Ni Nani Atakayefanya Siku ya Mapambano Itufaraidi?
“Basi mimi naweza kufanyaje Mungu ainukapo? Na atakapo hesabu mimi naweza kumjibuje?”—Ayubu 31:14, NW
1. Ni kwa sababu gani sisi tunaotaabishwa na hali pasipo msaada tunatamani sana kuona siku ya mapambano katika muda wa maisha yetu, na kwa kadiri gani?
SIKU ya mapambano ni kitu kizuri. Wako wengi sana kati yetu wanaotaka sana mambo yanyoshwe kwa faida ya kila mtu. Ndiyo, tena tungeweza kufurahia sana siku ya namna hiyo. Tunapatwa na matokeo ya makosa yanayofanywa, uonezi na kupunjwa (kudanganywa), nasi hatuwezi kuwaadhibu hao watendao makosa. Kinachoweza kutufariji ni kwamba kuna kitu kinachofanya kazi kiitwacho “sheiria ya kulipa kisasi.” Kwa hiyo mwishowe haki ya hukumu itatimizwa. Ee hilo na litukie katika muda wa maisha yetu wenyewe! Ndiyo, litukie ulimwenguni pote! Ndipo atakapofaidika kila mtu anayedhulumiwa.
2. Ni jambo gani linaloweza kusemwa kwa habari ya mazingira yetu ya kijamii na ya asili, nalo latokeza woga gani?
2 Leo mazingira yetu ya kijamii yako vibaya. Hata mazingira yetu ya asili yanachafuliwa na kuharibiwa. Hakika lazima kuwe na siku ya kumaliza tatizo hilo, karibuni—ndivyo wanavyotuambia wataalam wa mazingira. Jamii ya kibinadamu haiwezi kuendelea kuharibu usawa wa mazingira ya asili ya dunia bila mwishowe kupatwa na matokeo yake. Inahofiwa kwamba huenda jamii yote ya kibinadamu ikafa, katika dunia isiyofaa kwa maisha.
3. Ni jambo gani linaloweza kusemwa kwa habari ya kupambana kwa sababu ya tabia, kujitayarishia vita na juu ya kitu ambacho huonwa kuwa kitu kisichogusika, kitakatifu?
3 Huenda tukaifikiria siku ya kupambana inayokaribia kwa sababu katika nchi zote kunakuwa na uharibifu wa tabia njema. Vilevile kwa sababu ya mataifa kushindania atakayekuwa na silaha nyingi zaidi, bila ya tengenezo la Umoja wa Mataifa kuyasihi yapunguze shindano hilo, bali mataifa yote yakianza kutegemea matayarisho ya kijeshi yawape usalama. Lakini, kuna sehemu nyingine ya mambo ya kibinadamu itakayoadhibiwa, sehemu ambayo huenda wengi wetu tukaiona kuwa kitu kisichogusika, kama kitu chenye utakatifu mwingi. Kitu gani? Ni dini!
4. Sababu gani dini inastahili kufikiliwa na siku ya mapambano, nayo matokeo yatakuwa nini siku hiyo itakapofika?
4 Watu zaidi na zaidi wanaiondoa dini maishani mwao kama kitu kisichofaa, kitu ovyo, hata chenye kuumiza. Hata hivyo, dini ingali ni mojawapo za nguvu zenye kuongoza sana maisha ya wanadamu. Ikiwa kunao, ni watu wachache sana wanaoweza kuepuka maongozi yake. Dini imeleta ubaya mwingi sana katika mwenendo wa watu na wa mataifa hata inastahili kufikiliwa na siku ya kuadhibiwa. Hilo litakapotukia, mamia ya mamilioni ya watu watashangaa, nayo matokeo yatakuwa ya kuogopesha sana.
5. (a) Dini . imekuwaje nguvu iliyo kuu zaidi katika kuleta mgawanyiko duniani? (b) Ni kwa sababu gani dini nyingi za Jumuiya ya Wakristo na zile za sehemu nyingine ya ulimwengu haziwezi zote kuwa za kweli na zenye kufaa?
5 Katika historia ya kibinadamu dini ndiyo nguvu ambayo imegawanya watu zaidi duniani. Imetenganisha mbari za watu, mataifa, makundi ya watu, makabila na hata washiriki wa jamaa. Hivyo imeleta mafarakano kati ya wanadamu. Tofauti za dini zimeleta chuki kali sana na kuwapa watu maoni mabaya juu ya wenzao bila sababu nzuri, na looo, zikaleta mapigano yenye jeuri, mashambuliano ya ukatili ambayo yameendelea kame nyingi hata sasa. Ile sehemu ya watu wa kidini iitwayo Jumuiya ya Wakristo imeshiriki mambo hayo pia. Kwa kweli, hiyo ndiyo imeyafanya zaidi. Kwa sababu ya vita vyake vyenye kuudhi makao yake yametiwa madoa ya mtiririko mwingi sana wa damu ya kibinadamu. Kilichotokeza hayo ni vile imegawanyika katika mamia ya madhehebu za kidini. Mgawanyiko huo peke yake wahakikisha kwamba jumuiya hiyo haiko namna inavyojidai kuwa—ya Kikristo. Mvurugo wa dini nyingi za Jumuiya ya Wakristo na dini zenye kutofautiana za sehemu ile nyingine yote ya ulimwengu hauwezi kuwa unafaa. Kweli ni moja, nayo ni kamili, tena ina umoja yenyewe.
6. (a) Ni kwa sababu gani lazima mataifa yote yakutane na siku ya mapambano, na yakiwa sasa yote pamoja? (b) Ni lazima yule atakayepambana nayo awe mtu wa namna gani?
6 Dini zenye kuhitilafiana, mazingira ya asili, kanuni za tabia, usimamizi wa mambo ya kibinadamu—hayo ni mambo ambayo mataifa yamekuwa nayo. Hakuna taifa limekuwa bila kosa. Mataifa yote yamevunja sheria zifaazo za mwenendo na za serikali. Kulingana na vile mambo yamekuwa katika historia yote ya kibinadamu iliyopita, lazima mataifa yakutane na siku ya mapambano. Sasa tu mataifa yataingia katika siku hiyo ya kupambana pamoja, yakiwa na njia zote za mawasiliano na usafirishaji na kutegemeana yanavyotegemeana. Lakini ni kitu gani au ni nani atakayepambana nayo? Je! ni mungu wao wa kitaifa au kundi la miungu yao? Je! ni yeye yule aitwaye “ng’ombe mtakatifu,” sayansi? Je! ni Umoja wa Mataifa, au chama kinginecho cha mataifa yote chenye kuendesha uhusiano kati ya mataifa ya Kikomunisti na mataifa ya kibepari (ya walio huru kujitafutia utajiri wao wenyewe) au kati ya jamii ya wafanya kazi na mabwanawakubwa wao? Hata kidogo, kwa maana kushindwa kwa vyama hivyo ndiko kumeingiza wanadamu katika hali ya sasa inayowahuzunisha. Basi, inaonekana wazi kwamba lazima hicho kiwe kitu halisi chenye akili kinachoyaweza kabisa magumu yote makubwa ya watu na ambacho hakipendelei mbari za watu wala mataifa, lazima iwe ni Akili yenye nguvu zote iwezayo kuigeuza siku hii ya kupambana iwe ya kufariji wote wapendao yaliyo haki.
NI NINI KINACHOHITAJIWA ILI HUKUMU IWE ISIYOPENDELEA?
7. (a) Mataifa yatakuwa katika hali gani katika siku hiyo ya mapambano tunayozungumza juu yake hapa? (b) Ni mwenye Mamlaka ya Hukumu wa namna gani angefaa kupambana na mataifa?
7 Hapa hatuizungumzi “Siku ya Hukumu” katika ulimwengu wa roho baada ya kufa kwa raia za mataifa. Tunazungumza siku ya kupambana na mataifa yote yakiwa bado yanaendesha shughuli (kazi) zao na kujitahidi kuendeleza daima utawala wao kwa namna za serikali yanazopendelea. Je! mataifa yataiokoka siku ile inayokuja ya kukaguliwa na kupambana na Mwamuzi mwenye nguvu zipitazo za kibinadamu ambaye mataifa yote yanapaswa kumjibu? Hilo ndilo ulizo linalotuhangaisha sisi tulio washiriki wa mataifa hayo yenye hatia. Kwa hiyo, kwa ajili ya siku ya kupambana, tunataka Mwamuzi aliye mkuu kuliko miungu yote ya mataifa isiyojiweza, Yeye asiyeweza kuhongwa na mataifa matajiri yenye maendeleo mengi, Yeye asiyeyaogopa mataifa makuu ya ulimwengu yaliyo na majeshi yenye nguvu nyingi, kama vile United States of America na Urusi wa Kikomunisti.
8. (a) Kwa hiyo, mioyo yetu inatamani nani awe Mwamuzi wa Mwisho na Msimamizi wa hukumu? (b) Pasipo kuwako kwa Mtu kama huyo, ni mambo gani yanayohusu mbingu na dunia hayangeelezeka kwa akili yalikotoka?
8 Ah ndiyo, mioyo yetu inataka kwa asili Yeye Aliye Juu Zaidi awe Mwamuzi wa Mwisho na Msimamizi wa hukumu. Ulimwengu mzima, acha kadunia ketu kadogo, ungeweza kufanya nini pasipo huyo Mwenye Enzi Kuu wa Ulimwengu Wote? Upatano, utaratibu, na usawa kamili wa utendaji wa ulimwengu wetu wote ungekuwa wapi bila Mpajisheria huyo wa ulimwengu wote? Ushirikiano wenye faida wa vitu vyote vyenye kutegemeana vinavyofanyiza mazingira yetu ya asili ungekuwa wapi bila Mbuni na Muumba huyo, Chanzo cha uhai wa wanyama wote, mimea na viumbe vya kibinadamu? Visingekuwako. Visingeweza kuwako bila kumtegemea Mtu huyo Mkuu Zaidi, Mwenye Nguvu Zote.
9. (a) Kuwako kwa milele na utendaji wa Mtu kama huyo kumeonyeshwaje? (b) Musa alimwitaje kwa kufaa, naye ana uhusiano gani na mataifa yote?
9 Mtu huyo hakulazimika kutokea kwa sababu ya kuhitajiwa hivyo, bali kuwako kwa viumbe vyote kabla ya mwanadamu kutokea duniani kwahakikisha na kuonyesha kwamba Yeye amekuwako tangu milele na anafanya kazi. Kwa kufaa anaitwa “Mungu wa miungu, na Bwana wa mabwana.” Ndivyo alivyoitwa na mpajisheria aliye mashuhuri zaidi wa nyakati za kale, yaani, Musa. Musa aliweza kutoa ulinganifu huo kwa akili, maana yeye mwenyewe aliifahamu miungu ya Misri ya kale na vilevile alisomea “hekima yote ya Wamisri.” (Kum. 10:17; Matendo 7:22) Karne nyingi baadaye Mungu huyo Mkuu Zaidi alitajwa kwa mahakma kubwa zaidi katika Ugiriki ya kale, mahakma iliyoketi juu ya Kilima Mars katika Athene. Huo ni wakati Paulo mtume Mkristo alipoiambia mahakma hiyo: “Mungu aliyeufanya ulimwengu na vitu vyote vilivyomo . . . alifanya kila taifa la wanadamu kutoka katika [mtu] mmoja, wakae juu ya uso wa nchi yote.” (Matendo 17:2426) Kwa sababu ya ukuu wake juu ya vikundi vyote vya kitaifa anaitwa “mfaIme wa mataifa.”—Yer. 10:7.
10. Sababu gani huyu “mfalme wa mataifa” anaweza kushinda wapinzani wake wote ambao ni mamlaka za leo za kijeshi na kisiasa zenye nguvu nyingi kupita nyingine zote?
10 Tunaweza kusoma mengi zaidi juu ya Mungu huyu aliye mkuu kuliko mataifa katika Kitabu kitakatifu kilichoandikwa na Musa, Paulo na watu wengine ambao, mara nyingi, wao wenyewe waliyaona matukio waliyoandika juu yake ili kutupasha sisi habari leo. Hakuna mataifa yanayoweza kushindana na Mungu huyu. Yeye aliweza kuzishinda mamlaka za uliaiwengu kama Misri ya kale, Ashuru na gabeli. Ni upumbavu kudhani kwamba yeye alikuwa mungu mdogo tu kama miungu ile mingine ya historia ya kale na kwamba alitoweka wakati kitabu cha mwisho cha Biblia kilipoandikwa karne 19 zilizopita. Mungu huyo hawezi kufa, anajitegemea kwa habari ya uzima. Leo anaweza kukabiliana (kukutana) na wapinzani wake, mataifa yote ya kisiasa ya ulimwengu wa kisasa yaliyo na nguvu nyingi kupita mengineyo. Kama “mfalme wa mataifa,” yeye atapambana na yote. Kutatokea faida ya milele kwa wote wapendao haki na wema.
WAKILI WA MUNGU WATAKAYEPAMBANA NAYE
11. Kulingana na Matendo 17:31, Mungu amejiwekea nini kwa ajili ya siku ya mapambano, naye ametoa uthabiti gani?
11 Kwa ajili ya siku hiyo ya kupambana inayokuja Mungu ameweka mjumbe wake mwenyewe, mwamuzi mwenzake. Paulo mtume Mkristo alimtaja naibu huyo alipoendelea kuiambia hivi Mahakma Kuu Zaidi juu ya Kilima Mars katika Athene, Ugiriki: “[Mungu] ameweka siku atakayohukumu walimwengu kwa haki, kwa mtu yule aliyemchagua; naye amewapa watu wote uthabiti wa mambo haya kwa kumfufua katika wafu.”—Matendo 17:31.
12. Kwa sababu gani kuwako kwa uthabiti huu si jambo la kudharauliwa, kama walivyofanya mahakimu Wagiriki waliomsikia Paulo?
12 Ni “uthabiti” gani zaidi wa ajabu ambao Mungu Mwenye Nguvu Zote angeweza kutoa juu ya siku ya hukumu aliyowekea wakaaji wote wa dunia kuliko kumfufua mwamuzi mwenzake kutoka kifo cha kupigania imani? Kwa sababu tu huenda tukawa tuna maoni tofauti ya kidini, haitupasi kuupuza “uthabiti” wa Mungu kama wengi wa mahakimu hao wa Mahakma Kuu Zaidi walivyofanya juu ya Kilima Mars. “Uthabiti” huo umetolewa na “mfalme wa mataifa.” Si jambo la kudhihakiwa ya kuwa si la kisayansi na kuwa ni lenye kuchekesha tu. Katika kame ya kwanza W.K. walikuwako watu zaidi ya 500 waliojionea wenyewe kuwako kwa “uthabiti” huo kutoka kwa Mungu, kutia na mtume Paulo mwenyewe.
13, 14. (a) Kama ushuhuda wa uthabiti wa Mungu, sababu gani Yesu Kristo aliyefufuliwa hako duniani leo? (b) Imekuwaje kwamba Mungu hakuendelea kuwa peke yake katika makao yake ya kiroho?
13 “Mtu” ambaye kufufuliwa kwake kwa wafu ndio “uthabiti” wa siku ijayo ya hukumu ‘iliyowekwa’ anatajwa kuwa Yesu Kristo. (1 Kor. 15:38, 1220) Sababu ya yeye kutokuwapo duniani leo ni kwamba aliutoa uhai wake mkamilifu wa kibinadamu kama dhabihu kisha akafufuliwa, ili wanadamu waliokufa waweze kufufuliwa pia wawe na nafasi ya kupata uzima usio na mwisho katika dunia itakayosafishwa igeuzwe kuwa paradiso ya dunia nzima. Kwa sababu hiyo amepewa thawabu ya kupandishwa mbinguni naye yuko mkono wa kuume wa Mwamuzi Mkuu Zaidi, yule Mungu aliye na uwezo wa ufufuo. Yesu Kristo alijitaja kuwa ‘Mwana pekee’ wa Mungu na “mwanzo wa kuumba kwa Mungu.” (Yohana 3:16; Ufu. 3:14) Kwa sababu gani?
14 Ni kwa sababu yeye ndiye aliyekuwa wa kwanza kuumbwa na Mungu mbinguni kisha Mungu akamtumia kama mfanya kazi mwenzake katika kufanya vitu vingine vyote, kutia na dunia yetu na wakaaji wake wa kwanza, Adamu na Hawa. (Kol. 1:15-18) Malaika wa kimbinguni wasioonekana ndio walioumbwa kabla ya mwanadamu. Kwa sababu ya kuumba “Mwanawe pekee” na malaika wote watakatifu, Mungu hakuendelea kukaa peke yake katika makao yake mwenyewe ya kiroho. Kulingana na masimulizi ya Biblia, hesabu ya malaika hao wenye nguvu zipitazo za kibinadamu ni mamia ya ihamilioni.—Zab. 104:4; Dan. 7:9, 10; Ebr. 1:7; 12:22.
15. Mwana mzaliwa pekee wa Mungu alifanywaje pindi moja kuwa “mdogo punde kuliko malaika”?
15 Maelfu hayo ya malaika wataitika wamfuate Mungu katika siku ya kupambana na mataifa yote ya dunia. Wao wanamtumikia pia mwamuzi mwenzake ambaye atamtumia kuhukumu dunia ikaliwayo na watu katika siku aliyoiweka. (Mt 25:31, 32) Wakati Mungu alipomtuma Mwanawe pekee kwa mwujiza awe mwanadamu mkamilifu duniani kwa kuzaliwa na bikira Myahudi, Mwana huyo wa Mungu alifanywa “mdogo punde kuliko malaika.”—Ebr. 2:9; Zab. 8:4, 5.
16. Yesu Kristo alifufuliwa kwenye cheo gani, na kwa kusudi gani lenye faida?
16 Hata hivyo, huyo Mwana pekee wa Mungu ana cheo gani leo—sasa? Yeye amefufuliwa na Mungu akainuliwa kwenye cheo cha mbinguni kilicho juu hata zaidi kuliko kile cha malaika kwa sababu ya kuonyesha uaminifu wake kwa Mungu mpaka kifo cha dhabihu pasipo kuwa na hatia. Ili Mwana huyu wa Mungu aliye mfano wa mwanakondoo aweze kuwafaidi wanadamu wote kwa dhabihu yake, Mungu alimfufua katika siku ya tatu, walakini, hakufufuliwa kama mwanadamu, kwa kuwa alikuwa ametoa hali yake ya ubinadamu kama dhabibu milele. Kwa hiyo Mungu alimfufua akamwinua kwenye maisha ya mbinguni, kwenye kutokufa na kwenye ukuu mwingi kuliko malaika wote. (1 Pet. 3:18) Hivyo angeweza kutumikia kama “uzao” ambao Mungu alimwambia hivi Ibrahimu rafiki yake mwaminifu kuuhusu: “Katika uzao wako mataifa yote ya dunia watajibarikia.”—Mwa. 22:18; Gal. 3:8-16.
17. Katika Waebrania 1:3-9, Paulo aliandika nini kuhusu kutukuzwa kwa Kristo akiwa Mwana wa Mungu?
17 Basi, haitupasi tufurahie kutukuzwa huko kwa Yesu Kristo katika mbingu? Ndiyo, kwa maana sasa tuna matazamio mazuri zaidi ya uzima wakati ujao. Paulo mtume Mkristo, aliyemwona kwa mwujiza Yesu Kristo aliyefufuliwa aliandika habari za kutukuzwa kwake. Katika barua moja aliyoandikia Waebrania waliomkubali Yesu kuwa Masihi wa unabii wa Biblia, Paulo aliandika hivi: “Alipokwisha kufanya utakaso kwa ajili ya dhambi zetu aliketi mkono wa kuume wa Mfalme katika sehemu zilizoinuka. Kwa hiyo amekuwa bora kuliko malaika, kwa kadiri ambayo amerithi jina bora zaidi kuliko lao. . . . Pia, kwa habari ya malaika, yeye asema: ‘Naye afanya malaika zake roho, na watumishi wake wa hadhara mwali wa moto.’ Lakini kwa habari ya yule Mwana: ‘Mungu ndiye kiti chako cha enzi milele, nayo fimbo ya ufalme wako ndiyo fimbo ya unyofu. Wewe umependa haki, nawe ukachukia ukosefu wa kufuata sheria. Hiyo ndiyo sababu Mungu, Mungu wako, amekupaka kwa mafuta ya shangwe zaidi ya wenzi wako.”—Ebr. 1:3-9, NW.
18. Kupitia kwa Mwana huyu, Mungu atafanya nini kwa habari ya siku ijayo ya mapambano?
18 Kupitia kwa Mfalme huyu aliye na nguvu zipitazo za malaika aliye Hakimu wake Mdogo, Mungu atafanya siku ijayo ya kupambana na mataifa yote itufaidi milele.
[Picha katika ukurasa wa 8]
Kuhukumiwa kwa Wakaaji Wote wa Dunia katika Haki Kunathibitishwa na Kifo, Kuzikwa na Kufufuliwa kwa Kristo