Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w79 8/1 kur. 23-24
  • Mahubiri ya Mlimani—Wakristo kama “Chumvi” na “Nuru”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mahubiri ya Mlimani—Wakristo kama “Chumvi” na “Nuru”
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • NURU ING’AAYO KWA UTUKUFU WA MUNGU
  • “Ninyi Ni Chumvi ya Dunia”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Chumvi Ni Bidhaa Muhimu
    Amkeni!—2002
  • Yesu Angejibuje?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Mafundisho ya Kikristo Yanasaidiaje Jamii?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
w79 8/1 kur. 23-24

Mahubiri ya Mlimani​​—⁠Wakristo kama “Chumvi” na “Nuru”

BAADA ya zile “heri” tisa za Mahubiri yake ya Mlimani, Yesu alizungumza juu ya namna wafuasi wake wangekuwa na matokeo juu ya jamii ya kibinadamu. Yeye alisema hivi: “Ninyi ni chumvi ya dunia.”​—⁠Mt. 5:13; linganisha Marko 9:50; Luka 14:34, 35.

Wasikilizaji wa Yesu walifahamiana vizuri na chumvi. Ilitumika kuzidisha ladha (utamu) ya chakula na kukihifadhi kisiharibike. Kwa wazi, kwa sababu chumvi ilifananisha kutokuharibika au kutooza, Mungu aliamuru kwamba ifuatane na “kila toleo la sadaka” juu ya madhabahu yake. (Law, 2:13) Wakati wa siku za Yesu makuhani waliotumikia hekaluni mwa Yehova katika Yerusalemu walitia chumvi kwenye nyama, nafaka na matoleo ya sadaka za uvumba zilizotolewa juu ya madhabahu ya sadaka za, kuteketezwa. Historia ya Kiyahudi yasema kwamba kwa ajili ya kusudi hili chungu la chumvi liliwekwa karibu na jukwaa iliyoongoza kwenye madhabahu hayo. Katika eneo la hekalu mlikuwa na ghala kubwa, iliyoitwa “chumba cha chumvi,” ili kutosheleza mahitaji.

Wanafunzi wa Yesu walipaswa kuwa “chumvi ya dunia.” Hii ingalikuwa kweli katika utendaji wao wa kutolea wengine ushuhuda juu ya ufalme wa Mungu na katika mwenendo wa mtu binafsi. Kutoa ushuhuda wa Kikristo kumewafanya wengi wamkubali Yesu kuwa Masihi aliyeahidiwa na kuiamini dhabihu yake iondoayo dhambi. Hii imetokeza nafasi ya kuyahifadhi milele maisha za waamini hao. (Yohana 6:47; Rum. 10:13-15) Tena, kwa kuongoza watu waishi kulingana na kanuni za Biblia, wafuasi wa Kristo wanapunguza ongozeko la kuharibika kwa tabia njema na hali ya kiroho katika jamii ya kibinadamu.

Hata hivyo, Yesu aliongeza onyo, akisema: “Lakini chumvi ikiwa imeharibika itatiwa nini hata ikolee? Haifai tena kabisa, ila kutupwa nje na kukanyagwa na watu.” Mfafanuzi wa Biblia Albert Barnes anaonyesha kwamba, tofauti na chumvi ya kawaida (sodium chloride), chumvi ambayo Yesu na watu wa wakati wake walifahamiana nayo “ilikuwa na taka, na ilichangamana na mboga na vitu vya mchangani; hata kwamba ingeweza kupoteza ladha yake, na vitu vingi vya mchangani kubakia. Hii haikufaa kitu ila kutumiwa, kama inavyosemwa, kuwekwa barabarani, au mapitoni, kama sisi tunavyotumia kokoto.”

Wakristo wanapaswa kujihadhari kutoacha jitihada yao ya kuzishiriki “habari njema” za ufalme wa Mungu pamoja na jirani zao. (Marko 13:10) Pia, lazima wajilinde wasiangukie katika mifano ya mwenendo usiopatana na uongozi wa Maandiko. Ama sivyo, hali yao ya kiroho itaharibika na kuwa kama chumvi iliyoharibika​—⁠isiyokolea, isiyo na utamu, isiyo na ladha​—⁠ambayo haifai tena kabisa,​—⁠-Linganisha Waebrania 6:4-8; 10:26-29.

NURU ING’AAYO KWA UTUKUFU WA MUNGU

Akionyesha zaidi matokeo yenye faida ambayo wafuasi wake wangetokeza juu ya jamii ya kibinadamu, Yesu alisema: “Ninyi ni nuru ya ulimwengu.”​—⁠Mt. 5:14.

Kutokana na Neno la Mungu aliloliongoza, sana sana mafundisho na mfano wa Yesu Kristo, unatoa nuru inayosaidia watu waone mambo kama vile Mungu ayaonavyo. (Mit. 6:23; Isa. 51:4; Mt. 4:16; Luka 1:79; 2:32; Yohana 1:4-9; 3:19-21; 8:12; 9:5) Kwa utendaji wao wa kutoa ushuhuda hadharani, wanafunzi wa Yesu wanatolea watu nuru kuhusu hali ya dhambi ya wanadamu, kusudi la Mungu la kuondoa dhambi kupitia kwa Yesu Kristo, na mipango yake ya ufalme ya kuwabariki pamoja na uzima wa milele kwa wote wanao mwamini Yesu.​—⁠Yohana 3:16, 36; Rum. 3:23, 24.

Walakini kuwa “nuru ya ulimwengu” kunatia ndani mengi zaidi. Mtume Paulo anaandika hivi: “Enendeni kama watoto wa nuru; kwa maana kuwa tunda la nuru ni katika wema wote na haki na kweli.” (Efe. 5:3-9) Lazima Wakristo wawe mifano ing’aayo ya mwenendo unaolingana na kanuni za Biblia.

Kuhusu wanafunzi wake kuwa kama wachukuaji wa nuru, Yesu aliendelea kutangaza hivi: “Mji hauwezi kusitirika ukiwa juu ya mlima. Wala watu hawawashi taa na kuiweka chini ya pishi, bali juu ya kiango; nayo yawaangaza wote waliomo nyumbani.”​—⁠Mt. 5:14, 15.

‘Mji ulio juu ya mlima’ waweza kuonekana kwa urahisi, hata kutoka mbali sana. Vivyo hivyo, watu wanaomwiga Yesu Kristo huonekana mara moja kuwa watu “walio na juhudi katika matendo mema.” (Tito 2:14) Jithihada zao za kuonyesha waziwazi sifa za kimungu, kama vile kujiweza, usafi, bidii kazini, usemi wa kujenga na umoja wa jamaa huvutia wengine ifaavyo. (Tito 2:1-12) Vilevile wana nia ya ‘kutokuwa sehemu ya ulimwengu,’ kutojitia katika siasa zake, vita vyake na njia zake za maisha ya uasherati. (Yohana 15:19; 17, 14-16) Nyakati nyingine hii inatokeza dhihaka na mateso kwa Wakristo wenye kufuata uongozi wa dhamiri.​—⁠Mt. 24:9; 1 Pet. 4:4.

Akiwa na sababu nzuri, basi, Yesu anaongeza kusema kwamba watu huweka taa si “chini ya pishi [Kigiriki, modios, iwezayo kubeba galani mbili],” “bali juu ya kiango, ambapo inaweza kuangaza chumba chote. Wafuasi wa Yesu hawapaswi kuachilia upinzani kutoka kwa ulimwengu uwafanye wafiche au kujiwekea wenyewe kweli zile ambazo wamepata kujua juu ya Mungu. Wala hawawezi kufuata mwenendo usiolingana na kanuni za Biblia, kwa kuwa, hata ikiwa watu kama hao wangeendelea kwa juhudi kutangaza kweli ya Biblia matendo yao yangefunika thamani yake.​—⁠2 Pet. 2:2.

Akizungumza juu ya taa inayong’aa kiangoni, Yesu aliendelea kusema: “Vivyo hivyo nuru yenu na iangaze mbele ya watu, wapate kuyaona matendo yenu mema, wamtukuze Baba yenu aliye mbinguni.” (Mt. 5:16) Lo! namna ilivyo sababu kubwa sana kuendelea kuangaza “kama mianga katika ulimwengu”! (Flp. 2:15) Kwa kuyatazama “matendo mema” ya Mkristo, watu mmoja mmoja wanaweza kuufahamu wema wa Mungu. Mara nyingi watazamaji kama hao husukumwa na moyo “wamtukuze” Mungu na kuwa waabudu wake pia. Kwa hivyo, mtume Petro alionya kwa upole hivi: “Mwe na mwenendo mzuri kati ya mataifa, ili, iwapo huwasingizia kuwa watenda mabaya, wayatazamapo matendo yenu mazuri, wamtukuze Mungu siku ya kujiliwa.”​—⁠2 Pet. 2:12.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki