Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w78 6/15 kur. 7-9
  • “Ishara” ya Ufalme Yatimizwa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Ishara” ya Ufalme Yatimizwa
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • SEHEMU NYINGINE ZA “ISHARA”
  • Zile “Siku za Mwisho” na Ule Ufalme
    “Ufalme Wako Uje”
  • Ambayo 1914 Ungemaanisha Kwako Wewe
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • Ufalme wa Mungu Huanza Kutawala Katikati ya Adui Zake
    Kweli Iongozayo Kwenye Uzima wa Milele
  • Uharibifu wa Ulimwengu Uliotabiriwa Utakuja Lini?
    Amani na Usalama wa Kweli—Wewe Unaweza Kuupataje?
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
w78 6/15 kur. 7-9

“Ishara” ya Ufalme Yatimizwa

LOOO! kilikuwa kishindo cha namna gani! Mwaka 1914 W.K. dunia hii ilipatwa na wasiwasi mwingi ambao haujakwisha mpaka sasa. Hiyo ni kwa sababu Vita ya Ulimwengu ya Kwanza iliingiza wanadamu katika nyakati za hatari zinazoendelea hata leo hii. Ni kama vile mwanafilosofia Mwingereza, Bertrand Russell, alivyoeleza: “Tangu mwaka 1914 ulimwengu umekuwa ukipepesuka kama mlevi kuelekea kwenye msiba.” Na miaka zaidi ya 50 baada ya 1914, msimamizi mmoja wa mambo ya serikali, Konrad Adenauer wa Ujeremani, alisema hivi akikumbuka mambo ya zamani: “Nakumbuka mambo . . . yaliyokuwako kabla ya mwaka 1914, wakati kulipokuwa na amani halisi, utulivu na usalama juu ya dunia hii​—wakati ambao hatukuwa tukiogopa. . . . Usalama na utulivu umekwisha katika maisha ya wanadamu tangu mwaka 1914.”

Looo! mwaka huo wa 1914 ulileta geuzo kubwa namna gani! Mataifa makubwa ya dunia yalipoingia katika vita ya kutumia vifaa vyote vya nchi zao, serikali zilitetemeshwa sana. Kufika wakati huo, sehemu kubwa ya dunia ilikuwa imetawalwa na falme zenye wafalme halisi. Lakini falme hizo zilitetemeshwa zikaanguka moja baada ya nyingine. Utawala wa zamani wa wafalme wa Kirusi ulimaliziwa mbali, na baada ya muda mfupi mahali pake pakachukuliwa na Ukomunisti usioamini Mungu yuko. Serikali za kijamaa zikapata nguvu za kutawala.

Lakini hayo yote yana uhusiano gani na ufalme wa Mungu? Wakati Yesu alipokuwa hapa duniani, wanafunzi wake walitaka sana kujua habari za ufalme huo. Wakati mmoja walimwuliza hivi: “Tuambie, Mambo haya yatakuwa lini, na ni nini itakayokuwa ishara ya kuwapo kwako na ya mwisho wa taratibu ya mambo?” “Kuwapo” huku kuna maana ya kuwapo kwake akitawala kama mfalme kwa kusudi la kuhukumu mataifa duniani. Tunajuaje? Tunajua kwa sababu wakati Yesu alipokuwa akiwajibu wanafunzi wake, alisema hivi: “Wakati Mwana wa watu atakapokuja katika utukufu wake, na malaika yote pamoja naye, halafu ataketi juu ya kiti cha utukufu wake; na mbele yake mataifa yote watakusanyika.” (Mt. 24:3, NW; 25:31, 32, ZSB) Basi “kuwapo” kwake kunakuwa katika makao ya kiroho. Ndiyo sababu “ishara” yenye kuonekana inatolewa ili kuonyesha wanadamu duniani kwamba ameanza kutawala akiwa Mfalme.

Acheni tuchunguze mambo fulani ya “ishara” ambayo Yesu alitoa. Tunapofanya hivyo, tunaweza kujiuliza hivi, Je! kweli mambo hayo yanaonyesha nyakati tunazoishi tangu mwaka 1914 ndio “mwisho wa taratibu ya mambo”? Kwanza, Yesu alisema kungekuwa na vita kati ya mataifa, “taifa . . . na taifa, na ufalme . . . na ufalme.” (Mt. 24:7, 8, ZSB) Tangu mwaka 1914, vile vita viwili tu vya ulimwengu vilimaliza watu milioni 69. Na sasa tunakaribia sana vita ya silaha za atomu. Ni jambo la maana kujua kwamba aliyekuwa Katibu wa Serikali wa United States, Henry A. Kissinger, alisema hivi Januari 10,1977, muda mfupi tu kabla ya kuondoka katika cheo chake: “Lazima watu wa Amerika wafahamu kwamba silaha za atomu zinawaelekea wanadamu wote zikiwa na hali mpya ya kwamba, kwa mara ya kwanza katika historia wanadamu wanaweza kujiangamiza kabisa wao wenyewe.” Huo ni uwezekano wenye kuogopesha kama nini! Hakika, utimizo wa sehemu nyingine ya “ishara” ya Yesu unaweza kuonekana na watu wote waziwazi:

“Kutakuwa . . . katika dunia taabu ya mataifa, na matata . . . watu wakizimia kwa woga, na kwa kutazamia maneno yanayokuja katika dunia.”​—Luka 21:25, 26, Z8B.

Msukosuko uliopo duniani unaonyesha kwamba “nyakati za Mataifa” za kutawala bila kumtegemea Mungu zilikwisha mwaka 1914. Sasa tunaishi katika wakati wenye taabu kuu ulimwenguni pote inayotokea muda mfupi tu kabla ufalme wa Mungu haujauondoa utawala wa wanadamu ili kuwapa watu faida za milele.​—Luka 21:24, ZSB.

SEHEMU NYINGINE ZA “ISHARA”

Lakini, ziko sehemu nyingine nyingi za “ishara” ya Yesu. Alisema kwamba kungekuwa na “upungufu wa chakula” katika “mwisho wa taratibu ya mambo.” Baada ya Vita ya Ulimwengu ya Kwanza njaa kubwa sana ziliua mamilioni ya watu, na sasa watu milioni mia tano hawana chakula cha kuwatosha, au wanakaribia kufa njaa kwa sababu hesabu ya watu imeongezeka sana ulimwenguni pamoja na ugomvi na pupa ya kutaka kutawala. Yesu alisema kungekuwa na “matetemeko ya dunia mahali hapa na mahali hapa.” (Mt. 24:7, NW) Hakika matetemeko yameonekana tangu mwaka 1914, nalo lililokuwa kubwa zaidi ni lile lililotokea Tangshan, China, mwaka 1976, ambalo mwenyekiti wa Chama cha Wakomunisti, Huo Kuafeng, alisema hivi juu yalo: “Liliua watu wengi na kuharibu mali nyingi kwa njia isiyoonekana kwa kawaida katika historia.” Watu zaidi ya 655,000 walikufa na 790,000 wakaumia, kisha jumla ya watu waliouawa na matetemeko ya dunia tangu mwaka 1914 ikawa zaidi ya 1,500,000. Hakika matetemeko ya dunia yameongezeka tangu mwaka 1914​—nayo yamekuwa ni sehemu ya ile “ishara.”

Hatuna nafasi ya kueleza sehemu zote za “ishara” ya Yesu. Lakini inaonekana waziwazi. Hata maaskofu wa Kanisa Katoliki wameiona maana ya “ishara” hiyo. Katika barua yake yenye kuenezwa sana ya Novemba 1, 1914, Papa Benedikti wa XV alisema Vita ya Ulimwengu ya Kwanza ndiyo iliyokuwa “mwanzo wa maumivu makali ya kufa kwa ulimwengu.” Naye aliyemfuata, Papa Pius wa XI, alieleza hali yenye kusikitisha iliyomo ulimwenguni katika Barua yenye kuenezwa sana iitwayo “Miserentissimus Redemptor,” kisha akamalizia hivi: “Kwa hakika, haiwezekani kuepuka kufikiri kwamba hizi ndizo ishara za siku za mwisho, zilizotangazwa na Bwana Wetu.” Mbona basi Kanisa Katoliki halijayafuata maneno aliyosema Yesu baada ya hapo juu ya ile “ishara”? Yesu alisema: “Na Habari Njema hii ya ufalme itahubiriwa katika ulimwengu wote kuwa ushuhuda kwa mataifa yote; na halafu mwisho utakuja.”​—Mt. 24:14, ZSB.

Linalosikitisha ni kwamba, Wakatoliki na Waprotestanti pia wameshindwa kuutangazia ulimwengu kwamba ufalme wa Mungu sasa unakaribia. Mashahidi Wakristo wa Yehova ndio wameachwa waifanye kazi hiyo. Na kama mwanahistoria mmoja wa kisasa alivyosema: “Mashahidi wa Yehova wametoa ushuhuda wao katika dunia nzima.”a

Huu ndio wakati wa kuusikiliza sana unabii wa Yesu. Kwa sababu gani? Kwa sababu muda mwingi umekwisha pita tangu kizazi hiki chetu kilipouona “uchungu” huo ukianza kuwapata wanadamu. (Mt. 24:8, ZSB) Tunaukaribia kwa haraka sana upeo wa ile “ishara,” ambayo Yesu alisema hivi kwa habari zake:

“Wakati huo kutakuwapo dhiki kubwa, ambayo haijatokea namna yake tangu mwanzo wa ulimwengu hata sasa, wala haitakuwapo kamwe. Na kama siku hizo zisingalifupizwa, asingeokoka mtu ye yote; lakini kwa ajili ya wateule zitafupizwa siku hizo.”​—Mt. 24:21, 22, 34.

Je! wewe unataka kuwa kati ya watu watakaopendelewa wakati dhiki ile ya mwisho itakapotokea? Basi lazima ujifunze jinsi Ufalme wa Mungu unavyoweza kukufaidi!

Kuanzia ukurasa wa 10, tutachunguza zaidi tuone jinsi uhitaji mkubwa ulivyotokea wa kuwa na serikali hiyo ya Ufalme, mambo ambayo Mfalme wake lazima ayatimize, na sababu ambayo imemfanya Mungu atumie maelfu ya miaka kufanya matayarisho ya Ufalme huo.

[Maelezo ya Chini]

a Kitabu cha 1950 cha C. S. Braden, These Also Believe (Hawa Pia Wanaamini).

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki