Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w79 7/15 kur. 5-7
  • Mahubiri ya Mlimani—Heri ya 6 Mpaka ya 9

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mahubiri ya Mlimani—Heri ya 6 Mpaka ya 9
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • “WENYE FURAHA” WANAKUWA WANA WA MUNGU
  • WAKITESWA, LAKINI BADO Nl WENYE FURAHA
  • Jinsi Maneno ya Yesu Yanavyoleta Furaha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Ni Wenye Furaha Ingawa Wanateswa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2004
  • Wenye Furaha Ni Watu Wanaomtumikia “Mungu Mwenye Furaha”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2018
  • Watumishi wa Yehova Wenye Furaha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2004
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
w79 7/15 kur. 5-7

Mahubiri ya Mlimani​—Heri ya 6 Mpaka ya 9

YESU alisema ‘heri’ ya sita ya Mahubiri yake ya Miimani kama ifuatavyo: “Heri wenye moyo safi; maana hao waiamwona Mungu.”​—Mt. 5:8.

“Wenye moyo safi” ni watu walio safi kindani. Usafi wao ni wa mapendo, tamaa, kuthamini na nia. Unatofautiana sana na usafi wa nje au unaofuatwa kwa ukawaida tu. (Mt. 23:25-28; Marko 7:3, 4) Mahali pa kukazia wonyesho wa nje-nje wa utawa, Maandiko yanatia moyo wonyesho wa “upendo utokao katika moyo safi na dhamiri njema, na imani isiyo na unafiki.”​—1 Tim. 1:5.

Wenye moyo safi wanapata furaha sana kwa sababu ”‏watdmwona Mungu.” Kwa lazima hii haimaanishi kuona kwa halisi kwa macho ya kibinadamu, kwa maana ‘hakuna mwanadamu awezaye kuona Mungu akaishi.’ (Kut. 33:20; Yohana 1:18; 1 Yohana 4:12) Walakini kuna njia nyingine ambazo kwazo waabudu wenye nia nzuri duniani wanaweza ‘kumwona Mungu’ wakati huu. Kwa mfano, kuangalia Mungu akitenda kwa ajili ya mtu kwa sababu ya ukamilifu wa mtu ni njia mojawapo ya ‘kumwona Mungu.’ (Ayubu 19:26; 42:5) Ziara kwenye hekalu katika Yerusalemu ili kuabudu zinaelezwa kuwa kama mtu akienda ‘‘kuona uso wa Yehova,” au kujihudhurisha mbele zake.​—Kut. 34:24; Kum. 31:11, NW; Isa. 1:12.

Neno la Kigiriki analotumia Mathayo kwa ‘kuona’ lamaanisha pia “kuona kwa fahamu, kutambua, kujua.” Kwa kuwa Yesu alionyesha utu wa Mungu kwa ukamilifu, yeye angeliweza kusema: “Aliyeniona mimi amemwona Baba.” (Yohana 14:7-9) Wenye moyo safi waliomkubali Yesu kuwa Masihi na kumsikiliza walipata ufahamu mwingi kuhusu utu wa Mungu. Kwa kuiamini dhabihu ya Yesu iondoayo dhambi walipata msamaha wa dhambi pamoja na uhusiano na Mungu na kuweza kutoa ibada inayokubalika mbele za kiti chake cha enzi. (Efe. 1:7) Kwa habari ya Wakristo waliotiwa mafuta kwa roho kumwona Mungu katika maana hiyo kutafikia upeo wake wafikapo mbinguni, kwa maana huko watamwona Mungu na Kristo kwa macho.​—1 Yohana 3:2; 2 Kor. 1:21, 22.

Hata hivyo, nafasi ya kumwona Mungu kupitia kwa maarifa sahihi ni ya wale wenye moyo safi peke yao. Maandiko yanaonyesha kwamba wanaozoea dhambi hawajamwona wala kumjua Mungu na Mwanawe. “Yeye atendaye mabaya hakumwona Mungu.”​—1 Yohana 3:6; 3 Yohana 11; Zab. 24:3, 4.

“WENYE FURAHA” WANAKUWA WANA WA MUNGU

Yesu alitoa heri ya saba ya Mahubiri ya Mlimani hivi: “Wenye furaha ni wenye amani, kwa kuwa wataitwa ‘wana wa Mungu.’”​—Mt. 5:9, NW.

Wenye amani wanaonekana waziwazi kwa yale wanayoepuka na kwa yale wanayotenda pia. Watu wenye amani hawachokozani au kufanya vita; wala hawalipi uovu kwa uovu wanapokosewa. (Rum. 12:14-21) Walakini pia kuna upande ufaao kwa nia yao.

Neno la Kigiriki linalofasiriwa wenye amani lamaanisha “wapatanishi.” Si kwamba tu wanajiendesha kwa amani bali pia wanajitahidi kufanya amani na mapatano kati ya pande zenye mzozo. Wao wanakataa kuachilia au kushiriki katika jambo lo lote liwezalo ‘kutenganisha rafiki.’ (Mit. 16:28; 17:9) Kwa usemi na kwa matendo wao hutia moyo kuwe na amani ndani na nje ya kundi la Kikristo.​—Rum. 14:19; Ebr. 12:14.

Wenye amani wanafurahi, “kwa kuwa wataitwa ‘wana wa Mungu.’ “Wao wanafurahia uhusiano wa karibu na Mungu. Kama watoto wake. Hata hivyo, ili wadumishe uhusiano huu wanahitaji kuiga sifa za utu wa Mungu, unaotia ndani kuwa na amani. (2 Kor. 13:11; Flp. 4:9; 1 The. 5:23; Ebr. 13:20; Yak. 3:17) Mtu ye yote anayeendeleza uadui na mwenzake pasipo upendo “hatokani na Mungu.”​—1 Yohana 3:10.

Katika siku za Yesu Wayahudi waliamini kwamba wao walikuwa wana wa Mungu kwa sababu ya kuwa viumbe Vyake vya kibinadamu. (Yohana 8:39, 41) Kwa kweli, Yesu alitangaza kwa watu fulani hivi: “Ninyi ni wa baba yenu, Ibilisi.” (Yohana 8:44) Kwa kuwa jamii yote ya kibinadamu inarithi dhambi kutoka kwa Adamu ambaye aliumbwa awe mwana “wa Mungu” wa kidunia, kuwa wana wa Mungu si jambo ambalo mtu anazaliwa nalo.​—Rum. 3:23; 5:12; Luka 3:38, NW.

Wenye amani peke yake waliomkubali Yesu kuwa Masihi na mchukuaji wa dhambi ndio “waliopewa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake.” (Yohana 1:12; Isa. 53:12; 1 Pet. 2:24) “Mkutano mkubwa” wa “kondoo wengine” wa Mchungaji Mwema Yesu Kristo watakuwa naye akiwa kwao “Baba wa milele” wakati wa ufalme wake wa miaka elfu, walakini baada ya hapo yeye atawarudisha kwa Baba yake mwenyewe wa kimbinguni wapate kuwa wazao wa Mungu.​—Ufu. 7:9-17; Yohana 10:14-16; Isa. 9:6; 1 Kor. 15:27, 28.

WAKITESWA, LAKINI BADO Nl WENYE FURAHA

Ikiwa ndiyo heri ya nane katika mfuatano huu, Yesu alitangaza hivi: “Heri wanaoteswa kwa sababu ya kufanya atakavyo Mungu, maana Utawala wa mbinguni ni wao!” (Mat. 5:10, Habari Njema kwa Watu Wote) Akiongezea hayo, yeye alisema heri ya tisa hivi: “Heri yenu ninyi kama watu wakiwatukana, wakiwadhulumu na kuwasingizia kila aina ya uovu kwa sababu yangu. Furahini na kushangilia maana tuzo lenu ni kubwa mbinguni. Hivyo ndivyo watu walivyowadhulumu manabii walio kuwako kabla yenu.”​—Mat. 5:11, 12, Habari Njema kwa Watu Wote; linganisha Luka 6:22, 23.

“Wanaoteswa” ni Wakristo waliopata kushutumiwa, kusingiziwa na kufukuzwa kutoka katika jamii “kwa ajili ya haki,” au “kwa ajili ya Mwana wa Adamu.” Taabu zao ni kwa ajili ya kumwabudu Yehova Mungu na kulichukua jina la Yesu Kristo na kufuata sana nyayo zake.​—1 Pet. 2:19-21.

Sababu ya kushangilia hapa ni sawa na ile inayotolewa katika heri ya kwanza, yaani, ”‏ufalme wa mbinguni ni wao.” (Linganisha Mathayo 5:3.) Ijapokuwa inaweza kumaanisha kushufumiwa, kufukuzwa kutoka katika ujamaa wao na hata kifo katika visa vingine, Wakristo wanafahamu kwamba ‘shangwe’ ya kutawala pamoja na Krisfo katika ufalme wa kimbinguni wa Mungu au kufurahia uzima mkamilifu wa kibinadamu kama raia zake za kidunia inastahilisha mambo hayo.​—Mt. 25:21, 23; Ebr. 12:2; Ufu. 21:1-5.

‘Thawabu hii ya mbinguni’ (yaani, kutoka kwa Mungu) haimaanishi mshahara unaolipwa mtu kwa kazi inayofanywa. Kwa vyo vyote wanadamu wenye dhambi hawawezi kupata kibali ya Mungu kama malipo na kumlazimisha Yeye awabariki. (Gal. 2:16, Yak. 2:10) Thawabu ya baraka za ufalme ni ‘zawadi isiyo na kifano’ ya bure! ni ushuhuda wa wema wa Mungu na ukarimu wa Mungu. (2 Kor.:915; Yak. 1:16-18) Ni zawadi inayolipwa Wakristo kwa ajili ya kuvumilia kwa uaminifu mashutumu mateso na uongo mbaya wanaonenewa kwa sababu ya kujitoa kwao kwa Mungu kusikovunjika.

Vilevile Yesu alitoa tofauti ya hizi heri mbili za mwisho, akisema: “Ole wenu ninyi watu wote watakapowasifu, kwa kuwa baba zao walitenda manabii wa uongo mambo kama hayo.” (Luka 6:26) Badala ya kutangaza kweli ya Mungu, “manabii wa uongo” wa Israeli wa kale walisema ambayo watu walitaka kusikia na ,watu hao ‘wakapenda mambo yawe hivyo.’ (Yer. 5:31) Walakini umaarufu huu haujapata hata kidogo kuwa ishara ya kibali ya Mungu. Kibali ya Yehova Mungu i juu watu wanaozungumza na kutenda kulingana Neno lake. (Zab. 15:​1, 2) Hata hivyo wale wafanyao hivyo, wanaweza kutazamia mateso, maana Yesu alisema: “Ikiwa wamenitesa mimi, watawatesa na ninyi pia.”​—Yohana 15:​20, Habari Njema kwa Watu Wote.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki