Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w76 1/15 kur. 46-48
  • Yehova Ni Kimbilio la Mamilioni

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Yehova Ni Kimbilio la Mamilioni
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • MIFANO YA BIBLIA
  • VITA YA MWISHO
  • UHAKIKA NA USALAMA
  • MIPANGO KWA WAOKOKAJI
  • “Vita ya Siku Ile Kuu ya Mungu Mwenyezi” Inayokaribia Sana
    Usalama Ulimwenguni Pote Chini ya “Mwana-Mfalme wa Amani”
  • Kitabu Cha Biblia Namba 38—Zekaria
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
  • Kaa Katika Bonde La Yehova La Ulinzi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Kimbilio Letu Chini ya “Ufalme wa Mbinguni” Usioharibika
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
w76 1/15 kur. 46-48

Yehova Ni Kimbilio la Mamilioni

Makala hii ni ya kutumia kwa mafunzo ya kitabu ya kundi

1, 2, (a) Wanadamu wanakabiliwa na hali gani ya vita? (b) Watu wengine wanaonaje wanaposikia Mungu atayaharibu mataifa, lakini kwa sababu gani uharibifu huo unafaa?

KATIKA kizazi hiki cha ufundi wa kisayansi mataifa yametumia silaha za kutisha kati ya wao kwa wao​—hewa yenye sumu, makombora yanayotengenezwa kwa petroli na kutoa moto pamoja na yale ya atomiki yanayoweza kufutilia mbali maelfu ya maisha za kibinadamu. Hiyo imefanya kuwe na woga mwingi kwamba silaha mbaya zaidi sana zinaweza kutumiwa wakati ujao​—hewa zenye kuharibu neva na nguvu za kupumua, vyombo vya kisayansi, makombora ya haidrojeni na pengine hata vyombo vyenye kuogofya zaidi. Wataalamu wa kijeshi wanasema kwamba kukiwa na vita yenye silaha hizo kusingekuwa na washindi wo wote​—wote wangeshindwa.

2 Lakini watu wengine wanaoshauri silaha zenye kuharibu zaidi ziwekwe akibani wanaona kwamba Mungu ni mkatili anaposema ataharibu mataifa. Uhakika ni kwamba, kila taifa linaendelea kujikaza lipate silaha nyingi zaidi kuliko lile jingine. Njia ya pekee ya kumaliza jambo hili ni kuiondoa taratibu ya kibinadamu iliyopo, mahali pake pachukuliwe na utawala wa Mungu mwenyewe, si na namna nyingine ya utawala wa mwanadamu.

3. Biblia inaonyeshaje kwamba lazima mataifa yaharibiwe?

3 Bei ya kuleta amani duniani bila shaka ni kuwaondolea mbali wanadamu waovu wenye kujitafutia yao wenyewe, wenye kutaka kujipatia faida wenyewe au utukufu badala ya kutaka kuona watu wakiwa na furaha. Biblia inasema hivi: “Mwovu ni ukombozi wa wenye haki; naye anayefanya hila ni pahali pa wenye haki.”​—Mit. 21:18, Swahili Congo Bible.

MIFANO YA BIBLIA

4. Kwa sababu gani Mungu alichukua hatua kuharibu ulimwengu wakati wa Gharika?

4 Tuna mifano katika Biblia inayoonyesha Mungu anachukua hatua kuwaondolea mbali waovu ili afaidi wenye haki. Kwa mfano kulikuwa na gharika ya siku za Nuhu. Maandishi yanasema, “Dunia ikayala na yeuri. . . . na tazama, imeharibika; kwa sababu wenye mwili wote wameyiharibia njia duniani.” (Mwa. 6:11, 12, Swahili Congo Bible) Walakini Nuhu ‘alitembea pamoja na Mungu’ ‘akapata neema machoni mwa Yehova.’ Ulimwengu wa wakati huo ulipoharibiwa, Nuhu na jamaa yake waliokolewa na mkono wa Yehova.​—Mwa. 6:8, 9; 8:18.

5. Ni kwa sababu gani Mungu aliharibu Sodoma na Gomora?

5 Baadaye, miji ya Sodoma na Gomora ikawa yenye ufisadi wa kupindukia. Upotovu wao ulikuwa wa kumakisha na wenye kuharibu amani ya wengine, hata watu wote wakafikia hatua ya kulalamika. Yehova “akasema: kwa sababu kilio cha Sodomo na Gomora ni kikubwa, na kwa sababu zambi zao ni nzito sana.” (Mwa. 18:20, Swahili Congo Bible) Miji hiyo iliharibiwa ili kuondolea maeneo hayo uovu wa kupindukia, ili wenye kutaka adili waweze kupata usalama na amani.​—Mwa. 19:1, 12, 13, 24, 25.

6. Kuharibiwa kwa mataifa kunamaanisha kwamba hakuna watakaookoka?

6 Kwa hiyo hatua ya Yehova ya kuharibu inafaa. Nayo haiepukiki, kwa sababu mataifa kwa ujumla yana maelekeo ya kusonga mbele katika njia yao yenye uharibifu, kama vile walivyokuwa watu kabla ya Gharika. Lakini, watu mmoja mmoja wanaweza kuepuka uharibifu. Kungali na wakati kwa ye yote anayetaka kujifunza habari za Mungu apate upendeleo wake na kumkimbilia ajikinge na uharibifu.

VITA YA MWISHO

7. Zekaria sura ya kumi na nne inahusu sehemu gani ya vita ya Mungu yenye uharibifu?

7 Ni kwa kadiri gani watu wanaosimama upande wa Yehova na ulimwengu mmoja, serikali moja, chini ya enzi kuu Yake wanavyoweza kuwa na uhakika wa kulindwa? Kitabu cha Biblia cha Zekaria, katika sura yake ya kumi na nne, kinatuambia kwa unabii juu ya usalama watakaopata wale watakaokuwa upande wa Yehova wakati wa mwisho kamili wa taratibu hii ya mambo. Unabii huo unahusu matukio yatakayotukia baada ya dini yote ya uongo kuharibiwa na mamlaka za kisiasa. (Uharibifu wa dini ya uongo, inayofananishwa na “kahaba,” unaonyeshwa katika Ufunuo 17:16.) Wakati huo ndipo wafalme (watawala) wa dunia na majeshi yao watakapopigana na “Mwana-Kondoo,” Yesu Kristo, nao watashindwa.

8, 9. Ni wakati gani unabii wa Zekaria katika sura ya kumi na nne, mstari wa kumi na mbili utakapotimia, nao “Yerusalema” utashambuliwaje?

8 Zekaria aliandika hivi: “Hii ni tauni [Yehova] atakayopiga nayo mataifa yote waliopiga vita yulu ya Yerusalema; nyama ya mwili wao itaharibika wangali wanasimama yulu ya migulu yao, na macho yao yataharibika ndani ya vitundu vyao; na ulimi wao utaharibika kinywani mwao.”​—Zek. 14:12, Swahili Congo Bible.

9 Hakuna kumbukumbu linaloonyesha matukio yanayosimuliwa katika sehemu hii ya unabii wa Zekaria yalitimizwa ndani ya Yerusalemu au karibu yake nyakati zilizopita. Kwa hiyo unabii huo utatimizwa baadaye, si juu ya mji halisi wa Yerusalemu. Mji huo si “mji mtakatifu” wa Mungu tena. “Yerusalemu wa mbinguni” ndipo panapokusanyikiwa na Wakristo nao wanapaona kuwa patakatifu. (Ebr. 12:22) Bila shaka, mataifa hayawezi kufika mbinguni na kuushambulia mji huo, lakini wanaweza kushambulia wale wanaouwakilisha walio duniani. Unabii wa Zekaria unasema watafanya hivyo. Watakapokuwa wakishambulia wajumbe wake watakuwa wakiushambulia mji wa kimbinguni.

UHAKIKA NA USALAMA

10, 11. (a) Je! watu wa Mungu waliogope shambulio kali la adui? (b) Toa mfano wa ulinzi wa Mungu wa nyakati za kale.

10 Je! wale wanaotumainia kuwa washiriki wa mji huo wa kimbinguni mwishowe, wakiwa ndugu za kiroho za “Mwana-Kondoo,” Kristo Yesu, waogope? Je! wenzao waliojiunga nao kuzitangaza habari njema za ufalme wa Mungu wateteme kwa woga wanapotazamia shambulio kali litakalokuja? Sivyo. Wao wamemfanya Yehova kimbilio lao, naye hatakosa kuwaangalia. Kumbuka vile majeshi makuu yalivyoushambulia ufalme wa Yuda siku za Mfalme Yehoshafati. Mungu alimwambia Yehoshafati hivi: “Msiogope, wala msifadhaike kwa ajili ya jeshi kubwa hili; kwani vita si yenu bali ni ya Mungu. . . . Hamtahitaji kupigana vita.” (2 Nya. 20:15-17) Kwa hiyo Mungu akaleta mvurugo kati ya majeshi ya adui hata wakaanza kuchinjana. Mfalme Yehoshafati na watu wake walikuta adui wote wamekufa.​—2 Nya. 20:22-24.

11 Baadaye, jeshi lenye kushinda la mfalme wa Ashuru Senakeribu, lililokuwa likikumba kila kitu kilichokuwa mbele yao, liliishambulia nchi ya Yuda. Mmoja wa majemadari, Rabshake, alimtisha na kumfanyia mzaha Mfalme Hezekia wa Yerusalemu na Mungu wake Yehova, akiwa mbele ya kuta za Yerusalemu. Lakini Yehova alimfariji Hezekia, akisema hivi: “[Mfalme wa Ashuru] hatauingia mji huu, wala hatapiga mshale hapa, wala hatakuja mbele yake kwa ngao, wala hatajenga boma juu yake.” (2 Fal. 19:32) Usiku huo Yehova alituma malaika akaharibu mashujaa na wakuu wa Senakeribu 185,000. Mabaki ya jeshi hilo lililoshindwa yalirudi Ashuru bila hata kugusa wakaaji wa Yerusalemu.​—2 Fal. 19:35; 2 Nya. 32:21.

12, 13. Unabii wa Zekaria unaonyeshaje kwamba adui hawataweza kudhuru wale ambao wamemfanya Yehova kimbilio lao?

12 Ndivyo litakavyokuwa shambulio la mataifa juu ya watu wa Mungu katika hali ya ulimwengu inayoitwa “Har–​Magedoni.” (Ufu. 16:16) Kwa habari ya maneno ya Zekaria yaliyokwisha tajwa, kama “tauni” itakuwa halisi au sivyo, vinywa vya walio tayari kupaza sauti wakitoa amri, mayowe ya vita au matisho vitafumbwa. Ndimi zao ama zitaoza kwa halisi, au watashindwa kusema lo lote kana kwamba hawana ndimi. Kwa ghafula nguvu za kuona zitatiwa giza! Minofu na mishipa ya nguvu ya mashujaa wastadi, wenye miili iliyopirikana itanyong’onyea isiweze kufanya lo lote wasimamapo juu ya miguu yao. Mabohari yao ya silaha, kutia na vyombo vyao vya kuongozea silaha za kutupa, yataharibika. Unabii unasema hivi ukitumia kwa njia ya mfano vitu vya kijeshi vilivyotumiwa siku hizo:

13 “Hivi vilevile litakuwa pigo la farasi, na la nyumbu, na la ngamia, na la punda, na la nyama zote watakaokuwa katika kambi zile zote, kama pigo hili.”​—Zek. 14:15, Swahili Congo Bible.

14, 15. Zaidi ya tauni itakayopiga washambuliaji, ni njia gani nyingine atakayotumia Yehova kuwashinda?

14 Bila shaka hiyo itaogofya wale watakaopigana na Mungu wakati huo. Mvurugo ambao Mungu Mwenye Nguvu zote atachochea kati ya washambuliaji hao utaongezea hofu. Watapigana kiwazimu wao kwa wao, kama wale adui wa kale wa Yehoshafati. Unabii wa Zekaria unasema hivi: “Na itakuwa siku ile makelele [“mvurugo,” NW] makubwa toka [Yehova] yatakuwa katikati yao; nao watakamata kila mutu mukono wa jirani yake, na mukono wake utanyanyuliwa yulu ya mukono wa jirani yake.”​—Zek. 14:13, Swahili Congo Bible.

15 Uharibifu huo mkubwa wa adui wote wa Mungu utatukia katika kila sehemu ya dunia. Njozi inayolingana na hiyo katika kitabu cha Ufunuo inaonyesha “mnyama,” ambaye anafananisha serikali za dunia, akipigana na Yesu Kristo, “MFALME WA WAFALME NA BWANA WA MABWANA.” Majeshi yao yote yanaonyeshwa yakijiunga vitani na kuangamia kwa kushindwa kwa njia yenye aibu.​—Ufu. 19:16, 19-21.

MIPANGO KWA WAOKOKAJI

16, 17. Kuharibiwa kwa adui za Mungu duniani kutaacha hali ya mvurugo, na je! waokokaji watakuwa maskini?

16 Je! uharibifu huo utaacha mvurugo mtupu duniani? Je! wale watakaokuwa wamekimbilia kwa Mungu watakuwa wametawanyika-tawanyika ivi hivi tu, wasijue la kufanya? Je! watakuwa maskini?

17 Sivyo, kwa maana unabii unasema hivi juu ya hilo: “Na utajiri wa mataifa yote wanaozunguka utakutanishwa, zahabu na feza, na mavazi, mingi sana.” (Zek. 14:14, Swahili Congo Bible) Bila shaka kutakuwa na vya kutosha kuruzuku wote ambao watakuwa wamemtegemea Yehova awalinde, mpaka watakapoweza kuweka utaratibu wa mambo na kufanya kazi duniani kulingana na mapenzi ya Mungu yatakayofunuliwa wakati huo. Watapata habari zake kupitia kwa “Yerusalemu mpya.”​—Ufu. 21:1-4.

18. Vitu ambavyo Israeli walipata walipoingia Nchi ya Ahadi vinaonyeshaje mpango wa Mungu kwa wanaomtumaini?

18 Akiisha kukomboa watu wake wenye kumtumaini kwa kufagilia mbali majeshi yaliyoungana ya dunia, mkono wa Yehova hautafupika usiweze kuwaruzuku watu wake. Tunaweza kuwa na uhakika huo! Mfano wa mpango huo unapatikana katika maneno ambayo Yehova aliwaambia Israeli muda mfupi kabla hawajaiingia Nchi ya Ahadi. Mungu alisema kupitia kwa Musa kwamba Yeye angewatangulia awasaidie kushinda mataifa ya huko na kwamba, wakiisha kuimiliki nchi hiyo, wangepokea “miji mikubwa mizuri [wasiyoijenga wao], na nyumba zimejaa vitu vyema vyote [wasizojaza wao], na visima vimefukuliwa [wasivyofukua wao], mashamba ya mizabibu na mizeituni [wasiyopanda wao].” Walivipokea vitu hivyo ‘wakala na kushiba.’​—Kum. 6:10, 11.

19. Waokokaji watafurahia jambo gani hasa, na nini kinachoonyesha pengine mamilioni wataokoka?

19 Kwa hiyo waokokaji wa vita ya Mungu hawatakuwa na wasiwasi wa kupata vifaa vya kimwili. Lakini, watalihesabu kuwa jambo la maana zaidi kuweza kuendesha ibada ya kweli bila kusumbuliwa. Pengine mamilioni ya watu yatapata kukombolewa na Yehova, kwa maana tayari wako zaidi ya watu milioni mbili sasa ambao wamemfanya Yehova na ufalme wake wa Kimasihi kimbilio lao. Hao wanazitangaza habari njema za ufalme huo katika karibu sehemu zote za dunia, na mamia ya maelfu ya watu wanaweka tumaini lao katika ufalme huo na kujiunga katika utangazaji wake kila mwaka. Kweli Yehova anakuwa kimbilio la mamilioni!

​—Kutoka Kitabu Paradise Restored to Mankind​—by Theocracy!

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki