Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w79 7/15 kur. 12-18
  • Yesu Kristo—Mfalme Mshindi Atakayepambana na Mataifa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Yesu Kristo—Mfalme Mshindi Atakayepambana na Mataifa
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • MANENO YANAYOONGOZWA NA ROHO ANAYOAMBIWA MFALME
  • MWEKWA ATAKAYEPAMBANA NA MATAIFA
  • Msifuni Kristo​—Mfalme Mtukufu!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Uendeshaji wa Wale Wapanda-Farasi Wanne Ni Ishara
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Namna Siku ya Mapambano Itakovyotuletea Faida
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Kulitatua Daima Suala la Ulimwengu Wote Mzima
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
w79 7/15 kur. 12-18

Yesu Kristo​—Mfalme Mshindi Atakayepambana na Mataifa

1. Katika Waebranla 1:8, 9 Paulo aliwaandikia nini Wakristo waliokuwa Yerusalemu ili kuthibitisha kwamba Mwana wa Mungu alikuwa mkuu kuliko malaika?

KABLA Yerusalemu haujaharibiwa na Warumi katika mwaka 70 W.K., Wakristo waliokuwa ndani ya mji huo walihitaji kuhakikishiwa kutokana na Maandiko ya Kiebrania yaliyoongozwa na Mungu kwamba Yesu Kristo, Mwana wa Mungu, alikuwa amefanywa mkuu kuliko malaika wa mbinguni. Kwa hiyo, alipokuwa akiwaandikia Wakristo hao katika Karne ya kwanza, mtume Paulo alivuta fikira zao kwenye maneno haya ya unabii yaliyomhusu Yesu Kristo aliyetukuzwa: “Mungu ndiye kiti chako cha enzi milele, nayo fimbo ya ufalme wako ndiyo fimbo ya unyofu. Wewe umependa haki, nawe ukachukia ukosefu wa kufuata sheria. Hiyo ndiyo sababu Mungu, Mungu wako, amekupaka kwa mafuta ya shangwe zaidi ya wenzi wako.”​—Ebr. 1:8, 9, NW.

2. Sababu gani Mungu akawa ‘kiti cha enzi’ cha Mwanawe, na katika njia gani?

2 Ufalme wa mpenda haki hivyo na mchukia ukosefu wa kufuata sheria hakika ungetufaidi sana sisi sote tuliopo duniani. Kwa hiyo, fimbo anayotumia ni “fimbo ya unyofu.” Si ajabu kwamba Mungu anakuwa ‘kiti chake cha enzi,’ maarta Mungu ndiye Chanzo cha pekee cha ufalme wake na ndiye anayeusaidia ufalme wake kuendelea. Mataifa yote ya ulimwengu huu hayawezi kuupindua ufalme wake kama vile yasivyoweza kumpindua Mungu asiwe Mwenye Enzi Kuu wa Ulimwengu Wote na “mfalme wa mataifa.” Lazima sasa mataifa yote yaonane na Mwanawe aliyetawazwa.

3. Paulo alitaja maneno ya Waebrania 1:​8, 9 kutoka wapi, na hilo lathibitisha nini?

3 Maneno aliyotumia mwandikaji aliyeandikia Waebrania waliogeuzwa kuwa Wakristo kumhusu Mwana wa Mungu aliyetukuzwa yalitolewa katika kitabu cha Biblia cha Zaburi, au kutoka Zaburi 45:6, 7. Hiyo inahakikisha kwamba zaburi yote hiyo ilikuwa ya unabii. Kwa kuichunguza tutapata habari kuhusu yale ambayo mfalme mtiwa mafuta wa Mungu atafanya kwa utukufu wa Mungu na furaha ya milele ya wanadamu.

4. Shauku inayoonyeshwa na Zaburi 45 inaonyeshwa juu ya nini?

4 Zaburi hiyo inaonyesha shauku nzuri, nao walioiandika ni Walawi rasmi waliotumikia katika hekalu la Mungu Yerusalemu. Shauku iliyopo ni shauku inayoonwa kwa sababu ya kuingia kwa serikali nzuri ikiwa mikononi mwa mtawala mwenye haki asiyepotoka. Kipindi hicho kinasisimua moyo, kwa maana mtunga zabari aingia moja kwa moja na maneno haya: “Moyo wangu umesisimuliwa na jambo jema. Mimi ninasema: ‘Kazi zangu ni kuhusu mfalme fulani.’ Ulimi wangu na uwe kalamu ya mwandishi mstadi.”​—Zab. 45:1 na maneno yaliyo juu ya sura katika tafsiri ya New World.

5. Jambo jema la Zaburi 45 ndilo lililokuwa kichwa kikuu cha mahubiri ya nani, nalo lilistahili kutangazwa kadiri gani?

5 “Jambo jema” lililousisimua moyo wa mtunga zaburi mwenye kuongozwa na roho ya Mungu limekuwa ni sehemu ya maana sana ya zile ambazo Yesu Kristo aliziita “habari njema hizi za ufalme.” Ujumbe wa Ufalme ulikuwa ‘mwema’ sana hata ukastahili ‘kuhubiriwa katika dunia yote inayokaliwa na watu kwa ushuhuda kwa mataifa yote,’ kwa sababu “mwisho” wa hayo lazima uje. (Mt. 24:14 NW) Leo, je! mioyo yetu inasisimuliwa na, kichwa cha habari ‘njema’ hizo za ufalme wa Mungu kupitia kwa Kristo?

6. (a) Sana sana ‘‘kazi” zetu zahusu nini? (b) “Ulimi” wetu unakuwaje kama kalamu ya mwandishi mstadi?

6 Je! tunajiunga na mtunga zaburi na kusema kila mtu asikie kwamba: “Kazi zangu ni kuhusu mfalme fulani”? Hatuna sababu ya kumwaibikia mfalme huyo, mtiwa mafuta wa Mungu mwenyewe. Kwa hiyo “kazi” zetu kuu zapasa ziwe kusema kwetu, kufundisha na kuhubiri juu ya Masihi huyo wa kifalme. Tunafanya kazi hasa kwa ajili ya faida za Ufalme wake, si kwa ajili ya falme zo zote za kilimwengu zinazokaribia mwisho wazo wenye msiba. Tunasisimuliwa tutumie ndimi zetu kutangaza ufalme wa Mungu na Mfalme wake mtiwa mafuta. Yatamkwayo na ndimi zetu yanatoka kwa uzuri kama mwandiko uandlkwao kwa kalamu ya mwandishi mwenye ustadi wa kufanya hati za nakala za Maandiko Matakatifu. Yatokayo katika ndimi zetu sisi pia tunataka tuyaandike ili wengine wafurahie kuyasoma. Tena lililo zuri zaidi ni kwamba leo tunaweza kuyachapisha na kutokeza mamilioni ya nakala zinazolingana katika lugha nyingi kwa kuyapitisha katika mashine zenye mwendo wa haraka sana ili zikaenezwe kati ya wasomaji ulimwenguni pote.

MANENO YANAYOONGOZWA NA ROHO ANAYOAMBIWA MFALME

7. Ni ulizo gani linalotokea juu ya maelezo yanayotolewa katika Zaburi 45:2?

7 Je! sisi tunapendezwa na mfalme mtiwa mafuta wa Mungu? Yatupasa tupendezwe, ikiwa tunapendezwa na maelezo yanayotolewa na mtunga zaburi. Mwandikaji huyo aliyeongozwa na roho anasema naye na kumlinganisha na wafalme wa zamani katika ukoo wa kifalme tangu Mfalme Daudi wa Yerusalemu, akisema: “Hakika wewe u mzuri wa uso zaidi ya wana wa watu. Mapendezi yamemiminwa juu ya midomo yako. Hiyo ndiyo sababu Mungu amekubariki hata wakati usiojulikana.”​—Zab. 45:2, NW.

8. Ni jambo gani linaloongezea uso wa Yesu Kristo uzuri?

8 Yesu Kristo alikuwa mwanadamu mkamilifu, mkamilifu kama mwanadamu wa kwanza Adamu katika bustani ya Edeni. Hakika zile picha ambazo wachoraji wa Jumuiya ya Wakristo wamechora hazilingani na sura yake halisi alipokuwa duniani. Maelezo ambayo mtunga zaburi anatoa juu yake yanatofautiana kabisa na yale yaliyotolewa katika Isaya, sura ya 53, ambapo anaonyeshwa kuwa mtumishi wa Mungu mwenye kuteseka. Lakini tumchukuapo kulingana na alivyo hasa na vile anavyofanya, anakuwa na uzuri usiotegemea maumbo ya uso lakini bado unaupita uzuri wa nyuso za wanaume wengine wote, hata ule wa Adamu.

9. Ni kitu gani kilichoongezea midomo ya Yesu Kristo mapendezi, nacho ni kitu gani kinachoongezea midomo yetu mapendezi?

9 Midomo ya mfalme ilikuwa na umbo zuri. Lakini yaliyomiminika kupitia midomo hiyo ndiyo yaliyoiongezea mapendezi, nayo mapendezi hayo yalitoka kwa Mungu. Adui wenye nia mbovu waliishtakia midomo yake kusema makufuru juu ya Mungu. Lakini, hata wakuu wa polisi waliotumwa wakamkamate na kumleta mahakmani walilazimika kuwaambia hivi wenye lawama: “Hajanena kamwe mtu ye yote kama huyu.” (Yohana 7:46) Ujumbe wa ufalme wa Mungu aliounena ulitia mapendezi katika midomo yake. Sisi tunaomtambua kuwa Mwalimu wetu tunapendezwa sana na anayosema. Kama wanafunzi wake tunaongeza mapendezi katika midomo yetu kwa kurudia kusema aliyosema.

10. Ni kwa sababu gani Mungu alimpa Yesu Kristo baraka hata wakati usiojulikana, nayo hiyo ilionyeshwaje?

10 Mfalme huyo mwenye sura nzuri na mwenye kupendeza amepewa na Mungu baraka ya milele na milele. Sababu ya kupewa ni kwamba yeye alinena mambo ambayo Mungu alimfundisha kuyanena. Aliihubiri kweli ya Mungu na kuifundisha juu ya serikali ya kitheokrasi itakayobariki wanadamu wote. Wakati Yesu Kristo aliopokuwa akijaribiwa kama astahili kufa kisha liwali Mrumi Pontio Pilato akamwuliza kama yeye alikuwa mfalme, yeye alijibu kishujaa kwamba: “Wewe wasema, kwa kuwa mimi ni mfalme. Mimi nimezaliwa kwa ajili ya haya, na kwa ajili ya haya mimi nalikuja ulimwenguni, ili niishuhudie kweli. Kila aliye Wa hiyo kweli hunisikia sauti yangu.” (Yohana 18:37) Kwa sababu ya kueleza watu kweli juu ya Ufalme kwa uaminifu, Mungu alimbariki kwa kumfufua kwa wafu. Zaidi ya hilo, Mungu alimpa ufalme wa mbinguni, si juu ya raia za Mfalme Daudi tu, bali pia juu ya wanadamu wote. Baraka ya milele na milele ambayo Mungu alimpa ni dalili nzuri kwetu sote.

MWEKWA ATAKAYEPAMBANA NA MATAIFA

11. Kabla tu ya kifo chake, Yesu aliwaambia wanafunzi wake jambo gani juu ya chuki ya ulimwengu, nayo mataifa yatalazimika kupambana naye katika vita yenye jeuri kwa sababu gani?

