Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w76 4/15 kur. 189-191
  • “Ukomeshe Hasira”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Ukomeshe Hasira”
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • NAMNA HASIRA INAVYOWEZA KUZUIWA
  • Biblia Inasema Nini Kuhusu Hasira?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Hasira
    Ufahamu wa Kina wa Maandiko
  • Je! Ni Vibaya Nyakati Zote Kuwa na Hasira?
    Amkeni!—1994
  • Hasira—Ni Nini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
w76 4/15 kur. 189-191

“Ukomeshe Hasira”

SI VYEPESI kuzuia hasira mtu anapotendewa udhalimu au wakati wasiotii sheria wanapofanikiwa. Lakini chini ya hali zizi hizi Biblia inasihi hivi: “Ukomeshe hasira, uache ghadhabu, usikasirike, mwisho wake ni kutenda mabaya.”​—Zab. 37:8.

Kuna hekima ya ‘kukomesha hasira.’ Hasira inaweza kudhuru sana. Mtu anapoachilia hasira, mkazo wa mishipa ya damu unaongezeka na damu inapiga kasi zaidi na mtu anapumua haraka zaidi. Hasira inapokwisha, kwa ujumla kila kitu kinarudia hali yake ya kawaida. Lakini kwa wazi kuhamaki-hamaki kwa hasira kunadhuru mwili. Kwa upande mwingine, huenda mtu akawa na hasira lakini aifungie ndani yake mwenyewe. Kwa nje huenda akaonekana mtulivu sana, lakini kwa ndani huenda akawa na udhia. Ikiwa hivyo, huenda akaanza kuona maumivu mwilini na bado akatae kwamba masumbufu ya moyoni siyo yanayomletea taabu. Hivyo hasira inaweza kuleta magonjwa mengi, kutia na matata ya moyo na mishipa ya damu, maumivu ya kupumua, magonjwa ya ngozi, masumbufu ya meno na ya kuyeyusha chakula, na kuumwa na kichwa.

Zaidi ya kuleta magumu mwilini, hasira inaweza kudhuru sana kiroho kwa kufanya mtu avunje sheria ya Mungu. Ikikaza fikira kwenye hatari hii, Biblia inasema hivi: “Yeye aonaye hasira upesi atatenda kwa ujinga.” (Mit. 14:17) “Asiyetawala roho yake ni mfano wa mji uliobomolewa, usio na kuta.” (Mit. 25:28) Nyakati za kale mji wenye ukuta wenye matundu haukuwa na ulinzi, bali ulikuwa wazi kuingiliwa na majeshi ya maadui. Vivyo hivyo, mtu mwenye hasira hasira anajifanya aingiliwe na mawazo yasiyofaa, yakimwongoza kufanya matendo ya kipumbavu.

Kadiri ambavyo inaweza kuwa hatari inaonyeshwa katika kisa cha Kaini. Alipoona upendeleo wa Mungu umeonyeshwa juu ya ndugu yake Habili, lakini si juu yake mwenyewe, Kaini alikasirika sana. Ingawa alipewa onyo la kimungu, Kaini alishindwa na kuwaza kubaya akamwua ndugu yake.​—Mwa. 4:4-8.

NAMNA HASIRA INAVYOWEZA KUZUIWA

Bila shaka hakuna mmoja wetu angetaka kuwa kama Kaini, ama katika nia ama katika tendo. Kwa hiyo imetupasa tujitahidi kuzuia hasira. Hiyo haimaanishi kuzuia mawazo ya moyoni kwa nje tu. Uzuiaji wa hasira unaanza mtu anapoweza kutenda kwa akili​—bila kuudhika kwa nje au kwa ndani​—anapokabiliwa na hali zisizofaa.

Chukua kisa cha mtu anayesahihishwa kwa sababu ya kuwa mwenye hatia ya kutojali jambo fulani au kwa sababu ya kosa. Akiacha kiburi kiingie, huenda akakasirika sana kwa sababu ya kusahihishwa. Ndivyo ilivyokuwa kwa Mfalme wa Kiyahudi Asa. Aliposahihishwa na nabii Hanani kwa sababu ya kuonyesha ukosefu wa imani, Asa alikasirika sana. Akamtia Hanani “nyumbani mwa mkatale” na kuanza pia kuonea wengine wa raia zake. (2 Nya. 16:7-10) Badala ya kuacha akasirike, ingalimpasa Asa kuwa na maoni ya akili ya hali hiyo. Ingalimpasa kukumbuka kwamba Hanani hakuwa akisema yake, bali alikuwa akisema kama mjumbe wa Yehova. Huo ulikuwa wakati wa Asa wa kukubali kosa lake na kuonyesha toba ya unyofu. Unyenyekevu ungaliweza kumsaidia Asa azuie hasira. Kwa hiyo ikiwa sisi tutatii shauri la Biblia ‘kukomesha hasira,’ sisi pia tumepaswa kusitawisha unyenyekevu.

Nyakati nyingine watu wanatutendea na kutuambia mambo yasiyotakiwa kabisa. Huenda yakatuudhi sana. Tunaweza kufanya nini? Imetupasa tufikirie makusudi ya wale wanaotuudhi.

Je! wanajaribu kutukasirisha kwa makusudi? Ikiwa ndivyo, tungekuwa tukiwapa nafasi ya kutufanyia watakavyo tukijiacha tuhamaki kwa hasira. Ingekuwa afadhali zaidi kupuza maneno yenye kuumiza au matendo yanayokusudiwa kutuchochea tukasirike. Ndipo shauri la Yesu Kristo lingetumika: “Mtu akupigaye [kofi la] shavu la kuume, mgeuzie na la pili.” (Mt. 5:39) Kofi halikusudiwi kuumiza kimwili bali kuchochea vita. Kwa hiyo, kwa kulipiza kisasi, mtu angekuwa akiharibu mambo tu.

Lakini namna gani ikiwa mambo yanayotuudhi hayakusemwa au kufanywa kwa kusudi la kutukasirisha? Ikiwa hivyo, tunaweza kufikiri wenyewe. Je! pengine tunataka kutokeza matata makubwa juu ya mambo madogo? Je! haliwezi kuwa jambo la upendo zaidi kulifunika kosa dogo?

Kwa upande mwingine, huenda tukawa na sababu halisi ya kukasirika. Lakini je! upendo haupaswi kutuongoza tutake kumsaidia mtu anayehusika aache kuudhi watu wakati ujao? Wakristo wanashauriwa hivi: “Mwe na hasira, ila msitende dhambi; jua lisichwe na uchungu wenu bado haujawatoka; wala msimpe Ibilisi nafasi.” (Efe. 4:26, 27) Ikiwa kusudi letu kubwa ni kumsaidia mtu aliyetukosea ashinde udhaifu wake, hatutamwonea uchungu moyoni na kupita kiasi cha kukasirika. Hatutamwachia Ibilisi mwanya atumie hali yetu ya kukasirika kwa faida yake na kutuchochea tulipize kisasi.

Bila shaka, yako mambo tusiyoweza kuzuia. Katika taratibu hii isiyo kamilifu, udhalimu mwingi unatendeka. Kuudhika sana kwa sababu ya mambo hayo, pengine kufikia hatua ya kuharibu afya yetu, kusingefaidi ye yote. Badala yake, tunaweza kufarijiwa na uhakikisho wenye msingi wa Biblia unaoonyesha kwamba Yehova atakomesha udhalimu na uonezi wote kupitia kwa ufalme wake. (Dan. 2:44) Kwa sasa tunaweza kumtegemea atusaidie tuvumilie jaribu lo lote linaloweza kutupata.​—Yak. 1:2-5.

Zaidi ya kuwa na maoni ya kiasi juu ya mambo yanayoweza kupandisha hasira, tukiepuka ushirika wa wale walio wepesi wa kukasirika tutasaidiwa kuendeleza kujiweza. Biblia inatuonya hivi kwa upole: “Usifanye urafiki na mtu mwenye hasira nyingi; wala usiende na mtu wa ghadhabu nyingi; usije ukajifunza njia zake; na kujipatia nafsi yako mtego.”​—Mit. 22:24, 25.

Kwa upande mwingine, kushirikiana na watu wasiokasirika upesi bila shaka kutatufaa. Watu kama hao hawachochei hasira za wengine kwa kusema maneno yenye kukasirisha. Upole wao una uwezo mwingi sana wa kukomesha ugomvi mkali na upinzani mwingi. Wao wako kama inavyosema Biblia: “Jawabu la upole hugeuza hasira.” (Mit. 15:1) “Asiye mwepesi wa hasira hutuliza mashindano.” (Mit. 15:18) “Ulimi laini huvunja mfupa.”​—Mit. 25:15.

Kwa kweli ziko sababu nzuri za ‘kukomesha hasira.’ Tunafaidika kimwili na kiroho pia. Kwa hiyo, na tujitahidi kuepuka kukasirisha wengine, nasi wenyewe tuangalie mashirika yetu, tusitawishe unyenyekevu na kuendelea kuwa na maoni ya akili na kiasi juu ya yale yanayoweza kufanywa au kusemwa na wanadamu wenzetu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki