Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w79 7/15 kur. 18-22
  • Namna Siku ya Mapambano Itakovyotuletea Faida

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Namna Siku ya Mapambano Itakovyotuletea Faida
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • NDOA NA WATOTO
  • “WANA WA KIFALME KATIKA DUNIA YOTE”
  • Shangilieni kwa Sababu ya Ndoa ya Mwana-Kondoo!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Kutoka Katika Taabu ya Ulimwengu Kuingia Katika “Nchi Mpya” Yenye Amani
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
  • Kubaki Tukiwa Tumejipanga Kitengenezo Ili Tuokoke Kuingia Katika Mileani
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Yesu Kristo—Mfalme Mshindi Atakayepambana na Mataifa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
w79 7/15 kur. 18-22

Namna Siku ya Mapambano Itakovyotuletea Faida

1. Kwa sababu gani mataifa hayatashinda katika Har–​Magedoni, nayo hesabu yao italipwaje katika siku hiyo ya mapambano?

“VITA ya siku ile kuu ya Mungu ‘ Mwenyezi” katika Har–​Magedoni iko mbele ya mataifa yote. Ijapokuwa yamejiwekea silaha sana kuliko wakati mwingine wo wote. uliotangulia kwa ajili ya vita ya ulimwengu wote, hayawezi kutazamia kumshinda Mungu Mwenye Nguvu Zote. Akiwa Amiri Jeshi Mkuu wa jeshi lote la mbinguni, yeye atampa uShindi Yesu Kristo Mkuu wa Majeshi yake, kwa kuwa huyu ndiye “Bwana wa mabwana na Mfalme wa wafalme.” Yeye atakuwa na siku ya mwisho ya kupambana na mataifa yote yenye upinzani. Yakipimwa katika mizani ya hukumu ya haki ya kimungu, yataonekana kupungukiwa. Hesabu yao italipiwa na uharibifu wao wa milele.​—Ufu. 19:11-21; 17:14, Habari Njema kwa Watu Wote.

2. Ni kwa sababu gani maneno ya Zaburi 45:​6, 7 yaliambiwa Mfalme baada ya vita hiyo, nako kuinua kwake fimbo ni dalili nzuri ya jambo gani kwa wanadamu?

2 Ushindi katika Har–​Magedoni utaitetea enzi kuu ya ulimwengu wote ya Mungu Mwenye Nguvu Zote. Kwa sababu Mungu amtumia Yesu Kristo afaulu kupata ushindi huo, atamhesabu kuwa astahili kubaki na kiti chake cha enzi cha mbinguni. Maadamu Mungu yuaendelea kuwapo, nacho kiti cha enzi cha Mfalme wake mtiwa mafuta Yesu Kristo kitaendelea kuwapo. Jambo hilo la maana linakaziwa na maneno ya Zaburi 45:6, 7 (NW), ambayo mtunga zaburi amwambia Mfalme akisema: “Mungu ndiye kiti chako cha enzi kwa wakati usiojulikana, hata milele; fimbo ya ufalme wako ni fimbo ya unyofu. Wewe umependa haki nawe wachukia uovu. Hiyo ndiyo sababu Mungu, Mungu wako, amekupaka kwa mafuta ya shangwe zaidi ya wenzi wako.” Tunayajua maneno hayo kwamba ndiyo yaliyotumiwa na mtume Paulo katika Waebrania 1:7-9 kuhakikisha kwamba Kristo ni mkuu kuliko malaika. Kwa sababu alipenda haki na kuchukia uovu au ukosefu wa kufuata sheria, ilikuwa lazima fimbo ya Kristo itumiwe ili kutetea unyofu. Hiyo ni dalili nzuri kwa wanadamu.

3. Ni nani waliokuwa “wenzi” wa Yesu Kristo, na kwa sababu gani “mafuta ya shangwe’’ ambayo kwayo alipakwa mafuta yalikuwa zaidi ya wao?

3 Alipokuwa mwandamu duniani, Yesu alikuwa na wafalme na mababu. Mtunga zaburi ataja kwamba angekuwa na mababu wa kidunia. Wengi wao, tangu MfaIme Yehoyakini kurudi nyuma mpaka Mfalme Daudi, walikuwa wamekuwa “wenzi” wake katika kuushiriki ufalme uliosimamishwa na Mungu na katika kukalia ‘kiti cha enzi cha Yehova.’ (1 Nya. 29:23; 2 Nya. 13:5, 8; Mt. 1:6-12) Bila shaka mababu hao wa kifalme walishangilia ufalme wao juu ya watu wateule wa Mungu. Lakini hakuna mmoja wa “wenzi” hao wa kifalme aliyeweza kuwa na shangwe kama vile Yesu Kristo aliyetukuzwa alivyo nayo. Ufalme wake ni mkuu kuliko wao, maana ni wa mbinguni, ndiyo, wenye nguvu kupita za malaika. Yehova, Mungu wa Yesu Kristo, alimpaka kwa wingi zaidi “mafuta ya shangwe” kwa sababu ya kujitoa kwake kwa ukamilifu, kusikoweza kuharibika, ili kutimiza haki ya Mungu.

NDOA NA WATOTO

4, 5. Katika Zaburi 45:​8-14a, mtunga zaburi anamwonyesha Mfalme mshindi akifanya nini baada ya hapo, na sababu gani hili laweza kutushangaza sisi?

4 Yesu Kristo atakapokwisha kufanya vita ashinde adui zake duniani, hapo anaweza kuelekeza fikira zake kwenye shughuli (kazi) za amani. Mtunga zaburi aliyeongozwa na roho amwonyesha kama akioa na kulea jamaa. Huenda hilo likaonekana kushangaza, kwa sababu Mwana wa Mungu hakuwa mwanadamu duniani apate kuoa mmoja wa mabinti za wanadamu. Yeye hakufuata mwendo wa ‘wana fulani wa Mungu’ wa kimalaika wa siku za Nuhu. (Mwa. 6:1-4) Kwa hiyo huenda mtu akakosa kujua jinsi maneno haya mengine ya Zaburi 45 yanavyoweza kuwa kweli:

5 “Mavazi yako yote hunukia manemane na uudi mdalasini. Katika majumba ya pembe vinubi vimekufurahisha. Binti za wafalme wamo miongoni mwa akina bibi wako wastahiki. Mkono wako wa kuume amesimamama malkia, amevaa dhahabu ya Ofiri. Sikia, binti, utazame, utege sikio lako, uwasahau watu wako na nyumba na baba yako. Naye mfalme atautamani uzuri wako, maana ndiye bwana wako, nawe umsujudie. Na binti Tiro analeta kipawa chake, nao matajiri wa watu watajipendekeza kwako. Binti mfalme yumo ndani ana fahari tupu, mavazi yake ni ya nyuzi za dhahabu. Atapelekwa kwa mfalme na mavazi yaliyofumwa kwa uzuri.”​—Zab. 45:8-14a.

6. Huyu “binti mfalme” anayeletwa kwa Mfalme ni nani, naye Yohana Mbatizaji alihusianaje naye?

6 Sasa, ni nani huyo “binti mfalme” anayepelekwa kwa mfalme mwenye kumtamani wafanye ndoa huku kipindi hicho kikiwa chenye furaha kwa kupigwa vyombo vya muziki rasmi? Hakika yeye ndiye binti ya Mfalme, yaani, ya Yehova Mungu, “Mfalme wa umilele.” (Ufu. 15:3, NW) Hivyo yeye ni binti wa kifalme. Yeye ndilo kundi la Kikristo lililotukuzwa la washiriki 144,000, ambao wanaonwa kuwa na umoja, jamii iliyoungana. Yohana Mbatizaji alikuwa na pendeleo lenye kuheshimika la kuwaleta washiriki wa kwanza wa kundi hilo la bibi-arusi wajuane na Yesu Kristo duniani. Yohana alisema hivi: “Aliye naye bibi arusi ndiye bwana arusi; lakini rafiki yake bwana arusi, yeye anayesimama na kumsikia, aifurahia sana sauti yake bwana arusi. Basi hii furaha yangu imetimia.”​—Yohana 3:29; 1:35-42; Ufu. 14:1-5.

7. Kwa kufanya wanafunzi, mitume waliwaposa hawa kwa nani, nao wote pamoja wanakuwa nini mbinguni?

7 Vivyo hivyo, kwa kufanya wanafunzi wa Kristo, mtume Paulo na mitume wale wengine waliwaposa wanafunzi wao wawe kama’“bikira safi” kwa Yesu Kristo, yeye aliye “mume mmoja.” (2 Kor. 11:2) Kama msichana aliyechumbiwa aondokaye nyumbani kwa wazazi wake akajiunge na mumewe na kuishi pamoja naye, wanafunzi walioposwa kwa Bwana-arusi wa mbinguni lazima wawasahau watu wao wenyewe wa kidunia na nyumba ya kidunia ya baba yao na kuweka mapendo yao juu ya Mhebi wao wa mbinguni, Yesu Kristo. Baada ya kumaliza mwendo wao wa kidunia kwa uaminifu wakiwa na usafi kama wa bikira, lazima waingojee sauti ya Bwana-arusi wao awaitapo katika ufufuo kutoka kwa wafu. (1 The. 4:16, 17; Yohana 6:54) Katika mbingu wale wote 144,000 wanakuwa pamoja “binti” ya Yehova Mfalme, kwa maana aliitumia roho Yake akawazaa akiwa Baba yao mlezi. Kwa umoja wanakuwa Yerusalemu Mpya, unaoitwa “Bibi-arusi aliyekwisha kupambwa kwa mumewe.”​—Ufu. 21:2, 9.

8. Kwa sababu ya asili ya tukio hilo, kwa kufaa ni nani wanaohudhuria kulingana na Zaburi 45, nao hao wanaohudhuria katika utimizo wa zaburi hiyo ni nani?

8 Ni tukio la kifalme, hii ndoa ya mwana wa Mfalme kwa binti ya Mfalme. Hiyo inafanya watu wa kifalme wafae kuhudhuria, “malkia” na mabinti wa kifalme pia. Tengenezo lote la Mungu la mbinguni lililo kama “mke” wa kimalaika wa huyu “Mfalme wa umilele” linafurahi. Pia washiriki wote wa kimalaika wa tengenezo hilo wanafurahi pamoja kama mabinti za kifalme. Viumbe vyote hivyo vya kimbinguni vinakumbuka kwamba Yehova Mungu ndiye aliwezesha hayo yote, kwa hiyo vinasema: “Na tufurahi, tukashangilie, tukampe utukufu wake; kwa kuwa arusi ya Mwana-Kondoo imekuja, na mkewe amejiweka tayari.”​—Ufu. 19:7.

9. “Wanawali wenzake wanaomfuata” wanafurahia wapi, na kwa sababu gani huko?

9 Walakini, je! kuna ye yote duniani atakayefurahi pamoja na mbingu takatifu juu ya tukio hilo lenye fahari lenye ubora katika ulimwengu wote? Ndiyo! Zaburi 45:14, 15 inaonyesha hivyo, inapoendelea kusema: “Wanawali wenzake [bibi-arusi] wanaomfuata, watapelekwa kwako [Mfalme Bwana-arusi]. Watapelekwa kwa furaha na shangwe, na kuingia nyumba ya mfalme.” Sasa, ni wapi wanawali hao wenzake wanapofurahia? Ni kweli kamba wanasemekana kwamba wanaingia nyumba ya mfalme, ambaye ni wa mbinguni, lakini je! wanaolewa na mfalme? Hapana! Sivyo ilivyo, kwa maana wao hata hawafikii hatua ya kuposwa naye. Kwa hiyo hawazaliwi kwa roho ya mungu kwa maisha ya mbinguni.​—Yo-hana 3:3, 5.

10. “Wanawali wenzake wanaomfuata” wanafananisha nani leo, na inakuwaje kwamba wao wako duniani hali ndoa inafanyiwa mbinguni?

10 Washiriki wa jamaa ya “binti mfalme” wameposwa kwa Kristo hapa chini duniani, kwa hiyo wameposwa wakiwa bado wanadamu. Basi wanawali wanaomfuata bibi-arusi tu bila kutazamiwa wakaolewe na Mfalme Bwana-arusi wanapasa wawe ni jamii ya kidunia. Wanaonekana duniani wakati ndoa ya mbinguni inapokuwa karibu kukamilishwa. Kwa hiyo wenzi hao bikira wanafananisha “mkutano mkubwa” walioanza kutokea katika huu “wakati wa mwisho” na ambao wanajiunga na mabaki ya jamii ya bibi-arusi kabla ya kuondoka duniani wakajiunge na Bwana-arusi Yesu Krista mbinguni. Kwa kupatana sana na hilo, “mkutano mkubwa,” kama ulivyotabiriwa katika Ufunuo 7:9-l7, ulianza kufanyika mwaka 1935 na kujishirikisha na washiriki wa mwisho wa jamii ya bibi-arusi iliyozaliwa kwa roho. Kwa kuhifadhiwa hai wapite ‘dhiki kubwa’ inayokuja watakuwa hai hapa duniani wakati ndoa ya mbinguni itakapotokea. Watafurahia sana tukio hilo.​—Zab. 45:15.

“WANA WA KIFALME KATIKA DUNIA YOTE”

11. Je! utukufu wa Kristo wa sasa na wa wakati ujao unategemea umashuhuri wo wote wa babu zake za kidunia, nayo Zaburi 45:16 inaoyeshaje kwamba ndoa yake kwa kundi huko mbinguni inatokeza watoto?

11 Alipokuwa dunaini, Yesu Kristo alikuwa na mababu mashuhuri. Lakini utukufu wake wa sasa na wa wakati ujao hautegemei ubora wo wote aliopewa na mababu hao. Baada yake ukoo wa kifalme wa Mfalme Daudi hausongi mbele hata kidogo, kwa maana yeye ndiye Mrithi wa Daima wa Mfalme Daudi na hakuna mri-thi atakayepitishiwa ufalme wake hata kidogo. (Luka 1:31-33) Walakini, Zaburi 45:16 (NW) yaonyesha ndoa yake na kundi la wanafunzi 144,000 waliotukuzwa kuwa yenye matunda, sawasawa na vile ndoa ilivyokusudiwa iwe. Kwa hiyo, mstari huo, anaoambiwa Mfalme Bwana-arusi, wasema hivi: “Katika mahali pa babu zako kutakuwako wana wako, ambao utawaweka kama wana wa kifalme katika dunia yote.”

12. Cheo kilicho cha juu zaidi ambacho “wana” hawa duniani waweza kufikia ni cheo gani, na kwa sababu gani Mfalme atakuwa na wana wa kutosha wa kuwekwa “katika dunia yote”?

12 Hakuna ye yote wa “wana” hao atakayekuwa mrithi wa Mfalme wa mbi-nguni. Cheo cha kuwa mwana wa kifalme duniani ndicho cheo cha juu zaidi ambacho ye yote wa “wana” hao aweza kufikia. Ili kuweze kuwekwa “wana wa kifalme katika dunia yote” watapaswa wawe wengi. Mfalme atakuwa na “wana” wa kutosha kwa kusudi hilo, kwa maana, zaidi ya cheo chake “Mungu mwenye nguvu,” kingine cha vyeo vyake kitakuwa “Baba wa milele.” (Isa. 9:6) Dhabihu yake kamilifu.ya kibinadamu iliyotolewa wanadamu wote ilimwezesha kuwa hivyo. Kwa dhabihu hiyo ya ukombozi aliwanunua wote.

13. Mfalme atakuwaje Baba mpaji-uzima kwa wafu wote waliokombolewa, nao “mkutano mkubwa” utawezaje kumtolea Mfalme “wana wa kifalme’’ wa kwanza?

13 Kwa hiyo Mfalme anaweza kuwa mpaji-uzima kwa “mkutano mkubwa” wa wanawali wa bibi-arusi watakaookoka “dhiki kubwa” na kuja chini ya ufalme wake wa miaka 1,000. Anaweza pia kuwa baba ya wanadamu wote waliokufa, kutia na babu zake wa kidunia. Namna gani? Kwa kuwafufua warudie uzima hapa duniani kutoka kwa wafu. (Yohana 5:28, 29) Wanaume wenye kumwogopa Mungu wanaostahili kati ya watoto wote hao wa kidunia anaweza kuwafanya “wana wa kifalme katika dunia yote.” Kwa njia hiyo atatumia utawala wake katika dunia nzima. Kwa kufaa, “mkutano mkubwa” utakaoiokoka ‘dhiki kubwa’ na kuwa raia za kwanza za kidunia za ufalme wake ndio utakaomtolea mfalme ‘wanawe wa kifaIme’ wa kwanza kutumikia kama wajumbe wake wa kidunia.

14. Hawa “wana wa kifalme” kutoka katika “mkutano mkubwa” wataungwaje na wengine katika utumishi rasmi duniani, nao mpango huu wa kiserikali utahakikishia wanadamu wote kitu gani?

14 Litakuwa pendeleo kubwa namna gani! Hao “wana wa kifalme” waliotoka kati ya “mkutano mkubwa” wataungwa na wengine katika utumishi rasmi. Namna gani? Babu za Yesu Kristo na wanaume wengine waaminifu kutoka Habili mpaka Yohana Mbatizaji watafufuliwa wafanywe wajumbe wake wa kifalme. Lo! namna itakavyohakikishia wanadamu wote kupata serikali tukufu isiyopotoka! Hiyo ndiyo iie serikali inayohitajiwa sana iliyopangwa mapema ichukue mahali pa serikali zote za leo za kitaifa ambazo karibuni zitapambana na Mfalme mshindi Yesu Kristo.

15, 16. (a) Kulingana na Zaburi .45:​17, ni kwa sababu gani mtunga zaburi alitaka kuishi kwa muda mrefu? (b) Ni nani ajuaye jina hasa la Mfalme, na je! lastahili kutajwa na kusiflwa kwa muda wote huo?

15 Je! mioyo yetu haisisimuliwi na mataraja hayo ‘mema’ ya wakati ujao ulio karibu? Ndiyo, nazo ndimi zetu zinayafuatisha maneno ya kumalizia ya mtunga zaburi aliyomwambia Mfalme mwenye mapendezi ambaye Mungu amemwekea serikali hiyo juu ya mabega yake; “Mimi nitalitaja jina lako katika vizazi vyote vitakavyokuja. Hiyo ndiyo sababu makundi ya watu yenyewe yatakusifu wewe kwa wakati usiojulikana, hata milele.”​—Zab. 45:17, NW.

16 Mtunga zaburi alitaka kuishi muda mrefu​—“katika vizazi vyote vitakavyokuja”​—ili tu alitaje jina la mfalme. Yeye hakutaja jina la mfalme. Kwa kweli, yeye hakujua jina la mfalme ambaye aliandika juu yake kwa njia ya unabii chini ya uongozi wa roho. Lakini sisi leo twaweza kumfahamu Mfalme ambaye mtunga zaburi aliandika juu yake kwa njia ya unabii, nasi twalijua jina lake. Ni Yesu Kristo, Mwana wa Yehova Mungu. jei jina lake lastahili kutajwa “katika vizazi vyote vitakavyokuja”? Mtunga zaburi alitabiri kwamba kungekuwako “watu” ambao wangefikiri hivyo na ambao kwa sababu hiyo ‘wangemsifu’ mwenye jina hilo “kwa wakati usiojulikana, hata milele.”

17. Kwa hiyo sasa ni wakati utufaao sisi kufanya nini, nako kufanya hivyo kutamaanisha nini kwetu?

17 Leo nafasi i mbele yetu ya kuipita tukiwa hai ile siku ya kupambana na mataifa yote na kuingia katika baraka za ufalme wa Mungu utakaochukua mahali pa mataifa yote. Hata sasa kwa imani tunaweza kushangilia pamoja Mfalme wake mtiwa mafuta, kwa maana ni hakika atashinda katika Har–​Magedoni, tena ni hakika atatawala dunia iliyosafishwa muda wa miaka 1,000. Ah, basi, sasa​—leo​—ndio wakati unaotufaa tujiweke kati ya watu wale watakaomsifu Mfalme mshindi “kwa wakati usiojulikana, hata milele.” Hii itamletea Yehova Mungu, Baba yake wa mbinguni utukufu, ambaye yeye mwenyewe ndiye “Mfalme wa umilele” na “mfalme wa mataifa” aliye mkuu zaidi, Kufanya hivyo kutamaanisha kwetu maisha yenye kuendelea ya kumsifu Mfalme Wake aliyetiwa mafuta “hata milele.” Hii itaipa maisha maana kweli kweli. Itaweka mbele yetu kusudi tukufu sana la kuishi kwa umilele wote.​

—Kutoka The Watchtower Jan. 15, 1979.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki