“Kuwa Unapopaswa Kuwa”
ALASIRI ya Julai 15, 1976, Mashahidi wa Yehova walikuwa wamehudhuria kipindi cha pekee cha vijana katika “Utumishi Mtakatifu” Kusanyiko la Wilaya katika Oakland, California. Wakati huo huo kukawa na kisa cha ajabu sana kisichopata kuonekana na watu miaka mingi, cha kutorosha wanafunzi 26 pamoja na dereva wao, waliokuwa katika basi wakielekea kusikiliza hotuba za shule wakati wa likizo.
Wawili kati ya watoto wenye kuhudhuria kusanyiko lile wangalikuwa katika basi hiyo kama wasingaliomba ruhusa ya kutokuwa shuleni wakahudhurie kusanyiko. Baba ya wavulana hao alisema: “Nashukuru sana tulikuwa kusanyikoni. Kuwa unapopaswa kuwa kunafaa.”