Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w76 4/15 kur. 183-189
  • Serikali Moja Ile ya Ulimwengu Mmoja Chini ya Enzi Kuu ya Mungu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Serikali Moja Ile ya Ulimwengu Mmoja Chini ya Enzi Kuu ya Mungu
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • “ULIMWENGU MMOJA” CHINI YAKE
  • Uzuri wa Enzi Kuu ya Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
  • Je, Unaitegemeza Enzi Kuu ya Yehova?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Enzi Kuu ya Yehova na Ufalme wa Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Enzi Kuu
    Ufahamu wa Kina wa Maandiko
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
w76 4/15 kur. 183-189

Serikali Moja Ile ya Ulimwengu Mmoja Chini ya Enzi Kuu ya Mungu

1. Washauri wa ulimwengu wanalazimika kukata shauri gani?

WASHAURI juu ya mambo ya ulimwengu wanapata vipingamizi sikuzote. Walipende au wasilipende wazo hili, wanalazimika kukata shauri kwamba, ijapokuwa jamaa ya kibinadamu ina umri wa miaka elfu sita sasa; haiwezi kujiongoza yenyewe. Yenyewe haikuleta aina ya serikali ambayo imefanya au yaweza kufanya wanadamu wote kuwa ulimwengu mmoja.

2. Kulingana na mwanzo ambao Mungu aliwapa wanadamu, kwa nini siwe wa kulaumiwa kwa sababu wanadamu si “ulimwengu mmoja” leo?

2 Wa kulaumu ni nani? Si Muumba wa jamaa ya kibinadamu, Baba yao wa kimbinguni. Wanadamu wote walitokana na mtu mmoja wa kwanza ambaye Bwana Mungu Yehova, Mwenye Enzi Kuu, aliumba duniani. Kisha, kutokana na sehemu ya mwili mkamilifu wa mwanamume huyu ambao Muumba alitumia kama msingi, akamfanya mwanamke wa kwanza, ili wanadamu wote wapate kuwa mwili mmoja, wazao wa wanadamu wawili hawa wa kwanza. Uhakika huu ulielezwa waziwazi kwa wanafilosofia wa Mahakma Kuu ya Ugiriki ya Areopago katika Athene, Ugiriki, miaka miaka kumi na tisa iliyopita. Paulo mtume wa Kikristo aliwaambia mahakimu hao wenye cheo hivi: “[Mungu] alifanya kila taifa la wanadamu kutoka katika mmoja, wakae juu ya uso wa nchi yote, akiisha kuwawekea nyakati alizoziamuru tangu zamani, na mipaka ya makazi yao; ili wamtafute Mungu, ingawa ni kwa kupapasa-papasa, wakamwone, ijapokuwa hawi mbali na kila mmoja wetu.”​—Matendo 17:22-27; Mwa. 2:7-25; 1:26-31.

3, 4. (a) Tangu mwanzo, kusudi la Mungu kwa wanadamu lilikuwa nini? (b) Adamu alionyeshwaje kwamba kutii enzi kuu ya Mungu kulikuwa njia ya kutazamia uzima wa milele?

3 Mungu alikusudia jamaa ya kibinadamu iwe “ulimwengu mmoja” wa wanadamu, jamii moja ya kibinadamu wote wakiwa wa mfupa, mwili na damu ile ile. Jamii hii ya kibinadamu yenye umoja ilipaswa ikae katika uso wote wa dunia kama makao yao milele, hii ikigeuzwa kuwa bustani iliyo kama shamba zuri lenye miti, maua, ndege na wanyama au paradiso. Wanadamu walipaswa kutawala samaki, ndege na wanyama wa nchi kavu, lakini wanadamu wenyewe walipaswa wawe chini ya utawala wa enzi kuu ya Mtawala na Muumba wa Ulimwengu Wote, Aliye Juu Zaidi, ‘ambaye jina lake peke yake ni YEHOVA.’ (Zaburi 83:18, AV) Kama Mwenye Enzi Kuu wa mwanadamu, Yehova Mungu alimweleza mwanadamu wa kwanza sheria ya kimungu, ambayo kwa kuitii mwanadamu angeweza kuishi duniani milele.

4 Sheria hii iliamuru utii mkamilifu kwa Mwenye Enzi Kuu wa Ulimwengu Wote, kwa maana Mungu alimwambia mtu yule, Adamu hivi: “Matunda ya kila mti wa bustani waweza kula, walakini matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya usile, kwa maana siku utakapokula matunda ya mti huo utakufa hakika.” (Mwa. 2:16, 17) Mtu huyo, Adamu, na mkewe, Hawa, waliishika amri hiyo ya kimungu ya utii wa uaminifu kwa muda. Jamaa ya kibinadamu ilikuwa na mwanzo mkamilifu. Kumtii Yehova Mungu, Mwenye Enzi Kuu wa Ulimwengu Wote, kulikuwa ndiyo njia ya uzima wa milele. Kanuni iliyowekwa wakati huo yatuhusu sisi leo. Je! tutaifuata?

5. Ukosefu wa umoja katika ulimwengu wa wanadamu leo unaonyesha ni nini kilichotukia, nacho kilitokea wakati gani na kwa kusababishwa na nani?

5 Itambidi kila mtu akubali kwamba jamaa ya kibinadamu si “ulimwengu mmoja” leo, si jamii ya kibinadamu isiyogawanyika, ijapokuwa mwili mmoja na damu moja. Ziko enzi nyingi za kibinadamu duniani sasa zenye kujitanguliza, nazo zinagawanya uaminifu wa wanadamu. Ni jambo lisilokanika kwamba zamani sana, kabla mwana hajazaliwa kwa Adamu na Hawa, kulikuwako mtengano kutoka kwa enzi kuu ya ulimwengu wote ya Mungu Muumba, Aliye Juu Zaidi. Ni nini kilichosababisha mtengano huu? Biblia Takatifu, Neno la Mungu lililoandikwa peke yake, ndilo laweza kutoa jibu la kweli. Sababu mbaya ilitokana na makao yasiyoonekana, ulimwengu wa roho. Huko mmojawapo wa raia za kiroho za enzi kuu ya Yehova aliona nafasi ya kusimamisha enzi yake mwenyewe ya kujitegemea.

6. Majina aliyopewa mwasi huyo wa kiroho yanapatana na mwendo gani aliofuata kufanya wanadamu waasi enzi kuu ya Mungu?

6 Shetani likawa jina lenye kumfaa mwasi huyu, maana jina hilo humaanisha “Mpinzani,” yaani, wa Yehova Mungu. Ibilisi likawa jina la kumfaa, kwa kuwa neno hilo humaanisha “Mchongezi,” na Shetani alitumia uchongezi juu ya Bwana wake Mwenye Enzi Kuu ili adanganye na kupoteza. Basi Ibilisi alimwonyesha Hawa kwamba Baba yake wa kimbinguni alikuwa mwongo-mchoyo asiyestahili kutiiwa sana. Kwa kusadiki uongo huu, Hawa akala kutokana na tunda lililokatazwa na kuvunja utii wake kwa enzi ya Baba yake wa kimbinguni. Kupatana na mpango wa Ibilisi, Hawa alifanya zaidi ya hilo: alimshinda mumewe Adamu akamfanya ajiunge naye katika kutokutii enzi halali ya Mungu na Baba yake. Imekuwa sawasawa na alivyokusudia Shetani Ibilisi: Mpaka leo hii ulimwengu wa wanadamu umezaliwa katika dhambi juu ya Mungu, katika hali ya kutokutii enzi kuu ya Yehova Mungu Aliye Juu Zaidi.​—Mwa. 3:1 mpaka 4:16; Rum. 5:12.

7, 8. (a) Tangu wakati huo wanadamu wamegawanywaje kuhusu kutii enzi? (b) Mungu alitumiaje enzi ya kigeni katika kushughulika na mwenye enzi mwasi huyo?

7 Tangu uasi huo katika Bustani ya Edeni, wazao wa Adamu na Hawa wamegawanyika kati ya kutii enzi kuu ya ulimwengu wote ya Yehova Mungu na kutii enzi ya Shetani Ibilisi, ambaye Yesu Masihi aliita “mkuu wa ulimwengu huu.” (Yohana 12:31; 14:30; 16:11) Yehova Mungu hakupatana hata kidogo na enzi ndogo hii iliyosimamishwa. Akitumia uwezo wake kama Mwenye Enzi Kuu wa Halali mwenye uwezo wa kushughulika na serikali za kigeni, Yehova Mungu alitangaza vita juu ya mwenye enzi adui. Akionyesha dharau kuu sana kwa mwenye enzi huyu wa Kishetani, Yehova Mungu alimfananisha na nyoka-mtambaa chini akamwambia hivi, kana kwamba akimwambia nyoka ambaye Ibilisi alikuwa ametumia kumdanganya Hawa:

8 “Nitaweka uadui kati yako na huyo mwanamke, na kati ya uzao wako na uzao wake; huo utakuponda kichwa [kama kukanyaga kichwa cha nyoka ili kuponda-ponda bongo zake], na wewe [kama nyoka mwenye kuotea] utamponda kisigino.”​—Mwa. 3:1-15.

9. Mungu alitangaza vita ya muda gani juu ya enzi wa kigeni, naye Paulo alionyeshaje hili katika Warumi 16:20?

9 Yehova Mungu alitangaza huko vita ya daima juu ya mwenye enzi mwasi na wale wote wanaoshikamana na enzi ya mwasi mjanja huyu, ambaye tangu mwanzo alijaribu kuficha viumbe vya kibinadamu wasijue alivyo. Yehova Mungu hakusahau ‘maongozi yake ya kushughulika na mambo ya kigeni’ ya vita juu ya adui yake Yeye na wanadamu. Zaidi ya miaka elfu nne baada ya Adui Mkuu kusimamisha enzi ya kigeni katika Edeni, Yehova Mungu alimwongoza Paulo mtume wa Kikristo kuandikia kundi lililokuwa katika makao makuu ya Milki ya Kirumi hivi: “Mungu wa amani atamseta Shetani chini ya miguu yenu upesi. Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo na iwe pamoja nanyi.”​—Rum. 16:20. Linganisha Kutoka 17:14; Isa. 45:7.

10. (a) Ni nani atakayetumiwa kumponda Nyoka Mkuu chini ya miguu, na hilo litatukia karibuni aje? (b) Uzao wa Mungu ulioahidiwa ulipondwaje “kisigino,” nao uliponywaje?

10 Wakati wa kumponda “upesi” Nyoka Mkubwa Shetani Ibilisi na “uzao” wake umekaribia sasa, baada ya kupita miaka zaidi ya mia kumi na tisa. Sasa Yesu Kristo mkuu wa “Uzao” ulioahidiwa wa mwanamke wa Mungu amepewa uwezo wa kutosha kumponda mwanzishi huyu wa Kishetani wa enzi zote za kidunia ambazo ni ngeni kwa Yehova Mungu, Mpaji wa amani peke yake. “Uzao” huu wa “mwanamke” wa Mungu ulipondwa kisigino katika karne ya kwanza ya Wakati wetu wa Kawaida. Hii ilitukia kwa sababu ya shauri baya lile kati ya “watu wa Israeli” na Mfalme Herode Antipa na Gavana wa Kirumi Pontio Pilato. Jeraha la “kisigino” lililotiwa na Nyoka Mkuu lilimwua Yesu Kristo katika Sikukuu ya Kupitwa ya mwaka wa 33 W.K., lakini ilikuwa mauti ya kimwili tu. Na, kwa vyo vyote, ilimpasa Yesu afe kifo cha dhabihu, kulingana na kusudi la Mungu. Lakini mwendo huo wa kufa kama dhabihu haukukosa thawabu. Katika siku ya tatu ya kufa kwa Yesu, Mungu Mwenye Nguvu Zote alimfufua kutoka kwa wafu kumpeleka kwenye uzima wa kiroho katika mbingu asiweze kufa. Mungu alimketisha kwenye mkono Wake mwenyewe wa kuume, angojee wakati wa kupondwa kichwa kwa Nyoka Mkubwa.​—Ebr. 10:12, 13; 12:2.

11. Alipokuwa mwanadamu Yesu alihubiri serikali gani hadharani, naye alifanya hivyo tangu wakati gani na kuendelea?

11 Wakati Yesu Masihi alipokuwa duniani bado akiwa mwanadamu mkamilifu, aliihubiri bila kukoma Serikali itakayowatawala wanadamu wote na kuwafanya walio watiifu kuwa “ulimwengu mmoja” chini ya enzi kuu ya Mungu. Alianzia mahali ambapo Yohana Mbatizaji, mtangulizi wake alikuwa ameachia, kwa maana habari yatuambia hivi: “Basi Yesu aliposikia ya kwamba Yohana amefungwa, alikwenda zake mpaka [jimbo la] Galilaya. . . . Tokea wakati huo Yesu alianza kuhubiri, na kusema, Tubuni; kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribia.”​—Mt. 4:12-17.

12. Yesu alihakikisha alistahili kuuhubiri ujumbe huo wa Ufalme kwa sababu ya uchaguzi gani alioufanya alipokuwa chini ya shawishi la Ibilisi?

12 Kama Yesu hangalifanya uamuzi miezi kadha iliyotangulia, asingalistahili kamwe kuanza kuhubiri ujumbe huo. Katika pindi hiyo yenye maana Yesu alikuwa nje katika jangwa la Uyahudi, alikokuwa amefunga kula akiwa katika upweke kwa siku 40. Ndipo mwenye enzi mwasi alipomkaribia amshawishi atoke katika mwendo wake wa Kimasihi. Kwa habari ya shawishi la tatu na la mwisho, habari yatuambia hivi: “Kisha Ibilisi akamchukua mpaka mlima mrefu mno, akamwonyesha milki zote za ulimwengu, na fahari yake, akamwambia, Haya yote nitakupa, ukianguka kunisujudia.” Ile ambayo Ibilisi alimtolea Yesu haikuwa “serikali moja” ambayo ingewafanya wanadamu watiifu wote kuwa “ulimwengu mmoja.” Haikuwa serikali ya ulimwengu chini ya enzi kuu ya Mungu, bali iliyo chini ya enzi ya Ibilisi. Habari inaendelea kutuambia mwenye enzi ambaye Yesu aliamua kufuata pasipo shaka, ikisema: “Ndipo Yesu akamwambia, Nenda zako, Shetani [Mpinzani]; kwa maana imeandikwa, Msujudie [Yehova] Mungu wako, umwabudu yeye peke yake.”​—Mathayo 4:1-10.

13, 14. Baada ya kulisha umati wa watu kwa mwujiza, kwa sababu gani Yesu hakuwaruhusu wamfanye mfalme, lakini kwa sababu gani alijitokeza kwa sherehe kutimiza Zekaria 9:9?

13 Katika kuamua kwa ajili ya enzi kuu ya Mungu wake, Yehova, Yesu alikuwa ndiye mfano mkamilifu kwa sisi sote leo. Lakini lazima tushikamane na uamuzi wetu kwa ajili ya enzi kuu ya Mungu, kama Yesu alivyofanya. Baadaye, akiisha kulisha kwa mwujiza makutano ya wanaume elfu tano na jamaa zao, wengi walitaka kumfanya mpaji huyu wa chakula cha mwujiza awe mfalme wao wa kidunia. Lakini Yesu alipinga jitihada zao kwa kuwaepuka. Alijua kwamba wakati ulikuwa haujaja ajitokeze kwa sherehe kwa Wayahudi kama mfalme wao wa Kimasihi, ili kutimiza unabii. (Yohana 6:1-15) Katika wakati wa Mungu, Jumapili, Nisani 9, 33 W.K., Yesu alipanda, kama ilivyotabiriwa na Zekaria 9:9, akaingia Yerusalemu na kwenda hekaluni ambako kuhani mkuu wa taifa alikuwa akifanya kazi. Yesu hakuzuia makutano makubwa waliokuwa wakimfuata waache kumpendekeza kwa sauti kuu kama mfalme kwa kupiga kelele hivi:

14 “Okoa, twakuomba! Mbarikiwa ni yeye ajaye katika jina la Yehova! Wenye kubarikiwa ni ufalme unaokuja wa baba yetu Daudi! Okoa, twakuomba, katika makao ya juu juu!”​—Marko 11:1-11, NW.; Diaglott.

15. Ni wakati gani “watu wa Israeli” walipotangaza hadharani uamuzi wao juu ya enzi, naye Pilato alifuatanaje na uamuzi wao?

15 Ndipo ukawa wakati kwa “watu wa Israeli,” kama walivyowakilishwa na viongozi wao wa kidini, waamue na kuonyesha enzi waliyoshikamana nayo. Siku tano baadaye walitangaza waziwazi kuonyesha mwenye enzi ambayo walichagua. Wakati waadhimishaji wa Sikukuu ya Kupitwa kwa kuongozwa na makuhani wao walipompigia kelele Gavana wa Kirumi Pontio Pilato aagize mfungwa Yesu auawe penye mti, Pilato aliwauliza walifikirie shauri hili tena kwa kusema: “Je! nimsulibishe mfalme wenu!” Ulizo la enzi kuu sasa liliwekwa sawasawa mbele ya “watu wa Israeli.” Wangechagua enzi ya nani? Habari ya Biblia yaonyesha, inaposema hivi: “Wakuu wa makuhani wakamjibu, Sisi hatuna mfalme ila Kaisari.” Pilato, mwakilishi wa Kaisari alifuata uamuzi wao, kwa maana habari yasema hivi: “Basi ndipo alipomtia mikononi mwao ili asulibiwe.”​—Yohana 19:12-16.

16. Karibuni Nyoka Mkuu atapondwa kupitia kwa nani. nayo Zaburi 2:8, 9 inaonyeshaje kupondwa kwa “uzao” wa Nyoka duniani?

16 Huo ulikuwa utimizo mdogo wa maneno ya unabii ya Mfalme Daudi katika Zaburi 2:1, 2. (Matendo 4:24-28) Uliweka mfano wa utimizo ulio mkubwa, unaotukia katika wakati wetu, wakati ambapo ulizo kubwa la utawala wa ulimwengu lapaswa lijibiwe mara moja tu. Shetani mwenye enzi mwasi amepata wakati wake katika kuponda kisigino cha “Uzao” ulioahidiwa wa “mwanamke” wa Mungu. Sasa Nyoka Mkubwa huyu, mponda kisigino, lazima apondwe kichwa chake mwenyewe, na wakati uo huo hili lahusu “uzao” wote wa Nyoka huyu. Zaburi ile ile ya Pili yaonyesha jinsi kupondwa kwa “uzao” unaoonekana wa Nyoka Mkubwa kungefanywa. Katika mistari ya nane na tisa, Yehova anamwambia Mtiwa Mafuta wake, Yesu Kristo hivi: “Uniombe, nami nitakupa mataifa kuwa urithi wako, na miisho ya dunia kuwa milki yako. Utawaponda kwa fimbo ya chuma, na kuwavunja kama chombo cha mfinyanzi.”

17. Kitabu cha Ufunuo kinaonyesha nini kuwa chombo cha Mungu cha kuponda mataifa yenye enzi duniani, naye Yesu Kristo anaonyeshwa akishiriki kufanya nini?

17 Kitabu cha mwisho cha Biblia Takatifu (Ufunuo 12:5) chasema juu ya ufalme wa Mungu wa Masihi wake kama chombo cha kimungu ‘kitakachochunga mataifa yote kwa fimbo ya chuma.’ Sura ya kumi na tisa, inayosimulia vita inayokuja ya kupigana na mataifa ya kidunia penye Har–​Magedoni, yasema juu ya Mwana wa Mungu, Yesu Kristo, kama yeye ‘atakayewachunga kwa fimbo ya chuma,’ na huongeza kwamba “anakanyaga shinikizo la mvinyo ya ghadhabu ya hasira ya Mungu Mwenyezi.” (Ufu. 19:15; 16:14, 16) Kupondwa huku kwa mataifa pamoja na madai yao ya enzi ya kitaifa kunaonyeshwa waziwazi sana kwetu katika unabii wa Danieli, sura ya pili.

18. Fasiri ya Danieli ya ndoto ya Nebukadreza inauonyeshaje mwisho mbaya sana wa taratibu ya mambo ambayo imetokeza mamlaka za ulimwengu, nasi twajuaje kwamba mwisho wa taratibu hii unakaribia?

18 Katika sura hiyo Danieli anafasiri ndoto ya unabii ambayo Mungu wa mbingu alimpelekea Nebukadreza, mfalme wa Mamlaka ya Ulimwengu ya Kibabeli, katika mwaka wa pili alipokwisha kuuharibu mji wa Yerusalemu na hekalu lililojengwa na Mfalme Sulemani, mwana wa Daudi. Mfuatano wa mamlaka za ulimwengu ulioanzia na mamlaka ya Kibabeli ukaendelea mpaka mamlaka ya Wamedi na Waajemi, ya Ugiriki, ya Kirumi na ya Waingereza na Waamerika, ulifananishwa na sanamu kubwa, yenye kung’aa mno, yenye madini mengi, yenye miguu ya chuma na udongo. Ndipo jiwe lililochongwa kutoka mlima wa mbali, bila msaada wa mikono ya mwanadamu, lilipoipiga sanamu miguu hiyo na hatima yake likaisaga tikitiki sanamu yote iliyoanguka ikawa unga, ambao upepo wenye nguvu ulipeperusha mbali. Kupondwa huko kwa sanamu ya mfano kuwa unga kulifananisha mwisho wa taratibu ya mambo wenye kuletwa na chombo kisicho cha kibinadamu ambacho hakikufanyizwa kwa mikono ya mwanadamu kwa uongozi wa akili za wanadamu. Utimizo wa unabii ambao Yesu Kristo alitoa juu ya “mwisho wa taratibu ya mambo” waonyesha kwamba kupondwa-pondwa kwa taratibu hiyo ku karibu!​—Mt. 24:3-22, NW.

19. Kulingana na Danieli 2:44, ni nini litakaloyapata mataifa yenye kujiunga na Umoja wa Mataifa, lakini namna gani juu ya enzi ya ufalme wa Mungu wa Kimasihi?

19 Leo, kwa kujipanga na tengenezo la Umoja wa Mataifa lisilo la Kikristo, watawala wa ulimwengu wanaonyesha upande waliko juu ya ulizo la enzi kuu. Hivyo maneno ya fasiri ya nabii ya Danieli yawahusu watawala hawa wa kisiasa, wa Kikomunisti na wasio wa Kikomunisti: “Katika siku za wafalme hao Mungu wa mbinguni si mikono ya kibinadamu atasimamisha ufalme ambao hautaharibiwa kamwe, wala enzi yake kuachiwa watu wengine. Utavunja vipande vipande falme zote hizi na kuzikomesha, nao utasimama milele.”​—Dan. 2:1-14, Revised Standard Version Bible.

20, 21. (a) Ni nani watakaoshiriki wa Masihi katika ufalme huo wa kimbinguni? (b) Danieli 7:26, 27 inaonyesha enzi juu ya dunia ikipewa kwa watu gani?

20 Huo ndio ufalme wa Kimasihi wa mbinguni ambao mashahidi wa Yehova wa Kikristo wamekuwa wakitangaza ulimwenguni pote tangu mwaka wa kusimamishwa kwake katika mbingu mwishoni mwa Majira ya Mataifa mwaka wa 1914. (Luka 21:24; Mt. 24:14) Wafuasi wa nyayo za Masihi, waliotiwa mafuta kwa roho ya Mungu kama yeye, watashiriki katika ufalme huo wa kimbinguni pamoja na Masihi. Hili lilitabiriwa katika njozi iliyotumwa kwa Danieli mwenyewe. Katika njozi hiyo ya unabii mfululizo wa mamlaka za Mataifa kutoka mamlaka ya Kibabeli na kuendelea ulifananishwa na wanyama-mwitu wanne. Kwa habari ya hukumu ya kimungu iliyotekelezwa na Mahakma Kuu ya ulimwengu wote juu ya mnyama huyo wa nne wa mfano, Danieli 7:26, 27 hueleza hivi:

21 “Kisha kutakuwako na hukumu, naye atanyang’anywa enzi yake, ili mwishowe ipate kuharibiwa na kukomeshwa kabisa. Mamlaka ya kifalme, enzi, na ukuu wa falme zote chini ya mbingu itapewa kwa watu wa watakatifu wa Aliye Juu Zaidi. Mamlaka yao ya kifalme ni mamlaka ya milele na enzi zote zitawatumikia na kuwatii.”​—NE; The Bible in Living English.

“ULIMWENGU MMOJA” CHINI YAKE

22. Ni nani atakayepewa enzi juu ya ulimwengu wa wanadamu ili kuwe na “serikali moja’’ juu yao?

22 Utimizo wa unabii huo u karibu sasa kutukia. Karibuni itakuwa lazima enzi zote za kitaifa za sasa ziiizo duniani ziutii ufalme wa Kimasihi mikononi mwa Mwana wa Mungu wa kimbinguni. (Dan. 7:1-12) Hilo litaacha nafasi ya kuwako “ulimwengu mmoja” tu wa wanadamu wote. Kama Danieli 7:14 anavyosema: “[Mwana wa Adamu wa Kimasihi] akapewa enzi, utukufu na ufalme, na watu wa jamaa zote, mataifa na lugha wakawa watumishi wake. Enzi yake ni enzi ya milele ambayo haitapita kamwe, wala milki yake haitaharibiwa milele.”​—The Jerusalem Bible.

23. (a) Kutimizwa kwa unabii huo kutamaanisha nini kwa kizazi hiki cha wanadamu? (b) Ni nafasi gani ina- yofaa inayotolewa kwetu?

23 Utimizo wa unabii huo utamaanisha nini kwa kizazi hiki cha wanadamu? Hili: Enzi za kitaifa za sasa na wazalendo wazo wataharibiwa katika taabu ya ulimwengu iliyo kubwa kuliko zote inayokaribia haraka, lakini wategemezaji wa enzi kuu ya ulimwengu wote ya Yehova watahifadhiwa kwa mwujiza na kuiokoka “dhiki kubwa” hiyo. (Mt. 24:21, 22; Marko 13:19, 20; Ufu. 7:14, 15) Je! sisi tutakuwa miongoni mwa waokokaji hao wa “mwisho wa taratibu ya mambo” wenye pendeleo? Nafasi ya kuwa miongoni mwao inatolewa kwetu na Neno la Mungu lililoandikwa. Linalotakiwa sasa tufanye ni kujipanga imara upande wa enzi kuu ya Mungu na upande wa ufalme wake wa Kimasihi na kushikamana nazo bila kujali jitihada zote za wakati ujao za kisiasa, za kidini na za kijamii za kutaka kutuondoa.

24. Sasa mateso yanayotupata kwa sababu ya kushika- mana na enzi kuu ya Yehova yataendelea mpaka lini?

24 Huenda hii ikatuletea mateso fulani maadamu watesi wetu wanaruhusiwa kuendelea kuwako. Katika mateso hayo twaweza kukumbuka kilio cha mashahidi wa zamani wa Bwana Mungu Yehova walioteswa, hata kufa: “Yapaswa iwe mpaka lini, Bwana mwenye enzi kuu, mtakatifu na wa kweli, kabla hujatutetea na kulipiza kisasi cha damu yetu juu ya wakazi wa dunia?” Walihakikishiwa kwamba ingekuwa “kitambo kidogo” tu kabla ya hili kutukia.​—Ufu. 6:10, 11, NE; Moffatt; RS; NW.

25. Ni wakati gani na kwa njia gani Shetani, Nyoka Mkuu, atapondwa chini ya miguu ya wanafunzi wa ? Kristo “upesi”?

25 Kitakuwa kitambo kidogo tu kabla wategemezaji waaminifu wa enzi kuu ya ulimwengu wote ya Yehova hawajatetewa katika hali yao kwa ushindi wenye kukata maneno juu ya enzi zote za kitaifa zinazowakilishwa ndani na nje ya Umoja wa Mataifa. Upesi baada ya hapo yule mwasi wa kwanza wa enzi kuu ya ulimwengu wote ya Yehova, yaani, Shetani Ibilisi, na malaika zake wa kishetani, wataadhibiwa. Watatengwa wakiwa wamefungwa minyororo katika shimo lisilo na mwisho wasipate uhusiano wo wote na dunia hii. (Ufu. 20:1-3) Kwa njia hiyo yule Nyoka Mkubwa atakuwa kana kwamba amepondwa kichwa; naye Mungu atamponda hivyo Nyoka Mkubwa na uzao wake wa kishetani chini ya miguu ya warithi waaminifu wa Kristo kupitia kwa “Uzao” mwaminifu ule wa “mwanamke” Wake.​—Rum. 16:20.

26. Ni kwa njia gani “taratibu mpya” ya Mungu itaanza ikiwa na “ulimwengu mmoja” chini ya “serikali moja”?

26 Waokokaji wa kibinadamu wa matukio haya yenye maana sana watakuwa ni wote wale wanaoshikamana na ufalme mmoja wa Kimasihi wa Mwana wa Yehova mshindi Yesu Kristo. Kwa hiyo, mwanzoni mwenyewe mwa taratibu mpya ya mambo yenye haki ya Mungu, utakuwako “ulimwengu mmoja” duniani, chini ya “serikali moja,” bila kujali makabila, jamaa, mataifa na lugha ambazo zamani zilikuwa za waokokaji wa “dhiki kubwa.” Wote watakuwa jamii moja ya kibinadamu katika dunia safi, wote wakimwabudu Mungu mmoja aliye hai na wa kweli, Yehova, na wote wakimtii Mwana wake, Yesu Kristo, ambaye utawala wa kifalme utawekwa begani mwake. Lo! hiyo itakuwa nguvu yenye kuunganisha iliyoje!

27. Hali hiyo itakuwa nguvu ya kuleta hali gani kati ya wanadamu, chini ya enzi moja gani?

27 Pia, itakuwa nguvu ya amani ulimwenguni pote kama nini! Hakuna vita vya kidini tena! Hakuna kugombana tena juu ya mipaka ya nchi! Hakuna vita vya kati ya makabila na vya mataifa yote tena! Hakuna tena mashindano ya kisiasa! Unabii wa Biblia wasema hivi: “Ni lazima Yehova awe mfalme juu ya dunia yote. Siku hiyo Yehova atakuwa mmoja, na jina lake moja.” (Zek. 14:9, NW) Wakati uo huo “serikali moja” itakayosimamiwa naye, ufalme wa Kimasihi wa Mwana wake aliyetawazwa Yesu Kristo, itakuwa wonyesho wa enzi kuu Yake ya ulimwengu wote.​—Isa. 9:6, 7.

28. Wakati huo wanadamu wote watashirikiana kufanya kazi gani njema, kwa utimizo wa ahadi gani aliyotoa Yesu kwa mtenda mabaya mwenye kufa?

28 Wanadamu wote walio hai watamtumikia Bwana Mungu, Yehova Mwenye Enzi Kuu “kwa nia moja.” (Sef. 3:8, 9) Kama “ulimwengu mmoja” jamii mpya ya kibinadamu itashirikiana pamoja katika kazi nzuri. Watashirikiana katika kuugeuza uso ulioharibiwa wa dunia hii kuwa katika hali ambayo awali Muumba wake aliikusudia, ile ya bustani ya Edeni, paradiso ya furaha. (Mwa. 1:27, 28; 2:7-15) Ndipo litakapojibiwa ombi lile la mtenda mabaya mwenye huruma aliyekufa kando ya Yesu Kristo katika mti wa mateso: “Yesu, unikumbuke mimi utakapoingia katika ufalme wako.” Naam, ndipo Mfalme anayetawala atakapomtimizia ahadi hii: “Kweli mimi nakuambia leo, Utakuwa pamoja na mimi katika Paradiso.”​—Luka 23:42, 43, NW; Rotherham.

29. ta) Ni kwa njia gani wanadamu wanaweza kuwa watoto wa milele wa Kristo? (b) Yeye atawawekeaje mfano wa kutii enzi kuu ya Mungu kwa uongozi wake?

29 Si mhalifu huyo peke yake mwenye huruma, bali wote wengine pia kati ya wanadamu waliokufa wanatiwa ndani, wote ambao Yesu Kristo alifia kama dhabihu kamilifu ya kibinadamu. Atawaita hawa pia wafufuke kutoka kwa wafu. (Mt. 20:28; Yohana 5:28, 29; 1 Tim. 2:5, 6; Matendo 24:15) Watiifu wote wataunganishwa katika “ulimwengu mmoja” huo. Wote watakuwa ndugu na dada, kwa maana watakuwa watoto waliokombolewa, waliokuzwa wa Baba wa Milele mmoja, Yesu Kristo, aliyetoa uhai wake wa kibinadamu kwa ajili yao. (Isa. 9:6, 7; Ebr. 2:9). Kwa kumtii yeye wanaweza kuwa watoto wake wa milele. Yeye mwenyewe atawaongoza katika njia ya kuitii enzi kuu ya ulimwengu wote ya Baba yake mwenyewe wa kimbinguni, Yehova Mungu. Baada ya kutimizwa kwa kazi yake ya kukamilisha wanadamu watiifu katika paradiso ya kidunia, yeye ataonyesha utii wake mwenyewe kwa enzi kuu ya Mungu wake kwa kumkabidhi ufalme. Kwa sababu gani? “Ili kwamba Mungu awe yote katika wote.”​—1 Kor. 15:24-28.

30. Wale ambao wamekatishwa tamaa na mgawanyiko wenye msiba unaoletwa na enzi za kitaifa wanaombwa wafanye nini?

30 Kwa kuwa ndivyo yalivyo mambo yote haya ya ajabu, jipeni moyo, enyi nyote ambao mnepingwa na kukatishwa tamaa na mgawanyiko wa ulimwengu wenye msiba, na enzi za kitaifa zenye kupingana zisizotegemea enzi kuu ya kimungu! Sasa lishikeni sana tumaini tukufu lile la “ulimwengu mmoja, serikali moja, chini ya enzi kuu ya Mungu”! Mwishi kwa ajili yalo kuanzia sasa mpaka litakapotimizwa kwa baraka.

—Kutoka The Watchtower, Oct. 15, 1975.

[Picha katika ukurasa wa 187]

UFALME WA MUNGU UTAKUWA NDIO SERIKALI MOJA YA WANADAMU WOTE

UFALME WA MUNGU UTAHARIBU ENZI ZOTE ZA KITAIFA

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki