Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w78 1/15 kur. 20-21
  • Mwenye Hekima Alikuwa na Maana Gani?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mwenye Hekima Alikuwa na Maana Gani?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Uwe na Kiasi Katika Kazi
  • Ukatili Ambao Mwanadamu Anatenda Mwanadamu Mwenzake
  • Mwenye Hekima Alikuwa na Maana Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Ni Nini Kinachofanya Maisha Yawe Yenye Kusudi?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Mwenye Hekima Alikuwa na Maana Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
  • Hekima ya Kutuongoza Maishani
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2022
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
w78 1/15 kur. 20-21

Mwenye Hekima Alikuwa na Maana Gani?

Uwe na Kiasi Katika Kazi

Mtu anastahili sifa anapokuwa na nia ya kufanya kazi kwa bidii na ujuzi. Lakini furaha haitokani na kufanya kazi kwa bidii na ujuzi tu. Mfalme Sulemani mwenye hekima aliandika hivi: “Tena nikafikiri amali zote, na kila kazi ya ustadi, ya kwamba inatoka katika mtu kupingana na mwenzake. Hayo nayo ni ubatili na kujilisha upepo.”​—⁠Mhu. 4:4.

Huenda mtu akafanya kazi kwa bidii na ujuzi, lakini huenda kusudi lake likawa si kufanya jambo lenye manufaa, bali kushinda watu wengine. Wakati watu wanaofanya kazi pamoja wanapoongozwa na tamaa ya kujionyesha kuwa bora kuliko wafanya kazi wenzao, kunatokea mashindano na ugomvi badala ya kushirikiana kwa urafiki. Huenda chuki na wivu ukatokea. Huenda maamuzi yasiyofaa yakafanywa, bila kufikiria hata kidogo kwamba wengine wanapungukiwa na uwezo wa mambo fulani. Kwa hiyo, kufanya kazi ili kushinda wengine ni “kujilisha upepo,” ni kazi bure. Matokeo ya kufanya hivyo ni mabaya sana. Mwenye hekima ataepuka kufanya hivyo.

Lakini, uvivu mwingi sana unapaswa uepukwe pia. Sulemani alisema, “Mpumbavu huikunja mikono yake, naye hula chakula chake mwenyewe [au, “anakula mwili wake mwenyewe,” NW].” (Mhu. 4:5) Badala ya kutumia mikono yake afanye kazi yenye mazao, mvivu anakunja mikono na kufanya kazi ndogo sana kama awezavyo. Yeye ni mpumbavu kwa sababu uvivu wake unamletea shida. Anapokosa chakula kinachofaa na vitu vingine vya lazima kwa sababu ya ulegevu wake, anaelekea kuwa na afya mbaya na huenda akafa mapema isivyo kawaida. Anapojiumiza kwa njia hiyo, “anakula mwili wake mwenyewe.”

Kwa kuwa kazi ya kushindana na wengine ni mbaya, na uvivu ni mbaya pia, ni kiasi gani cha kazi kinachofaa? Sulemani alisema hivi: “Heri konzi moja pamoja na utulivu, kuliko konzi mbili pamoja na taabu; na kujilisha upepo.”​—⁠Mhu. 4:6.

Jambo la hekima ni kuepuka kufanya kazi nyingi mno kiasi cha kukosa wakati wa kufurahia matunda ya jasho lako. Basi inampasa mtu atosheke na vitu alivyo navyo. Mtu asiyetosheka hapumziki. Maisha yake yanakuwa ya kusumbukia mali zake na jinsi anavyoweza kupata zaidi.

Ni afadhali zaidi mtu anayetosheka kuwa na mali chache. Yeye haogopi kuzitumia afurahie chakula na vinywaji na tafrija zinazofaa. Anafikiria wengine pia na kusaidia wenye shida kwa furaha. Jambo hilo linapatana na shauri la Maandiko linalosema: “Afanye juhudi, akitenda kazi iliyo nzuri kwa mikono yake mwenyewe, apate kuwa na kitu cha kumgawia mhitaji.” (Efe. 4:28) Je! wewe u kati ya wale wanaofurahia “konzi moja pamoja na utulivu” kwa sababu ya kuwa na maoni ya kiasi juu ya kazi?

Ukatili Ambao Mwanadamu Anatenda Mwanadamu Mwenzake

Jamaa ya kibinadamu imeonewa na kutendwa udhalimu muda mrefu. Mfalme Sulemani aliandika yafuatayo kulingana na mambo aliyoona karibu miaka 3,000 iliyopita: “Kisha nikarudi na kuona madhalimu yote yanayotendeka chini ya jua; na tazama, machozi yao waliodhulumiwa, ambao walikuwa hawana mfariji; na upande wa wale waliowadhulumu kulikuwa na uwezo, walakini wale walikuwa hawana mfariji. Kwa hiyo nikawasifu wafu waliokwisha kufa kuliko wenye uhai walio hai bado; naam, zaidi ya hao wote nikamwita heri yeye asiyekuwako bado, ambaye hakuyaona mabaya yanayotendeka chini ya jua.”​—⁠Mhu. 4:1-3.

Inaonekana kwamba, kwanza Sulemani alikuwa ameona kidogo tu ukatili ambao mwanadamu anatenda mwanadamu mwenzake. Lakini, ‘aliporudi,’ yaani, aliporudia kuliangalia jambo hilo, alishtuka kuona jinsi udhalimu huo ulivyokuwa mwingi. Kwa sababu wenye kutenda udhalimu ndio waliokuwa na uwezo au mamlaka, wenye kudhulumiwa (kuonewa) walilazimika kuvumilia huzuni yao wasiwe na mtu wa kuwafariji. Hali hiyo iliwataabisha sana hata Sulemani akakata maneno kwamba wafu ni afadhali, kwa sababu wao walikuwa wamekwisha kufa wasiweze kuumizwa na udhalimu. Katika maana hiyo, yeye asiyezaliwa bado yu afadhali kwa sababu haoni wala hapatwi na mabaya hayo.

Jambo hilo linaonyesha sana kwamba mwanadamu hawezi kumaliza udhalimu wala uonezi! Hata Mfalme Sulemani asingeweza kuondoa huzuni nyingi inayoletwa na kutokamilika kwa wanadamu, ingawa alikuwa na hekima na mamlaka nyingi. Yehova Mungu peke yake ndiye anayeweza kufanya hivyo kwa kumtumia Yesu Kristo. Ni habari njema kweli kweli, kwa sababu ameahidi kukomboa wanadamu na taabu katika wakati unaowafaa sana wote wanaohusika.​—⁠Ufu. 21:3, 4.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki