Washiriki Wapya wa Baraza Inayoongoza
Septemba 7, 1977, Baraza Inayoongoza ya Mashahidi wa Yehova iliamua kukaribisha ndugu watatu watiwa mafuta wajiunge nao katika utumishi huko Brooklyn. Washiriki hao wapya wa Baraza Inayoongoza ni Carey W. Barber wa United States (Amerika), John E. Barr wa London, Uingereza, na Martin Poetzinger wa Jamhuri ya Ujeremani. Ndugu Barber amekuwa katika utumishi wa wakati wote tangu mwaka 1923 na ametumikia katika Betheli ya Brooklyn na katika utumishi wa kusafiri. Ndugu Barr amekuwa katika utumishi Wa wakati wote zaidi ya miaka 37 katika Visiwa vya Uingereza; amekuwa katika Betheli ya London katika utumishi mbalimbali, na hivi majuzi amekuwa katibu mweka hazina wa International Bible Students Association. Martin Poetzinger aliingia utumishi wa Ufalme mwaka 1926 na akaingia upainia mwaka 1930. Alihitimu katika Watchtower Bible School of Gilead. Utumishi wake wa wakati wote ulikatizwa kwa muda alipotiwa gerezani katika kambi ya mateso wakati Wanazi walipoleta mateso ya miaka mingi. Sasa washiriki wa Baraza Inayoongoza ya Mashahidi wa Yehova ni kumi na wanane.