11 Wakati Yesu Kristo alipokuwapo duniani akiwa mwanadamu mkamilifu, alikuwa na adui. Basi, si ajabu kwamba angali ana adui duniani baada ya kutawazwa kwake kama mfalme mbinguni tangu “nyakati zilizowekwa za mataifa” zilipokoma mwaka 1914. Saa kadha kabla hajafia imani aliwaambia wanafunzi wake hivi: “Iwapo ulimwengu ukiwachukia, mwajua ya kuwa umenichukia mimi kabla ya kuwachukia ninyi.” (Yohana 15:18) Leo ulimwengu haujabadilika ukaanza kunipenda Yesu Kristo. Hata Jumuiya ya Wakristo yenyewe haijaanza kumpenda. Hilo linahakikishwa na vile inavyotesa wanafunzi wa kweli walio mfano wa Kristo. Mataifa ya kilimwengu yangependa kumzuia Yesu Kristo aliyetawazwa asiwatawale wanadamu. Yangependa kupunguza utawala wake uwe wa mbinguni tu na kujiwekea wenyewe utawala wa dunia milele. Kwa hiyo kweli, unyenyekevu na haki zinahusika. Kwa kuwa mataifa ya kilimwengu yamesimama yaendelee kupingana naye hivyo tangu Majira ya Mataifa yalipokoma mwaka 1914, lazima Yesu Kristo apigane nayo kweli kweli. Mataifa hayo yataonana naye katika vita yenye jeuri.

12. Kwa sababu ya kile ambacho kingemkabili Mfalme mpya aliyetawazwa, Zaburi 45:​5-5 ilimwambia afanye nini?

12 Kile ambacho kingemkabili mfalme wa Kimasihi aliyetawazwa karibuni kilitangulia kuonwa na mtunga zaburi kwa uongozi wa roho. Kwa hiyo, yeye aliendelea kuandika hivi kama kwamba kwa kutumia “kalamu ya mwandishi mstadi”: “Jifungie upanga wako pajani, wewe uliye hodari, utukufu ni wako na fahari ni yako. Katika fahari yako usitawi uendelee kwa ajili ya kweli na upole [unyenyekevu, NW] na haki. Mishale yako ni mikali, watu huanguka chini yako; imo mioyoni mwa adui za mfalme.”​—Zab. 45:3-5.

13. Maelezo ya mtunga zaburi huyo yanatusaidiaje kutambua yule aliyeonwa katika njozi katika Ufunuo 6:1, 2, naye anatambulishwa kuwa nani?

13 Mishale huhitaji uta wa kutupia. Kwa hiyo, maelezo ya mtunga zaburi yanatusaidia kumtambua anayeonyeshwa katika Ufunuo 6:1, 2, ambayo Yohana mtume Mkristo anataja njozi fulani na kusema: “Nikaona hapo Mwana-Kondoo [Yesu Kri-sto] alipofungua moja ya zile muhuri saba, nikasikia mmoja wa wale wenye uhai wanne akisema, kama kwa sauti ya ngurumo, Njoo! Nikaona, na tazama, farasi mweupe, na yeye aliyempanda ana uta, akapewa taji, naye akatoka, ali akishinda tena apate [kumaliza] kushinda” kwake. Mtumia uta huyo aliyevikwa taji mwenye kumwendesha farasi mweupe alifananisha Yesu Kristo aliyetukuzwa akielekea kupigana na adui zake. Lengo lake ni kumaliza kwa kushinda. Lazima ashinde duniani pote.

14. Ni kwa sababu gani Mfalme mpya aliyetawazwa ni “hodari,” kama vile ilivyotabiriwa katika Isaya 9:6?

14 Katika utukufu wake na fahari kama ya mfalme aliyepewa cheo, Yesu Kristo ajivika upanga wa vita ayainulie mataifa yenye upinzani duniani. Kwa kuwa yeye si mtu mwenye nyama na damu tena, bali amevikwa nguvu za kimbinguni, sasa yeye ni mtu “hodari” kweli kweli. Unabii wa Isaya 9:6 unasema kwamba kimojawapo cha vyeo vyake kingekuwa “Mungu mwenye nguvu.” Wakati bado unakuja ambapo mataifa ya leo yenye silaha nyingi yatamjua kwamba yeye ni hodari hivyo.

15. Tofauti na ilivyokuwa wakati alipopanda kwenda Yerusalemu katika mwandamano, ni kwa sababu gani Yesu Kristo atapanda farasi atakapokuwa akipambana na mataifa?

15 Kama Mfalme Sulemani katika sherehe ya kutawazwa kwake, wakati mmoja Yesu Kristo alipanda punda mwenye amani alipouingia Yerusalemu kwa ushindi, akajitolea mji huo kama mfalme wa ukoo wa Daudi. (Mt. 21:1-14; Zek. 9:9) Lakini karibuni, atakapopanda kutetea kweli, unyenyekevu na haki, kwa usemi wa mfano atapanda farasi wa vita. Itafaa afanye hivyo, kwa maana atapaswa kuonana na wale wasiofuata kweli, unyenyekevu na haki.

16. Ni ukweli gani ambao mataifa wamekanyaga chini ya miguu yao ijapokuwa wameutangaziwa na Mashahidi wa Yehova?

16 Siku chache baada ya Yesu kumpanda yule punda na kuingia Yerusalemu, alimwambia Liwali Pilato kwamba alikuwa ameingia ulimwenguni kuishuhudia ile kweli. Hiyo ilikuwa kweli hasa juu ya ufalme wa Mungu, ambao wakati huo tu alikuwa amemaliza kumshuhudia Pilato. (1 Tim. 6:13) Leo serikali za mataifa zinaikanyaga kanyaga kweli hiyo kwa kuipuza, hata ingawa Yehova amewatumia mashahidi wake kuzijulisha kwamba Majira ya Mataifa ya utawala wa ulimwengu yalikwisha mwaka 1914.

17. Yesu Kristo ametetea jamii gani ya wanadamu, na sababu gani lazima yeye apiganie. kusimamishwa kwa taratibu mpya ya haki?

17 Watawala wa kilimwengu hawaonyeshi unyenyekevu wo wote mbele za Mungu. Hawamwondokei kwa amani Mtawala wa dunia astahiliye, Yesu Kristo, aliyeonyesha unyenyekevu ulio mwingi zaidi mbele za Mungu na kuwatetea wanyenyekevu wote wasiojiweza duniani, sana sana wanafunzi wake wenye kuteswa. Sasa katika hizi “siku za mwisho” uovu wa wanadamu umeharibika zaidi, nao ukosefu wa kufuata sheria unazidi kuenea ajabu. Wanadamu wanahitaji kupewa mwanzo mpya wa kufuata haki. Kwa hiyo, lazima Shujaa Mfalme Yesu Kristo apande akatetee haki na kupigania kuanzwa kwa taratibu mpya juu ya dunia yote.​—Isa. 26:9.

18. Ni onyo gani linalotolewa mataifa kwa maneno haya yanayoambiwa Mfalme “mkono wako wa kuume utakufundisha mambo ya kutisha,” nako kuchinjwa kwa watu wengi sana kunaonyeshwaje katika Zaburi 45:5?

18 Katika nyakati za kisasa si panga wala mishale peke yake inayotumiwa katika vita. Mataifa makubwa yaliyo na majeshi yenye nguvu kuliko yale mengine sasa yanasema yanaweza kutumia makombora ya nuclear na neutron na mengine yanayoweza kurushwa kutoka bara moja mpaka bara nyingine. Lakini yasidhani kwamba Yesu Kristo aliyetukuzwa hawezi kuwajia kwa ghafula akiwa na silaha za kisayansi za vita zilizo bora kupita zao. Zaburi 45:4 inayatangazia mataifa onyo la kwamba mkono wa kuume wa Kristo utamfundisha “mambo ya kutisha.” Makombora yake yaliyo bora kupita yale ya kibinadamu yatazilenga sawasawa shabaha zake ambazo ni wanadamu, kama vile makombora ya wanadamu yanavyopata shabaha bila kuikosa. Yakiwa na lengo la kufisha yataipiga ‘mioyo ya adui za mfalme.’ Habari za vita zinazotolewa kwamba chini yake “watu [wanazidi kuanguka, NW] huanguka” katika vita yake ya kupigania kweli, unyenyekevu na haki, zinaonyesha kwamba watu wengi watachinjwa.​—Zab. 45:5.

19. Watu ‘wanaoshtuka’ kwa kuona Yesu Kristo na Babaye wa mbinguni wakionyeshwa namna hiyo wanapaswa kujiuliza maulizo gani kuhusu mataifa yao wenyewe, nayo dunia iliyochafuliwa kwa damu isiyo na hatia itasafishwaje?

19 Huenda watu wa Jumuiya ya Wakristo leo wakasema kwamba hiyo inamwonyesha Yesu Kristo kuwa mmwaga damu na Baba yake wa mbinguni kuwa Mungu mkatili, mwenye kutaka sana kuona damu ikimwagika. Huenda watu hao wakadai wameshtuka kuona Mungu na Yesu Kristo wakionyeshwa kuwa hivyo. Lakini namna gani mataifa ya Jumuiya ya Wakristo ambayo watu wake ni raia zake wenye kuyatetea? Je! mikono ya mataifa hayo haina madoa ya damu, damu iliyomwagwa si katika vita vya kitheokrasi, bali visivyo vya Kikristo? Mataifa hayo yenye hatia ya damu na yakumbuke kwamba, baada ya gharika iliyowafagilia mbali wakaaji wote wa dunia isipokuwa Nuhu na jamaa yake waliokuwa ndani ya safina, Mungu aliwaambia hivi: “Atakayemwaga damu ya mwanadamu, damu yake huyo itamwagwa na mwanadamu; maana kwa mfano wa Mungu alimfanya mwanadamu.” (Mwa, 9:6) Jumuiya ya Wakristo imeyaongoza mataifa kumwaga damu kwa vita vya kisiasa, vita vya kidini na kwa kutesa Wakristo wenye kufuata dhamiri walioshikamana na Biblia. Ni kwa njia gani nchi iliyochafuliwa na damu ya kibinadamu itakavyosafishwa? Ni. kwa njia moja tu ya kuimwaga damu ya wenye hatia ya damu ili kusawazisha haki ya hukumu.

20. Hii inapatanaje na sheria ya Mungu kuhusu miji ya makimbilio kwa ajili ya wauaji wasiokusudia, nayo dunia yetu itafanywaje ifae kusimamishwa Paradiso juu yake?

20 Hiyo inapatana na sheria ya Mungu iliyohusu miji ya makimbilio aliyoanzisha katika Israeli kwa ajili ya wauaji wasiokusudia. Kupitia kwa nabii Musa, yeye alisema: “Hamtaitia unajisi nchi ambayo mwaiketi; kwa kuwa damu huitia nchi unajisi; wala hapana sadaka itoshayo kwa ajili ya nchi, kwa ajili ya damu iliyomwagwa ndani yake, isipokuwa ni damu ya huyo aliyeimwaga. Kwa hiyo msiitie unajisi nchi muiketiyo, ambayo naketi nami kati yake; kwa kuwa mimi [Yehova] nakaa kati ya wana wa Israeli.” (Hes. 35:33, 34) Ikiwa dunia yetu itafanywa ifae ili Paradiso iwe huku kukaliwa milele na wanadamu, lazima isafishwe. Lazima damu isiyo na hatia iliyomwagwa juu yake ilipiwe na damu ya wenye kushughulikia vita na wauaji wengine, ndiyo, ilipiwe na damu ya mataifa ambayo leo yanatutisha na vita ya tatu ya ulimwengu.

21. Kwa habari ya haki ya hukumu, kwa sababu gani, ni lazima Mungu ampe Kristo ushindi, nako kuunganisha majeshi ya mataifa yote katika Umoja wa Mataifa kutawafaidi nini mataifa?

21 Kwa sababu hiyo iliyo haki mataifa yote lazima yapambane karibuni na Yesu Kristo. Lazima yeye ayashinde. Ama sivyo wenye kudai haki hawataridhishwa. Yehova Mungu atampa ushindi juu yao. Kuungana kwa vikosi katika tengenezo la Umoja wa Mataifa hakutayaepusha yasishindwe kabisa. Yatapigana na faida za Ufalme wa Mwana-Kondoo wa Mungu aliyetolewa dhabibu wakati moja, nacho kitabu cha mwisho cha Biblia kinasema hivi juu ya jambo hilo: “Hawa wana shauri moja, nao wampa yule mnyama [Umoja wa Mataifa] nguvu zao na mamlaka yao. Hawa watafanya vita na Mwana-Kondoo, na Mwana-Kondoo atawashinda, kwa maana Yeye ni Bwana wa Mabwana, na Mfalme wa Wafalme.” (Ufu. 17:13, 14) Juu ya pigano hilo, tunaendelea kusoma hivi:

22, 23. (a) Ufunuo 19:11-16, 19 unatuambia jambo gani zaidi juu ya vita hiyo? (b) Vita hiyo inapiganiwa wapi, nayo damu isiyo na hatia iliyomwagwa duniani inafunikwaje, katika kuisafisha dunia?

22 “Tazama, farasi mweupe, na yeye aliyempanda, aitwaye Mwaminifu, na Wa-kweli, naye kwa haki ahukumu na kufanya vita.: . . juu ya kichwa chake [ana] vilemba vingi . . . amevikwa vazi lililochovywa katika damu, na jina lake aitwa, Neno la Mungu. Na majeshi yaliyo mbinguni wakamfuata, wamepanda farasi weupe na kuvikwa kitani nzuri, nyeupe, safi, . . . Naye ana jina limeandikwa katika vazi lake, MFALME WA WAFALME, NA BWANA WA MABWANA.

23 “Kisha nikamwona huyo mnyama, na wafalme wa nchi, na majeshi yao, wamekutana kufanya vita na yeye aketiye juu ya farasi yule, tena na majeshi yake,” (Ufu. 19:11-16, 19) Kwa sababu mataifa yaliyokusanyika yanazidi kushikilia enzi zao za kitaifa na kutaka utawala wa kibinadamu uitawale milele dunia yote, hayo ndiyo yanayolitokeza kwa lazima pigano litokealo. Upeo wa hali ya ulimwengn wanayoleta unafananishwa na uwanja wa vita ambao, katika Kiebrania, unatiwa Har–​Magedoni. (Ufu. 16:14-16) Hapo ndipo inapopiganwa “vita ya siku ile kun ya Mungu Mwenyezi.” Hapo ndipo lazirna damu ya mataifa yote iilipie damu yote isiyo na hatia waliyoichafua dunia nayo. Hivyo dunia nzima itasafishwa ili Paradiso ianzishwe duniani pote.

24. Je! taifa lo lote litaokoka siku hiyo ya mapambano, nasi watu mmoja mmoja twapaswa tuhangaikie jambo gani?

24 Lo! itakuwa siku ya mapambano namna gani kwa mataifa yote ya dunia, yawe sehemu ya Jumuiya ya Wakristo au hapana! Je! lo lote la mataifa hayo litaokoka siku hiyo? Hilo ndilo ulizo la maana sana tulilouliza mapema katika mazungumzo haya. Na sasa bila shaka jibu ni, Hapana! Hata moja! Ndiyo sababu sisi, tulio raia za mataifa hayo yaliyohukumiwa kupatwa na msiba, twapaswa kuhangaishwa sana na jambo hilo. Twapaswa tutake kujifunza namna sisi kama watu mmoja mmoja tunaweza kuokoka bila kuwa na hatia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki