Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w78 11/1 kur. 21-22
  • “Changamkeni”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Changamkeni”
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
  • Habari Zinazolingana
  • Imba Wimbo wa Uchangamshi wa Ufalme
    Mwimbieni Yehova Sifa
  • Anaijaza ‘Mioyo Yetu Kikamili’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Kushikilia Tumaini Letu
    ‘Mwimbieni Yehova kwa Shangwe’
  • Kushikilia Tumaini Letu
    Mwimbieni Yehova
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
w78 11/1 kur. 21-22

“Changamkeni”

UPEPO wa namna ya tufani wenye kuvuma unaijilia merikebu, na kuishika merikebu kwa nguvu. Merikebu inarushwa huku na huku katika bahari yenye msukosuko. Katika wakati kama huu, inawezekanaje mtu ye yote achangamke?

Alipokutana na hali kama hiyo alipokuwa safarini kwenda Rumi, mtume Paulo aliwaambia wanaume waliokuwa hatarini: “Changamkeni.” (Matendo 27:14-22) Mtume Paulo alikuwa na hakika kwamba hakuna uhai hata mmoja ungepotezwa kwa sababu aliamini ahadi ya kimungu aliyokuwa amepewa: “Usiogope, Paulo, huna budi kusimama mbele ya Kaisari; tena, tazama, Mungu amekupa watu wote wanaosafiri pamoja nawe.”​—Matendo 27:24.

Hata ingawa hatuko hatarini ya kuvunjikiwa na merikebu katika bahari yenye msukusuko, sisi leo tunaishi katika ulimwengu unaojaa msukosuko na taabu. Watu wengi wamevunjika moyo na kushuka moyo na wanajiona kutokuwa na msaada wanakutana na magumu yanayozidi kuongezeka. Je! tunaweza ‘kuchangamka’ katika wakati kama huo?

Mtume Paulo alikuwa mchangamfu katika hali inayoelekea kutokuwa na matumaini, kwa sababu ya ahadi ya Mungu. Kwa hiyo, ni jambo la akili kuona kwamba sisi kuwa wachangamfu kunategemea yale ambayo Muumba anakusudia kwa ajili yetu. Uwezekano wa dunia wa kutoa mahitaji ya wanadamu kwa wingi unaonyesha kwamba Yehova Mungu anataka sisi tuchangamke. Hata watu wenye kuabudu sanamu wa Listra (Asia Ndogo) waliambiwa hivi: “[Mungu] hakujiacha pasipo ushuhuda, kwa kuwa alitenda mema, akiwapeni mvua kutoka mbinguni, na nyakati za mavuno, akiwashibisha mioyo yenu chakula na furaha.”​—⁠Matendo 14:17.

Ndiyo, ijapokuwa hali zisizopendeza za maisha, kuna mengi ambayo yanaweza kutuletea furaha. Yanayotiwa ndani ni mambo ya kawaida kama kila chakula kizuri, machweo ya jua yenye kupendeza, kutembea katika bustani yenye maua mazuri na kutembea katika msitu. Zaidi ya hayo, hata ingawa hali zetu za sasa si nzuri sana, tunayo ahadi ya Mungu inayotuhakikishia kwamba atakomesha uovu na kuondolea wanadamu huzuni yote, taabu, magonjwa na hata mauti (kifo) yenyewe.​—Ufu. 21:4.

Tusipoachilia magumu ya wakati huu yatuzuie tuyaone mambo mengi mema yanayotuzunguka pamoja na wakati ujao wa ajabu sana ambao Mungu amewawekea watumishi wake, tunaweza kuchangamka. Kama inavyosema Mithali 15:15 tunaweza kufurahia “karamu ya daima’.” Hali zisizofaa za maisha zinatoweka wakati mtu anapofikiria baraka na tumaini tunalopewa na Mungu.

Maoni machangamfu vilevile yanamsaidia mtu avumilie magumu. Kwa kuwa mtu hayafikirii nyakati zote, inakuwa vyepesi kuyavumilia. Uchangamfu unazuia mtu asikuze makosa ya wengine na unaelekea kumfanya mtu ayavumilie. Kwa kuwa mtu hafikirii sana mambo yasiyofaa, yeye haelekei sana kuwasengenya wengine na kuwanung’unikia. Hiyo inaweza kusaidia afya ya mtu, kwa sababu inazuia mambo yenye kudhuru kama vile chuki, hasira, husuda, kisasi na kutakia wengine mabaya. Katika kitabu chake Cancer, Dakt. J. E. Hett anasema kwamba upendo, uchangamfu pamoja na upole yanaongeza hali njema ya mtu. Hii inapatana kabisa na Mithali hii ya Biblia: “Moyo uliochangamka ni dawa nzuri.” (Mit. 17:22) Kuongezea hayo, mtu anayeridhika na mwenye furaha, anaweza kuwachangamsha wengine.

Ni jambo la hekima kufikiri juu ya mambo yanayofaa. Biblia inatutia moyo hivi: “Mambo yo yote yaliyo ya kweli, yo yote yaliyo ya staha, yo yote yaliyo ya haki, yo yote yaliyo safi, yo yote yenye kupendeza, yo yote yenye sifa njema; ukiwapo wema wo wote, ikiwapo sifa nzuri yo yote, yatafakarini hayo.” (Flp. 4:8) Mambo kama hayo yanapokuwa vichwa vya mazungumzo yetu, wanaotusikiliza watajengwa, ndiyo, wachangamshwe.

Kwa kweli, inafaa kujitahidi kusitawisha na kuendeleza nia yenye uchangamfu, kwa kuwa inasaidia hali njema ya mtu mwenyewe na ya wengine. Shauri la mtume Paulo alilolitoa wakati wa tufani yenye hatari baharini ni shauri zuri kwetu sisi katika nyakati hizi zenye taabu. Kwa hiyo, “changamkeni.”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki