kujitayarisha kwa ajili ya mikutano na kushiriki katika Shule ya Kitheokrasi kumewapa maarifa ya msingi ya kweli ya Biblia wayatumie katika mahubiri ya Kikristo. Wamefaidika pia na masomo shuleni. Lakini yawapasa wasome elimu ya kilimwengu mpaka wakati gani? Isingekuwa sawa kijana akijiamulia mwenyewe kuendelea na masomo zaidi kinyume cha sheria na mapenzi ya wazazi wake. Kulingana na Timotheo wa Kwanza 6:20 isingekuwa hekima kujaza akili na filosofia za wanadamu wasiokamilika: “Ee Timotheo, ilinde hiyo amana; ujiepushe na maneno yasiyo ya dini, yasiyo na maana, na mashindano ya elimu iitwayo elimu kwa uongo.” Kwa hiyo huenda kukaa miaka zaidi katika chuo kikuu kukaleta mitego. Huenda mtu akavurugwa akili na filosofia za kibinadamu hata akaacha kumwamini Mungu na Biblia. (Kol. 2:8) Masomo mengi ya vyuo vikuu yanategemea makisio ya uongo, kama vile mageuzi, nayo yanaunga mkono taratibu ya zamani ya mambo, ambayo itapita milele karibuni. (1 Yohana 2:17) Wataalamu wengi sana hawamwamini Mungu wala Biblia nao hufundisha kwa bidii imani zao za kutomwogopa Mungu. Tena, tabia za watu huharibiwa katika vyuo vikuu, kutia na hatari ya kuzoea kutumia dawa za kulevya.

Katika nchi nyingi shule za serikali na za watu wenyewe zinazidi kujawa na uasi, jeuri na upotovu (na vilevile dawa za kulevya) kuliko zilivyokuwa miaka iliyopita. Ni wazi kwamba shule nyingine ni mbaya sana. Lakini je! sasa imekuwa haiwezekani vijana waende shuleni tena katika mitaa yao? Ulizo hilo lijibiwe na wazazi wenyewe. Lakini, inaelekea vijana kadha Wakristo wametisha wazazi wao kwamba watafanya jeuri au kuingia katika ufisadi wakikusudia kuwafanya wawaruhusu waache shule mapema. Wameshinda wazazi wao, ambao wametaka sana kulinda watoto wao kwa sababu ya huruma, wakakubali kuwatoa katika shule hizo za msingi. Katika visa vingi watoto hao wameharibika.

Ujuzi waonyesha kwamba vijana Wakristo wenye bidii na wasiofanya mchezo, ambao wamezoezwa vizuri katika mambo ya kinyumbani na kufundishwa kiroho kanuni za Biblia, wanaweza kuepuka matatizo kwa kawaida. Kwa kufanya mambo yao wenyewe bila kuingilia ya wengine, wanaona wanaweza kwenda shuleni kwa kawaida na kuwa salama. Ndivyo ilivyo hasa wanapojiepusha na matata, na kutohusika katika michezo na mambo mengine yanayofanywa masomo yaishapo. Wanapata ulinzi pia wanapoacha nuru yao ya Kikristo iangaze, wakiwachukua wanadarasa wenzao kama shamba la kuhubiri habari njema za Ufalme. Lakini wale vijana wanaoacha shule mapema hutoa ushuhuda kiasi gani kwa kweli? Mara nyingi wanang’ang’ana wakijitafutia riziki, au wanaoa mapema na kujikuta wakiwa na jamaa ya kutafutia riziki.

Katika makundi mengi ya mashahidi wa Yehova imeonekana kwamba wale wachache ambao hawakumaliza elimu yao ya msingi waliona baadaye ilikuwa vigumu kutatua matatizo ya maisha, kufaulu katika utumishi wa painia au kuchukua sawasawa madaraka ya ndoa.

Kusudi letu si kuwekea jamaa za Kikristo sheria hapa. Bali, tunatoa mawaidha ya kuwaongoza. Wazazi na vijana wapange masomo ya kutosha yatakayowezesha vijana watimize mapendezi na miradi yao maishani kwa njia safi, yenye kuheshimika. Vijana wa leo waliozoezwa vizuri ndio watakaokuwa watumishi wa Yehova waliokomaa na wenye bidii kesho. Kuwa na maoni ya kiasi juu ya elimu sasa kwaweza kuwasaidia wakamilishe furaha yao juu ya paradiso ya kiroho ya Mungu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki