Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w79 3/1 kur. 15-16
  • Je! Wewe Unaenenda kama Kwamba Uko Mbele za Mungu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Wewe Unaenenda kama Kwamba Uko Mbele za Mungu?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Habari Zinazolingana
  • Unaweza Kutembea Pamoja na Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Tembea Kwa Imani, Si Kwa Kuona!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
  • Enenda kwa Imani!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Ufalme wa Mungu Utakuja Wakati Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
w79 3/1 kur. 15-16

Je! Wewe Unaenenda kama Kwamba Uko Mbele za Mungu?

KWA sababu ya udhaifu wa mwili uliorithiwa, kunakuwa na lazima ya kuwaangalia wafanya kazi wengi ama sivyo wanaweza kuiba au kupitisha wakati bila kufanya kazi yao. Kwa mfano, ndio sababu kila afisi kubwa ya posta huko United States ina wakaguzi wanaokaa katika chumba kilicho juu ya makarani wanaofanya kazi ya kupokea na kupeleka barua katika afisi za posta. Kazi yao ni kumwona mfanya kazi ye yote anayeweza kuvutwa na kitu chenye thamani katika barua hizo na kukiiba. Wakaguzi hao wanafanya kazi nyuma ya vioo vinavyoweza kuona kutoka upande mmoja tu; nao wanaweza kuwaona makarani walakini makarani hawawezi kuwaona.

Si kwamba wafanya kazi wa posta peke yao ndio wanaohitaji kuangaliwa. Udanganyifu kati ya wafanya kazi umeenea sana ulimwenguni pote, nao unaleta hasara inayofikia maelfu ya mamilioni ya fedha. Tarakimu za hesabu zaonyesha kwamba udanganyifu mwingi wa fedha, unafanywa na walio na vyeo vikubwa.

Kwa wazi, hakuna ye yote wa watu hawa angalikuwa akifanya makosa hayo kama wangalikuwa wakienenda kama kwamba wako mbele za Mungu. Kuenenda kama kwamba uko mbele za Mungu kunamaanisha, kwanza kabisa, kuamini kwamba Mungu yuko. Ushuhuda unaopatikana kupitia kwa milango yetu ya maarifa kila mahali kutuzunguka unashuhudia kwamba, Yehova Mungu yuko. Kurasa za Neno Lake, Biblia zaonyesha hivyo pia. Walakini, kuamini tu kwamba Mungu yuko hakutoshi, kama vile Neno lake linavyotukumbusha: “Wewe waamini ya kuwa Mungu ni mmoja; watenda vema. Mashetani nao waamini na kutetemeka.” (Yak. 2:19) Lazima tuchukue hatua zaidi. Lazima tuamini haki ya hukumu ya Mungu, hekima pamoja na uweza wake; lazima tufahamu kwamba Yeye anajua na anajali juu ya yale yanayoendelea duniani kati ya wafu.

Ndiyo, Mungu anaona yote; nguvu zake za kuona ni kuu zaidi ya zile za mkaguzi wa posta Naye hahitaji vioo vinavyoona kutoka upande mmoja tu ili wanadamu wasimwone. Jambo la maana hapa si kwamba yeye mwenyewe hujionea kila kitu au anafanya hivyo kupitia kwa tengenezo lake lililo kubwa mno la kimalaika. Kwa vyo vyote matokeo ni yale yale: “Macho ya [Yehova] yako kila mahali; yakimchunguza mbaya na mwema.” Twaweza kuwa na hakika ya kwamba “hakuna kiumbe kisichokuwa wazi mbele zake, lakini vitu vyote viko utupu na kufunuliwa wazi machoni pake yeye tutakayemjibu.” Angalia kwamba, tutamjibu Mungu.​—⁠Mit. 15:3; Ebr. 4:​13, NW.

Kweli hii ya kwamba tutamjibu Mungu yapasa kutufanya tuchukue kwa uzito huku kuenenda kama kwamba fuko mbele zake. Yamaanisha tuenenda, yaani, tujiendeshe, tukijua kwamba wakati wote yeye anaangalia tunalofanya. Musa nabii wa Yehova aliyekuwa kiongozi wa kale wa Israeli, alikubali kabisa kweli hiyo, kwa kuwa kwa habari yake tunasoma kwamba “alistahimili kama amwonaye yeye asiyeonekana.” Yeye aliamini kabisa kwamba Mungu yuko nasi pia twapaswa kuamini vivyo hivyo.​—⁠Ebr. 11:27.

Tukienenda kama kwamba tuko mbele za Mungu tutalindwa tusikosane naye, kwa kuwa inamaanisha kwamba sisi tutaogopa kumkasirisha, tukijua kwamba hakuna kuepa hukumu zake. Tutalindwa tusifuate mwendo wa aliye mwovu ambaye juu yake imeandikwa kwamba “hakuna hofu ya Mungu mbele ya macho yake.” (Zab. 36:1) Uhakika wa kwamba kumwogopa Mungu kutatulinda tusishindwe na majaribu na hivyo kuingia katika taabu unaonyeshwa na namna kijana mwanamume Yusufu, mwana mpendwa wa mzee wa ukoo Yakobo, alivyojibu, alipoombwa-ombwa na mke wa bwana wake Mmisri Potifa alale naye, alijibu hivi: “Nifanyeje ubaya huu mkubwa nikamkose Mungu?” (Mwa. 39:9) Yeye alienenda kama kwamba alikuwa mbele za Mungu, kama kwamba Mungu alikuwa akimtazama wakati wote, kama kwamba yeye alikuwa akimwona Mungu wakati wote. Kufanya hivyo kulikuwa ulinzi kwake.

Hata mashambulio ya adui yetu Shetani Ibilisi yawe ni kwa njia ya kufanya uasherati na namna nyingine za kichoyo, au mikazo ya kutuachisha ushikamanifu wetu kwa Yehova Mungu, jambo peke yake linaloweza kutulinda ni kuenenda kama kwamba tuko mbele za Mungu. Hiyo inamaanisha kwamba lazima sisi tuamini kweli kweli kwamba Mungu yuko. Kama msaada wa kufanya hivyo, lazima tufikiri juu ya Mungu. Njia moja ya kutuwezesha kufanya hivyo ni kusali kwa Mungu kwa ukawaida. Tukizoea sala tutamwita Mungu atusaidie mara tu tunapopatwa na majaribu au mikazo. Kusali kwa Mungu huongezea imani yetu nguvu, kwa kuwa sala ni wonyesho wa imani, naye Mungu hujibu sala anazotolewa kwa njia ifaayo na juu ya mambo yafaayo. (1 Yohana 5:​14, 15) Walakini, baada ya kusali lazima tutimize fungu letu; lazima tujikaze tutende yale tuombayo, kwa moyo wote.​—⁠Flp. 4:​6, 7.

Njia moja ambayo katika hiyo twaweza kufanya hivyo ni kuongeza maarifa yetu juu ya Yehova Mungu kwa kujifunza Neno lake na vifaa vya Biblia ambavyo Mungu ametupa. Tunaweza kufaidika na mikutano ya kundi ya kila juma. Kadiri tuzidivyo kumjua Mungu ndivyo tutakavyozidi kumpenda na ndivyo atakavyozidi kuwa mawazoni mwetu na kuwa wa kwanza katika maono yetu ya moyoni. Kwa kweli, yote haya yanachukua wakati, kwa sababu hiyo Paulo anatushauri kwa upole hivi: “Basi angalieni sana jinsi mnavyoenenda; si kama watu wasio na hekima, bali kama watu wenye hekima; mkiukomboa wakati maana [siku] hizi ni za uovu.” Ni kweli kwamba, tunahitaji kiasi fulani cha wakati ili kupata vitu kwa haki machoni pa watu wote, wakati fulani wa kula na kulala, lakini zaidi ya hayo, je! tunaharibu wakati mwingi kwa tafrija zizidizo, kutafuta anasa au mapendezi yetu wenyewe?​—⁠Efe. 5:​15, 16.

Mojawapo sababu zinazofanya uasi uongezeke katika siku hizi za mwisho zenye hatari ni kwamba kuliko wakati mwingine wo wote, watu hawajui kwamba Mungu anaona wote na kwamba wote watamjibu yeye. Ikiwa sisi tu wenye hekima hatutadharau kweli hizi ila nyakati zote tutaenenda kama kwamba tuko mbele za Mungu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki