Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w79 6/1 kur. 3-4
  • Je! Inawezekana Kuishi Bila Kupungukiwa Vitu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Inawezekana Kuishi Bila Kupungukiwa Vitu?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Habari Zinazolingana
  • Fuata Kielelezo Cha Yesu Kwa Kuwahangaikia Maskini
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • Mwisho wa Umaskini Wakaribia
    Amkeni!—1998
  • Kuna Tumaini Gani kwa Maskini?
    Amkeni!—2007
  • Ni Nani Anayeweza Kuwakomboa Wale Wanaolilia Msaada?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
w79 6/1 kur. 3-4

Je! Inawezekana Kuishi Bila Kupungukiwa Vitu?

DUNIA ina uwezo wa kutoa chakula kifaacho, pamoja na hali ya maisha yenye kufaa na yenye furaha kwa kila mwanamume, mwanamke na mtoto aliye hai leo. Hata hivyo, watu milioni nyingi hawajapata kuwa na chakula cha kutosha na nyumba nzuri ya kuishi. Wengi wanaishi katika vibanda ambavyo hutoa ulinzi mdogo tu kutokana na baridi na mvua. Huenda jamaa nzima zikawa zikiishi katika chumba kidogo katika nyumba ya kupangisha yenye vyumba vingi isiyotunzwa vizuri. Je! kuna tumaini lo lote kwamba hali kama hizo zitabadilika?

Yehova Mungu, Muumba wa wanadamu, anakusudia kukomesha taratibu zote mbovu zilizoko duniani, na mahali pake kusimamisha taratibu mpya yenye haki. “Ziko mbingu mpya na dunia mpya ambazo sisi tunangojea kulingana na ahadi yake, na katika hizi haki itakaa.” (2 Pet. 3:13, NW) Ahadi hii ni uthibitisho wa kwamba kutakuwako ulimwengu ambao katika huo itawezekana kuishi bila kupungukiwa vitu. Hata kama ni watu wachache tu ambao wangeendelea kutaabishwa na hali ya kupungukiwa vitu, “mbingu” hizo mpya za kiserikali pamoja na hiyo “dunia mpya” ambayo washiriki wake ndio raia washikamanifu ingeharibiwa na udhalimu. Lakini haitakuwa hivyo. Hizo “mbingu mpya” na “dunia mpya” zitakuwa zenye haki kabisa.

Kwa sababu ya maoni ya Mungu juu ya maskini na wenye taabu, tunaweza kutazamia mbele katika wakati ujao tukiwa na hakika ya kuuona ulimwengu ambao katika huo hakutakuwa kupungukiwa vitu.Maandiko yanamwita Yehova “baba wa yatima na mwamuzi wa wajane.” (Zab. 68:5) Nayo sheria yake aliyoitoa kwa Israeli inathibitisha hilo. Sheria hiyo iliwalinda maskini nayo ilikusudiwa imlinde kila Mwisraeli asipatwe na umaskini mbaya sana.

Isipokuwa Walawi peke yao ambao walipokea sehemu ya kumi ya mazao ya nchi kwa ajili ya utumishi wao hekaluni, jamaa zote za Waisraeli walipewa urithi wa sehemu ya nchi, na kwa hiyo, walikuwa na njia ya kujipatia riziki. Hata kama mwanamume alipatwa na msiba au labda akatumia vibaya mali yake na kuingiza jamaa yake katika umaskini, urithi wa shamba lake haungepotezwa milele. Sheria hiyo ilisema kwamba shamba peke yake (pamoja na mazao yake) ingeweza kuuzwa, na hiyo ingefanywa kwa muda uliobaki tu mpaka mwaka wa Yubile. Mwaka wa Yubile ulifika baada ya kila miaka 50 na katika huo mashamba yote yalirudishiwa wenyewe au warithi wake. (Law. 25:​13, 23-27) Katika muda wa miaka ambayo Waisraeli maskini walikuwa hawana urithi wa shamba, haikuwa lazima waomba-ombe mahitaji ya lazima ya maisha au wajivunjie heshima katika njia nyingine yo yote ili wajipatie walichohitaji. Waliruhusiwa na sheria waokote mavuno yaliyosalia katika mashamba ya nafaka na matunda na mizabibu yaliyokwisha vunwa.​—Law. 19:9, 10; 23:22; Kum. 24:19-21.

Kusudi la Mungu la kuwawezesha maskini kuishi bila kupungukiwa na vitu linafunuliwa katika yale yaliyotabiriwa kwa habari ya utawala wa Mfalme Sulemani. Katika Zaburi 72:​12-14 tunasoma hivi: “Atamwokoa mhitaji aliapo, na mtu aliyeonewa iwapo hana msaidizi. Atamhurumia aliye dhaifu na maskini, na nafsi za wahitaji ataziokoa. Atawakomboa nafsi zao na kuonewa na udhalimu.”

Maoni hayo ya upendo juu ya wenye kuonewa yataonyeshwa na utawala wa mbingu mpya za kiserikali juu ya wanadamu. Twajuaje hivyo? Kwa kuwa mtawala aliye mkuu wa taratibu hiyo mpya ndiye yule aliye mkuu kuliko Sulemani, yaani, Yesu Kristo, ‘Mfalme wa wafalme, na Bwana wa mabwana.’​—Ufu. 19:16; Luka 11:31.

Lakini huenda mmoja akauliza, ‘Sababu gani, baada ya karne nyingi hivyo kupita, hatumwoni Yesu Kristo akiwakomboa maskini?’ Biblia inafunua kwamba hili litatukia katika wakati uliowekwa na Yehova Mungu. Hata Yesu Kristo alipokuwa duniani hakujua barabara wakati wa kuharibiwa kwa taratibu iliyopo ya mambo na mahali pake kuchukuliwa na taratibu mpya yenye haki. (Marko 13:32) Hata hivyo yeye alionyesha kwamba kukombolewa kutokana na taabu zilizopo kungefanyika wakati wa kizazi fulani​—kizazi ambacho kwanza kingepata kuona vita vikuu, matetemeko ya nchi, njaa pamoja na woga mwingi juu ya matukio ya ulimwengu. (Luka 21:10, 11, 25, 26, 31, 32) Je! hayo siyo mambo ambayo tumeona katika karne hii? Hivyo, basi, tunaweza kuwa na hakika kwamba taratibu mpya yenye haki i karibu sana.

Uhakika wa kwamba Yehova Mungu hajachukua hatua juu ya taratibu ya mambo isiyomwogopa umekuwa kwa faida ya wanadamu. Akivuta fikira juu ya hili, mtume Petro aliandika hivi: “[Yehova] hakawii kutimiza ahadi yake, kama wengine wanavyokudhani kukawia, bali huvumilia kwenu, maana hapendi mtu ye yote apotee, bali wote wafikie toba.”​—2 Pet. 3:9.

Uvumilivu wa Mungu umewawezesha watu kuonyesha kama wanataka kuishi katika taratibu mpya yenye haki ambayo katika hiyo magumu yanayoletwa na kupungukiwa na vita yatakuwa mambo ya zamani. Bila kujali hali yao ya uchumi ilivyo, wanaweza kuonyesha msimamo wao juu ya jambo hili. Ikiwa kweli wanataka kuishi katika taratibu mpya yenye haki, wanahitaji kujifunza yale ambayo Mungu anatazamia kutoka kwa wale anaokubali, watubu juu ya makosa waliofanya zamani juu ya matakwa yake na kupatanisha njia zao na mapenzi yake wakiwa wanafunzi washikamanifu wa Yesu Kristo.

Lakini namna gani juu ya mamilioni wengi waliokufa? Wajapokuwa huenda walipata kudhulumiwa na kuonewa, hawakupata dhara lenye kuendelea milele. Sababu gani sivyo? Kwa sababu Yehova Mungu atahakikisha kwamba wafu wamerudishiwa uhai na kutolewa taraja la uzima wa milele. (Matendo 24:15) Kwa habari ya hao waliofufuliwa, miaka michache ya taabu ni kitu gani ikilinganishwa na uzima wa milele bila maumivu? Kwa kweli itakuwa si kitu. Wataona kama alivyoona mtume Mkristo Paulo: “Dhiki yetu [ni] iliyo ya muda wa kitambo tu.”​—2 Kor. 4:17.

Kwa kweli itawezekana kuishi bila kupungukiwa vitu katika taratibu mpya ya Mungu. Je! wewe umekwisha chukua hatua ya kuonyesha kuwa watamani kuona uwezekano huo? Je! sasa wewe unajifunza Biblia na kujaribu kuitumia katika maisha yako ya kila siku? Ikiwa ndivyo, unaweza kuwa mmoja wa wale watakaouona wakati unaokaribia ambao katika huo watu wote watafurahia kuishi bila kupungukiwa na vitu.

[Blabu katika ukurasa wa 4]

“Atamwokoa mhitaji aliapo, na mtu aliyeonewa iwapo hana msaidizi. Atamhurumia aliye dhaifu na maskini, na nafsi za wahitaji ataziokoa.”​—Zab. 72:12, 13.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki