Baraza Inayoongoza ya Mashahidi wa Yehova Yapanuliwa
Jamaa ya Betheli ya Brooklyn ilifurahi kupata habari Novemba 28 kwamba ndugu wafuatao walifanywa washiriki wa Baraza Inayoongoza ya mashahidi wa Yehova. Sasa watatumikia pamoja na waliokuwa wakitumikia katika Baraza Inayoongoza. Washiriki wapya ni kama ifuatavyo: W. Lloyd Barry, ambaye kwa sasa ni mwangalizi wa tawi Japan; John C. Booth, ambaye anafanya kazi afisini katika Watchtower Farm; Ewart C. Chitty wa London, England, ambaye ni katibu mwekahazina wa International Bible Students Association; Charles J. Fekel wa Brooklyn, New York, ambaye afanya kazi katika idara ya kuunganisha vitabu ya kiwanda cha Brooklyn; Theodore Jaracz wa United States, ambaye anatumikia kama mwangalizi wa mzunguko; Karl F. Klein wa Betheli ya Brooklyn, ambaye afanya kazi afisini; Albert D. Schroeder, ambaye amekuwa akitumikia kama mwalimu wa Shule ya Huduma ya Ufalme; na Daniel Sydlik, ambaye afanya kazi katika kiwanda cha vitabu katika Betheli ya Brooklyn. Ndugu wote hawa mwishowe watakuwa wakiishi katika makao ya Betheli katika Brooklyn nao watahudhuria mikutano ya kawaida ya Baraza Inayoongoza ya mashahidi wa Yehova inayofanywa asubuhi za Jumatano saa mbili. Pia watapokezana zamu kuketi kuongoza katika meza ya Betheli kila juma kulingana na herufi ya alfabeti ya jina la mwisho.
Sasa Baraza Inayoongoza ina washiriki kumi na wanane, wote wakiwa ni watiwa mafuta, na wale wengine kumi ni kama ifuatavyo: Frederick W. Franz, Raymond V. Franz, George D. Gangas, Leo K. Greenlees, John O. Groh, Milton G. Henschel, William K. Jackson, Nathan H. Knorr, Grant Suiter na Lyman A. Swingle.
Wana furaha kweli kuwa wakitumikia mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote.