Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w78 8/1 kur. 20-21
  • ‘Usimnunie Yehova’

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • ‘Usimnunie Yehova’
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • KATI YA WALE WANAOJIDAI WANAMTUMIKIA MUNGU
  • Yehova Si wa Kulaumiwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Usiwe Kamwe Na “Ghadhabu Juu Ya Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Je! Mungu Anajali?
    Je! Mungu Anajali?
  • Mungu Anakujali Kwelikweli
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2004
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
w78 8/1 kur. 20-21

‘Usimnunie Yehova’

Mambo yakienda kombo kwa sababu ya mtu kukosa hekima, au kwa sababu ya kosa la mwingine, anaelekea kumlaumu Mungu.

WANADAMU wana tabia ya kulaumu mtu mwingine ikiwa mambo hayakutendeka vizuri. Na mara nyingi Mungu ndiye anayelaumiwa. Kukiwako upungufu wa chakula mahali fulani, watu wanalaumu Mungu wakisema ni yeye anayeacha wafe njaa. Au, ikiwako taabu kwa sababu ya kukosa kuajiriwa kazi ya kimwili, wengine wanauliza hivi, ‘Ni kwa sababu gani Mungu anatutesa hivi?’ Lakini je! kweli Mungu ndiye mwenye lawama?

Kwa kweli, Mungu hawatesi watu namna hiyo, yeye hana upendeleo, “maana yeye huwaangazia jua lake waovu na wema.” (Mt. 5:45) Mabaya yote yanayopata watu leo yanatokea kwa sababu sisi sote ni watu wenye makosa, tunaishi katika mpango wa wanadamu ulio na makosa unaoongozwa zaidi na kanuni za uchoyo. Tena, huenda mtu akapata taabu kwa sababu yeye mwenyewe anachukua hatua ya upumbavu.

Mara nyingi, wanadamu hawakubali makosa yao, wala hata kukubali kwamba taratibu nzima ya mambo iliyofanywa na wanadamu imepotoka, nayo ndiyo yenye kuleta misiba ya ulimwengu, (2 Kor. 4:4; Efe. 2:2, 3) Imetukia kama Andiko linavyosema: “Upumbavu wa mtu hupotosha njia yake; na moyo wake hununa juu ya [Yehova].” (Mit. 19:3) Au, kama mtu mwingine anavyotafsiri: “Ujinga wa mwanadamu unachafua mambo yake, naye anamrukia Yehova.”​—⁠Biblia tafsiri ya Byington.

Ni hatari kufuata mwendo huo. Baba yetu wa kwanza Adamu alitutolea mfano wa kutuonya. Hapo mwanzo yeye alifurahia ufanisi mkubwa na amani, mwili mzuri na makao yaliyo kama bustani katika mahali penye kupendeza sana. (Mwa. 2:7-9) Alipenda alichopewa na Mungu lakini alikosa kuthamini na kumsifu Mpaji wake kwa vitu alivyokuwa amepewa kwa wingi. Mambo yalipokwenda kombo akawa tayari kumlaumu Mungu. Alimwambia Mungu hivi katika kujitetea kwa kutokutii kwake: “Huyo mwanamke uliyenipa [wewe] awe pamoja nami ndiye aliyenipa matunda ya mti huo, nikala.” Kwa kweli yeye alikuwa akijitetea kwa kushindwa kushikamana na Mungu na kwa kukosa kusimamia nyumba yake, akamshtaki Mungu kwamba alimpa mke mbaya.​—⁠Mwa. 3:12.

Basi fikira za Adamu za uchoyo na tendo lake zilipotoa njia yake. Hakumpenda Yehova tena kwa moyo wake. Alianza mwendo wake mwenyewe wa kujitegemea, akawa adui wa Mungu, akaharibu njia yake mwenyewe na ile ya jamaa yake. Ndiyo, kwa sababu ya kuwapo dhambi na makosa, kila mtu akifuata njia yake mwenyewe ya kujitegemea, hakuna mtu anayejua linaloweza kumpata, kwa maana “wakati na tukio lisilotazamiwa huwapata wote.”​—⁠Mhu. 9:11, NW.

Ingefaa wale wanaodhani kwamba Mungu analaumika kwa hali mbaya wajiulize hivi, Je! nimemsifu Mungu kwa vitu vyema nilivyo navyo? Ninapofanikiwa, je! nimemsifu kwa kunifanikisha, au nimejisifu mwenyewe nikisema ufanisi huo umetokana na mimi? Je! ninamshukuru kwa kuwa na uhai kama mmojawapo wa viumbe vyake? Tena, je! nimestahili kibali au msaada wake kwa kufuata kanuni zake zinazopatikana katika Biblia?

KATI YA WALE WANAOJIDAI WANAMTUMIKIA MUNGU

Viongozi wa dini Wayahudi katika karne kwanza ni mfano unaoonyesha yanayotukia kati watu wanaojidai kumtumikia Mungu wanapoacha kufuata neno lake la kweli na kutegemea ufahamu wao wenyewe. (Mt. 15:8, 9) Njia ilipotoka ‘wakamnunia Yehova.’ (Linganisha Matendo 5:34, 38, 39.) Walimwua Yesu Kristo kwa sababu alifunua mawazo yao mabaya. Wakati uliofuata, waliwakasirikia wanafunzi wa Yesu kwa sababu waliwaambia kweli kutokana na Neno la Mungu.​—⁠Matendo 7:54-60.

Huenda vilevile wengine katika kundi la Kikristo wakasitawisha nia mbaya, wakimlaumu Mungu kwa sababu ya magumu wanayopata. Huenda Mungu akalaumiwa kwa sababu ya mambo yanayokwenda kombo kwa upumbavu wa mtu, au kwa sababu ya makosa ya mtu mwingine. Kwa mfano, huenda mtu akakwazwa na maneno au matendo ya ndugu katika kundi. Huenda mwenye kukwazwa akasema, ‘Basi, yeye akiendelea kuwa katika kundi, mimi sitahudhuria tena mikutano.’ Au labda anaweza kusema, ‘Mungu akiruhusu mambo yaendelee hivyo, mimi sitaki tena kuwa katika kundi.’ Huenda tena akalalamika akisema, ‘Ikiwa hivi ndivyo kweli inavyomfanya mtu awe, mimi sitaki tena mambo hayo.’

Je! hayo yanaonekana kuwa mawazo ya busara? Ni kinyume kabisa kusema kwamba kweli ingemfanya mtu kuwa mbaya! Na mtu akikwazwa peke yake, kuna sababu gani ya kulitia kundi ndani na Mungu vilevile? Sababu gani mtu anayejidai kuwa Mkristo aruhusu mtu mwingine, au hali fulani ziharibu urafiki mzuri alio nao pamoja na Mungu?

Basi, kwa kweli mtu anayesema hivyo bila kufikiri, “hununa juu ya [Yehova].” Jambo hilo lina busara gani? Hata ikiwa mtu mwingine au ikiwa jambo fulani linalotukia katika kundi lilimchukiza au likamkwaza sana, bila shaka mtu huyo anapotoa njia yake, kwa sababu hazitumii akili zake sawasawa. (Ebr. 5:14) Ama sivyo, hangemwonyesha Yehova, Mwenye kundi la kweli la Kikristo nia ya kipumbavu, isiyo na ushikamanifu,​—⁠Zab. 119:165.

Hatari inayoweza kumpata Mkristo ni kwamba nia hiyo yaweza kuimarika katika moyo wake. Inakuwa imara, ikiharibu MOYO wake. Si mara nyingi ambapo Mkristo atamlaumu Yehova moja kwa moja hivyo. Lakini huenda moyoni mwake akakosa kumvumilia Mungu na kujiona ana sababu inayofaa kukasirika, moyo wake ukimwongoza vibaya amkasirikie Yehova.

Kila mtu anakasirishwa na hali fulani nyakati nyingine. Huenda wakati huo mtu akawa hana furaha na tumaini, labda hata kukasirika. Lakini imempasa aone ishara za kuonya ili aondoe ugumu huo kwa kutegemea Maandiko. (Efe. 4:26) Imempasa afanye bidii ya kuondoa ugumu huo bila kukawia, akisaidiwa na wazee katika kundi ikiwa lazima. Hata ikiwa ugumu huo haukuondolewa kwa njia anayofurahia, asiruhusu hasira zake zimwongoze atende kipumbavu. Imempasa aangalie kwamba njia ya kutembea kwake katika kweli haipotoshwi. Bila hivyo, urafiki wake pamoja na Mungu utaharibika, maono yake yatiwe giza na moyo wake ‘umnunie [Yehova].’

Kwa sababu ya hatari hii, Biblia inashauri hivi: “Linda moyo wako kuliko yote uyalindayo; maana ndiko zitokako chemchemi za uzima.” (Mit. 4:23) Kutunza akili zetu tusipotoe njia yetu kwa sababu ya hatua isiyo ya hekima au kufikiri kipumbavu, kutatuwezesha tushike usawa wetu. (1 Pet. 1:13) Ndipo tutakapomwomba Yehova kama Mungu mwenye upendo anayeangalia watu mahali pa kumlaumu. Yeye atatupa ufahamu na kuongoza mwendo wetu katika njia nyofu na salama.​—⁠Mit. 4:5, 6.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki