Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w78 10/1 kur. 4-5
  • Jina la Mungu Lilipatwa na Nini?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jina la Mungu Lilipatwa na Nini?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • KWA SABABU GANI WAKAACHA KUTUMIA JINA LAKE?
  • Yehova
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
  • A4 Jina la Mungu Katika Maandiko ya Kiebrania
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
  • Je! Mungu Ana Jina?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • Yehova
    Ufahamu wa Kina wa Maandiko
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
w78 10/1 kur. 4-5

Jina la Mungu Lilipatwa na Nini?

MWANAMKE aliyetajwa katika makala iliyotangulia alikuwa akitumia Biblia zilizokuwa zikisomwa “BWANA” na “Mungu” katika sehemu nyingi ambazo sasa alipata jina “Yehova.”‏

Lakini wakati mhudumu huyo alipomtolea sababu kwa fadhili na kumwonyesha kwamba BWANA ni jina la cheo, si la pekee, yeye alikubali. Ndipo alipomwonyesha Isaya 42:8, ambapo Biblia nyingi husomwa hivi: ”‏Mimi ni BWANA; ndilo jina langu; na utukufu wangu sitampa mwingine.” Mwanamke huyo alieleza kwamba bila shaka BWANA lilimaanisha Muumba, lakini akakubali kwamba lenyewe si jina. Kwa kuwa mstari huu unazungumza juu ya “jina” la Mungu, jina hilo ni gani?

Ili tujue jibu, tunahitaji kuchunguza kifupi mambo fulani juu ya Biblia, ambayo hapo mwanazoni iliandikwa katika Kiebrania na Kigiriki. Hata ingawa kwa kawaida huangalii mambo haya, fikiria mambo haya kwa kifupi, kwa kuwa yatahusiana (yatakamatana) sana na uchunguzi wetu wa jina la Mungu na lako baadaye.

Katika Kiebrania cha asili katika Isaya 42:8 utaona kwamba, mahali pa neno la jina la cheo “Bwana,” pana herufi nne za Kiebrania ambazo ndizo jina la Mungu יהוה (namna ya Kiebrania cha kisasa). Mara nyingi zinaitwa Tetragrammaton (maana yake, “herufi nne”) na katika Kiswahili zinaonyeshwa katika herufi hizi YHWH. Matamshi yanayojulikana sana ya herufi hizo nne katika Kiswahili ni “Yehova” na “Yahweh.” (Mengi zaidi yatasemwa juu ya hili baadaye.)

Watu wa kale wa Mungu Waebrania waliheshimu sana jina Lake na walilitumia. Lilitumiwa sana katika Biblia, linaonekana zaidi ya mara 6,900. Je! unajua maana ya hilo? Jina la Mungu lilikuwa mbele za waabudu wa kweli kila wakati walipokuwa wakisoma “neno” la Mungu au waliposikia likisomwa. (Yos. 1:8; 8:34, 35) Kwa mfano, Musa aliwaamuru watu hao wakusanyike mara kwa mara wasikilize torati ikisomwa katika Kumbukumbu la Torati, jambo lililomaanisha kwamba wangesikia jina la Mungu zaidi ya mara 500. (Kum. 31:10-12) Tena, inaelekea kwamba Zaburi 113 mpaka 118 ziliimbwa na kila jamaa kila wakati wa Sikukuu ya Kupitwa. Katika ile misfari 29 katika Zaburi ya 118 peke yake, jina la pekee la Mungu lingeimbwa mara 22.​—Linganisha Mathayo 26:30.

KWA SABABU GANI WAKAACHA KUTUMIA JINA LAKE?

Waabudu Waebrania walikuwa na sababu nyingi za kulitumia jina la Mungu. Biblia iliwasihi, “litajeni jina lake,” na ‘walipende jina lake.’ (Isa. 12:4; Zab. 69:36) Ingawa hivyo, wakati fulani baadaye, kwa sababu za ushirikina Wayahudi waliacha kulitaja jina hilo takatifu la Mungu. Walipolifikia, walipokuwa wakisoma Biblia, walisema Adonay (BWANA) au Elohim (Mungu). Kwa sababu gani?

Wengine wanasema kwamba hii ilisababishwa na hofu ya kulitumia vibaya jina hilo takatifu la Mungu. Ni kweli kwamba zile Amri Kumi zilisema kwamba jina hilo lisingetajwa bure. (Kut. 20:7) Kwa wazi hiyo iliondoa matumizi yo yote ya upuzi au ya hila ya jina hilo. Katika Walawi 24:16 amri ilitolewa kwamba ye yote atukanaye jina la Mungu, awe mwenyeji Mwebrania au mgeni, angeuawa. Lakini hiyo ilimaanisha kuepuka kulitukana, si kuepuka kulitumia. Kwa hiyo, ushuhuda unaonyesha kwamba mwingi wa wakati wa Biblia Waebrania wa kawaida walilitumia jina la Mungu, katika utendaji wa kidini na kwa heshima katika maisha ya kila siku.

Kwa mfano, katika mwaka 1961, pango la kale lililotumiwa kama kaburi lilichimbuliwa maili kama 20 (kilometres 32) hivi kusini magharibi mwa Yerusalemu. Pango hili linaelekea lilikuwa likitumika kuanzia siku za Mfalme Hezekia (745-716 K.W.K.). Katika kuta zake kulikuwako miandiko ya Kiebrania iliyotumia zile herufi nne, kama hivi ”‏Yehova ndiye Mungu wa dunia yote.”‏ Na katika mwaka 1966, ripoti ilichapwa juu ya vipande vya vyombo vya udongo vilivyopatikana katika Arad, katika kusini mwa Israeli, ambavyo vilikuwa na maandishi. Mojawapo ambacho unaona, kilikuwa barua ya kibinafsi katika lugha ya Kiebrania aliyoandikiwa Eliashibu na raia mmoja. Barua hiyo ilianza hivi: “Kwa bwanangu Eliashibu, Yahweh huenda akakutakia amani. Na sasa . . . ”​—Israel Exploration Journal, Vol. 13, Na. 2, kur. 74-92; Vol. 16, Na. 1, kur. 1-7.

Kwa sababu ya uhakika wa kwamba Waebrania wengi wa kale hata walilitumia jina la Mungu katika hali ambazo hazikuwa za kidini kabisa, huenda mtu akataka kujua ni wakati gani kuepuka kulitumia kwa ushirikina kulipoanza. Kwa kweli, hakuna mtu anayeweza kuwa na hakika leo. Wengine kwa sababu ya kufuata maandishi ya waalimu wa Kiyahudi wamesema kwamba, jina hilo halikutumiwa katika karne ya kwanza Yesu alipokuwa duniani. Lakini ikiwa kuepuka kulitumia huku kwa ushirikina kulikuwa kukienea wakati huo, haina maana kwamba jina la Mungu halikuwa likitumiwa hata kidogo. Juu ya jambo hili, Dakt. M. Reisel aliandika hivi: “Tetragrammaton [zile herufi nne] ni lazima ziwe ziliendelea kutamkwa na Kuhani Mkuu mpaka kuharibiwa kwa Hekalu la Pili katika mwaka 70 W.K.”

Lakini, huenda ukataka kujua juu ya Yesu na mitume wake. Je! wao wangetumia jina la Mungu katika kuandika, kusema au katika kusoma Maandiko? Kwa mfano, namna gani wakati Yesu aliposimama katika sinagogi katika Nazareti akasoma Isaya 61:1? Zile herufi nne zinapatikana katika andiko hilo, ambalo linaanza hivi: “Roho ya Bwana Yahweh imepewa kwangu, . . . ” (Jerusalem Bible) Je! wewe unafikiri kwamba hata ikiwa Wayahudi wengine waliofuata ushirikina walikataa kutamka jina la Mungu, Yesu angeepuka kulitamka kwa makusudi? Kumbuka kwamba alisema: “Jina lako nimewadhihirishia watu wale ulionipa katika ulimwengu.”​—Yohana 17:6.

Habari ile aliyoisoma Yesu alipokuwa akisoma Isa. 61:1 inapatikana katika Luka 4:18, 19. Ukiangalia mistari hii katika Biblia yo yote inayojulikana sana katika Kiswahili hutaona jina la Mungu la pekee. Mahali pake, utaona ikionyeshwa kwamba Yesu alisoma hivi: “Roho wa Bwana yu juu yangu . . . ”​—Union Version.

Je! wewe unafikiri hivyo ndivyo aliyosema Yesu? Ni kwa sababu gani Biblia nyingi zasema “Bwana” hapa mahali pa kutumia jina la pekee la Mungu? Jibu linahusu uchunguzi unaopendeza sana. Tunakukaribisha uufuate na kuangalia mambo ambayo yamefunuliwa.

[Picha katika ukurasa wa 5]

Tetragrammaton (herufi nne) katika barua iliyoandikwa katika chombo cha udongo

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki