Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w77 1/1 kur. 23-24
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
  • Habari Zinazolingana
  • Sababu Hatukuambiwa “Siku Ile na Saa Ile”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • “Tuambie, Mambo Haya Yatakuwa Wakati Gani?”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • “Tuambie, Mambo Haya Yatakuwa Wakati Gani?”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • “Ni Nini Itakayokuwa Ishara ya Kuwapo Kwako?”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
w77 1/1 kur. 23-24

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

● Je! Yesu Kristo anajua wakati “dhiki kubwa” itakapoanza?

Huenda akawa anajua, lakini hatuwezi kusema hakika kwamba anajua.

Yesu alitabiri “dhiki kubwa” itakayofutilia mbali uovu tunaouona kutuzunguka. Kwa habari ya wakati wa uharibifu huu, Yesu alisema hivi: “Habari ya siku ile na saa ile hakuna aijuaye, hata malaika walio mbinguni, wala Mwana, ila Baba peke yake.”​—⁠Mt. 24:3, 21, 3642.

Kwa hiyo, wakati Yesu Kristo alipokuwa duniani kama mfalme aliyekusudiwa na Mungu, hakuijua tarehe iliyowekwa ya kuanza kwa “dhiki kubwa.” Alikufa akafufuliwa kupewa uzima wa kimbinguni katika mkono wa kuume wa Mungu, akingojea kupewa mamlaka kamili ya kutawala na ‘kuponda’ mataifa vipande vipande. (Zab. 110:1; 2:6-9) Utimizo wa unabii wa Biblia waonyesha kwamba alipokea mamlaka hiyo mwaka wa 1914 W.K.; “kuwapo” kwake kulianza wakati huo. Hivyo, kizazi chetu ndicho kitakachopatwa na “dhiki kubwa” hiyo. (Mt. 24:34; Ufu. 11:15-18) Yesu ajua hilo pia, kama vile anavyojua tuko mbali kadiri gani katika historia ya mwanadamu tangu kuumbwa kwa Adamu na Hawa.

Sasa Yesu anafanya nini? Ufunuo 6:1-8 waonyesha kwamba mwaka wa 1914 W.K. alitoka “ali akishinda tena apate kushinda [“amalize ushindi wake,” NW].” Vita vya mwanadamu, upungufu wa chakula na magonjwa ya kipuku yanahakikisha kwamba huu ndio wakati anapoelekea kumaliza ushindi wake.

Yesu ataongoza majeshi ya kimbinguni katika “dhiki kubwa.” Sasa tumekwisha ingia ndani kabisa katika kipindi kinachojulikana kama wakati wa mwisho, kwa hiyo pengine Mungu amekwisha julisha Yesu maarifa yote ya kutumiwa katika pigano na mpango wa majeshi yake. Lakini ikiwa Yesu hajajua bado “siku ile na saa ile” ya ‘kumaliza ushindi wake,’ karibuni ataijua.

● Ikiwa lazima Mkristo atoe ushuhuda kortini (barazani), je! ni sawa kwake kushika Biblia na kuapa kwa kusema kweli yote?

Hakuna katazo la Maandiko kufanya hivyo, ingawa lazima kila mtu aamue kama atafanya hivyo au ataomba aruhusiwe asifanye hivyo.

Mazoea ya kuapa huku mtu akishika kitu fulani kinachoonekana kuwa kitakatifu yameenea pote. Kwa mfano, Wagiriki wa kale waliinua mkono kuelekea mbinguni au waligusa madhabahu walipokuwa wakiapa. Kati ya Warumi mwanabaraza (juror) alikuwa akishika jiwe mkononi na kuapa kwamba ikiwa alikuwa anasema uongo Jupiter amtupilie mbali huku akilitupilia mbali jiwe lenyewe.

Matendo hayo yalionyesha wazi maelekeo ya ndani ya wanadamu ya kutambua kwamba kuna mamlaka ya kimungu ambayo wanadamu wana wajibu kwayo na inayoona yanayosemwa na kufanywa. Bila shaka waabudu wa Mungu wa kweli, Yehova, walitambua hivyo. Na Biblia yaonyesha kwamba walikula viapo, mbele ya Mungu, twaweza kusema, au yeye akiwa shahidi. (2 Sam. 3:35; 1 Fal. 2:23, 24; Ruthu 3:13; Yer. 38:16) Waabudu wa kweli waliruhusu wengine pia wawaapize.​—⁠Mwa. 21:22-24; Mt. 26:63.

Nyakati nyingine kiapo kilipoliwa mbele ya Yehova, mwenye kuapa alitoa ishara pia. Malaika aliyekuwa akisema na nabii Danieli ‘aliinua mkono wake wa kuume na mkono wake wa kushoto kuelekea mbinguni; akaapa kwa yeye aliye hai milele na milele.’ (Dan. 12:7; Mwa. 14:22) Hata Mungu alijinena mwenyewe kwa njia ya mfano kama akiinua mkono aape. (Isa. 62:8; Kum. 32:40) Ishara nyingine ambayo kwa wazi ilitumiwa kuhakikisha kiapo ilikuwa ya kuweka mkono chini ya kiuno cha yule mwingine au chini ya paja lake.​—⁠Mwa. 24:2, 3, 9; 47:29-31.

Bila shaka, si lazima Mkristo wa kweli ale kiapo ndiyo ahakikishe kila usemi anaofanya katika maisha ya kila siku. Ndiyo yake yapaswa kumaanisha Ndiyo, na Sivyo yake, Sivyo. (Mt. 5:33-37; Yak. 5:12) Lakini kortini akiagizwa aape kuonyesha ushuhuda wake ni wa kweli, aweza kujisikia ataapa. Au huenda akaruhusiwa kufanya tangazo la uzito kwamba hasemi uongo.​—⁠Gal. 1:20.

Ikiwa mpango wa korti ni ule wa kuinua mkono au kuweka mkono juu ya Biblia mtu anapoapa, Mkristo aweza kufanya hivyo, akikumbuka mifano ya Biblia ya kuapa na kutoa ishara wakati ule ule. Lakini jambo la maana zaidi kuliko kama mtu anatoa ishara fulani pamoja na kiapo chake ni kwamba yeye anaapa mbele za Mungu aseme kweli. Kiapo kama hicho ni jambo zito. Kwa hiyo Mkristo akijisikia aweza na apaswa kujibu ulizo aliloulizwa katika hali hizo, basi yuko chini ya kiapo aseme kweli.

● “Siku za mwisho” ambazo Paulo alieleza katika 2 Timotheo 3:1-7 zilikuwa na utimizo wa kwanza juu ya taratibu ya mambo ya Kiyahudi katika karne ya kwanza?

“Siku za mwisho” zinazotajwa na Paulo katika 2 Timotheo 3:1-7 zinamaanisha wakati ambao ungefuata baada ya uasi wa imani kuendelea kwa muda mrefu ukiendeshwa na “mtu wa kuasi” anayetajwa katika 2 Wathesalonike 2:3-12. Mambo yote yaliyotajwa katika 2 Timotheo 3:1-7 ni ‘matunda’ ya uasi wa imani yanayoonekana sana wakati wetu. Hiyo haielekezi kwenye karne ya kwanza, kwa maana“mtu wa kuasi” hakuwa ameonekana wazi wakati huo. Kwa hiyo hizi “siku za mwisho” zinatofautiana na “wakati wa mwisho” unaotajwa katika 1 Yohana 2:18. unaomaanisha kipindi cha mwisho ambacho mitume walizuia uasi. “Azuiaye” aliondolewa Yohana alipokufa, naye ndiye aliyekuwa mtume wa mwisho. ​—2 The. 2:7.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki